bora umekiri umekiri mwenyewe kuzidiwa na hoja,ulidhani jf ni shamba la bibi unaingia na uyoga wako then unaanza kuuza ukafiri utapata support -never jipange upya matusi unayo mwenyewe ila ukianza na mimi namaliza mvivu wa kufikiri.
nenda kalale wapishe wenye hoja wachangie huelewi maudhui yake na hata ukielewa haitakusaidia wewe si raia wa tanzania.
umezidiwa unabakia kuweka katuni,tupia yako pia maana na wewe ni katuni.
Ningekuwa mzazi wako,nineumia sana.Sijashindwa kwenye hoja ila sababu ninajitathmini THAMANI yangu.Na ninapenda kupokea mawazo mbadala,na nina heshimu mawazo ya mtu kwa uamuzi wake anaoufanya,na sipendi hoja zinazoambatana na MATUSI.
Nilipoona mmejenga hoja zenu kwenye MATUSI,nimewavalue ZERO BRAIN,hivyo thamani yangu ni kubwa mno kubishana na watoto wadogo wasio na uwezo wa kukubaliana katika mawazo kinzani.
Na ndiyo maana nitaendelea kusema usipoteze muda wako kubishana na mimi tuko level tofauti.
Level yangu ya kufikiri outside the box ipo juu zaidi kuliko level yako.Na wazungu wanasema.."Never argue with a fool"sababu mwisho wa siku hatutakuwa na tofauti.
:bored::bored::bored::bored: .Nitashukuru sana kama utaheshimu mawazo yangu.Na kama ulitegemea nitakutukana ili nipate BAN basi umepotea haitakaa itokee.Ningekushauri tu binadamu tunamawazo tofauti inabidi tuheshiane hivyo hivyo.
Hata kama nitafanya kampeni ya HAPANA bado sikunyimi wewe kufanya kampeni ya NDIYO,hivyo heshimu mawazo kinzani haijalishi unataka au hautaki,bado kuna HAKI ya WATANZANIA kupiga KURA ya HAPANA au NDIYO kwenye KATIBA ya FISADI CHENGE,usilazimishe kwa matusi na kudhalilisha.Kuwa mtaarabu,
Ndugu umemjibu kwa busara ya hali ya juu, unaweza kukuta alikuwa mjumbe katika BMK. Hebu jaribu kuwaangalia waliokuwa wajumbe wa BMK ukiwatoa UKAWA wanapoitetea katiba pendekezwa mbona utapata raha, yaani unaona watu wanalazimisha kabisa hoja, na wakipigwa maswali kuhusu udhaifu hawana majibu zaidi ya blablaa na jazba juu. Fuatilia tu wote utagundua udhaifu huo kama huyu hapa uliyemjibu.
Na wanachofanya ni kuwatafutie watu wenye mawazo tofauti na wao wapate BAN ili wasipate wa kuzijibu hoja zao.Wengi wanatumia MATUSI na lugha za kudhalilisha sana.Ninachokishangaa ninamna mods wanavyowaacha watu hawa watusi wenzao bila sababu za msingi.
Hasa inapotokea HOJA kinzani inaumiza basi utapata MATUSI mpaka basi,kuna siku mmoja aliniwekea wazi intention yake kwamba alitaka tu nipate BAN na hana sababu za msingi.Sielewi JF ilikuwa eneo ambalo wengi tulipenda hoja zilivyokuwa zinajibiwa kwa hoja lakini sasa hivi hata usiependa kujibu utumbo unalazimishwa kujibu.Ni shida sana,na waanzilishi wa Jukwaa hili wanapaswa kulifanyia kazi ili kuitendea HAKI JF irudi kama ilivyokuwa.
Ninashaa ukisoma HOJA za Jukwaa la GT hukuti matusi ni HOJA kwa HOJA ,sijui pande hii imekuwaje.
Ndugu yangu hili jukwaa lilianza kuharibika rasmi siku kamati kuu ya ccm ilipokaa na kutoka na wazo la kuweka vijana wa kujibu hoja mitandaoni eti kurudisha haiba ya ccm. Nadhani unakumbuka Nape alitembelea vyombo vyote vya habari na kuhakikisha eti ccm inaandikwa vizuri kwani kwa mujibu wa mitazamo yao hawakuwa wanatumia media vizuri. Sio wazo baya kwani nilitarajia kama chama kikongwe kuona kinajenga hoja zenye mashiko, lakini looh!! Nilishangaa kuanza kuona zile mbinu za ulaya mashariki ya zamani za kuingilia mijadala na kuprovoke watu ili mada iharibike. Ninaweza kusema kweli wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwenye hilo, kwani hili jukwaa kwa sasa limekuwa ni kinyaa kabisa. Na usishangae wanaoleta post za kipuuzi ni viongozi wakubwa hata wa serekali kwa kujificha kwenye id fake huku wakifanya upotoshaji mkubwa kwa makusudi kabisa.
Tusome tusisome kura zetu ni hapana tu.
