Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

Jamani kwani hapa anayeongelea haki sawa ni nani?? Kwahiyo kwa sababu wanaume hampati madhara kama wanawake basi ndiyo tusiwaambie ukweli?? Lazima tuseme ukweli kwamba wanaume nanyi mnachangia katika uwepo wa single mothers

Na ni lazima ukweli usemwe kwa jinsia zote mbili na siyo kuangalia eti jinsia moja ndiyo inapata madhara kuliko nyingine yaani ni sawa na mtu badala ya kukemea wezi eti anawaambia wanaoibiwa ndiyo wawe makini utafikiri wezi hawana makosa kabisa ila wanaoibiwa tu ndiyo wana makosa!!

Tendo la ndoa limekatazwa kwa wote. Wote jehanam inawahusu, lakini wakijirudi mwanamke anabaki na madhara permanent.

Kwa mfano wako wa wezi, unapoonywa kwamba funga milango na madirisha unaposafiri, ama unapolala usiku, au usiwazoeshe wahuni kuingia ndani mwako wasije wakachora ramani ya kukuibia utanung'unika?? Utalalamika kwamba kwa nini msiwakemee wezi sisi tuishi kwa uhuru, tukiacha milango wazi, tukitembea na mamilioni mtaani? Ukifanya hayo ukaibiwa watu watakucheka wewe, sio wezi. Wataona kuwa uliyataka mwenyewe.
 
Hakuna anayetaka wanawake waendelee kuzaa hovyo nje ya ndoa ila unapoongelea tatizo lazima uongelee na mzizi wa chanzo na siyo shina tu wewe unaongelea shina la tatizo na unauacha mzizi wa tatizo hapo unategemea nani atakuelewa zaidi ya kukuoma mnafiki tu??

Hebu siku jaribu kuanzisha mada inayohusu maovu ya wote wanaume na wanawake huyo atakayekushambulia atakuwa na matatizo lazima tuongee ukweli haijalishi jinsia gani ndiyo inapata madhara sana sana kuliko nyingine kumbuka wanawake nao ni binadamu kama wanaume na siyo malaika
Mimi nasema wanaoumia ni wanawake sababu ya kiburi na ujuaji. Ukiona mwanamume anakuunga mkono kwenye mambo ya hovyo jiulize mara mbili.

Ndoa ni ya mwanamume, ukiuelewa huu msemo utaelewa uishije. Kuzaa hovyo nje ya ndoa halafu mnakimbiwa na waume, au wanazikataa mimba kwa vile baba haeleweki ni yupi vinamuumiza mwanamke. Wanawake mko kwenye disadvantage, playground haiko level.
 
Hiyo tofauti imeelezewa wapi kwenye maandiko??

Biblia yote haijamlinganisha mwanamke na mwanamume, siui unauloza nini hasa

Sawa umesema kuna watu wasio na dini wala wasioamini Mungu sasa hao utawaambia nini kuhusu maswala ya bikira maana kama mtu haamini dini wala Mungu basi pia haamini kama kuna dhambi yeye chochote anachofanya kwake anaona ni sawa tu je mtu huyo utamlaumu??

Nani kakudanganya? Sijui umri wako, ila fanya research, tamaduni zetu zilitaka binti aolewe bikra. Hao unaowaongelea labda ni hawa wazungu weusi, wanaojifanya kuiga ya ulaya.

Halafu kwani hapa dunia wanadamu tunaishi kwa kutenda mema kwa lengo gani si kwenda mbinguni tu au??

Tunatenda mema kwa sababu imetupasa kutenda hivyo. Tunatenda mema kwa sababu tunampenda na kumheshimu Mungu.

Sasa mwanamke akizini akatubu akasamehewa akaanza kutenda mema na kuacha kabisa uzinzi na uasherati utasema kwamba eti hataenda mbinguni kwa sababu tu yeye kapoteza bikira na hairudi ila mwanaume hajapoteza kitu??

Sijasema kuwa haendi mbinguni, au huelewi maana ya kutubu na kusamehewa?


[BHapa swala siyo kujilinganisha hapa tunaangalia kitu kinaitwa DHAMBI kama hakuna jinsia yoyote iliyoruhusiwa kutenda dhambi basi kila jinsia inatakiwa kukemewa kuacha dhambi haijalishi jinsia gani ndiyo inapata madhara zaidi halafu hayo madhara unayosema ni mitazamo ya kijamii tu tena hasa jamii za kiafrika ambazo hazijastaarabika lakini kwa Mungu mwanaume au mwanamke aliye malaya hauwezi kumfananisha na mwanaume au mwanamke asiye malaya hata kama kimaumbile watatofautiana kwani kuna sehemu maandiko yamesema kuwa anayepata madhara zaidi ndiyo aonywe zaidi??

