Wanaume kuwa na tabia za kikekike ni janga linaloikumba Nchi yetu

Wanaume kuwa na tabia za kikekike ni janga linaloikumba Nchi yetu

Yaani wewe nishakuona una viukorofi vya chini chini unauma unapuliza , unauma unapuliza huku ukitabasamu...kimoto kikikaribia kuzima unakimwagia tumafuta twa taa halafu unakaa pembeni kujichekelesha chekelesha. Yaani...🔥🔥🔥
🤣🤣🤣🤣🤣🤣 kwanini joomooni!!
Yani niko kucheka hapa mpk machozi.

Nimeona Mtibeli ana dukuduku limemkaba anashindwa kufunguka vizuri kwa kuogopa hali ya usalama yasije kumkuta km ya HAMAS na Israel 😂😂😂
Sasa kamati ya ulinzi namuhakikishia usalama upo yeye awatapike live tyuu!!
 
Hii post imewanyanyapaa sana wanawake na kukuonesha wewe kuwa ni mtu mbaguzi wa kijinsia mwenye stereotypical misogyny.

Zaidi, imekuonesha kuwa unaamini sana katika gender stereotypes nyingi ambazo hazina msingi wowote katika ukweli na sayansi.

Nimeandika kwa mujibu wa kasumba iliyopo kwenye jamii. Ambayo inahizo Gender stereotypes, kwamba tabia na matendo haya ni yakike na hizi nizakiume.
Nikaeleza kuwa zile stereotypes ambazo zamani zilimfanya Mwanamke aonekane ni dhaifu kwa tabia, mitazamo na mienendo ndio hizohizo ambazo wanaume kumbe nasi tunazo.
 
Huu uzi mbona umekaa kama kudhalilisha wanawake

Zile tabia mbaya zisizofaa kwenye jamii umezinasibisha na wanawake

Umesema kweli katika mtazamo uliouchukulia.
Lakini kimsingi ungeenda mbele zaidi usingeshindwa kupata kile ambacho nimekieleza ambacho ndio kusudi la uzi huu
 
Jomba umeishiwa kabisa nondo za kushusha hapa JF? Huu uzi wako umejaa tu chuki kwa wanawake kana kwamba wao ndo wamiliki wa tabia mbaya. Acha hizo fikra za kibaguzi. Mwanaume kuhonga ni jambo la kawaida na ni la kiasili. Wakati Isaka anaenda kuposa kabla hata ya maongezi alimpa yule binti vito vya thamani. Kama wewe ni mhanga wa jambo lolote baya ulilowahi kufanyiwa na mwanamke samehe endelea na maisha. Kuandika nyuzi za kuonyesha chuki dhidi yao kunakufanya uonekane MWANAUME DHAIFU. Unavyosema mwanamke sio wa kulazimishwa ni kama vila unataka kukimbia majukumu yako kama mwanaume... TOKA HUKO KWENYE FIKRA ZA KIVULANA UJE KWENYE UANAUME.

Huwezi kuelewa haya mambo kama unakosa moja ya haya; Haki, upendo, akili na Ukweli.
Kumlazimisha mtu iwe ni mwanaume au mwanamke ni kosa na ukatili.

Kingine, kuhonga/Rushwa ni tabia za Watu washenzi ambao hufanya jambo kuvunja Haki za mtu/Watu wengine.

Huwezi mhonga Mwanamke anayekupenda na unayetaka kumuoa.
Elewa, huyo Isaka hajawahi kumhonga yeyote.

Kuhonga ni kutafuta upendeleo ambao haupo upande wako.
Kuhonga ni kujaribu kutumia nguvu ya ziada ili ukubaliwe. Jambo ambalo ni kinyume na Haki.

Huwezi elewa kile nikisemacho kama utafikiri chini ya kiwango.

Weka akilini pia, Mwanamke aliyehuru hawezi kukubali umhonge. Hizo fanyeni kwa wapuuzi
 
Nimeandika kwa mujibu wa kasumba iliyopo kwenye jamii. Ambayo inahizo Gender stereotypes, kwamba tabia na matendo haya ni yakike na hizi nizakiume.
Nikaeleza kuwa zile stereotypes ambazo zamani zilimfanya Mwanamke aonekane ni dhaifu kwa tabia, mitazamo na mienendo ndio hizohizo ambazo wanaume kumbe nasi tunazo.
Wapi?
 
Hii kugombea mademu ni asili ya kiumbe chochote cha kiume.

Kwenye maandiko kwenyewe Ibrahim alitaka kunyanganywa mke wake na mfalme...
Wewe unachanganya mambo kuna KUGOMBEA na KUMLINDA mpenzi wako ndani ya himaya yako

Mwanamume/mume huwa analinda mwanamke/mke wake asitoke kwenye himaya yake

Kugombea mademu ni akili ya kivulana sio uanaume
 
Back
Top Bottom