Wamiliki wengi wa majokofu/friji wanauelewa mdogo juu ya utendaji kazi wake

Wamiliki wengi wa majokofu/friji wanauelewa mdogo juu ya utendaji kazi wake

Hapo uwezekani ni huo kwamba wanajua kuna mvujo ila hawako tayari kupoteza ulaji hivyo hawatokwambia ukweli ili arudi tena na tena.
 
Hongera mtoa mada

Ila kuna vitu umechanganya kidogo

Uhalisia ni kwamba

Gesi ikitoka kwenye compresor huwa inashika joto so direct inapitishwa kwenye condensor ili ipoozwe na hata ikipoozwa haiwi na ule ubaridi kabisa, ubarid unatokea kwenye expansion valve

Expansion valve inaletaje ubaridi?

Natolea mfano wa perfume, ukijipulizia perfume kuna kaubaridi fulan huwa unakapata na kale kaubaridi kanazalishwa na ile valve unavyoibonyeza pale ili kujispray, same same to refrigeration system expansion valve ndiyo inazalisha ubarid kwa kuspray freon gas kabla haijaingia kwenye evaporator.

Mengine upo sawa ila hapo tu ndo ulichanganya mtoa mada
Na we pia unachanganya, kazi ya expansion valve ni kupunguza ukubwa wa pipe ambayo gesi inapita ili kuiongezea pressure na sio kwamba expansion valve ndio inatia ubaridi....

Valve ile inafinya tu pipe ili gesi itoke ikiwa na pressure.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa mtoa mada, ila lengo langu nilitaka ujue kitu unachokichanganya, i hope hii kitu umeitoa darasani ila haya mambo kila siku huwa nadili nayo.

Ubard unazalishwa kwenye expansion valve hapa inabd ukubali tu mtoa mada hata kama huelewi ww meza kama lilivyo.

Kuna mengi kwenye hizi system
Sio kweli... Expansion valve haizalishi ubaridi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio sababu tunazisitiza elimu isiwe ya kukariri ili tupate wataalam wazuri , nimemsoma mtoa mada vizuri sana , anajua na kujitahidi , ila kuna vitu unaona kabisa kavimeza kama vilivyo , na hawezi tena kutoka nje ya hiyo knowledge cycle ,
Ubaridi kwenye freezer na fridge unaaznia kutoka kwenye expansion valve ,
Sio kweli..... We fuatilia utagundua..

Gas inafika kwenye valve ikiwa ya baridi... Valve inafinya tu kuiongezea pressure.

Ila sio inaipa ubaridi... Bali wewe ndio unaanza kuuona ubaridi pale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unless iwe ni hizi za mtumba ambazo zime njungwq jungwa na thermostat au timer haifanyi kazi...

Ipo hizi any refrigeration system ina kitu kinaitwa thermostat... Thermostat ina monitor temperature ya evaporator ambapo ndipo baridi utokea.. sasa kwenye fridge kuna knob ya kuchagua temperature unayotaka compartment yako iwe nayo.. mfano unataka compartment ya freezer iwe na temperature ya 3°c.. maana yake uta set ile thermostat to that temperature.. so compressor itafanya kazi mpaka ile temperature ifikiwe.. then ikifikiwa compressor itazima yenyewe.. then joto likipanda mfano to 4°c compressor itawaka tena ku maintain ile temperature..

Sasa hapa kwenye fridge kuna frost na non frost...

Sasa kwa fridge za non frost huwa zinakua na evaporator ambayo inakua ndani then kunakua na feni inayopuliza ule ubaridi wa evaporator kuja vitu vilivomo ndani ya fridge kuvigandisha.. sasa changamoto ya hapa ni kwamba kuna muda hii fridge hujaa barafu so kutoa hii changamoto fridge huwa zinakua na heater na timer, na sensors ya kuzuia ku trigger heater iwake. So timer inakua na circle ya kuwasha Heater ili kuyeyusha barafu inayokua imejaa kwenye evaporator ili evaporator isi restrict airflow, lakini pia mfano kipindi cha baridi kama hivi sasa kwakua joto si kubwa fridge huwai kutengeneza barafu kwenye evaporator kabla ya circle ya timer kuanza kazi, so hapa ile sensor ya ku ditect frost kwenye evaporator coil huzimisha compressor na kuwasha Heater ili kuyesha ile barafu... So hivo ndivo fridge hufanya kazi (but hizi ni kwa non frost fridges) kwa frost fridges (nyingi ni za kizamani) kidogo working principals zinautofauti kidogo hasa upande wa evaporator.. yenyewe evaporator yake unakuta ni part kitako mahala vitu vinakaa, na zingine unakuta kuna pipe zimepita ndani .

