GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
- Thread starter
-
- #101
Tanzania inawafungia ndani watu wake mithili ya mbuzi wezi, lakini Kenya imewapa uhuru wa kwake kutoka kwa kuwa inawaamini watu wake. Kwa nini basi, pamoja na Tanzania kuwafungia ndani raia wake na Kenya kuwaruhusu wa kwake kutoka, passport ya Kenya inaizidi ya Tanzania?Jambo Moja ni muhimu kuzingatia, passport lazima ilindwe na kudhibitiwa Ili iweze kuheshimika duniani, tukifanya mchezo itatuwia vigumu Sana kitembea nchi za watu, itafika wakati huko nje ukijulikana tu wewe ni mtanzania, watu wanatukimbia
Unasema Kenya imeathirika negatively kwa sababu ya raia wake wengi kwenda nje? Ni mtazamo wako lakini si sahihi. Ili kupata mzania sahihi, orodhesha hasara zote na faida zote, kama hutabaini kuwa faida ni nyingi kuzidi hasara.Kenya imeathirika pakubwa Sana kwa kuruhusu watu wake kutoka kwa wingi bila udhibiti;
1)Wasomi wengi na wataalamu wazuri wameikimbia Kenya wako nje ya nchi Yao, matokeo ni haya ya uchumi wao kuporomoka kwa Kasi kwasababu waliobaki Kenya ni wale wa daraja la chini, majumba yanaporomoka Kila siku na miradi Yao yote ipo "poorly done".
2)Wasichana wa kikenya wengi wanatumikishwa Kama watumwa, wengi wanauliwa huko Uarabuni, thamani ya raia wa Kenya huko Uarabuni ipo chini Sana.
3)Kiusalama huko ndio usiseme kabisa, wasomali wote wako na Passport ya Kenya, wakitaka kuingia na kufanya unyama ni kitu Cha kawaida Sana. Hoja ya kukosekana usalama Kenya kuhusisha na kupakana na Somalia au South Sudan, mbona Ethiopia yenye kupakana na nchi hizohizo haina tatizo la Kiusalama?, Mbona Uganda imepakana na DRC na South Sudan lakini haina hilo tatizo?
Mkuu, wewe ndio unawashangaza watu, inaonekana hujatembea na Wala hujui jinsi nchi zonavyojiendesha duniani, hakuna nchi yoyote inayotoa "Government documents" kwa urahisi, Wacha passport, hata leseni ya udereva tu kuipata ni ngumu Sana.Mkuu, unaishangaza dunia kwa huo mtazamo. Ni North Korea pekee ndiyo inaweza ikakubaliana na mtazamo wako, kwa kuwa haipendi raia wake wajue jinsi Dunia inavyoenda. Kule watu "wanafugwa" na "kutumikishwa" kwa maslahi ya watawala.
Mkuu, kwa akili ya kawaida tu jiulize, Kweli Kenya inaweza kuwa na wasomi wengi kuzidi Japan na Ujerumani?. Eti Kenya inawatafutia kazi wasomi wake kwenda kufanya kazi Ujerumani, hicho ni kituko Cha mwaka.Mkuu, inaelekea hata Kenya bado hujafika. Hakuko hivyo kama unavyofikiri. Ina wasomi wa kutosha na ziada, ndiyo maana Serikali yake inafanya jitihada kuwatafutia raia wake kazi katika mataifa mengine.
Kwanini Ethiopia au Djibout hazina hilo tatizo la usalama na zimepakana na Somalia?Kenya imekuwa ranked poorly kwa sababu inapakana na Somalia,
Somalia kila siku ni vita na mashambulizi ya al shabaab
Passport siyo kwa ajili ya anayetaka kwenda kufanya kazi nje tu, mwingine anaweza akahitaji kwa ajili ya kwenda kutembea.Mkuu, ni mtu mjinga pekee atakayewekeza pesa nyingi katika elimu nchini kwake, Kisha akasherehekea Wasomi wake kwenda kufanya kazi nchi zingine.
Ukisoma kwa mkopo wa serikali ndio kusomeshwa na serikali, hivi serikali ikiacha kutoa mikopo Kuna mtu ataweza kwenda kupata mikopo Bank na kujisomesha?. Kwa hapa Tanzania 98% husomeshwa na serikali kwa kupitia mikopo.Serikali haisomeshi, bali inatoa mikopo tena kwa baadhi tu.
Kuna wengine, wengi tu, walisoma kwa kujilipia au kulipiwa na wazazi au walezi wao.
Nitajie hizo Serikali, ukiacha Tanzania, zinazodhibiti utoaji wa passport kwa raia wake kama unavyosema, kama hutaona kuwa hakutakuwepo hata na Serikali Moja ya watu wanaojitambua yenye ukiritimba wa hovyo kama huo.Mkuu, wewe ndio unawashangaza watu, inaonekana hujatembea na Wala hujui jinsi nchi zonavyojiendesha duniani, hakuna nchi yoyote inayotoa "Government documents" kwa urahisi, Wacha passport, hata leseni ya udereva tu kuipata ni ngumu Sana.
