Wale Graduate mlioweza kujiajiri mlitumia mbinu (njia) kuweza kujiajiri?

Wale Graduate mlioweza kujiajiri mlitumia mbinu (njia) kuweza kujiajiri?

Tanzania kuna kasumba. Nilivyomaliza form 6 kwenye 1990s, nilitaka kufanya kazi ya kupiga debe Dar. Basi nikawaona watu wote waliokuwa kwenye business ya aina hiyo niliokuwa nawafahamu. Unajua nini? Wote walinikatisha tamaa na kusema siiwezi kwa vile eti ni msomi. Kila niliyemomba kazi ya aina hiyo, alisema siyo kzi yangu. Mwishoe sikupata japo nilikuwa tayari kuifanya.
Kwangu Mimi nakwepa aibu kwa namna hii.
Kwa mfano, mwanafunzi wa chuo ataona aibu kuwa day worker ya ukondakta. But najiuliza wale makonda wa daladala kwani hawana familia. Mbona unakuta Mtu sawa umri wa baba yangu na anafamilia na watoto anasomesha na Mbona haoni aibu. Sasa kwanini Mimi Kijana nione aibu Wakati Najua hii kazi Nitafanya kwa Muda mfupi na nitapata pesa na nitatimiza malengo yangu.
Mimi malengo yangu nayaweka mbele zaidi kuliko kituchochote.
Pia stori za watu maarufu Kama simbachawene Alikuwa mpiga debe kabla ya kuwa Waziri.
AY alikuwa analala kwenye kontena la washona nguo kabla hajawa super star
So Wanafunzi wa vyuoni na graduates wote wajue kwamba ili ufanikiwe lazima uanze chini.
Ni wachache Sana wanaofanikiwa kwa raha lakini wengi wameangaika.
Cha msingi malengo yako yawe mbele, na utatimiza unachotaka
 
