Wanajeshi wa Tanzania takribani 2000 walifyekwa na majeshi ya Idd Amin; huo ndio ulikuwa mwanzo wa vita ya Kagera

Wanajeshi wa Tanzania takribani 2000 walifyekwa na majeshi ya Idd Amin; huo ndio ulikuwa mwanzo wa vita ya Kagera

Hawakuwa wanajeshi waliopata mafunzo,waliopelekwa kwanza,walikuwa wanamgambo na wananchi waliopewa crush program ya mapambano,kwa muda mfupi,ndio wakapelekwa mstari wa mbele,ungekuwa msomaji mzuri wa historia,hili jambo limeelezwa vzr kwenye filamu ya vita ya Kagera,mpaka majarida mbalimbali yanayopatikana hata kwenye maktaba ya Taifa,mimi nalifahamu hili tangu mwaka 1996,
Usishinde kwenye whatsaap tu,kasome vitabu,
Muulize mpiganaji yyte aliye kuwa ktk kikosi kilichoelekea Lukaya na kikapigana huko atakusimulia,
Pale ndo ilikuwa vita
 
Mambo ya jeshi waachieni wanajeshi,,,, simulizi ndio nini hasa,,,,,, yaani wanajeshi 2000 ni zaidi ya battalion mbili,,,, unajua chochote wewe?
Kwani risasi huwa zinaogopa kuua watu wakiwa wengi?
 
Watu 2000 wana wa nchi waliuawa kikatili na jeshi la Uganda kwa msaada wa Gaddafi.

Halafu leo watu wanamsifia Gaddafi eti mzalendo, kiongozi bora wa Africa.

Inatia kichefuchefu.
Wajinga hao mkuu
 
Umefichwa na nani? au wewe ni Mento? inamaana ulifichwa na baba yako au nani haswa maana vita ya Uganga hadi sinema halisi zilihusika.. Waliofyekwa walikuwa ni Jeshi la Mgambo na hii ipo wazi kabisa ukisoma habari za vita ya uganda sasa unaleta takwimu zako za kipumbavu pumbavu ati ulifichwa au hujawahi sikia hata sikukuu ya Mashujaa waliopoteza uhai wao katika Vita hiyo ya Kagera? Kwa Taarifa yako waliuwawa na Wanajeshi wa Palestina waliokuja kumtetea Amin Ndio maana Siwapendi Wapalestina natamani wafutwe kabisa Duniani. Wana bahat sana Nyerere aliwasamehe
Hakuna snema halisi 100%
Acha utoto
La waparestina nakuunha mkono
 
hao BBc ambao walikuja kuomba radhi kwa kupotosha wakati wa vita vya Irak sio kila kitu wanachosema bbc ni sahihi wakati mwingine jaribu kufanya utafiti
 
Habari kwenu jukwaani.

Kuna simuluzi BBC Radio wanatujuza historia iliyofichwa. Mwanzoni mwa vita vya Kagera ni kuwa baada ya Amini kufanya uvamizi wake, Tanzania ilitanguliza kikosi cha wanajeshi 2000 mstari wa mbele na chote kilifyekwa na majeshi ya Amin.

Baada ya hapo jeshi letu lilijipanga upya na kusonga mbele hadi Kampala na Jinja ambapo Idd Amin alitimkia Libya na baadae Saudi Arabia.

Hii historia sijiwahi kuisikia, nilijua tulipigana bila upinzani mkali na hatukupoteza askari wengi kiasi hiki kwa mpigo mmoja.

Msimuliaji pia anadai jeshi la Uganda lilikuwa limegawanyika sana kwani baadhi hawakumtaka Amin aendelee kuongoza Uganda na hivyo kulisaidia jeshi letu lililojipanga upya kushinda vita hivyo.

Viva JWTZ.
Ulikuwepo? Wakati vita inakoma tulipewa takwimu ya wanajeshi mia tatu tu. Wengi wapo pale kaboya, na wwngine walifariki kwa ajali wapo pale mutukula.
Sasa idadi unaipataje bila kujua nchi ilideploy wanajeshi wangapi na waliorudi wangapi.
 
AISEEE KUMBE KUNA MENGI WANAFICHA KUHUSU VITA HII???!!!INAWEZEKANA HATA USHINDI HAUKUWA WA KISHINDO KAMA TUNAVYOAMINISHWA

Yaani tayari kuna watu wameshaaminishwa uzushi. Kweli chochote kitakachosemwa na mtu yeyote hata taahira kitapata watu watakaoamini ni kushabikia
 
Watu 2000 wana wa nchi waliuawa kikatili na jeshi la Uganda kwa msaada wa Gaddafi.