Hebu nenda Ulaya ukaombe leseni ya udereva uone hilo sakata lake. Kwahiyo mkuu, hizi serikali zote zinazodhibiti passpot zao unadhani ni wajinga au hawajui kitu, ila ninyi watu wachache ndio wenye akili?.
Mkuu, tatizo hujazunguka Dunia, na Wala hujui "International diplomacy" inavyofanya kazi. Passport ni document yenye kubeba utu wa Taifa nje ya nchi, mtu yeyote aliyebeba passport ya nchi lazima apewe heshima inayoendana na nchi yake huko ktk nchi anakokwenda, ni wajibu wa balozi zetu huko nje kuhakikisha mtu yeyote mwenye passport ya Tanzania anatetewa na kulindwa haki zake, huwezi kuwapa watu wa hovyo hovyo passport.
Mkuu, Kama nilivyokijibu hapo juu, huu uamuzi wa kuidhibiti passport umepitishwa na kukubalika hapa nchini na kupitishwa na vyombo vyote vyenye majukumu ya kusimamia Sheria za nchi na haki za binadamu. Sasa Kama wewe unadhani una akili nyingi kuwazidi hao wote waliopitisha na kusimamia jambo hili, basi Tanzania sio nchi sahihi kwako. Ila unayo haki ya kutoa mawazo yako, na serikali inayo haki ya kufanya vile inavyodhani ni sahihi.
Mkuu, Cape Town nimefika, nilikaa Century City kwa miezi mitatu. Century City ndio kuna Canal Walk Grand Mall.WalkMkuu, hivi utajiri unapatikana kwa kusafiri "aimlessly?". Sera ya nchi yetu ni kutoa passport kwa mtu mwenye sababu za msingi za kutaka kusafiri, ukiwa na sababu za kusafiri ndio unapewa passport.
Mkuu jaribu kufika CapeTown pale "Freedom square" uone jinsi watanzania wanavyoidhalilisha Tanzania, hutaki hata ujulikane Kama wewe ni mtanzania ukifika pale, wale jamaa wengi hawana passport, au walizipata kwa njia haramu.
Marekani kuna Wajapani wengi wanaofanya kazi huko, unataka kutudanganya kuwa Japan ina wasomi wengi kuizidi Marekani?Mkuu, kwa akili ya kawaida tu jiulize, Kweli Kenya inaweza kuwa na wasomi wengi kuzidi Japan na Ujerumani?. Eti Kenya inawatafutia kazi wasomi wake kwenda kufanya kazi Ujerumani, hicho ni kituko Cha mwaka.
Nchi kuwa na wasomi wengi lazima ionekane kwa vitendo, hivi ni jambo gani linakuonyesha kwamba Kenya Kuna wasomi wengi?. Uchumi inazidi kuporomoka, umasikini unaongezeka, ukabila inazidi kukomaa, viwanda vinafungwa, uzalishaji wa bidhaa viwanda I unapungua, kilimo kinakufa kwa kukosekana mifumo ya umwagiliaji, magonjwa ya kuambukiza Kama kipindupindu ndio nyumbani kwake, hao wasomi Kenya wanafanya nini zaidi ya kutoroka nchi Ili kutuma remittances?
Serikali ni jukumu lake kuwapa elimu watu wake, elimu ni haki ya raia. Hivi kwanini mnahusisha Sana elimu na ajira?, kwani wakulima, wavuvi, wafanyabiashara na wafugaji hawapaswi kupata elimu?.Kama umesoma, katika harakati zako zote za kusoma kwako hadi level uliyofika, KUNA PAHALA ULIKUBALIANA NA SERIKALI KWAMBA UTAKUJA KUFANYA KAZI SERIKALINI BAADA YA KUSOMA KWA KODI ZINAZOKUSANYWA NA SERIKALI? Haya, serikali imekaa miaka mingapi haijaajiri mtu, wale wahitimu wafanyeje? Kuna wakati tuwe waharisia tuachane na nadharia..!!
BTW, siku hizi elimu kwa mkopo ambao unakuja kuulipa baadaye...!!!
Kuna makampuni, wakikupeleka baadhi ya training, hasa zenye gharama kubwa, unasaini mkataba kuwa ukitoka huko utafanya kazi kwao kwa kipindi fulani, say mika mitatu..!! Ukimwacha mtu huru ujuzi uliompa anaweza akaenda kuutumia kwingine...!!
Turudi huko kwenye serikali. Kama serikali ingekuwa inaajiri kila aliyesoma kwa kodi za serikali, kungekuwa na wasomi mitaani wasio na ajira?
Kukujibu swali lako na huyo msichan kuolewa na mtu mwingine, TATIZO LIPO KWAKO WEWE ULIYEMSOMESHA. UMEWEKEZA BILA KUJIHADHARI. HIVI UNADHANI KWANINI HATA MAKAZINI TUNA MIKATABA? KWANINI HATA KUTOA HELA YAKO ULIYOIWEKA BENKI LAZIMA UWEKE SAHIHI? HUKO KUTOCHUKUA TAHADHARI MAPEMA NDO HUPELEKEA WATU KUUWA..!!