1. Hapa siongelei "dhambi" bali jamii na maadili. Ukitaka niongelee dhambi, basi nimeshasema hilo linasameheka
lakini damage done.

2. Jamii za koafrika ambazo hazijastaarabika!! Nikushauri tu ujijengee utamaduni wa kufuatilia kinachoendelwa huko duniani. Kama unataka nikuwekee mabandiko ya maoni ya hao waliostaarabika kama hutotoa machozi. Kinachoendelea Afrika ni ulimbukeni na kudandia mila zisizotuhusu, tukijidanganya ndio ustaarabu. Bikira sio mitazamo ya kijamii, niuhalisia across the board!!

3. Maandiko yanasema anayepata madhara asiolewe
 
Kwahiyo wanaume wasilelewe katika maadili mema siyo?? Kwamba wanaume imeshindikana kabisa kuwaasa waache maovu ndiyo maana mnawakwepa au??
Soma comment niliyokuwa najibu. Majibu hutoka kutokana na maelezo yaliyotolewa.
 
Sawa mimi naisubiri kwa hamu sana hiyo jamii ambayo wanawake watakaokuwa wanaolewa ni wale ambao hawajawahi kuzaa au wale mabikira tu (huku wanaume wakiendelea kufanya uhuni wao lakini) ila wale single mothers na non virgins watabaki kuwa manungayembe oh I just can't wait
Yaani umehama kwenye hoja kwa personal grievances. Hiyo jamii haipo,,ila maonyo yataendelea kuwepo na kweli itasemwa hata kama hampendi kuisikia. Kama unaonakuzaa hovyo ni sifa, its up to you lady.
 
Kumbe atheists kwenye haya maswala mnakuwaga na hoja kiasi hiki?? Ningesema Mungu akubariki ila kwa vile hauamini kuwa Mungu yupo basi niseme tu hongera kwa kujielewa na kusimamia ukweli kwenye haya maswala kuliko hata baadhi ya wanaume ambao wanaamini Mungu yupo maana ni wanafiki sana
Kuna kitu kinakula, dhamira yako inakushitaki, simple psychology.
 
Oohh I see kumbe na wewe ni mmoja wa wale wanaohangaika kusoma saikolojia za watu kupitia yale wanayoyaandika humu (hata kama kiuhalisia hawako hivyo)?? Okay umepata faida gani hadi sasa??
Faida ni kuelewa najadili na mtu wa aina gani, did I answer your question?
 
Oops kama ni hivyo basi mada yako tayari imekwishapoteza uhalisia na wanaume mnapokosea ni pale mnapodhani kuwa Mungu ni wa wanaume tu wakati Mungu ni wa wote wanaume na wanawake kama anaweza akampa mwanaume mzinzi mwanamke mtulivu anashindwa nini kumpa mwanamke mzinzi mwanaume mtulivu?? Au haujawahi kuona ndoa za aina hiyo ya pili kati ya nilizozitaja??
Biblia inasemaje kwani: mume mwema anatoka kwa Bwana au mke mwema anatoka kwa Bwana?
 
Sasa yule mwanaume ambaye ameoa single mother na ndoa yake imedumu na anaona ndoa za wanaume wenzie waliooa mabikira hazijadumu unadhani atakuelewa hapa??

Kwahiyo unataka wanaume wenzio waliojifunza kutokana na experiences zao waache kuamini wanachoamini na waamini unayoyasema na wajifunze kutokana na stories zako siyo??
Ni sawa na jambazi ambaye hajashikwa na amefaulu kuwekeza kwenye biashara kubwa, hizo zinaitwa rare cases. Sihitaji kuzijadili kwani hoja ni too low.
 
Wanaume wanaumia sana,tena sana Kuliko wanawake...Believe me...
ujuaji na kujihesabia haki kunawaponza sana

Mfano tu:Ushawahi ona nyuzi humu wanawake wakilalama kwa kuhusu single fathers ama kwa nini wanaume hawaoi?..

Ila nini kinawauma kwa jinsia ya pili?,,siku zote wanaume ndo wanapata tabu na wanawake

Mentality walizojiwekea kichwani hazi'work hivyo wana uchungu sana
Wishful thinking. Jaribu kutangaza wanawake wanaoumia kwa kutelekezaa uone kama utapata mahali pa kuwaweka. Imetokea hii!!
 
Kwahiyo mwanaume aliyemzalisha huyo mwanamke yeye ndiyo anapaswa kuoa mwanamke mwingine asiye na watoto si ndiyo??
Akitaka, kuzaa nje ya ndoa maana yake mwanamume hana malengo na mwanamke huyo, ama hajafikia maamuzi ya kumheshimisha kwa kumuoa.
 
Back
Top Bottom