Wamiliki wengi wa majokofu/friji wanauelewa mdogo juu ya utendaji kazi wake

Maelezo mazuri, asante. Nimekumbuka sayansi yangu ya sekondari. Una ujuzi wowote wa ufundi kwenye Fridge/Air condition?
 
Maelezo mazuri, asante. Nimekumbuka sayansi yangu ya sekondari. Una ujuzi wowote wa ufundi kwenye Fridge/Air condition?
Asante kaka. Nina ujuzi ila siufanyii kazi kwa sasa. Lakini kama una tatizo la kiufundi na uko Dar es salaam usisite, tuwasiliane. Kuna kijana ninayemuamini atakusaidia.
 
Naomba kujua Zaidi kuhusu hizi number. Mimi Nina Pinetech ndogo Ina namba 1-7 ila sijui maama yake
Nqmba1_7 hizi ni namba ya ku set temperature unayotaka kwenye compartment ya fridge yako.. kadiri namba zinavo panda ndivo unavo ongeza ubaridi kwenye compartment ya fridge yako lakini pia the same applies to power consumption.. number kubwa maana yake fridge inafanya kazi muda mrefu ku attain ile temperature so more energy consumption..
 
Asante kaka. Nina ujuzi ila siufanyii kazi kwa sasa. Lakini kama una tatizo la kiufundi na uko Dar es salaam usisite, tuwasiliane. Kuna kijana ninayemuamini atakusaidia.
Asante. Nilitaka tu kuuliza. Kuna dhana kuwa mabasi ya abiria yenye air condition, hizo air condition hazidumu kwenye mazingira ya nchi kama Tanzania, je ni kweli? Basi likinunuliwa jipya na air condition zinaweza kudumu muda gani?
 
Ila kaka uko unakokwenda sio unajua tabia za gesi? Unajua hata hii mitungi ya majumbani wakati inajazwa inakua katika hali gani? Na unajua gesi ingiwa kwenye mkandamizo kisha ukaifungulia gafla inakua kwenye hali gani?
 
Nina fridge yangu Hisense ilifika kipindi ghafla ikawa haipozi nikamwita fundi akasema gesi imeisha na kuna kijidude kilikuwa baina ya compressor na pipe za gas akasema nako ni kabovu akahamisha mfumo wa condenser kutoka ndani akaweka nyingine nje ila lilikuwa linakula umeme na kupiga kelele balaa.

Mimi nadhani vitu kama frij na umeitumia zaidi ya miaka nane kama mtu una uwezo usijihangaishe na mafundi wa kibongo nunua nyengine maana mimi nilimuuliza huyo fundi kitaalam kabisa kwamba ikiwa mwanzo ndani ya mwezi nilikuwa natumia umeme wa 20K nyumba nzima mbona baada ya wewe kuitengeneza huo umeme unaisha ndani ya siku 19?anasema nitakuja na kipimo kupima labda niliweka gas nyingi yupo “unajua gas ikiwa nyingi compressor inakula sana umeme” nikamwambia njoo upime akaja akapima still tatizo likaendelea.

Akasema ah ah tatizo litakuwa earth rod nikamwita fundi wangu wa umeme akakagua nyumba nzima hamna penye leakage fundi fridge akahamisha kesi akasema kile chuma cha earth rod ni fake madai yake ni nondo siyo copper halisi nikaita tena fundi akaichimbua akaikwaruza kwa sururu kiasi cha kuichimba kabisa ni original kwa ufupi hakuweza kutatua lile tatizo japokuwa fij ilikuwa inafanya kazi but target haikuwa lile umeme,nilijutia muda na gharama nilizotumia bora ningenunua jipya toka mwanzo.
 
Yeye ameanzisha wewe ongezea, iwe amekariri au laa!!

Tumenufaika na hili kwahyo ukiona kuna sehem pamesalia ongezea mkuu sio lazima yote tuyapate kutoka kwake
 
Lawama zoote ni mfumo wa elimu unaotukuza pass marks na si uelewa ,
Watoto wapo busy kutafuta past papers na possible questions , unapataje experts kwa mtindo kama huo? Watu wanakariri na kufaulu imeisha hiyo.
Huna shukrani,
We unafikiri huyo expert anapatikana darasani peke yake??

We subiri tu watu waanzishe ili ukosoe,,
 
buzitata
Mi naomba unifahamishe kuhusu hili,
Nina freezer ila hizi evaporator zimewekwa kwa nje(yaani zinaonekana ndani ya freezer Kuna shida ilitokea fundi akashauri kufanya hivo)

Sa shida ninayopata nikwamba halieleweki yaani Kuna siku unaweza kuweka namba moja(min) ikagandisha saana, siku nyingine ukiweka hapo utakesha.