So to conclude ni kwamba hakuna shida fridge kuiacha kwenye umeme na by the way ndivo inavotakiwa iwe.. kwakua ukizima fridge ukaiwasha baadae fridge itakula umeme mwingi kwakua it will work harder kufikia temperature ile ulii set kwenye knob yake.. but ukiacha kwenye umeme, fridge itakua inafanya kazi ya ku-mantain temperature tu. So itawaka kidogo na kuzima yenyewe.. na circle itaendelea.

Ila ikitokea thermostat imekufa basi fridge itafanya kazi muda mwingi bila kuzima na haitakua na mechanisms ya ku control temperature.. na ikitokea na sensor ya Frost direction imekufa au timer imekufa situation ndo itakua worse kwakua after sometime fridge itajaza barafu na ita perform vibaya hasa kama fridge ni non frost... Lakini pia kumbuka refrigeration kwakua inafanya kazi on principles of pressure difference between low side and high pressure ... So evaporator ikiwa na barafu sana itafanya low pressure ipungue sana nakufanya gas inayotakiwa irudi kwenye compressor ili iwe compressed isiwepo au iwe ndogo sana so compressor inaweza ku overheat na kufa kwakua hakuna enough cold refrigerant inayo rudi kupoza compressor... Na ndo maana ukiangalia AC system ya gari inakua na sensors/switch inayo monitor pressure ya low na high side kwamba pressure zikiwa out of range (both sides yaan low au high) basi the system shuts off to protect itself.

So ndo hivo.. sorry nimejibu kirefu kidogo japo system ina mambo kidogo..
Nina fridge hicense dogo mlango mmoja juu linagandisha chini ndio ile kawaida...

Ninapoishi kuna tatizo la umeme mdogo nikawa nalitumia bila fridge guard.

Baadae nikanunua guard shida ni hii sasa

Nyakati za mchana umeme unakuwa vizuuur lakini fridge inaweza ikawaka sometime inazima lakini guard inaonesha umeme upo stable na ikizima inapoooza kabisa ukifungua vitu vyoote vimeyeyuka...

Yaani naweza nikaliacha on siku nzima umeme upo safi ila unakuta maji tu ndani ambayo imegandisha na ikayeyusha.. lakini kitambo ilikuwa ukiacha masaa 12 vitu unakuta jiwe na usiku unazima unaiwasha teena asubuh ipo safi.

Usiku huwa naizima kutokana na umeme unakuwa mdogo inashindwa kusukuma mzigo.

Sollution yake ni nin hii mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio kweli..... We fuatilia utagundua..

Gas inafika kwenye valve ikiwa ya baridi... Valve inafinya tu kuiongezea pressure.

Ila sio inaipa ubaridi... Bali wewe ndio unaanza kuuona ubaridi pale

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ile inaitwa expansion valve!! Anzia hapo kwanza ndo tuendelee !
Exapansion maana yake ni kutanuka , na ndo hapo gas huwa inatoa ubaridi.
Halafu kwenye expansion valve gas haiongezwi pressure bali inapunguzwa pressure,
Ile hissing sound unayoisikia ndani ya jokofu ni freon inakuwa expanded .
 
Na we pia unachanganya, kazi ya expansion valve ni kupunguza ukubwa wa pipe ambayo gesi inapita ili kuiongezea pressure na sio kwamba expansion valve ndio inatia ubaridi....

