Watanzania fuatilieni kinachoendelea DRC. Hali kwa majirani zetu ni mbaya, ya hatari sana

Watanzania fuatilieni kinachoendelea DRC. Hali kwa majirani zetu ni mbaya, ya hatari sana

Tuache kujipendekeza hii vita ni hatari kwa usalama wa nchi yetu.
M23 Kina mkono mrefu na maslahi mapana ya watu, tukienda hovyo na kujipendekeza tutarudisha askari wetu kwenye majeneza.

Msisahau wale jamaa wako kusini kule, tayari kuna chokochoko ya wale IS wakitoke msumbiji, tukienda hovyo jamaa wanauwezo wa kutudestabilize.
 
Tuna mchango wetu katika kujaribu kuleta amani ya Congo, ingawa ni changamoto

TOKA MAKTABA :

29 January 2024

VITA MASHARIKI YA CONGO: Kikosi Kipya cha battalian ya Kitanzania Kilichopo Kivu Kaskazini Kikiwa na Mamlaka ya Kulazimisha amani
1737840635438.jpeg


Kikosi kipya cha wanajeshi wa Tanzania kimetumwa katika jimbo la Kivu Kaskazini lililokumbwa na vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kama kikosi cha pili cha ujumbe wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).

Kikosi cha Tanzania kitachukua nafasi ya jeshi la kikanda la Jumuiya ya Afrika ya Mashariki EAC na kuchukua jukumu la kushambulia, kulingana na vyanzo vya kijeshi.

"Wanajeshi wa Tanzania wanawasili ili kuongeza nguvu ya askari wa SADC ambao wana mamlaka ya kulazimisha waasi wakubali amani ," alisema Luteni Kanali Guillaume Ndjike, msemaji wa gavana wa kijeshi wa Kivu Kaskazini.

“Uko pale kupigana na adui, waasi wa M23. Haupo kwa doria za jiji au kufahamiana na watu wa Kongo. Tuko hapa kushughulikia lengo letu,” alisema Meja Jenerali Monwabisi Dyakopu wa Afrika Kusini SADF mkuu wa kikosi cha nchi wanachama wa SADC, katika hotuba yake ya kuwaribisha.

Wanajeshi hawa wa SADC, wakiwa na mamlaka ya kushambulia, watachukua nafasi zilizoachwa na jeshi la kikanda la EAC (Burundi, Sudan Kusini, Kenya na Uganda) kama ilivyoamuliwa na serikali iliyotaja kutoridhika na kuendelea kuwepo uasi katika maeneo yaliyovamiwa M23 na kutokuwa na utulivu.

Wakati huo huo, kikosi cha Afrika Kusini cha SADC ambacho kilikuwa cha kwanza kuwasili Goma Desemba 2023, hivi karibuni kilishambuliwa na kundi la waasi la M23.

Kutumwa kwa wanajeshi wa SADC mashariki mwa DRC kuliidhinishwa wakati wa Mkutano wa 43 wa Kawaida wa Wakuu wa Nchi na Serikali huko Luanda, Angola.

Kikosi hicho kipya kitaundwa na wanajeshi kutoka Malawi, Afrika Kusini na Tanzania kufuatia kuondolewa kwa wanajeshi 89 wa mwisho wa Kenya wa Jeshi la Kanda ya EAC ambao waliacha ardhi ya Kongo Alhamisi Desemba 21 kupitia Goma
 
Huu mgogoro wa Congo River Alliance na Serikali ya Congo DRC umalizwe kwa Dialogue.
 
GEOPOLITICS KANDA YA MAZIWA MAKUU, EAC NA SADC

16 January 2025
Kigali, Rwanda

KAGAME ALIPUA WANA diplomasia
: 'Tshisekedi Ni Mjinga; Hajawahi Kushinda Uchaguzi Kongo, Na Mnajua Lakini Hamwezi Kusema Hadharani, Leo Nawaambia Live / Mubashara'

View: https://m.youtube.com/watch?v=lxfdT9kYBLA

Rais wa Rwanda amezidisha mvutano kati ya nchi yake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kuwalipua wanadiplomasia wakati alipokutana nao katika mkutano wa kila mwaka na mabalozi wa nje wanaowakilisha nchi yao mjini Kigali Rwanda jana.

