Aliyekuambia Ccm wanategemea kura ili kupata ushindi ni nani ?Wewe ni miongoni mwa wale wasiokuwa na hekima au kichwanj wewe ni kichaa. Kauli zenu hizi zinamletea mazingira magumu sana kisiasa Rais Dr Samia. Kwa ufupi Rais Samia kura za kanda ya ziwa mpaka sasa hana kabisa na asikudanganye mtu.
Na huo unaita ujanja ?Wapo wanasiasa wajanja waliokuwa wafuasi kindaki ndaki wa Magufuli waliweza kutambua kiuhalisia Magufuli hayupo tena na siasa zake hazina nafasi na kwa haraka sana wakaanza kuimba nyimbo mpya za kumsifia Samia huku wakimdhihaki kimtindo Magufuli na siasa zake.
Hii ni kweli kila wapendwa wetu wakitangulia mbele ya haki tunakuwa ni hatuko nao kimwili tuu lakini kiroho tunakuwa tuko nao hivyo hata Magufuli ni kweli ametangulia ila kwa wale wanaomkubali bado yuko mioyoni mwao, na ndio maana nikashauri Life After Life: Je, wajua Magufuli huko alipo anayaona yote? Je, tuendeleze 'double standards' ya 'cherry picking' au tuiachie Karma iwashughulikie?Hao watu wanaamini kuwa japokuwa Magufuli kimwili alishakufa lakini kiroho bado anaishi katikati yetu, hivyo anaweza kuendelea kuathiri maisha yetu
No hatuamini siasa zake zote lakini zile siasa zake nzuri na mazuri yake lazima yaenziwe na Samia ayaendeleze. Mambo kama hayaau ipo siku utawala na siasa zake zitafufuliwa upya na kuendelea kuongoza Tanzania!
Sii kweli. Tuko akina sisi tulimkubali sana Magufuli na sasa tunamkubali sana SamiaWafuasi hao wa Magufuli hawafurahishwi na hatua yoyote ya maendeleo (kisiasa, kiuchumi, kijamii) inayopigwa na mama Samia ambayo Magufuli hakuifikia au hatua yoyote ya kufutwa kwa baadhi yq siasa za Magufuli zisizokuwa na maana kwa watanzania.
Hapana hatutaki Magufuli asifiwe, tusichotaka ni Magufuli asibezwe!. Tunaweza kumsifia Samia kwa mazuri yote anayoyafanya bila ya kumpondea Magufuli.Wao wanataka kuona Magufuli akisifiwa katikati ya utawala wa Samia (wakati Magufuli alikuwa kinara wa kubeza serikali zote za Tanzania zilizomtangulia) au kuona utawala wa Samia ukianguka kwa namna yoyote.
Kwa hawa angalau uchunguzi ulifanyika na kesi kufikishwa mahakamani. Ila akina Ben, Azory na Lissu, ngoma bilabilaR.I.P Daudi Mwangosi na Dr Sengondo Mvungi.
Haya ni maelezo tu kama UDAKU kama ule kila ghorofa au petrol stations ni vya RIZWAN ili ku justify kile unachisema attach USHAHIDI...MAOVU YA MAGUFULI NI SEHEMU YA HISTORIA YETU
ANDREW Jackson ni Rais wa Saba wa Marekani. Aliongoza mwaka 1829-1837. Historia ilimkweza. Mwaka 1928, sura yake ikawekwa kwenye noti ya dola 20.
Miaka 88 baadaye, Serikali iliamua kuondoa picha ya Jackson kwenye noti ya dola 20. Sababu, Jackson alikuwa mfanyabiashara ya utumwa, alionea watu weusi na kukandamiza wahindi wekundu.
Kisha, picha ya mwanamama mwanaharakati, Harriet Tubman, ikapendekezwa ichukue nafasi ya Jackson.
Ingekuwa Tanzania, wagonjwa wa Stockholm Syndrome (wenye mahaba na watesaji), wangesema wanashindana na marehemu.
Pokea habari, historia hufundishwa kwa ajili ya mwendelezo wa mema na mafundisho ya kukwepa maovu yasijirudie.
