Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Anahaki lakini nimemwambia aanzishe mada inayohusu ya wanaume wahuni ataona tukija kuchambua bila hofu. Mada hii ni wanawake.
Sasa mbona unaita maswali ya kijinga Kama unajua ana Haki!?
Umeona jinsi haya mambo yanavyoenda sambamba!?
 
Sasa mbona unaita maswali ya kijinga Kama unajua ana Haki!?
Umeona jinsi haya mambo yanavyoenda sambamba!?

Hata mjinga anahaki. Lakini haondoi haki ya kuambiwa yeye ni mjinga na aache huo ujinga.
 
Kwahiyo mwanamke aliyezaa bila ndoa kwa kubakwa au akaja kufiwa na mumewe utamjuaje?? Kwani si anaamua kukudanganya tu kuwa alibakwa au mume wake alifariki?? Mnavyojisifia kuwa wanaume hamtumii hisia mnatumia akili sasa hizo akili sijui mnatumia wapi kama mnashindwa kuzitumia hata kwenye vitu vidogo kama hivi!! Nonsense tumieni tu hisia maana hata akili zimeshawashinda!!
 
Ngoja siku nitulie niandike mwenyewe huo uzi halafu nione michango ya wanaume itakuwaje and I will prove to you wanaume wengi mnachofikiria vichwani mwenu
Jombaa mbona unalazimisha watu wale maparage wakati umewakuta wanakula pilau?

Nenda kafungue uzi wenye hiyo title unayoitaka kisha tutakuja kuchangia.
 
Marianah uko poa? Naona tumeamkia kujibu hoja za mijadala inayowanyanayasa karibu tuendeleze mpambano.....
Niko poa mkuu shukrani nikukaribishe wewe tuendeleze mpambano maana mimi nimeanza muda mrefu ila nikutahadharishe tu jiandae kuitwa FEMINIST
 


Mkuu leo umekamatika hapa. Sijui utatukia tawi gani. Maana ni kama mgonjwa wa dege dege.

Sasa kwa akili yako Kesi za ubakaji hapa nchini ni ngapi. Haya tufanywe umeniambia umebakwa. Hivi kwa akili yako mtu aliyebakwa si kunakuwa na kesi iwe ni mahakamani au polisi?

Tufanywe ulibakwa na mtu wa karibu unayekaa naye akakutishia usiseme. Hivi unadhani utaongea mambo hayo kirahisi rahisi ikiwa ni uongo na sisi wanaume tusijue.
 
Ahaa haaaa haaaa ... Joka acha uoga!


Hakuna uoga hapo. Huo ndio ukweli watu eanaoogopa kuusema.

Huoni wanaume wengine wanavyojificha huku.

Mtu akiwa malaya aitwe malaya. Mtu akiwa shoga aitwe shoga. Hakuna kuremba.

Hata ni mke wangu akinikuta nafanya upuuzi sitamlaumu wala kumzuia asinitaje kwa majina yanayofanana na tabia yangu mbaya.
 
Heaven Sent comment yake iko so impartial na objective.

Yaani imelenga kila mahali bila kufunika funika madosari ya jinsia yoyote, tofauti na nyie wengine ambao tangu mnaanza kuchangia mada hii mna one-dimensional perspective.
Basi ni aidha hautuelewi au hautaki kutuelewa hakuna aliyetetea wanawake kuzaa bila ndoa ila tunachosema ni kwamba kwanini tendo linalohusisha jinsia mbili lawama ziende kwa jinsia moja eti kwa sababu tu jinsia moja ndiyo inaumia zaidi nyingine haiumii?? Tukiwaambia hivyo mnasema mwanamke hatakiwi kujilinganisha na mwanaume wakati hapa sisi tunajaribu kukemea maovu kwa jinsia zote kwa sababu tukishikia bango jinsia moja jinsia nyingine itajiona haina hatia na haihusiki kabisa kitu ambacho siyo kweli!!
 
Wanajamvi watanisaidia labda kama nina shida kwenye uelewa wangu au la...... tunachojadili ni hii mada. lakini upande wangu siafikiani asilimia zote na mtoa mada mosi, kuwa single mothers wote wana matatizo waingiapo kwenye ndoa zao na akichagiza wanaume wasithubutu kuwaoa. tena anaenda mbali zaidi akisema wanawake wanaostahili kuolewa ni wale bikra tu. Pili natoa mtizamo wangu mpana kuwa si single mothers tu waingiapo kwenye ndoa ndo huwa na matatizo ya kurudia mahusiano na wazazi wenzao bali pia hata wanaume waliobahatika kupata watoto na baadae kuoa wanawake wengine huwa na matatizo kama hayo pia japo nao si wote.

Lakini kwenye mijadala hutokea watu wakaunga mkono moja kwa moja mada iliyopo mezani.....kitaaluma hawazuiliwi. lakini pia wapo ambao huikataa mada moja kwa moja kwa hoja zao walizotoa nao hukubaliwa. na mwisho huwa kuna upande wenye kufanya ulinganisho wa mada husika na nyinginezo/upande wa pili na hatimae hutoa pendekezo au ushauri juu ya mapungufu yaliyomo kwenye hiyo mada hili nalo linakubalika.

Sasa wewe mkuu unaweza kunifunza ni namna gani ya kujadili mada mbalimbali tukianzia na hizi za jukwaa hili. Sijawahi kuacha kujifunza mkuu.
 
Malizia na uasherati na kwa jibu hilo basi hata wewe ni malaya


Kama nafanya hayo ni kweli nitakuwa malaya.

Sasa nashangaa wewe unafanya uzinzi alafu ukiitwa Malaya unapasuka kama Pareto.

Ukitaka usiitwe mlevi acha pombe.
Ukitaka usiitwe mwizi acha wizi.
Ukitaka usiitwe malaya acha uzinzi.

Sasa mtu ametoa bikra kwa umalaya wake alafu akiambiwa ukweli anaviimba. Huo ni upuuzi.

Hayo ndio maisha Marianah. Ukitaka upewe heshima linda vya heshima. Ukitaka upewe majina ya matusi basi haribu vitu vya heshima.
 
Una uhakika anafanya umalaya!?
Kumbe unajua wazi hiyo sifa ya umalaya si yako bali amekubambikia tu...
Sasa mbona wewe unalazimisha akubali kuwa Ni Malaya wakati sio?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…