Waganga wa kienyeji na wachawi ni mawakala wa shetani, kwanini wanapingana

Waganga wa kienyeji na wachawi ni mawakala wa shetani, kwanini wanapingana

Lazima kwanza uwe umemkiri Yesu kuwa BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAko.

Lazima uwe na Roho mtakatifu ndani anayekushuhudia kuwa wewe ni mwana wa Mungu.

Na lazima uisikie sauti na maelekezo ya Roho mtakatifu ndani Yako,

Lazima uchukie dhambi na uishi maisha matakatifu,

Lazima uwe mtu wa maombi na kusoma neno lake,

Lazima uwapende wenye dhambi na kuwaombea na kuwahubiri Ili waokoke.


Ubarikiwe.
ubarikiwe mkuu
 
Ila kuna waganga waliotumwa na Mungu, ukiona mganga anaeagua tu bila pesa, anachukuwa kiasi cha mboga tu, ila tu ukipona utaona utampa nini. Hawa ni waganga wa kweli na wameshaokoa wengi.
 
Uchawi unaishia dimension 03
Sasa ukiona unalogwa ujue tatizo kubwa lipo kwako wewe unayelogwa.

Maana ili ulogwe lazima lango lako liwe wazi.

Kuna innocence na guilty ukiwa innocence- (Mnyongofu) haumdhuru MTU wala kumuazia MTU mabaya ukiishi hivyo hata Kama hauendi msikitini au kanisani huwezi kulogwa.

Ili ulogwe lazima ulogeke , na njia rahisi ya kulogeka ni kuwa guilty kinyume cha innocence ni guilty.

Ukiona MTU anasema uchawi Una nguvu au amelogwa basi ujue yeye ndo Ana matatizo ameruhsu Giza ndani yake.


Unaweza kuona hii michezo yao wachawi huwa wanafanyiana wao kwa wao na sio watu wengine.


Wanawake huwa wanapitia hizi changamoto za kulogana kwa sababu hawapo innocence.

Dimension zipo nadhani hadi 7+ na uchawi huishia dimension 3 tu sasa ili ulogwe unakuwa umekubali mwenyewe kulogeka.

Ndo wajanja huwa wakiiba wanatubu na kujaribu kutakatisha walichokiiba hii yote hufanya ili kupandisha dimension ili wasiwe guilty na wakitubu huwezi kupiga ramli (dogma) ukawapata.


So uchawi MTU anayesema Una nguvu ni muhongo uchawi umekuzwa na mashekh na wachungaji bila sababu za msingi.
kwahiyoili usifanyiwe uchawi ni lazima tutubu mara tu tunapokosea?
 
Lazima kwanza uwe umemkiri Yesu kuwa BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAko.

Lazima uwe na Roho mtakatifu ndani anayekushuhudia kuwa wewe ni mwana wa Mungu.

Na lazima uisikie sauti na maelekezo ya Roho mtakatifu ndani Yako,

Lazima uchukie dhambi na uishi maisha matakatifu,

Lazima uwe mtu wa maombi na kusoma neno lake,

Lazima uwapende wenye dhambi na kuwaombea na kuwahubiri Ili waokoke.


Ubarikiwe.
Hii ni faith.
Kama mtu hana hiyo faith hawezi pata hayo.
Mimi nilikuuliza umetumia vigezo gani kusema walokole wanaheshimika sana katika ulimwengu wa Roho. Ili hali wapo walokole wanafanya ushirikina.? Huoni ume generalize tu bila uhalisia?
 
hii mizimu ya ukoo ni kitu common sana kukisikia, utaambiwa mizimu ya ukoo inataka hiki au kile
tunaepukaje? tukiacha kufanya vile inataka hatupati madhara?
(Mathayo 10:36)

Adui wa mtu ni yule wa nyumbani mwake, na YESU asema, sikuja kuleta Amani duniani, Bali UPANGA, kati ya baba na mtoto, Binti na mamaye nk nk

Ukiokoka, ukaamua kuachana na Ibada ya Mizimu, ujue unaanzisha vita ya kiroho,

Na adui zako watakuwa hao wa ukoo na familia Yako ya Damu na nyama, Kwa nje wanasali, ila ukimwambia Mimi sitafanya Mila au maelekezo ya Mizimu ya ukoo au family unakuwa adui nao,

Na ukiogopa kujitenga nao na kubeba msalaba wako kumfuata Yesu , sahau kuhusu mbingu, ni ya Wachache,

Ndiyo maana walokole huitwa wamechanganyikiwa, Ukiwa upande wa Mungu Kweli Kweli, lazima uwe adui wa Dunia.

Maisha ya wokovu ni vita Si lelemama, ukiona mtu anafanya Mila na Kanisani anaenda, analewa na Kanisani anaenda, huyo Bado Hana Ile ALAMA kwenye paji la uso.

Ubarikiwe.
 
kwahiyoili usifanyiwe uchawi ni lazima tutubu mara tu tunapokosea?