Kagame alimtaja rais mlaghai wa DRC Felix Tshisekedi kama mjinga ambaye hakujua la kufanya kama kiongozi.

Alisema Tshisekedi hajawahi kuchaguliwa kihalali na ndiyo sababu vita mashariki mwa Kongo vinaongezeka.

Kagame anatuhumiwa kuwafadhili waasi wa M23 ambao sasa wanadhibiti maeneo makubwa ya mashariki mwa DRC.

“Mtu (Tshisekedi) anayesababisha matatizo kati ya Rwanda na DRC hajawahi, mara mbili, kuchaguliwa na nyote mnajua. NA ninajua.

“Mtu huyu Tshisekedi hakuwahi kuchaguliwa, kwanza, hakuchaguliwa kabisa. Na unajua. Ni kwamba tu hatuiongelei hadharani na ninaizungumza hadharani sasa.

“Hiyo ndiyo tofauti. Mnaijua. Mara ya pili, hakuna kilichotokea. Na mnajua.”

Kagame aliongeza kuwa Tshisekedi hakuwa na sifa za uongozi.

“Nawafahamu viongozi ninapowaona. Pia najua wajinga ninapowaona.

"Unaweza kufikiria mchanganyiko wa wote wawili, janga ni.

"Kama wewe ni kiongozi na mjinga, ni balaa kabisa. Ni mbaya zaidi, hata hatari zaidi, ikiwa watu walewale walioshikilia mamlaka mikononi mwao wataamua kuwa watatumiwa na kuchezewa kwa maslahi fulani na wajinga,” alisema Rais Kagame.

Nchini Kongo kuna watu wanaongea Kinyarwanda, pia wilaya kadhaa za nchini Uganda lakini Uganda haisemi wale siyo raia wa Uganda ila Kongo kwa ujinga wao wanaamini raia wa Kongo wanaoongea Kinyarwabda siyo Wakongomani ! Huu ni ujinga na mbaya zaidi sehemu ya Jumuiya ya Kimataifa inakubali mtizamo wa Kongo!

Hili suala la Umoja wa Mataifa kulinda amani kwa miongo 3 yaani miaka 30 bila kufikiwa lengo la kuleta amani nchini Congo.

Hivyo ni jukumu la Rwanda kutafuta njia mbadala kuhakikusha usalama wake kwa kuwa inapakana na nchi iliyoshindwa kulinda usalama wake, huku viongozi wa Kongo wakifumbia macho Intarahamwe waliopo nchi jirani waliohusika na mauaji ya ya kimbari nchini Rwanda..

Inasikitisha jumuiya ya kimataifa chini ya mamlaka ya Umoja wa Mataifa kuilaumu Rwanda wakati ni wao jumuiya ya kimataifa imeshindwa kusitisha vita nchini Kongo mbali ya kutumia mamilioni ya dolari, vifaa, na Majeshi ya Kulinda Amani chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa MONUSCO ...
 
Wanajeshi wa Tanzania wanasifika Kwa mizinga kule,unaambiwa wakipiga sehemu Hakuna jiwe linalobaki juu ya jiwe jingine.
Ila Kuna wale wa un walishikiwa mateka sadc wakitaka kushambulia m23 wanatishia kuwamalizia wale
 
Kuna kazi kubwa sana zaidi ya hiyo video, haohao wacongo hawako tayari.badala ya kupigania Nchi yao wako busy kucheza sebenee.
Tanzania wanalipwa kupeleka majeshi huko hela zinatoka UN, UNICEF.
Bahati mbaya sana wanauzwa na hao wapumbavu Wacongo kwa hahao wavamizi thethen wanauliwa.
Rudia kisa cha mammadou Ndala.
Kauliwa njiani na wacongo wenzie huko wakati anawafurusha ADF kwenda kwao Uganda.
Wabongo wapige hela warudi mtaani vita haiishi huko, mchawi wao ndo kwanza kagundua mafuta Ziwa kivu.
 
January 2025

KWANINI JESHI LA AFRIKA KUSINI LINAPIGANA KATIKA JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA KONGO & MSUMBIJI?


