Wale wenye GPA kuanzia 2.1 mpaka 3.4 tukutane hapa tuyajenge hapa

Sio kweli. Ukiwa na kichwa kigumu labda.
 
Wewe ulipata 4.3, mimi nilipata 2.5! Tunafanya kazi moja na mshahara ni mmoja, una kipi cha kujivunia kunizidi kutokana na GPA yako?
Ila ni kweli.....me nakumbuka nilikua kampuni flani nafanya kazi kitengo kimoja na wenye GPA kubwa lakini mshahara wote tunalipwa sawa.
 
Vichwa ngumu ndio nguvu inahitajika. Soma uelewe.
eeh ww mwenye kichwa chepesi komaa bob

sisi ngumu mambo ndo kama hayooo hutumii nguvu nyingi na unatoboa 😅😅😅
 
Halafu kuna GPA za Cambridge na za jalalani. Mnajikutaga magenious balaa vijana wa jalalani (mna conservative mindset).
 

Inategemea uko wapi. Kwenye elimu ni lazima GPA iwe kubwa. Sio una GPA kama kiatu cha mtoto ufundishe chuo.
 
Sometimes maapuuza tu

Mtu unasainiwa assignment hata kushiriki hushiriki kufanya kama ni ya group kama ni individual unasubiri mikeka na ukikosa mikeka unaenda stationary unajibanza wakisepa kwakua kazi ime kuwa saved unaenda mpa hela unamwambia itoe hii iliotoka kutolewa

Unafanyiwa quiz nyengine unazi miss wana wanakataa maana umezidi kuwafanya lofa

Kama PROf ni mtata au DEPARTMENt ya watu wasio na utani upo ghetto kitumbowazi unacheza fifa text inaingia oyaa wanahesabu namba au quiz mda huohuo unapanda pikipiki tu unafika umechelewa unajaza registration number tu maana bora hivyo kuliko kutokusanya

Utokei class unatuma registration number yako kwenye sms mwamba akujazie kwenye attendance sheet

Husomi hata ratiba za test unazisahau unasoma leo usiku kesho test au unasoma asubuhi unaanza kumuuliza wana kwenye simu oyaa PROf ame cover mpaka wapi

Hujui ratiba ya vipindi una kazi ya kuuliza tu baada ya hichi tuna kipindi gani kama kipindi ni saa nane saa nne ukitoka ndio hurudi tena mpka kesho

Wikiendi yako inaanzia Ijumaa kwa maana vipindi vya Ijumaa unaviua hutokei kabisa tukutane Jumatatu

Nitaendelea......
 
Kwenye test unapiga below mchawi anakuwa ni U.E hapo na U.E ukizungua imekula kwako


Kila semister lazima udakwe ukifaulu sana umeshikwa kimoja


C Kama zote na B chache A za kuokoteza nyingi za field na SP

Unaweza kaa wiki huonekani chuoni kabisa na ukisign boom ndio tunakusahau kabisa zikikaribia kuisha ndio unaonekana kwenye nyumba za ibada na venue

Umasainiwa kila kitu mpaka kwenye foleni ya boom unamtuma mwamba akakusainie wewe mazingira ya chuo una allergies nayo ukiutwa discussion unasinzia haposomeki Darasani napo simu isipokuwa na bando una sinzia ukiambiwa short break unatoka ndio urudi tena

Hata ada huendi kusaini mpka mtafutwe na ma cr kwenye course registration napo unachelewa mnaanza msumbua CR ila kwenye kukusanya assignment unakuwa wa kwanza sijui unazitoa wapi

Ukienda venue hubebi hata notebook ya kukopi upo na modo na mshati wako mkubwa wa chuga kama unapaa kwahyo ukitoroka mtu anajua unaenda chooni

Sasa hayo yote hayo kwa nini nisipate lower second mimi kunguru wa Manzese na wanangu
 
Mara nyingi (si Mara zote) GPA kubwa ina-matter,
ebu angalia Kuna vyuo vingapi Tanzania na vimeajiri watu wangapi? Wengi wameajiriwa kwa kuwa na GPA kubwa, wale wa GPA ndogo hawawezi kuajiriwa huko hasa kuwa academic staffs wa chuo.

kuwa na GPA kubwa inaonyesha you have something to deliver ingawa kuna baadhi ya wakati GPA hai-reflect huwezo wa mtu (Mara chache). Kuwa na GPA ndogo vilevile huonyesha uwezo mdogo wa mtu ingawa pia in some cases inaweza isiwe kweli.

Wenye GPA ndogo wanaamini Moja kwa moja kuwa wenye GPA kubwa hawana uwezo, sijui wanatumia LOGIC gani kusema hivyo? ila hii inathibisha kwanini wana GPA ndogo.
 
Huko Serikalini ndio wanaangalia GPA. Huko kwenye taasisi kubwa hawahitaji cheti chako wakati wa kuomba kazi, unaambiwa leta CV na motivation letter tu. Vyeti utavileta wakati umepata kazi
Kwenye CV si unaandika accademic qualifications?
 
GPA kama umepata Harvard sawa lakini asilimia kubwa za bongo ni za mchongo... Na wajuz wengi hawatishiki na GPA wanaangalia output.
 
Kuna wengine hawakujua umuhimu wa GPA kubwa wakiwa mwaka wa kwanza. Wanakuja kustuka wapo third year.

Wengine wanakumbana na majanga ya loan anasoma huku anawaza atakula vipi usiku.
Changamoto ni nying. Lakini GPA kubwa Ina matter koz inakupa options nyingi. Leo TCU imeshusha gpa kwa academicians mpaka 3.5 lakini bado vyuo vinakomaa na 3.8.
Kuna taasisi binafsi na za serikali wanaamini ubunifu, weledi na commitment au overt traits zina reflect covert behavior and actions. So, kwao high gpa matters.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…