Valve ile inafinya tu pipe ili gesi itoke ikiwa na pressure.



Sent using Jamii Forums mobile app
Haya ndio madhara ya kikariri , muwe mnasoma na kuelewa wazee sio kukariri. mwishowe tutaonekana tuna madharau !!!

Kinachoongeza freon pressure kwenye system ya jokofu au kiyoyozi ni compressor peke yake , baada ya kutoka kwenye compressor gas hiyo hupelekwa kwenye condenser ili ipoteze joto bila kupungua pressure then itaingia kwenye expansion valve kwa ajili ya kutoa ubaridi, baada ya hapo kunaanza cycle nyingine ya compreasion.
 
Pia kama una AC, hapa panakuhusu.

Twende moja kwa moja kwenye mada. Watu wengi tunamiliki majokofu au friji lakini tunauelewa mdogo juu ya utendaji wa hichi kifaa. Kimsingi, kama mtumiaji hautakiwi kuwa na uelewa sana juu ya utendaji wa jokofu lako. Wataalamu au mafundi wanaohudumia jokofu lako wakati wa matatizo ndio wanatakiwa wawe na uelewa na wakupe miongozo mbalimbali juu ya kifaa chako. Kwa bahati mbaya sana, mafundi wengi wa majokofu hawana uelewa huo. Hapa ndipo tatizo linapoanzia na kukulazimu mmiliki wa jokofu uwe na ABC fulani juu ya kifaa chako, kitu ambacho si cha lazima sana. Na hapo ndipo nilipoona kuna haja ya kuleta kwenu uzi huu.

Kiini cha uzi huu ni kuhusu tatizo la ujazaji wa gesi kwenye majokofu yetu Pamoja na AC za majumbani kwetu.

Ili tuweze kuelewana vizuri, naomba nielezee jinsi mfumo wa upoozaji ndani ya jokofu unavyofanya kazi.

Kimsingi mfumo wa upoozaji kwenye jokofu lako una sehemu kuu kama tatu hivi. Yaani COMPRESSOR, CONDENSER, NA EVAPORATOR.

Compressor kazi yake ni kuisukuma gesi iweze kuzunguka kwenye mfumo wa upoozaji. Inaisukuma gesi kwenda kwenye EVAPORATOR, ikitoka kwenye EVAPORATOR inaenda kwenye CONDENSER na kurudi tena kwenye COMPRESSOR, mzunguko unaanza tena na kuendelea. CONDENSER na EVAPORATOR ni mirija au tube katika muundo wa zigizaga zilizotengenezwa kwa shaba au malighafi nyingine yoyote inayoweza kubadilishana jotoridi kwa wepesi kama kielelezo cha mchoro kinavyoonyesha hapo chini.

View attachment 2278705
Wakati gesi inafanya mzunguko au inazungushwa kati ya CONDENSER na EVAPORATOR ndipo inapofanya upoozaji. EVAPORATOR huwa iko ndani ya jokofu, yaani mule kwenye kabati ya baridi. CONDENSOR huwa nje ya jokofu upande wa nyuma. Gesi wakati inazunguka, ikipita kwenye EVAPORATOR inachukua lile joto na kwenda nalo nje kwenye CONDENSOR. Ikifika kwenye CONDENSOR inaliachia lile joto na gesi kuwa imepoa, inarudi tena kwenda kukusanya joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Kwa gesi kufanya mzunguko huo na kazi ya kutoa joto ndani ya jokofu, ndani ya jokofu hubaki na ubaridi. Hapo chini kuna kielelezo cha picha
kikionyesha jinsi mpangilio wa COMPRESSOR, EVAPORATOR, na CONDENSER unavyokuwa kwenye jokofu.



View attachment 2278707

GESI

Tumeona kwamba, gesi kwenye jokofu kazi yake ni kuzunguka, kuchukua joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Inasukumwa kurudi ndani kuchukua tena joto kupitia EVAPORATOR, inakujanalo nje na kuliachia kupitia CONDENSER.

