Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Watanzania tuelezwe ni wapi alipo Rais wetu Mpendwa John Magufuli, ni haki yetu kujua

Status
Not open for further replies.
Niliwahi kumwambia mshkaji mmoja kuwa huyu anaweza kuvunja rekodi za wenzake waliopita kwa kukalia kiti awamu moja ss km ni kweli naona mkeka wangu unaelekea kutiki.

Mbadala utapatikana mapema mno na unaweza kuwa bora kuliko kawaida na somo ni atakayekuwa ameng'atuka.
Kwa mkuu huyu tegemea record ya vyote either awamu Moja tu
Au awamu zaidi ya mbili

Sijui Umenielewa
 
Kama mnasubiri avute basi naomba kuwa taarifu Milango yakuzimu kamwe haitomuweza Rais wa jamuhuri Ya muungano wa Tanzania.

Atatikiswa ila hawawezi kuigusa roho yake. Nikweli nimkali ila ni kiongoz shupavu alie na maono ya kweli kwa taifa letu.
Chuki na hasira sio za wananchi ila kundi lawapumbavu na n vilaza fulani. Ndugu zangu kama vile jina lilivyopita ndivyo usalama wake utakuwa naye. Wanyonge wengi sana wamepata haki zao utawala huu na sishangai chuki hii nikwa kaz nzuri anafanya.

Rais amkuwa na ratiba ambayo sio yakawaida nauwenda imemchosha. Kiufupi uwenda sasa atafuwata ratiba nakupunguza kazi. Pia ningeshauri wafanyakaz wa Ikulu wampeleke watoto acheze nao huwa ni wazuri sana kupunguza stress.

Naiman baada ya mapumziko rais wetu atarud kulitumikia taifa lake.
Mungu ibariki tanzania na watu wake na Viongoz wake. Amen
Kweli upumbavu wako hauna gharama
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi; Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili; Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu; Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
 
Rais JPM anatakiwa awe anapumzika, Watu wanao ratibu kazizake wanatakiwa wahakikishe anafuata ratiba. Rais anatakiwa afahamu taifa ili baadhi waliomba na kufunga ili apatikane Rais wa Kariba yake.
Mungu alisikia kilio cha watanzania ndiomaana alipata kibali cha kutuhudumia watanzania kwaiyo anatakiwa afahamishwe iikazi ya kulikomboa Taifa ni ngumu anahitajika awe anapumzika. Tunajua kuumwa ni sehemu ya maisha ya binadamu ila kufanya kazi kupita kiasi kutamletea shida yeye na taifa kwa ujumla.
Na wagamboshi walifanya nini? Usitubambikie maombi ya Gamboshi
 
Mh. Rais atarudi kwa kishindo zaidi, Watanzania wengi tuko na imani nae kwa miaka mingine 6 iliyobaki..

Mungu Mubariki Mh. JPM..

Mungu ibariki Tanzania, Amen...
Yupo wapi kwani? Maana me sielewi kinachoendelea
 
Nahisi huu ni muda muafaka kwa mamlaka husika kututoa hofu wananchi , c vyema kukaa kimya kwa mamlaka husika
 
Hii imedhihirisha kuwa Raisi John Joseph Pombe Magufuli ni kipenzi cha watanzania yeye anawapenda na wao wanampenda baada ya Raisi wa watanzania kujichimbia ikulu kama kawaida yake,
Watanzania wameanza kuwa na hamu naye wanahisi kukosa kusikia sauti ni kama kupoteza ala nzuri masikioni mwao,
Ni hakika 2020 Magufuli atachukua nchi kweupe saa asubuhi kwa mahaba wanayoyaonyesha!

Magufuli habagui watu kwa vyama wala dini wote anawapa maendeleo!
Poleni kwa kubaki wakiwa.

Naona km wenzio wametelekeza umebaki peke yako ukipiga ramli
 
meangalia clip inayotembea imeonesha alifukiziwa moshi wa KOROSHO !!! ka kweli naona wa kusini wana tekinolojia ya hatariiii.......

Mejiuliza JE kuna umuhimu wa misafara ya viongozi kuwa na WAGANGA waaguajiiii...wanaoweza weka makarai ya maji na kuongeza usalamaaa...IJAPOKUWA serikali haiamini uchawi/ushirikina
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom