Wakuu mwenye uelewa na hii fursa nasikia mwisho Feb 28 mwezi huu watu wanakuwa matrilionea

Uwekezaji wwt unahitaji umakini boss. Huyo jamaa yetu aliepoteza Kuna wezake pia wamenufaika mpaka leo
Ok, fanya hesabu hii, Tafuta idadi ya watu wote wanaocheza bitcoin, then tafuta walionufaika, then nipe percent yake af ilete hapa, unishawishi nifanye.
 
Kuna jamaa nilikuta kwenye biashara yake kaweka bango "tunapokea malipo kwa Bitcoin", halafu muda mwingi kuna watu wamekusanyika anawasaidia kununua na kuuza, nikawaza huyu mtu atalia sio muda.

Nilipopita baada yaa miezi miwili bango halipo na ukimuuliza kuhusu bitcoin, asipokutwanga ngumi basi tegemea tusi zito
 
Ok, fanya hesabu hii, Tafuta idadi ya watu wote wanaocheza bitcoin, then tafuta walionufaika, then nipe percent yake af ilete hapa, unishawishi nifanye.
Mkuu Mr IQ sipo hapa kwa ajili ya kumshawishi mtu ila tunapeana elim tu. Siwezi kukushawishi kitu ambacho hata Mimi sijawahi kukifanya.. ila ukweli ni kwamba hiyo kitu ipo na watu wananufaika nacho. Tambua mafanikio ya mtu ni bahati na wala si juhudi tu zako binafsi
 
Mkuu
Sijaelewa vizuri ila kuna mtu nilitaka nimkaribishe P, yeye akawa amefungua account ambayo sio ya kukaribishwa hivyo akawa hawezi kuchimba wakampa option ya kununua p
,pi unaweza kumine bila kukaribishwa.
Na hamna kenye app sehem ya kununua
 
Huwezi nunua salafu kama bitcon inadhaman kubwa namna hiyo. Crypto zinatabia za kupanda ghafla then kushuka ghafla halafu zikang'ang'ania late hiyo hiyo kwa muda kadhaa. Mfano btcn miezi mitatu nyuma ilikuwa Ina soma laki na elfu 2 na kwa sasa inasoma 90 elfu, ss kama ulinunua miezi iliyopita wkt imechanfanya tukiamini itapaa zaidi lazima uliwe kichwa mapema. Wanaonufaika ni wale walioanza nayo mapema wkt bado thamani yake ni ndogo
 
Kwann huamini kuwa ipo sarafu ambayo inaweza kuichalenji btcn kwa ss
Kwa sababuna uwepo wa mamia ya sarafu hakuna hata moja yenye thamani ya robo yake na pia bitcoin ni kama iko kwenye league ya peke yake.
We fikiria bitcoin leo ilikuwa karibu $96000 halafu inayoifuata kwa thamani ni ethereum ambayo ni kama $2700. Yani hata robo yake haifiki
 
Halafu hiyo ETH mwaka 2020 ilikuwa inasoma $4000 nashangaa imepolomoka namna hiyo
 
Halafu hiyo ETH mwaka 2020 ilikuwa inasoma $4000 nashangaa imepolomoka namna hiyo
Hata bitcoin ilishawahi poromoka kutoka $20000+ nadhani ikafika $14000 ni kawaida kupanda na kushuka.
 
Hata nikichimbua boss Sina Cha kuambulia Tena muda umeshanitupa
muda bado upo nao mkuu. cha msingi ni wewe kujua kwamba ad sasa hayupo aliye wahi benefit ktk hyo Pi net.
wanachofanya ni mining tu kuongeza account but kwa badae ndo hizo Pi zitakuja mfaa mtu, pengine ni baada ya kuanza kuwa traded. so hujachelewa na hakuna malipo wala investment yenye utafanya interms of money. so it's almost risk free....unaogopa nini?
 
Jf ni miyeyusho sana ukileta mada tofauti na mbususu lzm ukutane na upinzani mkubwa sn
Wana JF ukiwaletea fursa basi wanataka uwaambie ni wapi umepata soko zuri la kuuza viazi au vitunguu ni mbegu gani nzuri za matiki tiki maji ndio watakuamini na kukutilia maanani..

lakini ukiwaletea habari za BTC,$Trump, $link aisee hapo utakutana na maneno yote ya kejeli na kupuuzwa na hii ni kwa sababu wengi bado wako kwenye industrial age wanatengeneza pesa in traditional way japo dunia ya sasa iko kwenye information age, hauitaji kutumia miaka 20 hili uweze kuwa millionaire bali ni taarifa sahihi tu na kuwa mbele ya muda.

Kuna mwanangu mmoja sasa hivi yuko zake nje ya nchi huko kwa werevu, kwa mara ya kwanza yeye ndio alinipa taarifa za kuhusu Bitcoin ilikuwa 2015 nafikiri bei yake ilikuwa around $400 akanisisitiza sana na mimi nitafute hela lile ninunue hata moja kisha ni hold itanisaidia baadae yeye hapo ananiambia hivyo alikuwa ameshanunua kama 6 hivi...!!

Kama tu walivyo wabongo wengine na mimi nikapuuzia na kuona hizi mambo za kuweka hela mtandooni ni kutapeliwa tu na hakuna hela rahisi hivyo...

Basi miaka imeenda na mimi kuanza kupanua uelewa wangu kuhusu biashara za mitandaoni hasa kwenye crypto nikaja kumtafuta around 2021 hapo BTC price yake inasoma kama $60,000 hili anipe maujanja kama kuna namna yoyote ya kunisaidia hasa ukizingatia kipindi hicho zikaanza kuanzishwa cryptos nyingine nyingi.. jamaa wala hata hakutaka kuangaika na mimi.

saa basi hivi ndio wabongo wengi tunavyoachwaga na fursa kutokana na uoga na ufinyu wa kukosa maarifa.
 
Hata bitcoin ilishawahi poromoka kutoka $20000+ nadhani ikafika $14000 ni kawaida kupanda na kushuka.
Na hicho ndio kinachonifanya mpaka Leo nimekuwa mpenzi mtazamaji. Mwaka 2021 niliwahi kuchoma laki 9 kwenye meme ya Shiba Inu nikinunua coins nyingi sana nakumbuka late yake ilikuwa $0.0004. na ilikuwa inachukuliwa kama meme ambayo itakuja kuishangaza Dunia. Nikajiripua long hold... Chungulia ss hivi mambo ilivyo Ngoma inasoma 0.000015
 
Please alikuwa Ana trade au?

Kama Ali hold basi amekudanganya maana watu walio hold tangu mwaka huo sasa hivi hawashikiki kabisa na mifano ninayo... ila kama alikuwa anatrade basi huyo lazima ile kwake.
 
bado umeziihold? Inabidi kuwa makini kwenye crypto kuna watu wanazipandisha kisha wanazidump wanachukua mamilioni yao. Navyomwona elon musk nadhani ni michezo yake.
 
Na je hiyo KYC verification kwanini wanachelewesha namna hiyo
 
Please alikuwa Ana trade au?

Kama Ali hold basi amekudanganya maana watu walio hold tangu mwaka huo sasa hivi hawashikiki kabisa na mifano ninayo... ila kama alikuwa anatrade basi huyo lazima ile kwake.
Ni kweli Maana kutrade Haina tofauti na kamari ya kubet
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…