WARAKA: Maaskofu Katoliki waonya uminywaji wa demokrasia na uhuru wa vyombo vya habari nchini

Maaskofu wenyewe wamejiorodhesha mwisho wa waraka huo. Ni kweli ni authentic kutoka kwa Maaskofu Katoliki. Ni mara ya kwanza kwa Baraza la Maaskofu lenyewe kutoa waraka wenye ujumbe wa aina hii, yaani wenye kauli kali katika hali ya siasa ya nchi yetu. huko nyuma hizo nyaraka zilitolewa na Tume ya Haki na Amani ya Baraza hilo, ambayo husimamiwa na Askofu mmoja tu. Lakini hii ni kauli ya Maaskofu yote chini ya Rais wao, ambaye ndiye msemaji rasmi wa Kanisa Katoliki hapa Tanzania.
 
Ni kweli wengi tulikuwa tunashangaa iweje viongozi wa Makanisa wamekuwa kimya? mawazo mengi yalitolewa, yakiwemo kama haya ya kwako. Lakini basi kauli ndio imetoka, na ni kali haijawahi kutokea. siyo bure Serikali nayo inavuta pumzi kujiuliza ijibu vipi. la msingi ni kwamba kuna Historia imeandikwa hapa. Baraza la Maaskofu halijawahi kutoa kauli kali namna hii, tena kwa ngazi hii. hayo ni mambo muhimu. Kanisa limeshapiga mstari. tunasubiri viongozi wengine wa dini waungane na wakatoliki. kwa hiyo kuanzia sasa Serikali itatakiwa kujipanga inajieleza vipi kwa wananchi.
 
Hawa maaskofu wameshindwa kuhubiri siku hizi
wanapoikosoa serikali ndio huwa tunasema wameshindwa kuhubiri. Lakini wanapoisifia, tunafurahi wala hatuhoji mbona wanachanganya dini na siasa? Wanasiasa kutwa wanakwenda makanisani na wanatoa hotuba huko na kuomba waombewe. huwa wanafuata nini? Lakini basi, Siasa ni mfumo mzima wa maisha, huwezi kutofautisha na dini. cha kujiuliza ni je, wamesema kweli?
 
Sipati picha wangekuwa ma sheikh ndo wametoa waraka kama huu..wangeandamwa na tuhuma na vitishoo... dah
 

Kinga ni bora kuliko tiba,
Katika mtazamo wako unadhani huu Waraka unaweza kubadilisha chochote ndani ya nchi katika kipindi hiki ??
Mambo mengi sana yameharibika hapa nchini na madhara yake hatutayaona leo wala kesho lakini ni makubwa sana.
Huu waraka hauwezi kubadilisha kitu chochote wala lolote. Jiulize kama nyaraka za Kanisa Katoliki zingekuwa zinabadilisha uongozi basi Uongozi wa Awamu ya nne wa Rais Jakaya Mrisho Kikwete ungekuwa ulishabadilishwa muda mrefu sana maana kila kukicha kulikuwa na matamko makali ya Baraza la Maaskofu.

Sasa wao wamesubiri miaka miwili (2) imepita ndiyo wametoa waraka,
Watu walivyokuwa wanapotea, demokrasia inaminywa, uhuru wa mahakama unadharauliwa na kuminywa upinzani wao walikuwa wapi ?? Umeongelea kuungwa mkono na madhehebu mengine lakini umesahau kwamba Madhehebu mengine yalianza kukemea haya maovu mapema sana. Mbona Kanisa Katoliki halikuunga mkono hizi juhudi za madhehebu mengine ?? Halafu usisahau kwamba wakati Madhehebu mengine na baadhi ya maaskofu wa Katoliki wenye uchungu na nchi wanakemea na huu Uovu Askofu Pengo alikuwa anamkingia kifua Raisi Magufuli na kusema huu siyo msimamo wa Kanisa, nauliza leo hii kimewakuta nini kuja na huu waraka ??