Tatizo ni kwamba Most of graduates tunashindwa kuwa wabunifu,katika kipindi hiki ambacho hata wafanyabiashara hali sio nzuri sana, ni lazima nasisi graduates tutumie akili nyingi pia kwenye kutafuta kazI hasa kama hauna connection. Tunalalamika kwamba kazi zinatolewa kindugu au kirafiki lakini ukijiuliza tu mwenyewe Mfano wewe ndo boss na unatafuta mfanyakazi,anatokea graduate wa kwanza anatafuta kazi lakini humfahamu kabisa,upande wa pili anatokea rafiki yako unaemwamini anakwambia anamfahamu graduate ambae anachapa kazi,muaminifu na pia anawafahamu mpaka wazazi wake,kama wewe ndo boss utamchukua mfanyakazi yupi katika position hiyo ya kazi? DIRECTLY wengi watamchagua huyu wa pili maana hata kama ataleta uharibifu wowote inakuwa rahisi kumpata maana vijana wa sasa hivi nao hatueleweki,Kwa hiyo kwa sisi ambao hatuna connection ni lazima kuwa na vitu vya ziada na pia kuwa ubunifu ili kupata kazi.
NJIA RAHISI NINAYO IONA ILI KUPATA KAZI HASA KWA KIPINDI HIKI.
Unajua katika hiki kipindi kila boss anapokutana na graduate anaetafuta kazi wengi wanakuwa na wasiwasi kwamba huyu mtu nikimwajiri nitamlipa kiasi gani na degree,masters au P.h.d yake.mtihani mkubwa uko hapa na maboss wengi wanashindwa kutuajiri sababu kwanza anajua kwamba hatuna experience,pili hajui tabia yako na tatu hali ya biashara pia sio nzuri sana hivyo ana wasi wasi atakulipa kiasi gani uridhike na masters yako au P.h.d yako.Njia rahisi ya kuli ruka hili kweli kama wewe ni graduate unaetafuta kazi kweli na ni mchapa kazi ni kwa kwa kujitofautisha na graduates wengine wanaohangaika na mabahasha mjini kutafuta kazi,WAKATI wao wanatafuta kazi wewe tafuta kitu unachokipenda hasa vitu ambavyo vitakupatia UJUZI na itapendeza zaidi kama ujuzi huo utakuwa katika field ambayo umeisomea.MFANO kama umesomea mambo ya Computer science na unapenda labda mambo ya kudesign Website,graphics design au software development Tafuta Kampuni zako kama tano ambazo kweli zinadeal na hizo kazi za designing,badala ya kuomba kazi wewe OMBA kujitolea katika moja ya kampuni utakayo pata kati ya hizo tano,Kuwa mbunifu pia kwenye kuomba nafasi hizi za kujitolea,Mfano unaweza ukatafuta hata watu watatu wakajifanya ni wateja labda wanataka huduma ya kutengenezewa website ukaenda na mmoja siku ya kwanza kwenye kampuni ya kwanza ukajieleza wewe ndo umemtafuta na umemleta kama mteja,baada ya siku mbili ukampeleka mteja wako wa pili anajifanya anataka kudesigniwa logo, baada ya siku nne ukampeleka mteja wa tatu alafu siku hiyo hiyo ukaacha na barua yako ya kuomba kujitolea,Haki ukifanya hivyo kwa kampuni zote tano huwezi kukosa hata moja.
WORKING PRINCIPLE
Hapa ninavyosema uombe kujitolea haitakuwa kujitolea kweli kweli kama kweli wewe una nia na ni mchapa kazi kweli kweli,kama kweli unachapa kazi haita pita hata mwezi mmoja asilimia kubwa za makampuni wataanza kukulipa japokuwa haitakuwa sawa na degree,masters au p.h.d yako.Kuomba kwa kujitolea itaifanya kampuni kuwa free kukulipa kutokana na uwezo wake maana sio kla kampuni zinauwezo wa kumlipa mfanya kazi kutokana na elimu aliyo nayo.Hata kama wasipokupa kitu komaa maana UJUZI utakaoupata ndio muhimu kuliko hata mshahara ambao wangekulipa kwa elimu uliyo nayo.Njia pekee ya kutukomboa sisi kama graduates sio kupata KAZI bali kuwa na UJUZI,Baada ya muda ukiona umeiva vizuri na pesa wanayokulipa hauridhishwi nayo YOU CAN MOVE ON na kuanza kufanya hizo shuguli mwenyewe.KIUKWELI biashara unayoweza kuianza bila ya kuwa na mtaji kabisa ni kwa kuwa na ujuzi maana EVEN if utapewa mamilioni ya fedha uanzishe biashara labda ya kuuza products,huwezi kuwa na uhakika 100 percent maana biashara pia zinaweza kufa muda wowote,cha kujiuliza utafanya nini baaada ya biashara kufa?UJUZI ni security yako milele na hakuna yeyote anaeweza kuuchukua au kuku nyang'anya,LET US BE CREATIVE.
goood .nimefurahi sana kuona namna gani ulivyo na point
 
Huu ujinga ndiyo sitaki kuusikia. Na kama kweli wewe ndiye msomi basi taifa limekufa hili. Unaanza kuuliza utalimia nn? Unauliza utang'oa vipi visiki shambani?

Huyo bibi na babu yako mpk leo wamekuwa wazee nani amekuwa akiwafanyia hizo kazi? Sasa wewe una kitu cha ziada "elimu" dhidi ya hao bibi na babu zako. Unashindwa vipi kuishi kwa kilimo?

Kwahiyo unataka upewe ajira ya mshahara wa laki 2 katikati ya jiji ama mji? Ambapo utaishia kuishi kwa kukopa kopa unga kwenye maduka ya Mangi. Acha ujinga kilimo kinalipa, ndiyo maana 80% ya watanzania wanakitegemea. Wewe msomi gani unakiogopa kilimo?

