Walimu wana wakati mgumu! Darasa limejaa wanafunzi zaidi ya mia moja hana hata pa kukanyaga!

Walimu wana wakati mgumu! Darasa limejaa wanafunzi zaidi ya mia moja hana hata pa kukanyaga!

Kwamba, hakuna hali hiyo kwenye shule za serikali?

ingekuwepo mwalimu asingeshangaa...

darasa la nne B limevuja mvua, wakasondekwa temporarily kwenye la nne A, zikaitwa camera

mwalimu ana maelezo ya kuandika
 
Assume hapo alipo kuna mtoto wako unayetegemea aje kuwa Dr au mwanataalumu mtaalamu. Katika kijiji chetu huko nyumbani hadi sasa darasa la kwanza wameandikisha wanafunzi zaidi ya mia tatu huku madarasa yaliyopo kwa ajili ya darasa la kwanza ni mawili tu.
Tunampongeza raisi kwa hili la kuwa na ndege zetu lakini sioni sababu ya kurundika mindege kibao wakati kuna mahitaji muhimu zaidi ya ndege hizo. Tushikamane kwa kuusemea ukweli pasipo kutanguliza itikadi za Kichama,Ukanda,Udini au Ukabila

Sent using Jamii Forums mobile app
 
ingekuwepo mwalimu asingeshangaa...

darasa la nne B limevuja mvua, wakasondekwa temporarily kwenye la nne A, zikaitwa camera

mwalimu ana maelezo ya kuandika
Seriously mzee? Mlundikano wa wanafunzi kwenye shule za serikali ni jambo lililopo. Kama kuna shule hazina madarasa, mlundikano utakosekanaje na hii ‘elimu bure’?
 
Natabiri:
Mpiga picha, mpigwa picha, Mkuu wa kituo na waambata wake kuadhibiwa kwa sababu ya clip hii, personally ningemshukuru msambazaji wa clip kwa kunifikishia taarifa ya hali halisi ili nichukue hatua za haraka kuondoa tatizo.
Hii itawa cost,mbaya zaidi mpiga picha hakuwaza kabisa kuhusu hii tshirt ya chalii...
IMG_20200123_060123.jpg
Screenshot_20200123-060041.png
 
Acheni umbumbumbu na nyie jamani. Dreamliner ziko hapa kukuza uchumi na siyo starehe. Jaribu kufikiria kama zisingekuwepo sasa hivi ingekuwaje? Maana ndugu zangu Precision weshatepeta na matapeli wetu Fastjet weshakata pumzi kitambo. Kwa videge viwili sijui vitatu vya precision nauli ingeshafika milioni mbili kwenda tu hapa KIA. ATC ni lazima iwepo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha propaganda mfu wewe, Fastjet wanakimbiza vibaya huku Kusini mwa Afrika na wanafanya vizuri. Fika Harare,Maputo,Zambia pale ndipo utawajua. Waliondoka huko baada ya figisu kuwa nyingi ili kuwapa mtelemko ATCL
Screenshot_20200123-061039_1579749243032.jpeg
Screenshot_20200123-061233_1579749258270.jpeg
Screenshot_20200123-061113_1579749277617.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
LOooh!

Huyo mwalimu, hata kama angekuwa mzuri kiasi gani, hawezi kumudu kuangalia kazi za wanafunzi wake kwenye madaftari yao.

Lakini, mkuu 'Return' hebu niambie, enzi hii kweli, karne hii ya ishirini na moja, wewe kama mzazi utampeleka mwanao kwenye mazingira ya namna hii?

Hawa wazazi wa hawa watoto, wengi wao watakuwa ni wazawa wa baada ya uhuru wa nchi yetu, 1961. Hata kama hawakubahatika kupata kisomo cha kutosha, zaidi ya darasa la saba tuseme; hawa wazazi wanaweza wakasimama na kusema walisoma katika mazingira ya aina hii yanayowakabili watoto wao?

Yaani kiukweli, hawa wazazi hawana sauti yoyote wanayoweza kupaza wakasikilizwa, hata kama wao hawana uwezo wa kuwajengea shule hawa vijana?

Hizi kura zao wanazopiga kila mara kuwachagua viongozi wasioona madhara haya, hawaoni kabisa kuwa kura hizo zina thamani kubwa inayoweza kabisa kubadili hali hii ya hawa watoto?

Ngoja nimwite rafiki yangu Erythrocyte. Picha hii haiwezi kukosa kuingia kwenye maktaba yake. Na kama kweli vyama vya upinzani wana nia thabiti ya kuibadili Tanzania, hakuna mahali pa kuanzia zaidi ya tatizo kama hili la elimu yetu.

Siwasikii wakisema chochote, sijui nao wanayo matatizo gani!

Hapa sio swala la kukosa uwezo wa kujenga shule. Huu ni uzembe na upumbavu wa viongozi na wananchi wanaowaongoza.
Mtu awe mkuu wa mkoa/wilaya, tarafa/kijiji. Uwe ofisa elimu ngazi yoyote katika eneo hilo, hali hii isikustue, wewe ni kiongozi wa namna gani!

Inatia hasira sana.
 
Watu wamekua waoga kiasi kwamba tayari washamuhukumu huyo mwalimu na aliyechukua hyo video...sikuwahi kuwaza kama Nchi watu wakifichua tatizo wanaonekana maadui wa nchi..
 
Namuonea sana huruma huyo mwalimu kwa nini amerocord kwenye huu utawala anaweza akaishia pabaya! Maana hii video imesambaa sio kidogo.
 
Kwakuwa wanajitapa awamu ya 5 ni Viongozi Wazalendo ..Iwe ni lazima sasa Watoto wote wa Viongozi na Wafanyakazi wa Serikali Wasome katika Shule za Serikali.

Iwe ni Lazima
 
Bado DIRIMULAINA na BOMBADIEE Zingine mbili zinaingia mwaka huu 2020.
 
Kwakuwa wanajitapa awamu ya 5 ni Viongozi Wazalendo ..Iwe ni lazima sasa Watoto wote wa Viongozi na Wafanyakazi wa Serikali Wasome katika Shule za Serikali.

Iwe ni Lazima
Hii ingesaidia sana kuboresha hizi shule zetu
 
  • Thanks
Reactions: prs
Katika pitapita zangu nimekutana na hii video ikionesha wanafunzi walivyorundikana kwenye chumba cha darasa kama ng'ombe tena wakiwa wamekaa chini, na bado tukiendelea kupiga makofi kuhusu ununuaji wa madege ya dreamliner. Kama Taifa tunapaswa kupaza sauti zetu kama wananchi wa Taifa Tanzania maana haya yanatokea hapa hapa nchini.


Hiyo video hujajiridhisha imepigwa lini na uhalisia wake unatuletea humu,si kila cha mtandaoni ni halisi
Hata hivyo kupanga ni kuchagua lazima tuimarishe utalii,na watalii hawaji kwa ungo
 
Back
Top Bottom