Wasichokijua Wengi Kuhusu Marko 10: 25 katika Biblia

Hii inaleta sense!
Binadamu kujinyenyekeza (humbleness), kama ngamia anavyopita ktk mlango mdogo (eye of the needle) wa ukuta wa Yerusalemu. Ngamia huondolewa mzigo mgongoni mwake na kukunja miguu yake (kupigishwa magoti) ili aweze kupita katika mlango huu mdogo wakati wa usiku. Ni rahisi ngamia huyu kupita ktk mlango huu mdogo na kuingia ktk mji wa Yerusalemu au ni rahisi ngamia kupita katikati ya miti miwili inayobana ili aweze kusafishwa uchafu ulio ktk ngozi yake.
Kumbe metaphor hii ni kwa ajili yetu sisi binadamu. Kama tunaweza kujishusha na kupitia mlango mdogo/njia nyembamba baada ya kushusha mizigo yetu ( viburi, majivuno, husda, visasi, wizi, uzinzi ...), tunaweza kuingia ktk Yerusalemu mpya.
If we humble ourselves and pray on our knees, we can approach the kingdom of heaven.
 
Umenena vyema mkuu!
 
Hii haina kona kona, uko sahihi.
 
Tundu la sindano ( vimilango vidogo vilivyokuwa vikitobolewa kwenye boma(ngome) au ukuta upiokuwa ukizunguka mji .
Hapo zamani miji mingi mfano mji wa Yeriko huko Mashariki ya kati ilikuwa inazungushiwa ukuta mnene.
Sasa ikitimia mida ya jioni miji hufugwa. Wafanyabiashara au wafugaji wakichelewa kuingia mjini hufunguliwa vimilango vidogo (Tundu la sindano) . Sasa kwa urefu wa ngamia basi ni mbinde kuingia kwa hivi vimilango. Technics za kuwabembeleza hutumika mpaka wanainama kwa hiari yao na kuingia kwenye vile vimilango (Tundu la sindano).
Chuo nilichosoma Mimi tundul la sindano maana yake ni vile milango midogo /mifupi ya dharura iliyowekwa kwenye ngome.
 

Here we go
 
Biblia si kitabu cha Mungu, pamoja na Quraan ni vitabu vilivyotungwa na watu kutokana na story za kuambiwa na kusikia. Vina makosa mengi sana ya tafsiri. Amini Mungu wako tu.
 
Eti watalaam ukiachana na mjadala wa kamba au ngamia mnyama , je kifungu hicho huyo tajiri aliyetajwa ni tajiri wa mali au tajiri wa nini? ( na nilivyosoma kichwa nilifikiri litazungumziwa hili). Kwamba kifungu hiki kinamuona masikini wa mali ni rahisi kurithi ufalme wa mbinguni?
 
Nafikiri hiyo ni hoja nyingine nzuri ya kuichambua! Tupe madini mkuu
 

Biblia imetafsiriwa na kubadilishwa mara nyingi sana, kiasi kwamba imebaki kuwa hadithi inayoweza kutafsiriwa vyovyote tu.

Una hakika nikisoma Biblia ya Kigiriki, lugha ambayo kitabu hiki kiliandikwa mara ya awali kwayo, nitakuta hivyo?

Hiyo haina Kiswahili wala Kiingereza. Haijatafsiriwa, ni lugha ya kwanza kitabu hicho kuandikwa.
 
Kwa bahati mbaya sijui Kihebrew ambacho ndiyo ndiyo lugha ya kwanza ya kitabu hicho. Ila ukisoma latin version utakutana na maana hiyohiyo... Kifungu hicho kwa Kilatini kinasomeka hivi: Facilius est camelum per foramen acus transire quam divitem intrare in regnum Dei. Tafuta maana ya hilo neno camelum!
 
Kwanza kabisa, hicho kitabu kiliandikwa kwa mara ya kwanza kwa Kigiriki, si "Kihebrew" (Kiebrania).
 
Kwanza kabisa, hicho kitabu kiliandikwa kwa mara ya kwanza kwa Kigiriki, si "Kihebrew" (Kiebrania).
Scholars generally recognize three languages as original biblical languages: Hebrew, Aramaic, and Koine Greek.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…