Umenichefua wewe!!
Alafu ukute wewe mwenyewe hujui hata mashamba yanafananaje...wewe jamaa umenichefua sana,kwa akili zako kilimo hakiitaji mtaji eti??
Unavyooongea kirahisi eti kuna mashamba ya bure....kwa hiyo wewe hata ukipita pale mikumi ukiyaona yale mapori,unadhani ni mashamba so akili yako inakutuma kuwa mtu yoyote akichukua tu jembe anaweza anza lima pale...akishalima akili yako inakutuma mbegu na mbolea huwa vinaokotwa tu or kugawiwa bure...alafu watu kama wewe ndo huwa mmekalia tu viti vya ofisi mlizoajiriwa kwa kujuana na kupeana na kina mjomba so unavyopigwa na kiyoyozi hapo unajiona mjanja ku comment ujinga kwenye post za watu wanaoumiza vichwa kutafuta namna gani wanatoka kimaisha
 
Alafu ukute wewe mwenyewe hujui hata mashamba yanafananaje...wewe jamaa umenichefua sana,kwa akili zako kilimo hakiitaji mtaji eti??
Unavyooongea kirahisi eti kuna mashamba ya bure....kwa hiyo wewe hata ukipita pale mikumi ukiyaona yale mapori,unadhani ni mashamba so akili yako inakutuma kuwa mtu yoyote akichukua tu jembe anaweza anza lima pale...akishalima akili yako inakutuma mbegu na mbolea huwa vinaokotwa tu or kugawiwa bure...alafu watu kama wewe ndo huwa mmekalia tu viti vya ofisi mlizoajiriwa kwa kujuana na kupeana na kina mjomba so unavyopigwa na kiyoyozi hapo unajiona mjanja ku comment ujinga kwenye post za watu wanaoumiza vichwa kutafuta namna gani wanatoka kimaisha
Umemjibu vizuri.
 
Nakumbuka ilikuwa 2017 mwezi wa 8...!!nilipostpone masomo baada ya kuona kuna kila dalili ya kurudi mtaani nikiwa sina kitu
Kumbuka hapo nilibakiwa na boom 1 tuuu

Nilichokifanya ni kununua diary...nkaandika business za kufanya nkiacha chuo

Kila biashara ilinicost kwenye kodi...coz nakumbuka boom ilibaki 520k

So nikakumbuka kuna frem pale hom waliitelekeza baada ya kushindwa biashara

Nikawapanga ndugu...nkampanga mzazi...nae akakubali(hapo hajui kama nmeacha chuo)

Nikaandika barua ya kuahirisha masomo
Nikauza vitu vyangu
Nkapanda ndinga kurudi town dsm

Kwenye gari nilitumia mda mwingi kuandika tactics za kuikuza biashara

Nikaingia kazini
Japo mtaji ulikuwa mdogo lakini nilijitahidi kuukuza kwa kuacha faida pia ijizungushe
Nilijinyima vingi mpk girlfriend aliniacha

Nikajitahidi kujifunza kwa wauza maduka wengine hapa jf na pia google

Taratibu mambo yameanza kunyooka
Nimepanga chumba
Vitu ndan vipo japo co vingi
Nakula nnchotaka
Na juzi BIKO wameniongezea mil.10

Kikubwa ni kuweka malengo..ukiweka anasa pemben na ukpambana...Mungu atakulipa
IMG-20180724-WA0018.jpeg
IMG-20180724-WA0024.jpeg
IMG-20190222-WA0003.jpeg
IMG_20191011_074802_252.jpeg
IMG_20191010_184944_817.jpeg
bikotanzania_3___B3b5-4HH_rn___.jpeg
 
hongera mzee, naamini tunaishi kwenye simulation kama the matrix, yani kila mtu ana ramani yake ambayo the great architect "God" ameshamchorea, ndio maana unakuta mtu kasoma wee hadi doctrate af anaishia kuimba mziki, big up mzee for responding that call since it was already decided as its said "you're not here to make a choice, but to understand why you made it"
Nakumbuka ilikuwa 2017 mwezi wa 8...!!nilipostpone masomo baada ya kuona kuna kila dalili ya kurudi mtaani nikiwa sina kitu
Kumbuka hapo nilibakiwa na boom 1 tuuu

Nilichokifanya ni kununua diary...nkaandika business za kufanya nkiacha chuo

Kila biashara ilinicost kwenye kodi...coz nakumbuka boom ilibaki 520k

So nikakumbuka kuna frem pale hom waliitelekeza baada ya kushindwa biashara

Nikawapanga ndugu...nkampanga mzazi...nae akakubali(hapo hajui kama nmeacha chuo)

