Wakili Mwakubusi: Vyama vya Upinzani kazi yao ni kufukuzia tu ubunge na ruzuku, haviwezi kulikomboa Taifa

Wakili Mwakubusi: Vyama vya Upinzani kazi yao ni kufukuzia tu ubunge na ruzuku, haviwezi kulikomboa Taifa

Naongezea.
Wakati suala la mkataba wa uwekezaji wa Bandari umezuka, na nipo tayari kusahihishwa, Mbowe et al walikaa kimya kwa mda mrefu kweli, nadhani, walitegemea vuguvugu lile liishe na mambo yaendelee kama kawa. Haikuwa hivyo!

Sasa baada ya kuona yale majaribio yao kujitambulisha tena kwa Wananchi(operation 255) yamekufa, manake yale maigizo-Kurukaruka na helikopta, mara kupigiwa saluti na Askari, mara mtoto wa miaka 9 kumlilia Mbowe, mara kutembelea kaburi la mwanasiasa mkongwe, mara yupo Ikulu kupiga picha n.k n.k kubuma Ikabidi waanze upya.

...na kuanza huko walibidi wateke headlines, ndio akatokea mbowe na kauli yake ile ya "Uzanzibari" after the fact

Kilichfanyika ni kufunika kabisa mijadala ambayo kwa wiki chache kulionekana uwepo wa Umoja, yaani ulikuwa hauwezi kuotofautisha uzalendo au itikadi za kichama, uwe CCM au chama kingine chochote au usiwe na chama, watu wengi walionekana wakitetea Rasilimali yao, Bandari.

...255, imebuma, Lissu kakimbilia kutomaswa(massage therapy) ubeligiji huku kukiwa na tetesi za mgawanyiko ndani ya CHADEMA, CHADEMA walikuwa wamekosa headlines chanya!

Opportunity ikatokea, wakabidi waingie kwenye reli pamoja na wanaharakati, lakini hawakuingia kuendeleza mjadala, hapana, waliingia kuufunika. Wakaanza kukimbizana na Kaburi la Hayat, mara Katiba, mara Uchaguzi na vimbwanga vingi tu kuwachanganya Wananchi kama walivyopaswa na masharti ya Maridhiano yao ya awali- Toka jela, Kula Ruzuku, Sifia SSH, kandamiza legacy and so forth badala ya kukalia papo tu, yaani, KUSITISHA mkataba, Urudishwe Bungeni uwe kalas.

Wameniudhi, wametuudhi, na ndio katika mlolongo huo wa kutuchanganya ndipo wananchi sasa wanaanza kuona Mbadala haueleweki, hususani ukija upande wa Upinzani, pamoja na kwamba nimeishikia bango CCM ijivue tu madaraka, Wanachama warudishe kadi, lakini sidhani kama CHADEMA wapo na Dhamira ya kutuvusha tulipo. Na kama ilivyosemwa huko juu, wapo kutaka kugawana madaraka 2025.

.... wapo lakini hawapo.
Nilishangaa sana kwanini ule moto wa bandari Chadema walikua nyuma nyuma sana?Watu wanapewa kesi ya UHAINI wao wapo wapo tu,mtu aseme Chadema ni chama cha SIASA?No,hili ni genge la wahuni.
 
Yupo sahihi 100%.Umesikia upinzani ukiongelea mgao wa umeme unaondelea?Umesikia upinzani ukipinga vikali mkataba wa bandari?Hii serikali ni ya ovyo kuwahi kutokea lakini upinzani upo kama haupo.
Wewe unataka waongee kwa namna gani ili uelewe?.Hakuna jambo ambalo halijaongelewa.labda kama masikio yenu yanachagua maneno yakusikia.au mnataka chadema wafanye siasa za namna nyingine ili mje tena na kauli kua wanaharibu amani.
 
Mbona mnasema Magufuli alikua anaua upinzani wakati tuliona akiwaalika akina Cheyo,Lipumba na wengine ikulu?Kwenye Positive mnaiweka Chadema kama ndio symbol ya upinzani ila kwenye negative mnaitoa mnataka wengine wawe included
Ungewauliza hao uliowaona wakisema sio mimi,

Je na wewe unakubali kwamba hakuna vyama vingine vya upinzani tofauti na Chadema au au unasema vyama vya upinzani vipo vingi ambavyo unaweza ukaviunga mkono kuitoa CCM?
 