NB: Unakumbuka Tanzania tulibakia sana hatua chache kufanya mapinduzi makubwa sana kwenye Mchakato wa Katiba miaka michache iliyopita ?? Hivi tukumbushane Madhehebu mengine yote yalivyokubali kusimama na wananchi ni nani aliyevuruga ile nguvu ya Umoja ?? Hawa Maaskofu wakiitwa Wanafiki na kufananishwa na Mafarisayo watakuwa wanaonewa kweli ?? Tafakari sana na Ukumbuke kwamba nyaraka za namna hii zinaweza kuwadanganya Watanzania wachache wasiojua lakini werevu wameshang'amua kwamba huku ni kufukuza upepo tu na kujisafisha mbele ya Umma kwamba siku yakitokea ya kutokea muwe na sababu ya kusema kwamba "Mbona na sisi tulikemea". Hii dhambi mnayoifanya dhidi ya roho za Watanzania karibia milioni 46 itawatafuna sanaa na Mungu wa Mbinguni anaona. Kama siyo leo mtajutia kesho!
 
Mkuu kwa Kanisa Katoliki, mkubwa ni mwenyekiti wa Baraza la Maaskofu kwa muda hubo sino Kardinali kama wengi wanavyodhani
Kwa kawaida mkuu akiwa kimya sana, na mdogo akawa ndio active zaidi, basi mdogo ndio huonekana mkuu. Na hata ukiangalia, utagundua kardinali ndio ambaye akiunguruma tu watu wanakaa sawa, sio Siri-kali tu, mpaka waumini wote.
 
Kuna watu ktk nyuzi kama hawatiagi mguu kabisa.
 
....Namsubiri yule mheshimiwa Alhadi mzee wa totoz ajitokeze tena kukemea viongozi wa dini kuingilia siasa.......
 
Sio rahisi kwani vinaitwa ''visakramenti'', kufungia ni kuingilia uhuru wa kuabudu!!!

Kwani mpaka sasa Uhuru wa kuabudu upo?Wale walioshiriki ibada huko Mufindi waliambiwa wasali haraka ili wakampokee Makamu wa Rais bado unaimba nyimbo za enzi ya JKN.
 
Mimi mwenyewe nimepinga sana kitendo cha Kanisa Katoliki kurudi nyuma katika kupigania haki za watanzania. Ila ninachofanya ni kuwa realistic. Kuhusu Katiba aliyevuruga ni Jakaya Kikwete baada ya kugeuka nyuma, sijui alionywa na akina Mkapa? Kanisa Katoliki lilifanya kazi kubwa sana, ingawa Kardinali Pengo alivunja nguvu jitihada hizo. lakini mvunjaji hasa ni Kikwete mwenyewe aliyeanzisha huo mchakato toka mwanzo.

Unasema madhehebu mengine yamekuwa yakikemea toka mapema? siyo sahihi! Ni juzi tu wakati wa Krismasi ndio Maaskofu walianza kukemea, nao ni KKKT na Katoliki. kabla ya hapo ilikuwa kimya kabisa. Lakini hata hivyo tofautisha kemea ya Askofu mmoja mmoja, na kauli ya Kanisa zima ambayo ni rasmi. hakuna dhehebu la kikristo wala waislamu ambao wametoa kwa kiwango hicho.

Unauliza Waraka unasaidia nini, kwa kweli hakuna chochote kinachoweza kumzuia JPM kufanya chochote anachotaka hivi sasa. isipokuwa, unapokuwa na Maaskofu wametoa tamko kama hilo, unaondoa ule uhuru wa serikali kuongea kwa kujinasibu. it is on the defensive. hiyo inapunguza kasi yake ya kutenda maovu. pia inagalvanise opposition both from outside and inside. pia taarifa kama hizi zinasaidia vyombo vya nje ambavyo vinaweza kufuta baadhi ya mikataba kutokana na kutoridhishwa na hiki au kile. Kumbuka pia kwamba Madikteta wote wanapenda kusikika vizuri. hivyo publicity kama hii inawakera sana, na watajitahidi kuiepuka. hiyo itatusaidia. pia angalau tutashuhudia kupungua kwa "ziara za Rais katika Makanisa na hotuba za kwenye mimbari" huku akiomba "kuombewa". haituongezei ubwabwa lakini angalau inatupunguzia kero.
 
Hao maaskofu wa kanisa katoliki Tanzania ni wasemaji maneno matupu bila matendo kama wenzao wa nchi ya DR Congo.

Waraka wa wajumbe TEC ni kelele za debe tupu hayana athari kwa serikali yao kama mnavyoona sasa kinachoendelea nchini.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…