Nikaandika barua ya kuahirisha masomo
Nikauza vitu vyangu
Nkapanda ndinga kurudi town dsm

Kwenye gari nilitumia mda mwingi kuandika tactics za kuikuza biashara

Nikaingia kazini
Japo mtaji ulikuwa mdogo lakini nilijitahidi kuukuza kwa kuacha faida pia ijizungushe
Nilijinyima vingi mpk girlfriend aliniacha

Nikajitahidi kujifunza kwa wauza maduka wengine hapa jf na pia google

Taratibu mambo yameanza kunyooka
Nimepanga chumba
Vitu ndan vipo japo co vingi
Nakula nnchotaka
Na juzi BIKO wameniongezea mil.10

Kikubwa ni kuweka malengo..ukiweka anasa pemben na ukpambana...Mungu atakulipa
View attachment 1235240View attachment 1235242View attachment 1235243View attachment 1235245View attachment 1235246View attachment 1235255
 
Ndo maana naamini yawezekana ilipangwa nifanikiwe kupitia biashara na co ajira...!!Mungu atujalie sote tufike tunapotaka...!!
hongera mzee, naamini tunaishi kwenye simulation kama the matrix, yani kila mtu ana ramani yake ambayo the great architect "God" ameshamchorea, ndio maana unakuta mtu kasoma wee hadi doctrate af anaishia kuimba mziki, big up mzee for responding that call since it was already decided as its said "you're not here to make a choice, but to understand why you made it"
 
Nakumbuka ilikuwa 2017 mwezi wa 8...!!nilipostpone masomo baada ya kuona kuna kila dalili ya kurudi mtaani nikiwa sina kitu
Kumbuka hapo nilibakiwa na boom 1 tuuu

Nilichokifanya ni kununua diary...nkaandika business za kufanya nkiacha chuo

Kila biashara ilinicost kwenye kodi...coz nakumbuka boom ilibaki 520k

So nikakumbuka kuna frem pale hom waliitelekeza baada ya kushindwa biashara

Nikawapanga ndugu...nkampanga mzazi...nae akakubali(hapo hajui kama nmeacha chuo)

Nikaandika barua ya kuahirisha masomo
Nikauza vitu vyangu
Nkapanda ndinga kurudi town dsm

Kwenye gari nilitumia mda mwingi kuandika tactics za kuikuza biashara

Nikaingia kazini
Japo mtaji ulikuwa mdogo lakini nilijitahidi kuukuza kwa kuacha faida pia ijizungushe
Nilijinyima vingi mpk girlfriend aliniacha

Nikajitahidi kujifunza kwa wauza maduka wengine hapa jf na pia google

Taratibu mambo yameanza kunyooka
Nimepanga chumba
Vitu ndan vipo japo co vingi
Nakula nnchotaka
Na juzi BIKO wameniongezea mil.10

Kikubwa ni kuweka malengo..ukiweka anasa pemben na ukpambana...Mungu atakulipa
View attachment 1235240View attachment 1235242View attachment 1235243View attachment 1235245View attachment 1235246View attachment 1235255
Duuh kumbe biko ni kweli aisee hongera sanaaa
 
kwa akili zako kilimo hakiitaji mtaji eti??
Mtaji unao tayari....nguvu na elimu yako.
akishalima akili yako inakutuma mbegu na mbolea huwa vinaokotwa tu or kugawiwa bure...
Acha kutafuta visingizio visivyo na mashiko. Mbegu shilingi ngapi? Acha kujificha kwenye changamoto, tumia elimu yako kuzitafutia ufumbuzi.
.
Unauliza kuhusu mbolea???
Zunguka kwa wafugaji omba samadi mwaga shambani kwako.
 
Mtaji unao tayari....nguvu na elimu yako.

Acha kutafuta visingizio visivyo na mashiko. Mbegu shilingi ngapi? Acha kujificha kwenye changamoto, tumia elimu yako kuzitafutia ufumbuzi.
.
Unauliza kuhusu mbolea???
Zunguka kwa wafugaji omba samadi mwaga shambani kwako.
Pesa ya mbegu
Pesa ya nauri na mizungoko yote
Pesa ya jembe
Pesa ya kusafirisha mazao
Pesa ya kula
Pesa ya madawa
Pesa ya malazi
Pesa ya
Pesa ya

Hacheni story zenu nyinyi mlivyopewa pesa na wazazi wenu munaongea tu.
 