TAMBUA

Katika hali ya kawaida, gesi katika jokofu lako haitakiwi kuisha. Tumeona hapo juu jinsi gesi inavyofanya kazi ndani ya jokofu lako. Haiungui kama mafuta ya gari tuseme kwamba inaisha. Gesi ipo kwenye mzunguko wa mduara ambao umefungwa na hufanya kazi kupitia mirija kama tulivyoelezana hapo juu. Yaani unaweza ukazaliwa mpaka unazeeka, jokofu lako likawa linapoza kama kawaida. Na bahati mbaya sana mafundi wengi wa mifumo ya kupooza hawajui kwamba gesi haitakiwi kuisha katika hali ya kawaida.

Sababu moja kubwa ya kuisha gesi kwenye jokofu ni kuvuja kwa gesi. Pale ambapo kunakuwa na tundu kwenye mfumo wa mzunguko wa gesi na gesi kuanza kuvuja.

Kwanza fundi anatakiwa atatue tatizo la kuvuja kwa gesi ndipo ajaze gesi kwenye kifaa chako. Tofauti na hapo anakupa suluhu ya muda mfupi tu kwa kujaza gesi bila kuzuia kuvuja. Baada ya muda mfupi utamtafuta akujazie tena gesi. Kisheria huu ni wizi. Yawezekana wanafanya makusudi, inawezekana pia hawajui kwamba lazima kutakuwa na tatizo la gesi kuvuja sababu katika hali ya kawaida gesi haitakiwi kuisha. Pia inawezekana fundi anajua ila hataki kujisumbu. Au anajua ila anauhakika hutamlipa gharama za kutafuta leakage au panapovuja.

Kama una jokofu lako ambalo unajaza gesi kila baada ya muda Fulani, sasa ni wakati wa kulitengeneza na kuzuia kuvuja ili kuepuka gharama zisizo za lazima. Fundi anatakiwa atafute gesi inapovujia, adhibiti hiyo sehemu. Baada ya hapo atafanya majaribio ya kuhakiki kama mfumo hauna sehemu inayovujisha gesi. Jaribio hilo atalifanya kabla ya kujaza gesi. Na jaribio hilo la kuhakiki afya ya mfumo linaitwa ‘pressure test’. Baada ya kufanya pressure test na kujiridhisha afya ya mfumo wa upoozaji, atafanya ‘vacuum’. Hapa ataondoa hewa iliyoingia kwenye mfumo wa upoozaji. Sababu baada ya gesi kuvuja na kuisha, hewa ya kawaida huchukua nafasi na kuingia kwenye mfumo. Hii hewa haitakiwi. Endapo gesi itajazwa bila kutoa hewa iliyoingia, ufanisi wa gesi kupooza utapungua na utashangaa kwamba jokofu langu sikuhizi halipoozi vizuri. Ni kama mafuta ya gari uchanganye na kimiminika kingine. Lazima ufanisi wa mafuta utapungua. Ndani ya mfumo wa kupooza inatakiwa iingie gesi peke yake ili ifanye kazi kwa ufanisi wa juu.

Katika pitapita yangu na kukutana na mafundi wa mifumo ya kupooza, sikumbuki kumuona fundi ana ‘vacuum pump’. Yaani pump au kifaa cha kuondolea hewa kwenye mfumo wa kupooza wa jokofu au AC.

Nawatakia upambanaji mwema.



Wakatabahu

Infopaedia
nilizan ww ni fund boss maana nilitaka musaada wako
 
Nina fridge hicense dogo mlango mmoja juu linagandisha chini ndio ile kawaida...

Ninapoishi kuna tatizo la umeme mdogo nikawa nalitumia bila fridge guard.

Baadae nikanunua guard shida ni hii sasa

Nyakati za mchana umeme unakuwa vizuuur lakini fridge inaweza ikawaka sometime inazima lakini guard inaonesha umeme upo stable na ikizima inapoooza kabisa ukifungua vitu vyoote vimeyeyuka...

Yaani naweza nikaliacha on siku nzima umeme upo safi ila unakuta maji tu ndani ambayo imegandisha na ikayeyusha.. lakini kitambo ilikuwa ukiacha masaa 12 vitu unakuta jiwe na usiku unazima unaiwasha teena asubuh ipo safi.