Mbowe anatakiwa aitishe maandamano nchi nzima kupinga ujinga unaondelea. Kama Raia wanagoma kuandamana maana yake hawana imani naye. Kenya Raia wana imani na Odinga ndio maana kila anachowaambia wanafuata.Raia wakielewa kama mtetezi wao watasimama nawe ila wakijua we tapeli watakupuuza.
Raia wana imani na serikali ya Samia ndio maana hawawezi kupelekwa barabarani kama manyumbu, kama unataka kuthibitisha hilo kamuite Polepole au Musiba waje waitishe maandamano uone watapata watu wangapi
 
Swala la kuikomboa nchi ni jukumu la kila mwananchi.sio swala la kuviachia vyama vya siasa na wanasiasa peke yake.Kwa upande huo chadema wamejitahidi sana kwasababu agenda ya kwanza kubwa ni kuelimisha jamii na chadema wametoa sana hiyo elimu kuanzia elimu ya katiba bora na haki msingi zakiraia.Chadema wamechagua siasa za kistarabu ambazo mwakubusi anaona hazisaidii kwasababu yeye anataka siasa za kufoka foka na kugomba kwa maneno makali yamsisitizo akifikiri hiyo ndio siasa sahihi,bila kujua kwamba unaweza ukafoka na ukatoa hadi wito wa maandamano bado ikawa kazi bure kama wananchi watakua hawajaelimika vya kutosha.Akumbushwe kua hili jukumu linatakiwa kufanywa kwa akili nyingi kulingana na aina ya siasa zinazoendeshwa na chama kilichoko madarakani.Ukifanya kwa mihemko na hisia atajikuta kaaribu badala ya kujenga.Aliye karibu naye amwambie mapambazuko yako karibu na kamba ukatikia pabovu.
 
Ndio mtajua kuwa hamjui,CDM ni lini watajifunza?wamepelekwa resi na Wakili Mwambukisi bila hata ya kushtuka ,haya sasa kashawapondo vibaya
Hajaitaja chadema lakini.😅😅
 
Huu ndio ukweli anaepinga ni mchawi.
Wananchi wanataka mabadiliko ila vyama vyote vimejaa matapeli ikiwamo CHADEMA.
Wananchi tumetelekezwa!
Ogopa wanasiasa na siasa zao
Hao Wananchi hawawezi kuunda chama cha maana?
 
Sina Mama anayeitwa Samia. Tungekua na upinzani wa maana leo hii kingenuka kwanini tukae giza miezi 6?Ilitakiwa Chadema waseme NO,Ilitakiwa Chadema waandamane kushinikiza viongoz wajiuzulu kwa huu ujinga. Chadema iko kimya kana kwamba Hitimisho la Samia kuhusu umeme ndio final na ni sahihi. Again,Hatuna Upinzani bali genge la wahuni na matapeli wanaotumia siasa kula kodi zetu.
Wewe umezuiwa kuanzisha huo upinzani madhubuti? Umekaa unakula keki na kuvimbewa halafu unataka wenzako wakupiganie? Hapana aisee.
 
Nilishangaa sana kwanini ule moto wa bandari Chadema walikua nyuma nyuma sana?Watu wanapewa kesi ya UHAINI wao wapo wapo tu,mtu aseme Chadema ni chama cha SIASA?No,hili ni genge la wahuni.
Wewe kama mwananchi ulifanya nini?.Au umekalisha makalio kwako unatupa tu visingizio kwa wengine wakufanyie.
 
Naongezea.
Wakati suala la mkataba wa uwekezaji wa Bandari umezuka, na nipo tayari kusahihishwa, Mbowe et al walikaa kimya kwa mda mrefu kweli, nadhani, walitegemea vuguvugu lile liishe na mambo yaendelee kama kawa. Haikuwa hivyo!

Sasa baada ya kuona yale majaribio yao kujitambulisha tena kwa Wananchi(operation 255) yamekufa, manake yale maigizo-Kurukaruka na helikopta, mara kupigiwa saluti na Askari, mara mtoto wa miaka 9 kumlilia Mbowe, mara kutembelea kaburi la mwanasiasa mkongwe, mara yupo Ikulu kupiga picha n.k n.k kubuma Ikabidi waanze upya.

...na kuanza huko walibidi wateke headlines, ndio akatokea mbowe na kauli yake ile ya "Uzanzibari" after the fact

Kilichfanyika ni kufunika kabisa mijadala ambayo kwa wiki chache kulionekana uwepo wa Umoja, yaani ulikuwa hauwezi kuotofautisha uzalendo au itikadi za kichama, uwe CCM au chama kingine chochote au usiwe na chama, watu wengi walionekana wakitetea Rasilimali yao, Bandari.

...255, imebuma, Lissu kakimbilia kutomaswa(massage therapy) ubeligiji huku kukiwa na tetesi za mgawanyiko ndani ya CHADEMA, CHADEMA walikuwa wamekosa headlines chanya!

