Watakiona chamoto watakaobainika Kuchezea fedha za Umma katika uongozi wa Rais Samia

Watakiona chamoto watakaobainika Kuchezea fedha za Umma katika uongozi wa Rais Samia

Wizi na ufisadi wa wakati huu, utavunja record zote trust me

Hakutakuwa na awamu ambayo ela zitaibwa na hakuna kitu cha maana hata cha kuonekana Kwa macho ambacho utakiona

Mnasema magu mwizi Sawa but wizi wake unafaida Kwa baadhi ya watu na wizi wake kuna vitu unaweza kwenda kushuhudia Kwa macho yako

Ila this time tutapigwa kama tulivyopigwa kwenye vyuma na vibao vya anuani za mitaa hahaha
Awamu hii ya Rais Samia hakuna atakayesalimika na kuishi kwa amani ikiwa atabainika kugusa pesa za umma,ndio maana unaona Takukuru wapo kazini muda wote kufanya uchunguzi na upelelezi wa kina kufuatilia fedha za watanzania
 
Uteuzi unatafutwa sana
Hapana ndugu yangu Mimi siandiki kusaka uteuzi Bali naandika kutoa mawazo yangu juu ya uongozi shupavu na madhubuti wa Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania mama Samia suluhu Hassani na namna alivyojipanga kuleta matokeo chanya kwenye maisha ya watanzania
 
Endelea tu kumwaga sifaaaaa lakini katika meza ya ulaji huwezi kumuweka nje sababu Ile system pia imemchafua
 
Huku mbali sana! Nenda kaanzie kule kule Mbozi,utapanda vyeo mdomdo! Tatizo umri nao
Huku mbali sana! Nenda kaanzie kule kule Mbozi,utapanda vyeo mdomdo! Tatizo umri nao
Serikali ya Rais wetu mpendwa mchapa kazi na mzalendo wa kweli nyota ya Matumaini hagawi vyeo kwa watu Bali anagawa majukumu kwa watu wa kumsaidia katika kuwahudumia watanzania,Pia Mimi siandiki hapa kwa ajili ya vyeo Bali naandika kwa hiyari yangu na uzalendo wangu kwa Taifa langu na nchi yangu,Mbozi inaendelea kumshukuru mh Rais kwa kuwapatia mbolea za Ruzuku zilizo Leta Tabasamu kwenye mioyo ya wakulima wa kata zote 29 za wilaya ya mbozi
 
Serikali ya Rais wetu mpendwa mchapa kazi na mzalendo wa kweli nyota ya Matumaini hagawi vyeo kwa watu Bali anagawa majukumu kwa watu wa kumsaidia katika kuwahudumia watanzania,Pia Mimi siandiki hapa kwa ajili ya vyeo Bali naandika kwa hiyari yangu na uzalendo wangu kwa Taifa langu na nchi yangu,Mbozi inaendelea kumshukuru mh Rais kwa kuwapatia mbolea za Ruzuku zilizo Leta Tabasamu kwenye mioyo ya wakulima wa kata zote 29 za wilaya ya mbozi
Kwenye Avatar hapo weka na picha yako kabisa! Itarahisisha kukumbukwa
 
Mimi nimetoa maoni yangu kuhusu Rais Samia na uthabiti na uimara wake kiuongozi katika kushughulika na wabadhirifu wa fedha za umma na siyo habari za uteuzi
ila weeeee tumghoje unazingua sana aisee...sijui mnyiha wa wp wewe hakyamungu, yaani unatia aibu sana .. sijui nani alikuleta mjini aisee, yaani huyo ndo wa kulaumiwa kbs kbs aisee. .ilitakiwa akuache huko huko nyimbiri na msangamweru uwe mtengeneza bunduki za kienyeji [emoji23][emoji23][emoji23]..huu uongo na nguvu unayoitumia hapa , lait ungeitumia kule kutengeneza magobore muda huu ungekuwa tajiri mkubwa hapo nyimbiri ... Chini ya chama kinachoitwa ccm upigaji hauwezi kuisha , na hata ww unatamani uteuliwe ili ukaibe ndo maana unaweka hiyo namba yko ya simu...weee veepi mnyiha weeee [emoji23][emoji1][emoji23]