Usiku huwa naizima kutokana na umeme unakuwa mdogo inashindwa kusukuma mzigo.

Sollution yake ni nin hii mkuu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Suluhisho iltakiwa upate fridge za lg au samsung zenye linear compressors na digital inverter, hizi hazihitaji fride guard maana zinatembea hata imeme ukiwa 100 volts , ni ghali sana though ila ni bora .
Linear compressors are known to have very few friction points, thus very efficient ,ndo maana huwa zina warranty ya hadi maika 15 .
 
Pole sana kiongozi, bahati mbaya sipo huko kwa sasa halafu pia sifanyagi kazi za individual. Ila naweza kukusaidia kutambua leakage

Fanya hiv

Chukua maji weka kwenye ndoo kisha changanya na sabuni (napendekeza ya unga kwasabab ya povu).

Ukishachanganya hakikisha unapata povu jingi.
Pia tafuta sponji au kipande cha godoro.

Washa friji lako na hakikisha compresor inafanya kazi.

Baada ya kuwasha sasa unaweza kuanza kazi ya kuitafuta hiyo leakage

Unachukua lile povu kwa sponji halafu unalikamulia kwenye viungio vyote bila kusahau ile sehem unayoingizia gesi.

Ukishakamulia lile povu kama kuna leakage lazima itaonekana.

Kwa msaada zaid ingekua vema uniambie huwa unaona dalili zipi mpaka unamuita fundi akujazie gesi (mafundi wetu muda mwingne sio waaminifu).

Ref na chiller huwa zina matatizo mengi na mengine yanataka kufanana dalili hivyo ni venga ungefunguka kodogo nikuambie wapi ukaguse kwenye friji lako
mi nisaidie mkuu!,, jokof langu linapiza kwa halaka sana upande wa frizer ni kuanzia 15min na kuendelea ila upande wa chin ina chukua mda mrefu kuanzia 1:30hr mpk 2 hr na hapa inakuwa imepoza kawaida tu yani ubarid kawaida sana,, unanisaidiaje hapa boss,, nina aina ya( HOME BASE)nipo chato
 
Haya ndio madhara ya kikariri , muwe mnasoma na kuelewa wazee sio kukariri. mwishowe tutaonekana tuna madharau !!!

Kinachoongeza freon pressure kwenye system ya jokofu au kiyoyozi ni compressor peke yake , baada ya kutoka kwenye compressor gas hiyo hupelekwa kwenye condenser ili ipoteze joto bila kupungua pressure then itaingia kwenye expansion valve kwa ajili ya kutoa ubaridi, baada ya hapo kunaanza cycle nyingine ya compreasion.
Samahani kama nitakosea mimi sio fundi. Ila kimsingi hakuna gesi inayotoa ubaridi duniani. Joto linakawaida kusafiri kutoka ambako lipo kubwa kwenda kwenye joto dogo kutengeneza "thermal equilibrium ". Kitendo hiko kikiendelea itafika hali ambayo joto la gesi ni sawa na joto la kwenye friji..

Ndio maana kuna mdau aliuliza kama anaweza kutumia friji kama AC? Akajibiwa inawezekana ila umeme utahitajika mwingi. Sababu ni hiyohiyo hewa ya chumba kizima inahitaji kugusa sehemu yenye ubaridi .
 
Samahani kama nitakosea mimi sio fundi. Ila kimsingi hakuna gesi inayotoa ubaridi duniani. Joto linakawaida kusafiri kutoka ambako lipo kubwa kwenda kwenye joto dogo kutengeneza "thermal equilibrium ". Kitendo hiko kikiendelea itafika hali ambayo joto la gesi ni sawa na joto la kwenye friji..