Ukiona kiongozi anatolewa mifano mingi hasi, ujue alifanya maovu yaliyovuka kiwango cha ubinadamu.
Kuna tofauti kati ya makosa (errors au mistakes) na maovu (evils). Kukosea ni ubinadamu, kutenda maovu ni ushetani.
Wafanyabiashara kudhulumiwa fedha benki. Wamiliki bureau de change kunyang'anywa na kufilisiwa kikatili. Watu kuuawa kisha miili yao kuokotwa kwenye viroba fukwe za Bahari ya Hindi, hayo hayakuwa makosa ya kibinadamu. Ni maovu.
Tundu Lissu baada ya kupigwa risasi, akanyimwa mpaka matibabu, ubunge akafukuzwa, akadhulumiwa stahiki zake za ubunge akiwa kwenye kitanda cha matibabu. Haya hayakuwa makosa. Ulikuwa unyama. Ni uovu.
Kuchota fedha za umma Hazina. Sh1.5 trilioni. Sh2.4 trilioni. CAG Mussa Assad akabaini ufisadi wa Rais. Akasema Bunge ni dhaifu, halifanyi kazi ipasavyo. Rais akavunja Katiba na kumfukuza kazi. Wizi mkubwa kama huu na uvunjifu wa Katiba, sio makosa. Yalikuwa maovu.
Watu kupotea na serikali kujikausha kufanya upelelezi, sio makosa ya kibinadamu, ni ushetani. Ni uovu.
Kama ambavyo nchi nyingine hupitia historia za viongozi wao na kurekebisha, nasi hatutakaa kimya. Maovu ya Magufuli ni sehemu ya historia ya nchi yetu. Tutayasema sana. Dunia haipaswi kupotoshwa.
Miaka miwili imepita tangu alipofariki dunia. Wasiwasi umeondoka. Maovu mengi yameondoka. Ikiwemo ujambazi wa kubambikia watu kesi za uhujumu uchumi na kulazimisha watoe fedha. Pesa zikaingizwa akaunti binafsi na kufichwa China.
Ndimi Luqman MALOTO
My taķe;
Haya nadhani ndio majibu yenu sahihi watu wa yule mwovu!
Naona umji shetani maana nyie mnaafanana Mai la kulwa na doto ,inawezaje kuwa na vyeti feki wakati Kunatoto kakomaa nakuni ,shule ,mlo mmoja shule mpaka chuo apati kazi ,ala shetani ww umetengeneza cheti feki sababu mjomba ana cheo kakipa kazi mashetani nyiyeKama MWENYEZIMUNGU alimundoa yule Lucifer hawezi shindwa kwa nyie shetani ndogondogo
Wewe tena na hivi alikuwa mkristo[emoji28][emoji28][emoji28]
Kosa letu kubwa hatukumskiza Mzee Kingunge
Vipi kuhusu fedha za plea bargain?
USSR bhana una id kibao za kulinda legacy fekiMbona kama wewe ndio bado hujaamini?
Huyu mtu alitungisha mimba nyingi sana hapa nchini!
Inafika hatua maiti ina nguvu kuliko walio hai! Haijawahi kutokea.
Mambo vipi SHOGA WA UBUNGO KIBANGU?USSR bhana una id kibao za kulinda legacy feki
Hizo zitarudi tu. Mradi zishajulikana zilipo, hakuna shaka.Zipo china zinapumua tu. Mama afanye mpaka zirudi kusaidia maendeleo nchini
Kwani huyo JPM alikuwa msafi hadi achafuliwe?Waziri wa habari uliwekwa kwenye nafasi hiyo kimkakati kumchafua JPM?
Walevi huwa hawajibiwiKwani huyo JPM alikuwa msafi hadi achafuliwe?
Gwajima mhuni sana
Ndiyo ni sawa ni Mchafu kupitilizaWaziri wa habari uliwekwa kwenye nafasi hiyo kimkakati kumchafua JPM?
Wema hawafiNdiyo ni sawa ni Mchafu kupitiliza