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
 
Aliweza magufuri hadi akajenga miundombinu.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais Samia alishaweka wazi na kujipambanua kimaneno na kimatendo juu ya hasira zake Kali na maamuzi yake magumu kwa yeyote atakaye chezea fedha za umma,Hana Cha Nani Wala Nani katika Hilo,hamuogopi mtu Wala haangalii sura katika hili, Hana uvumilivu Wala Subira katika suala la kumuwajibisha yeyote atakayebainika kwenda kinyume na utaratibu na miongozi ya matumizi ya Fedha za Umma, hapa Ni mwepesi kutumia kalamu yake kutengua na kuagiza uchunguzi wa haraka ufanyike ili wahusika wafikishwe haraka mahakamani kujibu mashitaka Yao.

Hii Ni kutokana na Rais wetu mpendwa Jasiri na shupavu mama Samia kutambua kuwa fedha za umma zinapaswa kutumika vizuri kwa Nidhamu katika kuwapatia huduma watanzania,Anatambua namna watanzania wanavyojinyima ili walipe Kodi,anatambua namna anavyohangaika huku na kule kutafuta fedha kwa ajili ya kupeleka huduma Bora kwa watanzania,Anatambua namna watanzania wanavyo vuja jasho kuchapa kazi na kulipa Kodi serikalini.

Rais wetu mpendwa anatambua watanzania wanyonge aliojitoa na kujitolea kuwatumikia kwa uzalendo Hadi kufikia hatua ya kukosa muda wa kupumzika na familia yake wanavyoumia,kusononeka ,kusikitika na kulia machozi pale wanaposikia Kuna watumishi au viongozi wachache walioapa au kulipwa mishahara mikubwa na minono yenye minofu kwa ajili ya kuwatumikia na kuwahudumia wamefuja na Kuchezea Fedha za Umma bila huruma Wala aibu kwa maslahi yao binafsi,Vijana waliomaliza vyuo vikuu wanaumia na kutokwa machozi wanapoona wanahangaika huku na kule kutafuta mitaji huku nyuma wengine wanakula pesa zao za Kodi bila huruma.

Rais Samia anatambua anaongoza Taifa la aina ipi,Anatambua anaongoza Taifa Ambalo wengi wanahitaji kusaidiwa kukwamuliwa kiuchumi,Anatambua wapo wazee huko vijijini wanahitaji usaidizi wa serikali yao kuwapatia huduma za matibabu pasipo malipo maana wengi wanakuwa hawajiwezi kifedha,Ndio maana Rais Samia hawezi kumvumilia yeyote atakaye chezea fedha za umma.

Rais Samia anatambua namna watanzania wanaolipa Kodi kwa uaminifu wanavyoumia wanaposikia Kuna watu waliopewa dhamana wamegeuka kuwa mchwa wa fedha zao,Rais Samia anatambua Jambo hili linawaumiza Sana walipa Kodi,linawapunguzia molari ya kulipa Kodi au kotoa risti au kudai risti,Rais wetu mpendwa mama Samia anatambua namna mijadala inavyokuwa mingi mitaani miongoni mwa watanzania wanaposikia halmashauli fulani mkurugenzi wake kafuja mamilioni ya Fedha bila huruma ili Hali wao Wana watoto majumbani mwao wanaoamka alfajili kufanya vibarua vya kubeba zege ili wajikimu kimaisha licha ya kuwa Wamesoma Hadi vyuo vikuu.

Hii ndio sababu Rais wetu mpendwa mama Samia amekuwa akichukua hatua za haraka Sana ikiwepo kutengua uteuzi na kuagiza uchunguzi wa haraka kupitia Takukuru, kwa kuwa anauchungu na maisha ya watanzania na anataka juhudi za kutafuta pesa anazozifanya zitoe matokeo chanya kwa watanzania badala ya kuwaneemesha wachache na familia zao huku kundi kubwa likibaki na unyonge.

