Wakuu wa Mikoa wote wangefanya kama anachofanya Makonda tungekuwa mbali

Wakuu wa Mikoa wote wangefanya kama anachofanya Makonda tungekuwa mbali

Tunapotaka mifumo ibadalike ni Ili wananchi waweze kuwajibisha viongozi wazembe, wezi na Wala rushwa. Haya mambo ya kutegemea viongozi wanaosaka kiki, hayawezi kutatua utendaji mbovu wa viongozi.
Mwenzako anatatua kero wewe umekalia uchawi tu
 
Kuna mama mmoja alilia sana akamuombea maombi ya baraka yaaan unaona kabisa mama kashusha mzigo baada ya kuongea.

Sio siri makonda hata km unajifanya kumlaaani huku ika kuna wafu wanamuombea sana. Sasa njoo Dar unakutana na mkuu wa mkoa anakuambia ww km una miaka 40 huna hela usiilaumu serikali wakati mkoa huu unachangamoto za barabara tangu mvua ziishe zimeacha mahandaki ila kiongozi kakalia mipasho facken kabisa
Watu wengi humu ni graduate hawajakutana na kashi kashi za watu wa serikalini,makonda anafanya kitu kizuri mno.Mafisadi na wafanyakazi wazembe wana nguvu na dhulma sana,mahakama hakuna haki kwa maskini.
 
Tunapotaka mifumo ibadalike ni Ili wananchi waweze kuwajibisha viongozi wazembe, wezi na Wala rushwa. Haya mambo ya kutegemea viongozi wanaosaka kiki, hayawezi kutatua utendaji mbovu wa viongozi.
Hivi hii mifumo uitakayo ni nini?
Mifumo bila watu sahihi wa kuiendesha au watu sahihi wanao unda mifumo kutakuwa na matokeo chanya?
Hakuna mifumo bila watu sahihi.
Watu sahihi hawawezi kuwa watu wasiopenda uwajibikaji au wasiopenda mabadiliko ya kiutendaji na ya kitabia.
Kile anafanya Makonda au alifanya Magufuli ni kuwaandaa watu na mabadiliko ya kuendana na hiyo mifumo. Ni maandalizi ya hatua moja kuelekea kuunda mifumo unayo pendekeza.
Hakukosekani makosa wakati wa kuunda mifumo, ndiyo maana kuna reviews, hizi hatua zipo katika 'system development cycles'.
 
Tumsifu Yesu Kristo.

Wakuu leo nipo kuwakumbusha ya kuwa utendaji anaofanya makonda kwenye ziara zake ndio unaotakiwa kwenye nchi kama hii, kuna watu watabishia hili kwasababu hawajawah kukutana na kadhia ya watendaji wa serikali kwenye maofisi.

Wengine hawajawah kufanya kazi za tender zinazotolewa na hizi manispaa au halmashauri, kwahiyo kazi zao ni kupinga kinachofanya na bwana yule...isitoshe na wengine hawajawah kukutana na issue zinazoitwa Ardhi iwe kudhurumiwa na kunyanyaswa na matapeli.

Ukikumbana na hayo hapo juu, ndio utajua umuhimu wa huyu bwana anafanya nini....na ndio ilitakiwa wakuu wa mikoa wote wafanye hivyo
Je umewahi kujiuuliza kwanini kuna Mambo ya hovyo kama yalivyo kwasasa
 
Wakuu wa mikoa wote huwa na ziara kama za makonda,tofauti yao ni kwamba hawatembei na macamera
 
Kwenye suala la ardhi hana Cha kuongea kwa sababu ni tapeli mzuri tuu gsm alitaka kumtoa mavi juzi juzi tuu hapo, kua mtendaji mzuri sio kubeba ma camera kwenda location kutafuta sifa kama anavyo fanya yule maskini wa akili
Bila hayo ma camera tusingeujua utendaji wake, mbona Arusha walikuwepo wasiotembea na ma camera lakini walishindwa kutatua shida za wananchi kama walikuwa watendaji wazuri?
 