Ndio maana kuna mdau aliuliza kama anaweza kutumia friji kama AC? Akajibiwa inawezekana ila umeme utahitajika mwingi. Sababu ni hiyohiyo hewa ya chumba kizima inahitaji kugusa sehemu yenye ubaridi .
Mwanafunzi mtoro , hebu rejea kwenye somo la kemia kidato cha pili, sijui kama mtaala wa sasa wanasoma hivyo ili sisi tulisoma
Freon inayowekewa kwenye ac na fridge ina tendency ya kutoa baridi inaporudi kwenye ground au natural state.
Compressor inachodanya ni kuzibana gas molecules na kuzifanya kuwa katika exiced states ndo maana gas hii hupata joto kali , expansion valve sasa hufanya kinyume , kuzitoa freon katika excited state na kuirudisha katika natural state , hapa ndo freon hutoa baridi
Cooling system kiufupi ni kwamba scientist walichunguza tabia za freon wakachukua faida zake kutengeneza baridi
 
Pia kama una AC, hapa panakuhusu.

Twende moja kwa moja kwenye mada. Watu wengi tunamiliki majokofu au friji lakini tunauelewa mdogo juu ya utendaji wa hichi kifaa. Kimsingi, kama mtumiaji hautakiwi kuwa na uelewa sana juu ya utendaji wa jokofu lako. Wataalamu au mafundi wanaohudumia jokofu lako wakati wa matatizo ndio wanatakiwa wawe na uelewa na wakupe miongozo mbalimbali juu ya kifaa chako. Kwa bahati mbaya sana, mafundi wengi wa majokofu hawana uelewa huo. Hapa ndipo tatizo linapoanzia na kukulazimu mmiliki wa jokofu uwe na ABC fulani juu ya kifaa chako, kitu ambacho si cha lazima sana. Na hapo ndipo nilipoona kuna haja ya kuleta kwenu uzi huu.

Kiini cha uzi huu ni kuhusu tatizo la ujazaji wa gesi kwenye majokofu yetu Pamoja na AC za majumbani kwetu.

Ili tuweze kuelewana vizuri, naomba nielezee jinsi mfumo wa upoozaji ndani ya jokofu unavyofanya kazi.

Kimsingi mfumo wa upoozaji kwenye jokofu lako una sehemu kuu kama tatu hivi. Yaani COMPRESSOR, CONDENSER, NA EVAPORATOR.

Compressor kazi yake ni kuisukuma gesi iweze kuzunguka kwenye mfumo wa upoozaji. Inaisukuma gesi kwenda kwenye EVAPORATOR, ikitoka kwenye EVAPORATOR inaenda kwenye CONDENSER na kurudi tena kwenye COMPRESSOR, mzunguko unaanza tena na kuendelea. CONDENSER na EVAPORATOR ni mirija au tube katika muundo wa zigizaga zilizotengenezwa kwa shaba au malighafi nyingine yoyote inayoweza kubadilishana jotoridi kwa wepesi kama kielelezo cha mchoro kinavyoonyesha hapo chini.

View attachment 2278705
Wakati gesi inafanya mzunguko au inazungushwa kati ya CONDENSER na EVAPORATOR ndipo inapofanya upoozaji. EVAPORATOR huwa iko ndani ya jokofu, yaani mule kwenye kabati ya baridi. CONDENSOR huwa nje ya jokofu upande wa nyuma. Gesi wakati inazunguka, ikipita kwenye EVAPORATOR inachukua lile joto na kwenda nalo nje kwenye CONDENSOR. Ikifika kwenye CONDENSOR inaliachia lile joto na gesi kuwa imepoa, inarudi tena kwenda kukusanya joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Kwa gesi kufanya mzunguko huo na kazi ya kutoa joto ndani ya jokofu, ndani ya jokofu hubaki na ubaridi. Hapo chini kuna kielelezo cha picha
kikionyesha jinsi mpangilio wa COMPRESSOR, EVAPORATOR, na CONDENSER unavyokuwa kwenye jokofu.



View attachment 2278707

GESI

Tumeona kwamba, gesi kwenye jokofu kazi yake ni kuzunguka, kuchukua joto ndani ya jokofu na kulileta nje na kuliachia. Inasukumwa kurudi ndani kuchukua tena joto kupitia EVAPORATOR, inakujanalo nje na kuliachia kupitia CONDENSER.

