Waliosambaza taarifa potofu dhidi ya Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kukiona cha mtema kuni. Waziri Nape atoa maelekezo

Waliosambaza taarifa potofu dhidi ya Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kukiona cha mtema kuni. Waziri Nape atoa maelekezo

Kuna mjadala ameanzisha Waziri Nape kuhusu kuchukuliwa hatua kwa wanaohusika na uzushi wa kifo. Wakati vyombo vya dola vikisubiri maelekezo ya maandishi kutoka kwa Mhe. Waziri kama mlalamikaji naomba wanaofahamu sheria za nchi watuambie kama kuna kosa kisheria au nikunyume na tamaduni zetu?

Kama ni kosa kisheria itatusaidia sana kuwachukulia hatua wale wote wanaokurupuka kutoa taarifa za misiba kwenye mitaa yetu. Tuelimishane hapa tuanze kuchukua hatua.....ni vyema unapochangia ukatuwekea na sheria husika japo kwa kufanya citation itusaidie kama Taifa kudhibiti kadhia hizi.
But lazime iwe two traffic pia kusingizia mtu uhai wakati alisha fariki na lenyewe litakua kosa pia?
 
Je Kassim Majaliwa aliyesema jiwe ni mzima anachapa kazi na ana mafile mengi ya kusoma alisema hayo March 13 , 2021.

Siku Samia anatangaza kifo , alisema jiwe alilazwa tangu tarehe 6 Machi ,2021.

Je nani hapo muongo na muongo aliyezusha mtu ni mzima kumbe taabani kitandani tumfanye nini?

Nape ni empty sana !
 
Mwalimu asipokuja kazini shuleni na mkuu wa shule hana taarifa au hazitoi KWA staff na wanafunzi je wakianza eti eti labda labda TSC itawashtaki wanafunzi?
 
Kupitia mtandao wa kijamii X, Waziri Nape Nnauye amesema kuwa ameelekeza vyombo vinavyohusika kuchukua hatua za mfano dhidi ya wote waliozusha na kusambaza taarifa za uongo dhidi ya Makamu wa Rais

Nanukuu

"Pole sana Mhe Makamu wa Rais. Tumekusikia. Kwakuwa tuna sheria zinazoelekeza mitandao itumike vizuri na kwakuwa tuna Taasisi na watu wa kusimamia sheria hizi, bila kuathiri uhuru wa watu, TUTACHUKUA HATUA kutokomeza matumizi haya mabaya ya mtandao! Naamini wote watatuelewa

Nimeelekeza vyombo vyote vinavyohusika kuchukua hatua za mfano, ili tujenge jamii inayoheshimu uhuru wa kila mtu. Uhuru wowote unapoingilia uhuru wa mwingine ni uvunjaji wa sheria, hatuwezi kujenga jamii inayoona hilo ni jambo la kawaida"
Padri Kitima atapona? Huyo si ndiye aliyemkaribisha Mwabukuzi awatukane Bunge amtukane Makamu wa Rais amtukane Rais na ajenda ya Waarabu?
 
Kupitia mtandao wa kijamii X, Waziri Nape Nnauye amesema kuwa ameelekeza vyombo vinavyohusika kuchukua hatua za mfano dhidi ya wote waliozusha na kusambaza taarifa za uongo dhidi ya Makamu wa Rais

Nanukuu

"Pole sana Mhe Makamu wa Rais. Tumekusikia. Kwakuwa tuna sheria zinazoelekeza mitandao itumike vizuri na kwakuwa tuna Taasisi na watu wa kusimamia sheria hizi, bila kuathiri uhuru wa watu, TUTACHUKUA HATUA kutokomeza matumizi haya mabaya ya mtandao! Naamini wote watatuelewa

Nimeelekeza vyombo vyote vinavyohusika kuchukua hatua za mfano, ili tujenge jamii inayoheshimu uhuru wa kila mtu. Uhuru wowote unapoingilia uhuru wa mwingine ni uvunjaji wa sheria, hatuwezi kujenga jamii inayoona hilo ni jambo la kawaida"
Huyo waziri kilaza labda amtishie mkewe...anajulikana ni lopolopo tu
 
Waziri Nape, jitahidi sana kufanya kazi yako kwa weledi na akili nyingi, na sio utumie nguvu kwenye mambo ya kufikiri.

