Siku hz nimekua mvivu kuandika ila tajitahidi.
Mtu ukiwa unaenda kariakoo mara Moja kufata mahitaji flan na kuondoka anahis kama kariakoo ili ufanye biashara inakutaka uwe na pesa nyingi kitu ambacho so kweli
Kuna watu kariakoo kama mawinga wana update zote za mchina au mchaga atashusha container lini atakachofanya yeye anawahi sample ambazo anaona zinatembea sana anaongea na wahusika anazuia kama katoni 70 au 100 then annapandisha Bei hata jero tu Kwa Kila sample ....hiii inataka uwe na connection nzuri ujue sample kabla haijafika store
Kuna anaingia kkoo anatafuta fremu yake anakua anauza Mali za watu, anachofanya yeye anakua anadesign order book ambayo inaweza kutoa mzigo store anakua analipwa Kwa commission eq kila pisi Moja 200
Kuna mwngn anatafuta tajiri huko china...then anakua anatumiwa mzigo yy anauza analipa taratibu hii wanaaply sana wahaya utakuta frame yake ina TV kapadesign anaweka picha nyingi alizopiga na viongozi wa kitaifa na wanajeshi wakubwa
Glenn
Wachache wanaingia kwa akili zao wanapambana mpaka wanatoboa
Kikubwa we fanya research jitose kua makini tafuta watu wakupe mbinu la sivyo utakuta frame yako itajaa leseni na vyeti kibao