TAMBUA

Katika hali ya kawaida, gesi katika jokofu lako haitakiwi kuisha. Tumeona hapo juu jinsi gesi inavyofanya kazi ndani ya jokofu lako. Haiungui kama mafuta ya gari tuseme kwamba inaisha. Gesi ipo kwenye mzunguko wa mduara ambao umefungwa na hufanya kazi kupitia mirija kama tulivyoelezana hapo juu. Yaani unaweza ukazaliwa mpaka unazeeka, jokofu lako likawa linapoza kama kawaida. Na bahati mbaya sana mafundi wengi wa mifumo ya kupooza hawajui kwamba gesi haitakiwi kuisha katika hali ya kawaida.

Sababu moja kubwa ya kuisha gesi kwenye jokofu ni kuvuja kwa gesi. Pale ambapo kunakuwa na tundu kwenye mfumo wa mzunguko wa gesi na gesi kuanza kuvuja.

Kwanza fundi anatakiwa atatue tatizo la kuvuja kwa gesi ndipo ajaze gesi kwenye kifaa chako. Tofauti na hapo anakupa suluhu ya muda mfupi tu kwa kujaza gesi bila kuzuia kuvuja. Baada ya muda mfupi utamtafuta akujazie tena gesi. Kisheria huu ni wizi. Yawezekana wanafanya makusudi, inawezekana pia hawajui kwamba lazima kutakuwa na tatizo la gesi kuvuja sababu katika hali ya kawaida gesi haitakiwi kuisha. Pia inawezekana fundi anajua ila hataki kujisumbu. Au anajua ila anauhakika hutamlipa gharama za kutafuta leakage au panapovuja.

Kama una jokofu lako ambalo unajaza gesi kila baada ya muda Fulani, sasa ni wakati wa kulitengeneza na kuzuia kuvuja ili kuepuka gharama zisizo za lazima. Fundi anatakiwa atafute gesi inapovujia, adhibiti hiyo sehemu. Baada ya hapo atafanya majaribio ya kuhakiki kama mfumo hauna sehemu inayovujisha gesi. Jaribio hilo atalifanya kabla ya kujaza gesi. Na jaribio hilo la kuhakiki afya ya mfumo linaitwa ‘pressure test’. Baada ya kufanya pressure test na kujiridhisha afya ya mfumo wa upoozaji, atafanya ‘vacuum’. Hapa ataondoa hewa iliyoingia kwenye mfumo wa upoozaji. Sababu baada ya gesi kuvuja na kuisha, hewa ya kawaida huchukua nafasi na kuingia kwenye mfumo. Hii hewa haitakiwi. Endapo gesi itajazwa bila kutoa hewa iliyoingia, ufanisi wa gesi kupooza utapungua na utashangaa kwamba jokofu langu sikuhizi halipoozi vizuri. Ni kama mafuta ya gari uchanganye na kimiminika kingine. Lazima ufanisi wa mafuta utapungua. Ndani ya mfumo wa kupooza inatakiwa iingie gesi peke yake ili ifanye kazi kwa ufanisi wa juu.

Katika pitapita yangu na kukutana na mafundi wa mifumo ya kupooza, sikumbuki kumuona fundi ana ‘vacuum pump’. Yaani pump au kifaa cha kuondolea hewa kwenye mfumo wa kupooza wa jokofu au AC.

Nawatakia upambanaji mwema.



Wakatabahu

Infopaedia
Tunaomba address ama mawasiliano yako binafsi nina hitaji huduma makini kama hii
 