Siku nyingine ukiweka namba saba(max) hakuna kitu au itachukua mda mrefu kugandisha

Sasa hi shida ni Nini na lipi suluhisho lake.
 
Inventor Compressor Friji/AC ulaji wake wa Units za Umeme ni mdogo mno zipo zinazotumia Units za Umeme wa kuanzia laki 3 kwa mwaka mzima (360 Days-Ikiwa ON siku zote hizo bila Kuzimwa).
Mawazo yako mazuri, lakini hujatoa hoja yako kitaalamu, Ulitakiwa useme itatumia unit kadhaa za umeme kwa mwaka badala ya kutaja pesa. Hapa Tanzania kuna viwango mbalimbali vya bei ya unit moja ya umeme, pia bei zinaweza kubadilika. Hivyo ungetaja kiwango cha unit ungeeleweka zaidi na mchango wako ungeishi miaka 100 ijayo.
 
Pole sana mkuu japo sijajua tatizo la mwanzo lilikua ni lipi mpaka mkafikia huko ila ngoja nielezee kwa uchache

Hili swala la condenser wengi huwa wanalipuuzia sana (gesi ikitoka kwenye compressor lazma inahitaji kupoozwa)

Watu wengi tumezoea kuyabananisha mafriji yetu ukutani na tunasahau mafriji mengi yanatumia air cooling system iwe kwa fani au naturally.


Jaribu kuliweka friji lako kwenye space nzuri ili kuruhusu mzunguko wa hewa.

Freon isipopoozwa vizur ule upande wa high pressure nao unakua juu jambo linaloweza kupelekea trip au friji lako lisilete ubarid uliokusudiwa.

Pia sometimes hewa nayo huwa inachangia (hapa sielezei sana mafundi mchundo wasije kuniharibia mood)

Gesi ikiwa nyingi ni tatizo, ni vema inapojazwa vitumike vifaa husika.


I hope umepata mwanga kidogo.
 
Asante. Nilitaka tu kuuliza. Kuna dhana kuwa mabasi ya abiria yenye air condition, hizo air condition hazidumu kwenye mazingira ya nchi kama Tanzania, je ni kweli? Basi likinunuliwa jipya na air condition zinaweza kudumu muda gani?
Kwakweli sifahamu wala hiyo dhana sijawahi kuisikia. Ila penye wengi hapaharibiki jambo.
 
Huna shukrani,
We unafikiri huyo expert anapatikana darasani peke yake??

We subiri tu watu waanzishe ili ukosoe,,
Tulia nawe tupate madini acha ghubu! Tunawahitaji wote wanaojua kitu watoe maoni,sisi tusiojua tujifunze,mimi nipo makini hapa nina friji kimeo ,kwahiyo usiwatibue waache washushe nondo
 
You had a very simple problem ambayo it could be fixed very easy... Fundi wako hajui alichokua anatakiwa afanye... Yawezekana fridge ilianza kula umeme kwakua ilikua inafanya kazi muda wote bila compressor kuzima... So fridge ilikua haina system inayo monitor temperature, na duty circle ya compressor.. kama fridge lako ni non frost maana yake pia yawezekana ali bypass sensor ya heater trigger lakini pia timer.. solution check kama thermostat inafanya kazi, timer kama ina fanya kazi, once replaced your problems will be solved
 
Kwanza check kama ikiwa inawaka je ina circle on and off inapokua imefikia baridi ulio set kwenye knob yake? Kama ina circle vizuri but ikifika muda wa timer kuzimisha fridge (after every 8hrs standard) inazima na hairudi tena kuwaka (common problem kwa fridge with manual timer) basi timer itakua na shida..

Na kama hai circle "on" and"off" na mashine muda wote inapiga kazi bila kuzima mpaka wa Timer, basi check vifatavo check timer, check temperature sensor ya heater (ipo kwenye evaporator)
 
Lawama zoote ni mfumo wa elimu unaotukuza pass marks na si uelewa ,
Watoto wapo busy kutafuta past papers na possible questions , unapataje experts kwa mtindo kama huo? Watu wanakariri na kufaulu imeisha hiyo.
Kukariri ndiyo msingi wa kuelewa. Kwa maana hiyo huwezi kuelewa bila kukariri
 
Kukariri ndiyo msingi wa kuelewa. Kwa maana hiyo huwezi kuelewa bila kukariri
Ndio sababu Tanzania hatuna uvumbuzi, ukishakariri tayafi umeshajifungia kwenye duara na hutotoka humo I kamwe..
 
Asante sana mkuu
 
Hongera sana mtoa Mada, haya sasa tuendelee kusoma uzi mwingineee..."- Anna Makinda Voice.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…