Wewe ambaye Hadi Leo unayehusisha elimu na kazi ya kuajiriwa ndiye unapaswa kubadili mawazo yako, unasikia huo mpango wa BBT unaosimamiwa na Hussein Bashe?Unazungumzia wasomi majobless? Yaani mtu amalize chuo leo, halafu amsubiri mwekezaji miaka minne bila ajira..!!!
YOU NEED TO CHANGE YOUR THINKING KWENYE JAMBO HILI..!!
Ingelikuwa ni mamlaka yangu, ningeagiza, hata kama hupendi, ushikilie nafasi ya UKAMISHNA UHAMIAJI, hata kama ni kwa kipindi cha mwaka mmoja tu.Mkuu, Cape Town nimefika, nilikaa Century City kwa miezi mitatu. Century City ndio kuna Canal Walk Grand Mall.
Hamna mtu ameshawahi idhalilisha nchi ya ya Tanzania 🇹🇿 pale.
Nchi zote duniani kuna mazuzumagic, Marekani kuna ombaomba,UK 🇬🇧 pia. Nimekaa The Hague miaka miwili, ombaomba walikuwepo.
Watanzania watoke nje ya nchi wakatafute riziki CCM acheni utaahira wenu. Jifunzeni kutoka Kenya 🇰🇪
Soma umalize hiyo paragraph, nimekutega na wewe unaingia kwenye mtego wangu. Nimekuambia Kuna watu wengi wenye akili na wameamua hivyo, kwahiyo haupo peke yako, usidhani kwamba wewe ndiye mwenye akili.Kumbe unafahamu hilo. Inawezekana na wewe uko kwenye system. Kama kuna mahali mmekwama, mseme msaidiwe. Kuna Watanzania wengi wenye mawazo mbadala na wako tayari kuyatoa bure, bila kudai malipo yo yote.
Serikali inatoa wapi hela kama siyo kwa wananchi wake? Serikali kuwadumia raia wake si fadhila, ni wajibu. Pesa iliyopo Serikalini ni ya wananchi.Ukisoma kwa mkopo wa serikali ndio kusomeshwa na serikali, hivi serikali ikiacha kutoa mikopo Kuna mtu ataweza kwenda kupata mikopo Bank na kujisomesha?. Kwa hapa Tanzania 98% husomeshwa na serikali kwa kupitia mikopo.
Sahihi na hata Nigeria ni kwa sababu ya boko haramuKenya imekuwa ranked poorly kwa sababu inapakana na Somalia,
Somalia kila siku ni vita na mashambulizi ya al shabaab
Mkuu, huko nje hawaendi hao watu waliokosa ajira hapa Tanzania, kawaida huko nje huchukua "top cream" ya wasomi huku Africa, wanatuachia vilaza ndio tuwaajiri hapa nchini.Unafahamu kuwa Tanzania kuna maelfu ya watu ambao tokea wahitimu Vyuo zaidi ya miaka kumi iliyopita, hawajapata ajira mpaka sasa?
Unafurahia unapowaona wakitembea na bashasha za khaki huku viatu vimeisha soli kwa kusaka ajira?
Mambo muhimu kwa binadamu niTanzania inawafungia ndani watu wake mithili ya mbuzi wezi, lakini Kenya imewapa uhuru wa kwake kutoka kwa kuwa inawaamini watu wake. Kwa nini basi, pamoja na Tanzania kuwafungia ndani raia wake na Kenya kuwaruhusu wa kwake kutoka, passport ya Kenya inaizidi ya Tanzania?
Unafahamu Kenya inajulikana zaidi duniani kuzidi Tanzania?
Bora tu ukomunisti na ujamaa zilikufa. Ni laana. Ni masalia ya mitazamo yake ndiyo inayoitesa Tanzania.
Mimi nimeweka sababu zonazoonyesha athari mbaya ya Kenya kutokana na kuruhusu raia wake kwenda nje ya nchi kwa wingi, Sasa wewe onyesha faida ambazo Kenya inazipata Ili tulinganishe.Unasema Kenya imeathirika negatively kwa sababu ya raia wake wengi kwenda nje? Ni mtazamo wako lakini si sahihi. Ili kupata mzania sahihi, orodhesha hasara zote na faida zote, kama hutabaini kuwa faida ni nyingi kuzidi hasara.
Usipoona faida, basi uanze dozi ya kula biringanya, nanasi, ndizi mbivu na mbegu ya maboga kwa ajili ya kurejesha afya ya ubongo.
UongoKenya imeathirika pakubwa Sana kwa kuruhusu watu wake kutoka kwa wingi bila udhibiti;
1)Wasomi wengi na wataalamu wazuri wameikimbia Kenya wako nje ya nchi Yao, matokeo ni haya ya uchumi wao kuporomoka kwa Kasi kwasababu waliobaki Kenya ni wale wa daraja la chini, majumba yanaporomoka Kila siku na miradi Yao yote ipo "poorly done".