Mwanafunzi mtoro , hebu rejea kwenye somo la kemia kidato cha pili, sijui kama mtaala wa sasa wanasoma hivyo ili sisi tulisoma
Freon inayowekewa kwenye ac na fridge ina tendency ya kutoa baridi inaporudi kwenye ground au natural state.
Compressor inachodanya ni kuzibana gas molecules na kuzifanya kuwa katika exiced states ndo maana gas hii hupata joto kali , expansion valve sasa hufanya kinyume , kuzitoa freon katika excited state na kuirudisha katika natural state , hapa ndo freon hutoa baridi
Cooling system kiufupi ni kwamba scientist walichunguza tabia za freon wakachukua faida zake kutengeneza baridi
Mkuu samahani kama nakukwaza . Lakini tangu nausoma uzi ni wewe na buzitata ndio nimewaona mmelielezea friji kwa 100% kuliko mleta mada. Shida yangu nami nilitaka mtumie maelezo sahihi katika kila hatua kama mlivyomtaka meta mada.
Kifupi tusiseme ile gesi inatoa ubaridi bali tuseme gesi ya baridi ina nyonya au kusharabu au kufyonza joto la ndani ya friji. Sasa tukisema linafyonza joto ndio mtu asiyejua chochote kuhusu friji ataelewa kwanini haitakiwi kuacha wazi mlango wa friji.

NB: Natambua ujuzi wako uliopevuka kwenye hivii vifaa
 
Na we pia unachanganya, kazi ya expansion valve ni kupunguza ukubwa wa pipe ambayo gesi inapita ili kuiongezea pressure na sio kwamba expansion valve ndio inatia ubaridi....

Valve ile inafinya tu pipe ili gesi itoke ikiwa na pressure.



Sent using Jamii Forums mobile app
Nilitaka nikujibu ila najikuta roho inakataa sijui kwann . Ila jaribu hata kugoogle mkuu
 
Na we pia unachanganya, kazi ya expansion valve ni kupunguza ukubwa wa pipe ambayo gesi inapita ili kuiongezea pressure na sio kwamba expansion valve ndio inatia ubaridi....

Valve ile inafinya tu pipe ili gesi itoke ikiwa na pressure.



Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hapa kuna issue kidogo... Kuna expansion valve, kuna capillary tube, kuna Orifice tube hizi zote zinafanya kazi moja but expansion valve kidogo yenyewe ina advance kwakua inakua ina regulate passage ya refrigerant kutegemeana na temperature.. na ndo maana inakua na kichwa flan hivi na kimkia hivi pamoja na pin hii inavofanya kazi ni kwamba siku joto linapokua kubwa maana yake ni kwamba more refrigerant inahitajika kuingia kwenye evaporator ili kutengeneza baridi kubwa na kwa haraka ili ku overcome heat load.. na panapo kua hakuna joto kabwa, basi expansion ita expand kidogo (itafunguka kidogo) kuruhu gas kiasi ya baridi kuingia ndani ya evaporator ili kupoza compartment ya fridge yako..

Expansion valve ni kama ule mdogo wa perfume unavofanya kazi.. kwakua ndani ya perfume kuna kua na compressed fluid, lle fluid ikiwa released kupitia kamdomo kadogo ile perfume itatoka kwenye liquid format na kutoka kama gas na itakua ya baridi.. sasa hivi ndivo pia expansion valve inavofanya kazi.. baada ya gas kutoka kwenye condenser hufika kwenye metering device (inaweza kua expansion valve, au orifice tube, au capillary tube depending on the system design but same working principles) gasi ikifika hapa itabana na kupita kwa kitundi kidogo sana.. so hapa pressure ya gas will change gafla from high pressure to low pressure na ile liquid refrigerant itachange to gaseous form na temperature ita drop significantly... Na ndipo ubaridi hutokea... Sasa huu ubaridi unakusanywa sehemu moja ili kua na larger surface for heat exchange (surface hii ndo tuna iita evaporator mkuu) so evaporator ikisha absorb temperature ile gas itarudi kwenye compressor kwa ajili ya mzunguko tena..


Bonus hint:
Compressor za Ac, fridge zipo designed ku compress Freon (refrigerant) in gaseous form and not in liquid form... U
So wakati wa kujaza gas ukijaza gas in liquid form uta hydro-lock compressor na kuiua..

ni kama enjini ya gari, ikiingiliwa maji na ika compress yale maji basi injini inaweza pasuka au ikakunja mkono wa piston kwakua maji ni non compressible, but only air is compressible.
 
Back
Top Bottom