Hivi hii mifumo uitakayo ni nini?
Mifumo bila watu sahihi wa kuiendesha au watu sahihi wanao unda mifumo kutakuwa na matokeo chanya?
Hakuna mifumo bila watu sahihi.
Watu sahihi hawawezi kuwa watu wasiopenda uwajibikaji au wasiopenda mabadiliko ya kiutendaji na ya kitabia.
Kile anafanya Makonda au alifanya Magufuli ni kuwaandaa watu na mabadiliko ya kuendana na hiyo mifumo. Ni maandalizi ya hatua moja kuelekea kuunda mifumo unayo pendekeza.
Hakukosekani makosa wakati wa kuunda mifumo, ndiyo maana kuna reviews, hizi hatua zipo katika 'system development cycles'.
Tayari kulikuwa na rasimu ya Warioba iliyokuwa na muundo wa hiyo mifumo kupitia maoni yetu wananchi. Lakini Magufuli na Makonda hawakuamini kwenye rasimu ile, bali walitaka mifumo inayoweza kulinda maslahi yao ya kimadaraka, ndio maana wakawa kikwazo Cha kupatikana katiba mpya.
 
Nilishadhulumiwa almashauri ya Karagwe sina hamu na kitu kinaitwa Halmashauri kabisa, acha Makonda adili nao.
 
Tayari kulikuwa na rasimu ya Warioba iliyokuwa na muundo wa hiyo mifumo kupitia maoni yetu wananchi. Lakini Magufuli na Makonda hawakuamini kwenye rasimu ile, bali walitaka mifumo inayoweza kulinda maslahi yao ya kimadaraka, ndio maana wakawa kikwazo Cha kupatikana katiba mpya.
Kumbukumbu zangu rasimu ya katiba mpya ilifanyiwa vurugu vipengele vingi wakati wa Kikwete.
Of course Makonda alionekana kuhusika kwenye vurugu za kukataa rasimu hiyo na kumvamia Warioba kabla ya uraisi wa Magufuli.

But we can not dwell on past forever. People change Makonda including.
 
Tayari kulikuwa na rasimu ya Warioba iliyokuwa na muundo wa hiyo mifumo kupitia maoni yetu wananchi. Lakini Magufuli na Makonda hawakuamini kwenye rasimu ile, bali walitaka mifumo inayoweza kulinda maslahi yao ya kimadaraka, ndio maana wakawa kikwazo Cha kupatikana katiba mpya.
Katiba bila watu sahihi wenye mindset sahihi, maadili sahihi bado haitajenga mifumo sahihi yenye matokeo chanya.
Kwani wizi na ubadhirifu unaruhusiwa kwenye katiba iliyopo?

Hujamsikia muheshimiwamoja kaita/kasema 'katiba ni kijitabu tu' akimaanisha kuidogosha au kuonesha haina uzito mkubwa kwenye utendaji mzuri.

Sasa watu Kama hao unadhani wataiheshimu hii ya sasa na hiyo mpya ya rasimu ya Warioba?
 
Kumbukumbu zangu rasimu ya katiba mpya ilifanyiwa vurugu vipengele vingi wakati wa Kikwete.
Of course Makonda alionekana kuhusika kwenye vurugu za kukataa rasimu hiyo na kumvamia Warioba kabla ya uraisi wa Magufuli.
Pia alikuwa mjumbe kwenye bunge maalum la katiba. Je alipambania maoni ya Wananchi? Mfano tulitaka mbunge awajibishwe kwa kutotimiza wajibu wake, lakini msimamo wa chama chake ulilazimisha akae mpaka amalize kipindi cha miaka mitano. Isitoshe wananchi tulitaka ukomo wa mbunge uwe ni kipindi Cha miaka 10, chama chake Bado kililazimisha akae zaidi ya miaka 10 ili mradi achaguliwe na wananchi! Yeye alikuwa upande wa maoni ya wananchi? Hii huruma ya Sasa inatoka wapi kama sio hadaa?