View: https://m.youtube.com/watch?v=2yfSUUNZJIg


Jeshi la Ulinzi la Taifa la Afrika Kusini SADF kwa sasa linapigana au niruhusu nitumie neno sahihi, wanashughulika na misheni za kulinda amani nchini DR Congo na hivi karibuni wameanza kujiondoa kutoka kaskazini mwa Msumbiji.

Misheni za kijeshi ambayo na inagharimu nchi mabilioni ya sarafu ya randi ya Afrika ya Kusini lakini kuna sababu muhimu ya usalama wa kitaifa na kikanda kwa hili na nataka tuijadili.

Kwa hivyo katika video hii ingawa itakuwa ndefu kidogo kuliko kawaida nataka uendelee kuitazama kwa sababu utaondoka hapa ukijua mengi zaidi juu ya ulimwengu unaokuzunguka.

Sisi kama Afrika Kusini kwa sasa na hivi majuzi tuko katika maeneo mawili yenye migogoro na pengine unapaswa kujua zaidi kuhusu hilo.

Kuanzia mwanzoni mwa mwaka 2024, tulikuwa na takriban wanajeshi 1495 kaskazini mwa Msumbiji wakipigana ingawa tunarudi nyuma kutokana na kupigana na waasi Mozambique waliojitenga na ISIS pamoja na wanajeshi 1200 wanaoshiriki katika ujumbe wa amani Mashariki mwa DR Congo . Idadi Hiyo ni wanajeshi 2700 katika maeneo yenye migogoro.

Hata hivi majuzi kama Okt 31, 2024 Jeshi la Ulinzi la Kitaifa la Afrika Kusini (SANDF) lilitengewa dola bilioni 3.6 za ziada na waziri wa fedha katika 'bajeti ndogo' iliyowasilishwa Jumatano, lakini wengi katika tasnia ya ulinzi bado wanahisi kuwa jeshi letu kutofadhiliwa vya lutosha ili ijitahidi kutimiza majukumu yake sawasawa
Source : Zimasa "mooshtaffa" Vabaza
 
Kuna kazi kubwa sana zaidi ya hiyo video, haohao wacongo hawako tayari.badala ya kupigania Nchi yao wako busy kucheza sebenee.
Tanzania wanalipwa kupeleka majeshi huko hela zinatoka UN, UNICEF.
Bahati mbaya sana wanauzwa na hao wapumbavu Wacongo kwa hahao wavamizi thethen wanauliwa.
Rudia kisa cha mammadou Ndala.
Kauliwa njiani na wacongo wenzie huko wakati anawafurusha ADF kwenda kwao Uganda.
Wabongo wapige hela warudi mtaani vita haiishi huko, mchawi wao ndo kwanza kagundua mafuta Ziwa kivu.
Ku Control Nchi Likubwa Vile, Tena Limeshaingia Kwenye Machafuko kweli Sio Rahisi
 
Ku Control Nchi Likubwa Vile, Tena Limeshaingia Kwenye Machafuko kweli Sio Rahisi
Rahisi sana sema hawajajipanga vizuri, serekali dhaifu, sometimes ili kuiweka nchi sawa ni lazima ukatili ufanyike ili wengine waishi kwa Utulivu, intelegent duni, spy system duni, ni lazima ufanye utaratibu wa kutoa funzo zito kwa waasi kuwaangamiza wote na kutengeneza intelegency ya mapandikizi miongoni mwao, with silence assassination tools (mkono wa chuma)
 
Wakuu wa dunia wapo upande upi katika hii vita?
Wanarushia mu Drone kwamu setelaiiti, banaangalia tu, bakiona mmehama, banachimba mugold, mukirudi, banatuma UN kulinda mahandaki.
Bila ya Juhudi za Nchi zote, nasisitiza nchi zote, tutakua kama wale wazungu waliopigana miaka 300.

Hata hivyo Wakuu ndi wachonganyishi, nasema kwelli bandugu?
 
Madikteta wanasababisha shida sana hapa duniani. Shida zote hizi ni Kagame.

Madikteta aina ya Putin na Kagame wanatakiwa kupingwa kwa nguvu zote.
Hata Donald Trump ni Dictator tyu. Na ameshasema, watashughulikia wachina kwanza, halafu waje kulokota "rare earth" minerals.

Hizi sio vita zamasikini.
Wenyewe banakunywa kofi
 
Back
Top Bottom