Unataka tukuone wewe ni mwema sana eti? Hivi kuna wakati huwa mnakumbuka kuwa mnaongoza watu wa aina gani? Tafakari sana mkuu.
 
Waziri Nape ameandika haya kwenye ukurasa wake wa X (zamani Tittwer):

"Pole sana Mhe Makamu wa Rais. Tumekusikia. Kwakuwa tuna sheria zinazoelekeza mitandao itumike vizuri na kwakuwa tuna Taasisi na watu wa kusimamia sheria hizi, bila kuathiri uhuru wa watu, TUTACHUKUA HATUA kutokomeza matumizi haya mabaya ya mtandao! Naamini wote watatuelewa!

"Nimeelekeza vyombo vyote vinavyohusika kuchukua hatua za mfano, ili tujenge jamii inayoheshimu uhuru wa kila mtu. Uhuru wowote unapoingilia uhuru wa mwingine ni uvunjaji wa sheria, hatuwezi kujenga jamii inayoona hilo ni jambo la kawaida!"
 
Makamu wa raisi ni mtumishi na kiongozi mkubwa katika nchi. Anapokua haonekani kwa muda mrefu ni haki ya wananchi, kujiuliza, kuuliza, kujenga dhana mbalimbali zinazotetea kutokuwepo kwake, Na hili ni kosa la serikali kushindwa kuwapa taarifa sahihi juu yanini kinaendelea juu ya kiongozi wao na kufanya kuwe na ombwe la habari linalojazwa na taarifa nyingi za ukweli na uongo. Serikali ndo mnatakiwa mjirekebishe kwa kuwapa taarifa wananchi kwa muda mwafaka kuepuka sintofahamu. Kuwachukulia hatua ni kuwaza kizamani na kishamba au kushindwa kutambua kwanini wewe ni kiongozi.
 
Kupitia mtandao wa kijamii X, Waziri Nape Nnauye amesema kuwa ameelekeza vyombo vinavyohusika kuchukua hatua za mfano dhidi ya wote waliozusha na kusambaza taarifa za uongo dhidi ya Makamu wa Rais

Nanukuu

"Pole sana Mhe Makamu wa Rais. Tumekusikia. Kwakuwa tuna sheria zinazoelekeza mitandao itumike vizuri na kwakuwa tuna Taasisi na watu wa kusimamia sheria hizi, bila kuathiri uhuru wa watu, TUTACHUKUA HATUA kutokomeza matumizi haya mabaya ya mtandao! Naamini wote watatuelewa

Nimeelekeza vyombo vyote vinavyohusika kuchukua hatua za mfano, ili tujenge jamii inayoheshimu uhuru wa kila mtu. Uhuru wowote unapoingilia uhuru wa mwingine ni uvunjaji wa sheria, hatuwezi kujenga jamii inayoona hilo ni jambo la kawaida"
Kwani Kigogo alipatikana?.
 
Mtu usipoonekana bila taarifa katika sehemu ambazo umezoeleka kionekana, ni kawaida watu kuweka speculations, either umesafiri, unaumwa, umekufa, umetekwa, umepotea n. K. Kushindwa kutambua jinsi mechanism ya akili ya binadamu inavofanya kazi na kutishia hatua ni ukilaza.
 
Si vizuri kumzushia mtu kifo.
Lakini yote haya ni serikali ndio sababu kwa kukaa kimya na mhusika mwenyewe kapotea haonekani hata kama yuko likizo au kwenye matibabu lazima wananchi wajulishwe kuzima uzushi
 
Back
Top Bottom