Halafu leo watu wanamsifia Gaddafi eti mzalendo, kiongozi bora wa Africa.

Inatia kichefuchefu.

Kwani Tanzania hawakusaidiwa? kwenye vita kila mtu atamsapoti wake wakaribu wanaofahamiana kwa muda ule. Mbona nyie mumewau waganda tele kwaio wao wasikupendeni pia? wasitake mashirikiano yoyote na nyie?
 
Watanzania watu wajinga sana. NA moja sifa ya mjinga ni kujiona yeye mwingi.

Hivi nani hajui kama tulisaidiwa na mataifa ya magharibi katika vita na Iddi Amini?
Hivi nani hajui kama mwanzo tulipigwa nyang'anya'ga?
Ila tukipewa ukweli hatukabali kabisa.
 
Habari kwenu jukwaani.

Kuna simuluzi BBC Radio wanatujuza historia iliyofichwa. Mwanzoni mwa vita vya Kagera ni kuwa baada ya Amini kufanya uvamizi wake, Tanzania ilitanguliza kikosi cha wanajeshi 2000 mstari wa mbele na chote kilifyekwa na majeshi ya Amin.

Baada ya hapo jeshi letu lilijipanga upya na kusonga mbele hadi Kampala na Jinja ambapo Idd Amin alitimkia Libya na baadae Saudi Arabia.

Hii historia sijiwahi kuisikia, nilijua tulipigana bila upinzani mkali na hatukupoteza askari wengi kiasi hiki kwa mpigo mmoja.

Msimuliaji pia anadai jeshi la Uganda lilikuwa limegawanyika sana kwani baadhi hawakumtaka Amin aendelee kuongoza Uganda na hivyo kulisaidia jeshi letu lililojipanga upya kushinda vita hivyo.

Viva JWTZ.

Wanajeshi 2000 kuuwawa siyo kweli kabisa, kwa sababu hiyo ingekuwa ni zaidi ya batallion moja ya wakati huo, na robo ya Brigade. Enzi hizo batallion moja ya JWTZ ilikuwa na askari 1800 tu kujumuisha na HQ COY ambayo haingeweza kwenda frontline, na Brigade ya Magaharibi ilikuwa na batallion kama tano tu; nazikumbuka Kaboya, Kiabakari, Mirambo, na nyingine kama mbili sizikukmbuki tena. Ila ni kweli kuwa hatua za mwanzo wa vita ile zilizoongongwa na Brigedia Himid, aliyekuwa Brigedi kamanda wa Magharibi wakati huo, zilikuwa si thabidti na zilisababisha wanajeshi wetu kuuwawa kwa kushtukizwa (ambush) hovyo hovyo; idadi kamili iliyouwawa kwa njia hiyo ni karibu platuni mbili au tatu hivi kutokea Batallion ya Kaboya, ambayo ni kama wapiganaji 250 tu. Hata hivyo ni kutokana na matukio hayo ndipo Brigedia Himid alipopata shinikizo la moyo na command yake kuchukulia na Kanali Kotta wati huo. Kama unamjua Faraja Kotta-mke wa Nyaradu, basi baba yake ndiye aliyechukua command ya West Brigade, na kuzuia mashambulio yoyote hadi plani kamili ya vita itoke Ngome pale Upanga. Plani ya vita ilipangwa na Kanali Lupogo, na tangu plani ikamilike na kuanza kutumika chini ya division tatu za kivita, siyo brigade tena, basi jeshi la Amini halikufurukuta kabisa. Kwanza ile Simba Batalion iliyokuwa Mbarara ilivurugwa kwa muda mfupi sana na kusababisha kiwewe kilichosababisha jeshi zima la Amini lisambaratika bila kujitetea kwa nguvu. Ni kweli baada ya vita yote kuisha, tulikuwa tumepoteza askari wengi takribani 2000 lakini hiyo ni sehemu ya matokeo ya vita pana iliyozunguka na kusababisha nchi nzima ya Uganda kutekwa.
 
Kwani Tanzania hawakusaidiwa? kwenye vita kila mtu atamsapoti wake wakaribu wanaofahamiana kwa muda ule. Mbona nyie mumewau waganda tele kwaio wao wasikupendeni pia? wasitake mashirikiano yoyote na nyie?
Wewe Mtanzania?
 
Back
Top Bottom