Wakuu mwenye uelewa na hii fursa nasikia mwisho Feb 28 mwezi huu watu wanakuwa matrilionea

kama huko kuchimba hakuna gharama zozote sio mbaya ukijaribu
Tulioanza kuchimba nyuma kidogo ni bure ila watu wapya wanaweza kupata sarafu ya Pai kwa kuinunua si chini ya elfu 30 kila moja.
Maana yake watu wapya wanatakiwa wacheze kamari kwa kununua Pai ili zikija kupanda wapate faida au zikija kushuka ndio basi tena
 
Halafu kamilisha usajiri wako zinatakiwa tick 5 hapo zikamilike tofauti na hapo unamaliza bando lako bure, wanadai mwisho kukamilisha KYC ni trh 28 mwezi huu. Ukichelewa hutaweza kunitumia hizo coins
Kyc naikamilishaje sasa maana nasikia hadi kitambulisho kinahitajika
 
Hata Mimi nasubiri hiyo trh 28 nasikia ndio watairuhusu kwenye list ya crypto currency. Hivyo wenye wallet za Pai wanaweza kuuza, kununua, na kutoa pesa zao kutoka kwenye wallet zao. Kwa ss PAI Moja inathamani ya usd laki 3+ kwa mujibu wa Pai network wenyewe ila ukiwauliza AI wao wanadai bado thamani yake sokoni haijapangwa kwahiyo hata Mimi inanichanganya ndiomaana nikaleta bandiko kama Kuna mtu yupo huko atumegee
 
Sikia P I ni pyramid scheme ,mfano mimi siwezi kufanya mining mpaka nijiunge kwako na nikifanya mining wewe unaona .sasa basi P I bado haipo kwenye blockchain wala binance ,SINA YA CRYPTOCURRENCY yoyote unaipata kwa kuinunua au kufanya mining kwa kutumia supercomputer na sio mobile mining ,huu ni utapeli wa wazi .Pia hawa jamaa walishasema mara itaachawi mwezi wa 12 mwaka 2024 ,ila ukapita pia walisema mwisho mwezi 6 mwaka 2024 nao ukapita .mwisho P I ni UTAPELI
 
Kyc naikamilishaje sasa maana nasikia hadi kitambulisho kinahitajika
Hata kadi ya mpga kura kama unayo unaipga picha mbele na nyuma unupload taarifa zako sahihi yani zisiende kinyume na account yako ya Pai hapo tayari utakuwa unaelekea ubilionea. Fanya chap mkuu
 
Sawa ila sio kwa PI ,
 
Hata kadi ya mpga kura kama unayo unaipga picha mbele na nyuma unupload taarifa zako sahihi yani zisiende kinyume na account yako ya Pai hapo tayari utakuwa unaelekea ubilionea. Fanya chap mkuu
Nina namba ya nida tu labda nifuatilie kitambulisho chake... Nilikuwa na leseni ya udereva ikapotea nikapuuza sikuenda kuripoti
 
Acheni kujidanganya hiyo tarehe 28 itapita na hakuna kitakachotokea
 
Muda umeisha ss boss hutaweza ss kukimbizana hiyo trh 28 ikukute umemaliza?
Nina namba ya nida tu labda nifuatilie kitambulisho chake... Nilikuwa na leseni ya udereva ikapotea nikapuuza sikuenda kuripoti
 
Nimekuwa nikishuhudia jinsi vijana wengi wanavyojinasibu kuwa wanafanya biashara(crypto) , lakini maisha yao yanaendelea kuwa magumu kama yangu tu!

Unapotembelea mitandao yao ya kijamii, hasa kwenye status za WhatsApp, unakutana na jumbe kama vile "Financial freedom" na kadhalika. Lakini ukweli ni kwamba, haya maneno hayana mashiko kama huwezi kuonyeshs ushahidi wa mafanikio yao.

Mimi binafsi, nitakuja kuamini biashara zao pale nitakapoona mabadiliko chanya katika maisha yao. Pale nitakapoona ushahidi wa wazi wa mapato yao, na kuona hatua kubwa walizopiga kimaisha.

Jambo lingine linalonishangaza ni jinsi wa Afrika, hasa wabongo, walivyo wachoyo na wenye roho mbaya. Wanaweza kweli kukupatia mbinu/maarifa jinsi wanavyo tengeneza hiyo mipesa?

Vijana tafuteni mapori mkafyeke na mfanye kilimo, hakuna hela ya kupakua kama unapakua SINGELI
 
Kampuni haina ofisi wala Tin number ushaibiwa hapo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…