Hakuna mfumo hata mmoja unaompa nafasi mwananchi kuwajibisha mamlaka, lengo ni ili waitwe wanyonge na kupatiwa haki zao kama hisani ya viongozi wanaosaka madaraka.
 
Tayari kulikuwa na rasimu ya Warioba iliyokuwa na muundo wa hiyo mifumo kupitia maoni yetu wananchi. Lakini Magufuli na Makonda hawakuamini kwenye rasimu ile, bali walitaka mifumo inayoweza kulinda maslahi yao ya kimadaraka, ndio maana wakawa kikwazo Cha kupatikana katiba mpya.
Warioba mwenyewe au Shivji alisema kwenye muhadhara wa katiba mpya tatizo kubwa ni maadili. Hata ukileta katiba mpya watu wasiokuwa na maadili mazuri wataivunja tu vipengele vyake.
 
Hii huruma ya Sasa inatoka wapi kama sio hadaa?
Pengine ametambua kosa lake anajisahihisha.
Nyerere alikiri kukosea akaja na kauli na kitabu TUJISAHIHISHE na ndiyo maana alipambania vyama vingi wakati alipopata fursa baada ya kuona udhaifu wa chama kimoja.
 
Warioba mwenyewe au Shivji alisema kwenye muhadhara wa katiba mpya tatizo kubwa ni maadili. Hata ukileta katiba mpya watu wasiokuwa na maadili mazuri wataivunja tu vipengele vyake.
Kama bado rais ataendelea kupata Kinga ya kutoshitakiwa akiwa au ametoka madarakani bado maadili yatakuwa chini. Tusipofikia mahali madaraka ya rais yakapunguzwa tusitegemee uwajibikaji wa mifumo ipasavyo. Kama Katiba haiwezi kuwajibisha Kila mtu, ni ngumu vipengele vya hiyo katiba kuheshimiwa.
 
Pia alikuwa mjumbe kwenye bunge maalum la katiba. Je alipambania maoni ya Wananchi? Mfano tulitaka mbunge awajibishwe kwa kutotimiza wajibu wake, lakini msimamo wa chama chake ulilazimisha akae mpaka amalize kipindi cha miaka mitano. Isitoshe wananchi tulitaka ukomo wa mbunge uwe ni kipindi Cha miaka 10, chama chake Bado kililazimisha akae zaidi ya miaka 10 ili mradi achaguliwe na wananchi! Yeye alikuwa upande wa maoni ya wananchi? Hii huruma ya Sasa inatoka wapi kama sio hadaa?

Hakuna mfumo hata mmoja unaompa nafasi mwananchi kuwajibisha mamlaka, lengo ni ili waitwe wanyonge na kupatiwa haki zao kama hisani ya viongozi wanaosaka madaraka.
Unaweza kuniambia kikomo Cha uwaziri mkuu wa Uingereza?
Kikomo Cha ukansela wa Ujerumani?
Lakini umeona kiwango chao chaaadili kinavyo wawezesha kutokuwa na waziri mkuu au kansela wa maisha?
Umeona Uingereza wanavyo jiuzuru mawaziri wakuu wanapo ona kuna umuhimu wa kuwajibika?
 
Pengine ametambua kosa lake anajisahihisha.
Nyerere alikiri kukosea akaja na kauli na kitabu TUJISAHIHISHE na ndiyo maana alipambania vyama vingi wakati alipopata fursa baada ya kuona udhaifu wa chama kimoja.
Sidhani kama atakuwa tayari na mabadiliko ya kweli maana hata yeye anajua anaweza kuwa muhanga wa mifumo ya haki ya kweli. Hata Nyerere alijisahihisha akiwa nje ya madaraka baada ya kujua Hana Cha kupoteza.
 
Back
Top Bottom