Wale mliokimbilia kujenga Dodoma poleni sana

Wale mliokimbilia kujenga Dodoma poleni sana

Pale dodoma ni katikati ya nchi,walipo wekeza majengo hawajakosea itawalipa tuu huko mbeleni,Kama so wao Basi wajukuu zao.
 
Mkuu sio kweli kwa sasa mzunguko wa pesa Dodoma ni mkubwa sana,kumbuka pesa ya Serikali kwa sasa 90% inaenda ni kwa Watumishi wa umma- na asilimia kubwa ya watumishi wa umma wapo Dodoma.

Kila bank unayoijua kwa sasa ipo Dodoma tofauti na awali ambapo walikuwepo NMB na CRDB pekee.
Sio tuu banks even biashara zingine zote zinazopatikana Dar is slum zimeshaanzishwa Dom.
 
Huo mji utakuja kutisha sana,, kama ni jua hata dubai jua kali, ,ngoja maji ya victoria yafike hapo mambo yatakuwa juu ya mambo
Sio tuu maji bali hata mradi wa Ring road, airport,uwanja wa mpira na arena na barabara za dual carriage kila upande.

Pia serikali ikihamia yote pale itakuwa moto.Saizi kuna mradi wa nyumba 1000 yaani estates na apartments za kuzidi.

Mahoteli yanajengwa etc,Dom Isha take off tayari ni suala la mda tuu.
 
Sasa huo ni ubishi Dar economically unaweza kulinganisha na mikoani? Wewe unadhani ni kwa nini Dar pamoja na udogo kieneo bado ina watu wengi sana kushinda mikoa yote?
Ndio maana sasa tunajenga Dom Ili ku diversify fursa..

Pia huu ni wakati muafaka wa serikali licha ya kuchelewa lakini ianze kuwekeza miundombinu hasa ya usafirishaji ya kisasa kwenye miji mikuu ya Kanda ya Mwanza,Mbeya,Arusha,Tanga na Mtwara Ili iwe centers za investment lengo ni ku diversify economic opportunities na kupunguza utegemezi kwa Dar pekee.
 
Hauijui dodoma mkuu, we itakuwa ulifikia chedegwa huko ila tuliopo dom kwa muda mrefu tunaelewa kasi ya maendeleo na uwekezaji kabla na baada ya serikali kuhamia dom.
Miaka 6 iliyopita Dom haikuwa hata na mapato kuzidi Kahama lakini kwa sasa Jiji la Dom liko second kwa Dar ,sijui watu bado wanaongea nini.
 
Wizara zimetawanywa pande zote za nchi kama njia ya kusogeza fursa kulingana na umuhimu wa eneo husika katika wizara hiyo!! Yapo mengi ya kujifunza
Sasa hiyo scotland si ni kama mkoa wa Tabora tu kwa ukubwa...
 
Miaka 6 iliyopita Dom haikuwa hata na mapato kuzidi Kahama lakini kwa sasa Jiji la Dom liko second kwa Dar ,sijui watu bado wanaongea nini.
Kweli kabisa mkuu miaka 6 iliyopita kulikuwa hapashawishi kabisa kuwekeza. Nyumba zilikuwa chache mno bila kusahau miundombinu. Wanaobisha wengi ni wale waliofika dom baada ya stendi kuhamia nane nane [emoji1]
 
Dodoma ninavyoiona ni kama mji wa kutengenezwa,Dar ni mji uliojitengeneza wenyewe,miji iliyojitengeneza yenyewe kibiashara haitetereki .....mpaka hapo haiwezi kuja kuwa sawa kibiashara hata uko mbeleni
Sasa italingana vipi wakati mmoja umekuwa kwa muda mrefu....
 
Huo utakuwa ujinga wa Hali juu sana,mutu ana shida wizara ya Afya ,mfano wako ,hiyo iwe morogoro,akifika hapo anaambiwa tunahitanji hiki kutoka wizara ya elimu,Sasa wizara hiyo iwe kagera-bukoba huko,huoni kama ni usumbufu wajinga sana huo,nilishawahi kuomba uhamisho kutoka Kwa katibu mkuu(wizara fulani-siitaji),nikaambiwa nenda Kwa katibu mkuu tamisemi,Sasa fikiria Mmoja awe mtwara na mwingine awe kigoma na wewe uwe umetokea mara usumbufu unaoupata ukoje?,vitu vingine mfikiri kabla ya kutoa comment,wizara ukizitawanya hivyo raia na maskini ndo wataumia,ukifika hapa unaambiwa nenda wizara fulani kwanza,Sasa hapo ziwe mbalimbali utakufa na shida yako
Hiyo ni imagination ya zamani kabla ya serekali Mtandao, futa mawazo ya enzi ya zamani, pia mambo mengi yapo kwa mtandao wizarani hakuna jipya labda kama una tenda ya stationary unatakiwa kwenda hapo
 
Back
Top Bottom