Mtaji unao tayari....nguvu na elimu yako.

Acha kutafuta visingizio visivyo na mashiko. Mbegu shilingi ngapi? Acha kujificha kwenye changamoto, tumia elimu yako kuzitafutia ufumbuzi.
.
Unauliza kuhusu mbolea???
Zunguka kwa wafugaji omba samadi mwaga shambani kwako.
Acha kuandika ujinga angalau itakusaidia kuficha upuuzi wako...kumbe unajua mbegu hazigawiwi bure...na hayo mashamba unafikiri yanagawiwa bure??or kwa akili zako ukisafiri na gari ukiviona vichaka huwa akili zako zinakutuma yale ni mashamba mtu yoyote anaweza chukua jembe na kuanza kulima...alafu mbolea unadai eti nizunguke kwa wafugaji nichukue samadi,kwa hiyo unadhani wakulima wanavyolalamikaga na kuiomba serikali iwapelekee mbolea wote ni wajinga na wavivu...we jamaa ni mjinga sana na hujui hata shamba linafananaje...icho kikazi ulichonacho najua kinakupa kiburi na kutuona sisi tunaohangaika hatuna akili...sawa mjanja wewe mimi nakuombea upoteze iyo kazi inayokupa kiburi uje huku mtaani tuangaike wote tukuone wewe mjanja mwenye akili unayeweza kuvamia milima na vichaka ukavigeuza mashamba na ukatumia samadi tu kulima...KARMA is watching you...vitu vingine acha kuleta ujuaji...we endelea kupigwa na kiyoyozi hapo ofisini kwenu
 
Mtoa post mm nitakusaidia kitu kimoja, ukitaka kuondokana na aibu nenda mbali na mkoa ulipo zaliwa/kuishi ambako hufahamiki.

Ukiwa huko utakua free kufanya mchongo wowote.
Mfano mm n graduate nimeacha kazi private nlikua nalipwa 300,000 sahizi npo mbali napiga issue ya carwash kwa mtu ili kupata experience baada ya siku chache ntakua na yangu. Carwash pays!!!
This z my dream. Ofisi yangu ya pili itakuwa hii au duka la simu na vifaa vyake
 
vp stationary ina faida nzuri? yaan return yake ikoje per day?
Mimi nilianza na mtaji nguvu zangu, nilikwenda Kigoma, nikafyatua tofali za kuchoma, nikauza kwa shule moja ilikyokua ikijengwa nikapata pesa, nikaamua kurudi town, nikatafta frame maeneo ya chuo kikuu nifungua stationery ambayo nimeitumikia kwa muda wa miaka mitatu ndipo nikapata ajira. Changamoto kubwa niliyoipata ilikuwa ni kufanya maamuzi ya kuanza.
 
Well,

Vipi kwa sasa hauendelei na hiyo biashara mkuu?
Lengo nipate information,
Nina lengo la kufungua hiyo biashara maeneo ya chuoni (preferably UDSM_Mabibo Hostel).
Well, kwa sasa nimesitisha biashara hiyo kutokana na kutokuwa karibu na eneo la tukio na kiukweli napata wakati mgumu sana kumuamini mtu anifanyie biashara kama nilivokuwa nimewazoesha wateja wangu. but nina plan ya kuiendeleza kama nitapata mtu amabye atakuwa tayari kujifunza kazi kutoka kwangu na aifanye kama nilivyokuwa nikifanya mimi.
Kama lengo lako ni kufanya biashara ya Stationery tena maeneo ya chuo, unapaswa kutambua kuwa wateja wako wengi (karibia wote) ni wanafunzi, na wanafunzi wengi huwa rational, so utapaswa kujua ni bei gani utoe copy na bei gani ufanye printing.
Pia utapaswa kujua u-base kwenye hudama zipi na zipi i.e. unaweza ku-base kwenye kutoa huduma pekee au ukaweka na bidhaa pia.
 
Back
Top Bottom