Unapojihisi upo guilty (Una-hatia)

Mfano umemuibia MTU , hii haijalishi wewe ni nani tayari dimension zinashuka 0-0 hivyo MTU akipiga dogma anakupata.

Kutubu pale unapokosea na kutumia kile ukichoiba kuinua maisha ya MTU Kama kindness act au charity tayari unakuwa umerudi dimension za juu.

MTU anayeelewa haya mambo hawezi tumia chale kujilinda bali anazingatia hayo mambo.


Fatilia vizuri watu wanaolalamika kulogwa utaona jinsi wali yo na Giza ndani yao.
 
Ni kama uislamu na ukristo ulivyo kila mmoja anajiona bora kuliko mwenzake japo woote ni Mawakala wa Mungu.
Ndivyo hata hao Mawakala wa shetani hupimana uwezo.
Kwa kawaida huwezi litengeneza Gari kisha usilifanyie test. Hivyo nguvu hasi ni muhimu kuithibitisha nguvu chanya iko na uwezo gani.
 
Hii ni faith.
Kama mtu hana hiyo faith hawezi pata hayo.
Mimi nilikuuliza umetumia vigezo gani kusema walokole wanaheshimika sana katika ulimwengu wa Roho. Ili hali wapo walokole wanafanya ushirikina.? Huoni ume generalize tu bila uhalisia?
Hayupo aliyeokoka mwenye Alama ya Mungu katika paji la uso wake na akafanya ushirikina. Huyo ni tapeli, au anetoka katika mstari.

Usichanganye mambo,

Wapo matapeli ambao huvaa suti na huja na vitambulisho kuwa ni wafanyakazi wa TRA Ili wakutapeli, wakati sio, ndio hao walokole Jina, hawatambuliki Mbinguni.
 
Hayupo aliyeokoka mwenye Alama ya Mungu katika paji la uso wake na akafanya ushirikina. Huyo ni tapeli, au anetoka katika mstari.

Usichanganye mambo,

Wapo matapeli ambao huvaa suti na huja na vitambulisho kuwa ni wafanyakazi wa TRA Ili wakutapeli, wakati sio, ndio hao walokole Jina, hawatambuliki Mbinguni.
Ndio ukubaki sasa kuwa uli generalize kimakosa.
Unaizunguziaje Matendo 8:18-20
 
Ila kuna waganga waliotumwa na Mungu, ukiona mganga anaeagua tu bila pesa, anachukuwa kiasi cha mboga tu, ila tu ukipona utaona utampa nini. Hawa ni waganga wa kweli na wameshaokoa wengi.
Hakuna. Hawajatumwa na Mungu
Shetani nae huwapa watu wake vitu vizuri ili kuwavuta kwake.
 
wakuu hebu tusaidiane.
waganga na wachawi ni wakala/agents wa ibilisi/shetani
kwanini wanapingana
mchawi anakuroga ufe, mganga anakutibu usife
cc rakims
ccmshanajr
walker water
Hakuna tofauti sana na kwenye imani ya Kimungu... Kabla ya kujiuliza ya wachawi hebu kwanza jiulize, "kwanini Waislamu wenyewe kwa wenyewe wanapingana? (Kuna madhehebu mengi ila Shia na Sunni ndo makuu na hayo ndo kila uchwao wanatupiana maneno cha ajabu Quran ni moja wanatumia) Uje kwa wakristo napo madhehebu ni mengi sana, wanapishana kila uchwao lakini Biblia ni moja, (jiulize swali hilo, maana hakuna swali lililo kosa jibu.. ukikosa jibu labda hujui tu)

Nilikuwa namsikiliza bwana mmoja anaitwa @Dr riziki mkali malela... Huyu bwana anajishulisaha na hayo mambo ya shirki... Anasema mhanga wa kienyeji ni mchawi pia.. ila tofauti ni kwamba mchawi anatumia uchawi kudhuru watu na kufanya uharibifu na mganga anatumia uchawi kuponya watu na kuwaokoa kutoka kwenye uharibifu uliosababishwa na shirk...

By the way mimi sio mtaalamu wa mambo ya Giza ila nafahamu kiasi... Bila Shaka umeelewa
 
Hili suala la uthibitisho ni tata maana mfano unakuta inajulikana hakuna dawa ya ugonjwa fulani lakini kuna watu huko wanatumia mitishamba yao kutibu ugonjwa huo huo ila kwa kuwa hakuna uthibitisho wa kisayansi kwa dawa hiyo basi inaendelea kubaki kuwa huo ugonjwa hauna dawa.
Nitishamba si uchawi.

Usiweke mambo ya mitishamba kama mfano kwenye habari ya uchawi.

Mitishamba ina chemical compositions ambazo zinaweza kuchunguzwa na kuthibitishwakisayansi.

Uchawi unathibitishwaje? Unapimwa kwa kipimo gani?
 
Back
Top Bottom