Opportunity ikatokea, wakabidi waingie kwenye reli pamoja na wanaharakati, lakini hawakuingia kuendeleza mjadala, hapana, waliingia kuufunika. Wakaanza kukimbizana na Kaburi la Hayat, mara Katiba, mara Uchaguzi na vimbwanga vingi tu kuwachanganya Wananchi kama walivyopaswa na masharti ya Maridhiano yao ya awali- Toka jela, Kula Ruzuku, Sifia SSH, kandamiza legacy and so forth badala ya kukalia papo tu, yaani, KUSITISHA mkataba, Urudishwe Bungeni uwe kalas.

Wameniudhi, wametuudhi, na ndio katika mlolongo huo wa kutuchanganya ndipo wananchi sasa wanaanza kuona Mbadala haueleweki, hususani ukija upande wa Upinzani, pamoja na kwamba nimeishikia bango CCM ijivue tu madaraka, Wanachama warudishe kadi, lakini sidhani kama CHADEMA wapo na Dhamira ya kutuvusha tulipo. Na kama ilivyosemwa huko juu, wapo kutaka kugawana madaraka 2025.

.... wapo lakini hawapo.
Unaangalia mambo kwa namna mbaya unayoitaka wewe.kama ukuona agenda za maana zilizozungumzwa kwenye ile mikutano wewe ndiye utakayekua na shida sio chadema.ndo maana Umeangaika na porojo za watu badala ya agenda ndo maana ukaondoka na porojo ukaacha mambo ya msingi.
 
Kwenye statement yake amedai vyama vya siasa na si vyama vya upinzani.
Umeweka kichwa cha habari ku fit narrative yako

On the otherside ni kweli vyama vya siasa including chama tawala na upinzani.
Kuikomboa nchi si anaamanisha kuitoa CCM madarakani!! ? Sasa hapo CCM haiwezi kuingia tena sababu CCM tunaamini nchi hii iliisha kombolewa na ni nchi huru, anaananisha vyama vya upinzani
 
"Vyama vyetu vya siasa nadhani aidha vimechoka sana vyote vinahitaji kupumzika au viongozi wake wamechoka sana wanahitaji kupumzika, na ndio maana wanapoteza ile hamu ya kulikomboa na kulisimamia taifa, wanakuwa watu wa kufukuzana na tuvyeo, ubunge, ruzuku, kugawana, kukaa kaa mezani.

Kila mmoja yuko bize, wanachotaka ni kugawana tu sio kupambana kwa ajili ya wananchi. Lakini kikubwa ninachojaribu kusema kwamba inawezekana katiba kupatikana bila wanasiasa.” – Wakili Boniphace Mwabukusi

Chanzo: Swahili Times
Aliyeongea haya hajui chochote. Anasahau kuwa katika taasisi huwa kuna malengo makuu mawili ambayo lazima yaende sambamba. Moja, lengo la kuendeleza taasisi husika na pili, lengo la kutimiza mahitaji ya wafanyakazi wa taasisi husika. Anataka hao wanasiasa waendelee kusukuma taasisi mbele huku wao wakiishije(chakula, mavazi, malazi, matibabu na mahitaji mengine ya familia)? Mimi nadhani kwa kupata nyenzo ya ubunge ndiko kunawawezesha kutimiza malengo yote mawili vizuri.
 
Mbowe angekua mpinzani wa kweli asingekaa ndani miezi 8 na raia wakawa kimya tu.Kitendo cha raia kupuuza Mbowe kukaa ndani maana yake hawana imani naye. Hapo Kenya unafikiri Odinga anaweza kaa ndani hata siku 1 na Raia wakawa kimya?Ukweli ni kwamba Mbowe na genge lake hawana ushawishi tena wa kuleta mabadiliko Tanzania. Nenda Kenya kajifunze upinzani unavyofanya kazi.Watu wanapigwa na polisi, Rais anatia mikwara mara IGP lakini watu wanaandamana. Swala ni upinzani kuwa na ushawishi. Huwez kuwa na ushawishi kama unapuuza mambo ya msingi ya raia. Tunalala giza, upinzani upo kimya tu then kesho utegemee Raia wakuunge kutafuta tume huru ya uchaguzi we uingie madaraka hahahahhah
Watanzania sio manyumbu wa kurndeshwa kwa mihemko ya siasa za kikabila kama Kenya , Watanzania wana imani na serikali ya CCM ndio maana hata aje mtu gani hawezi kuwashawishi watanzania waandamane wavuruge amani, hata akifufuka mwendazake awaambie waandamane hatapata watu labda huko kwao Chato
 
Back
Top Bottom