Watanzania tuchutame, Uchaguzi Mkuu nchini Kenya umetuacha uchi

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ngumu sana kuelewa hii nchi Tanzania kutumia mfumo wa kielektroniki kuhesabu kura ni sawa na kutaka VAR itumike kwenye ligi za afrika kitu ambacho FISIEMU hawawezi kukubali kutumia njia za kisasa kuhesabu kura wataangukia pabaya sana
 
Ushetani unanzia kuwambia watanzania kwamba ccm inahati miliki.
 
Nawaunga mkono ccm kwenye hili! maana hawana mbadala

Tukipata tume huru kwa wapinzani hawa tulionao sasa, tutatawaliwa na raisi mjinga kuliko tudhaniavyo.
 
Shida ya chaguzi za Africa wala siyo uwazi bali kutokuaminiana.
Hapana, hii si kweli. Uwazi hupunguza kama si kuondoa kabisa wasi wasi katika mwenendo mzima wa uchaguzi toka hatua za awali kabisa.

Uwazi hukuza kiwango cha imani kutoka pande zote zinazoshindana kwani kila moja si tu anashuhudia bali anashiriki katika kila hatua zote.

Usiri katika zoezi la kuhesabu kura ndicho kichaka kinachotumiwa na mafashisti kupora maamuzi huru na hujenga tabia ya kutoaminiana.
 
Wachawi ndio wanapenda giza/kificho, huogopa UWAZI
 
Uchaguzi wafanye Kenya harafu Tanzania ndio tuchutame,una wazimu wewe..

Unawesa hamia huko Kenya mkuu.
 
Tukipata tume huru kwa wapinzani hawa tulionao sasa, tutatawaliwa na raisi mjinga kuliko tudhaniavyo.
Hivi hapa unajua kweli unachosema? Tume isiyo huru kama hii tuliyo nayo hutekeleza tu matakwa ya chama tawala, CCM. Tume huru hutangaza tu maamuzi ya wapiga kura, haichagui Rais.

nyakubonga, si kosa lako, nadhani umechanganyikiwa...wahi dawa!
 
Uchaguzi wafanye Kenya harafu Tanzania ndio tuchutame,una wazimu wewe..
Unawesa hamia huko Kenya mkuu.
Sijui wewe taka taka uliwezaje kujiunga Jamii Forums. Wewe utakuwa wale waleeee...unatia aibu. Jifunze angalau kuandika Kiswahili, lugha yetu ya taifa
 
Nilichosema hakibadiliki boss, kiko hivyo hivyo.
Kusema na kutenda mbalimbali. Hili linajulikana, na ushahidi umejaa tele humu JF toka Sept. 28, 2011.

Na kama kawaida, swali lililoulizwa halina jibu!

Tuendelee na mengine.
 
Unaandika kitu na majibu unayo.
Nakuambia Tena kaa Mita 200 kutoka eneo la kuhesabia kura 2k25.
 
Huwezi kutufananisha sisi(Tanzania) na Kenya.
Viongozi wakuu wa Kenya wameonja pumzi ya moto ya "the Hague" na walinusurika kula mvua za kutosha.
Mtu yeyote mwenye akili timamu, akishaonja pumzi ya moto ya "the Hague", yuko tayari kuachilia vyote kwa ajili ya demokrasia.
 
Kama viongozi wa Kenya wasingepitia the Hague wangekuwa sawa tu na Tanzania.
( Rejea: michakato ya BBI, iliyoharamishwa na mahakama). Hivyo demokrasia hiyo ni kwa hisani ya the Hague.
 
HIVI UKIFANYA UCHAGUZI MWIZI KUNA UCHAGUZI GANI HAPO.TULITIA AIBU ULIMWENGU MZIMA NDIO MAANA UNAWEZA UKAONA MAISHA YA WATANZANIA YANASIKITISHA MNO KWA SABABU SAUTI YA MUNGU ILIKATALIWA BILA HAYA WALA SONI,NA NDIO MAANA YEYOTE AKATAAE SAUTI YA MUNGU HAWEZI KUJUA NN CHA KUFANYA NDIYO YANAYOENDELEA TANZANIA,SERIKALI HAIJUI NN IFANYE IMECHANGANYIKIWA SUALA DOGO TU LA MAFUTA IMESHINDWA NYANG'ANYANG'A HAKUNA KITU NI SIFURI TU.
 
Kwa mawazo yangu kutoka na yanayoendelea Kenya tuseme wazi tu Watanzania tuna mengi ya KUJIFUNZA, tufanye chaguzi kiushindani na kuheshimiana, sio kama ilivyo hapa kwetu mtu ukiwa mpinzani unaonekana kama Msaliti wa nchi, utachukiwa na Kila mtu hasa watu walio serekalini ndio utakosa rafiki, ushirikiano na kuonekana kama mtu aliepotea kwa fikra. Nadhani ni mda sasa watu kuamka na kubadilika, Ili hata mfanyakazi wa Taasisi za serekali atoe ushirikiano kwa Wapinzani, hii nchi ni yetu sote na daima kukubali kukosolewa.
 
K
Kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…