Hii ndio sababu ya Kuendelea kuaminika na kuungwa mkono na mamillion ya watanzania ambao wanatambua dhamira njema ya Rais wetu katika kulitumikia Taifa letu.

Songa mbele Rais wangu mh mama Samia,Mimi nitaendelea kukutetea na kukusemea kwa nguvu zangu zote katika yale yote unayolifanyia Taifa letu, nitaendelea kuwa mzalendo kwa Taifa langu na nchi yangu, Nitaendelea kutumia jukwaa hili kutoa ushauri wangu Kama mwananchi wa kawaida na mwenye upendo mkubwa Sana na Taifa langu.

usikate Tamaa Wala kukatishwa Tamaa na yeyote maana Tulio upande wako Ni wengi kuliko walio kinyume na wewe,Tumekukabidhi kila kitu Cha nchi hii na kukiweka mikononi mwako na tunaamini vyote vitakuwa salama,Tumia nguvu zako zote za kisheria na kikatiba kulinda Rasilimali za Taifa letu na kupambana na yeyote atakaye kuwa kikwazo katika kuwahudumia watanzania ikiwa ni pamoja na kumuweka pembeni na kumfikisha mahakamani, watanzania tupo bega kwa bega na wewe Rais wetu, Tunaendelea kukuombea Afya njema na nguvu za Kuendelea kututumikia.

Kazi Iendeleee , mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Kununua magari kwa 500M sio kuchezea fedha za umma?? 🤣🤣🤣
 
ila weeeee tumghoje unazingua sana aisee...sijui mnyiha wa wp wewe hakyamungu, yaani unatia aibu sana .. sijui nani alikuleta mjini aisee, yaani huyo ndo wa kulaumiwa kbs kbs aisee. .ilitakiwa akuache huko huko nyimbiri na msangamweru uwe mtengeneza bunduki za kienyeji [emoji23][emoji23][emoji23]..huu uongo na nguvu unayoitumia hapa , lait ungeitumia kule kutengeneza magobore muda huu ungekuwa tajiri mkubwa hapo nyimbiri ... Chini ya chama kinachoitwa ccm upigaji hauwezi kuisha , na hata ww unatamani uteuliwe ili ukaibe ndo maana unaweka hiyo namba yko ya simu...weee veepi mnyiha weeee [emoji23][emoji1][emoji23]

Sent from my DRA-LX5 using JamiiForums mobile app
Vijana waneona uchawa unalipa...ujinga mtupu.
Jamaa anaandika mashudu matupu hapa
 
Hakuna atakayebakia salama akibainika Kuchezea Fedha za umma
Hawa wote waliopo salama maana yake hawajabainika!!??
Basi hiyo serikali yako ina tatizo kubwa sana zaidi ya tujuavyo.

Tupo nao mitaani wakiwa full na amani wanachezea tuu fedha za umma.
 
CCM na serikali Yake ni imara Sana ndio maana imekuwa ikichukua hatua za haraka na Kali kwa yeyote atakayebainika kwenda kinyume na maadili ya utumishi wa umma
Huna hoja wewe bado chawa mchanga kisiasa na kiakili.
Hebu choma vitumbua kwanza akili ikomae ndipo uwe chawa mwenye hoja
 
Hawa wote waliopo salama maana yake hawajabainika!!??
Basi hiyo serikali yako ina tatizo kubwa sana zaidi ya tujuavyo.

Tupo nao mitaani wakiwa full na amani wanachezea tuu fedha za umma.
Vita dhidi ya ubadhirifu wa Mali ya umma ,ufisadi,Rushwa,matumizi mabaya ya madaraka na wizi wa fedha za umma Ni endelevu na haina kikomo ndio maana unaona muda wote serikali ipo kazini na silaha zake kupambana na watu wa aina hiyo
 
Back
Top Bottom