Unaposema kitu ambacho hukipendi toa mifano hai ili ujibiwe kwa ufasaha, ni wapi hapo ambapo unasema haijajali wananchi? wananchi gani hao? Au ukitaka matakwa yako binafsi? Kwa taarifa yako hii katiba inayopendekezwa imejali makundi mbalimbali na ukweli wa suala hili unapatikana katika katiba inayopendekezwa katika sura ya tano ibara ya 56 (haki za makundi madogo katika jamii), pia soma ibara ya 46 haki za wakulima, wafugaji, wavuvi na wachimba madini (watumiaji wa ardhi), kwa maneno hayo naamini nitakuwa nimekusaidia kukujibu na kukutoa wasiwasi kuhusu wananchi.
hakuna tatizo katika hilo kwani hata hiyo "kura ya ndiyo" inayopigiwa debe kwa nguvu sana itakuwa kura yake binafsi, wala si kura ya kundi lake.
kaka c umeombwa utoe jibu? Sasa mbona unazungulukazunguluka tuu humu ndani, kama umeishiwa maneno wewe chapalapa uwaache wenye kujua kazi ya kujibu hoja za watanzania.
Nani mwenye hati miliki ya kutoa elimu ya katiba mpya?
Kuna watu wanataka wenyewe tu ndo wasikilizwe. Akisema mtu mwingine wanasema 'anashawishi na kuongilia mawazo binafsi ya mtu mwenye maamuzi' akisema yeye anatoa elimu.
Watanzania tumegawanyika kwa sasa tupo:
1. Ambao hatujaisoma katiba lakini kwa kuwa fulani amesema poa au sio poa basi tutapiga kura ya ndio au hapana kwa kuwa tunamuamini huyo mtu 100% na maamuzi yake kwetu ni muafaka kabisa. Sisi hata mikutano au kusoma au makelele yoyote hayatuhusu msijisumbue na sisi. Tumeshafanya au tumeshafanyiwa maamuzi.
2. Tuko na sie ambao hatujaisoma katiba tunatamani tuipate tuisome tufanye maamuzi so kama ikitokea tukaipata mapema tukaisoma tunaweza kuikubali au kuikataa. Wenye jukumu chonde chonde mtuangalie muda uanisha. Muda ukiisha kabla ya kuisoma kura itakuwa ya hapana ila wengine hatutaenda kupiga kura.
3. Tuko wale tulioisoma kidogo na kuichukia rasmi. Tumesha fanya maamuzi hatuitaki mpaka iboreshwe. Kura ya hapana. Msijichoshe kutuhubiria.
4. Tuko ambao tumeshaona tulichotaka kwenye latiba pendekezwa tayari hata kama kwingine tunahisi hakutuhusu sana. Maadamu kikio chetu kimesikilizwa tumefurahi sana. Very risky kutokuipitisha katiba hii kwani vipengele vinaweza kutolewa. Lazima tutaipigia kura ya ndio. Hamna haja kuhangaika na sisi. Hakikisheni tu hamsogezi tarehe za upigaji kura mbele.
5. Sie ambao hatujasoma tunategemea kuendelea kusikiliza majukwaani au maredioni na kwenye vyombo vingine. Maoni ya wachambuzi. Sie ni watanzania halisi tunaenda na upepo nadhani tupo wengi endeleeni kutushawishi upepo utakapoishia ndio hapo maamuzi yetu yalipo.
Nadhani ni muda muafaka kwetu watanzania kuanza utamaduni wa kuisoma katiba pendekezwa kwa wale wenzangu ambao bado hatujaanza ili tuepuke upotoshaji unaofanywa na watu wachacheKwa muda mrefu nimekuwa nikijiuliza kwa watanzania wenzangu, kwa sasa kila mtu kwa anaweza kutunufaika na maendeleo ya technolojia ya mawasiliano bila kujalisha yupo mjini ama vijijini,kwa sasa ni rahisi hata kwa watu ambao hawana elimu ya kawaida, unamkuta yumo FB,Wasap na pia kuangalia taarifa zingine kupitia simu! Katika siku za hivi karibuni watu wengi wamekuwa wakilalamikia kutopata nakala za katiba,lakini mie kengele leo imegonga kichwani nikaona watu walivyo na ueledi mkubwa wa matumizi ya mitandao ya kijamii na katiba pendekezwa jitihada kidogo tu mtu waweza ipata kupitia mitandao hiyo.
Sasa je swali la kujiuliza kwamba kama si ushabiki wa kisiasa tu,kweli mtu ukipania kuisoma huwezi kuisoma kweli? AMA tukisikia kauli za kisiasa tunapandia hapo hapo,sidhani kama tunaweza kwenda kwa mfumo huu,nijuavyo mie watanzania waliowengi hawana utamanaduni wa kusomo mrundikano wa maandishi hilo hakuna hata mmoja anagusia,ila kusema nakala hazijasambazwa zile za hard copy,hiyo ndo inakuwa habari ya mjini.
Mie nadhani kutokana na umhimu wa katiba katika mstakabali wa nchi kwa siku zijazo kila mtu angepumnzika kidogo tu kuchat na kuingia online kuisoma katika inayopendekezwa,na si kuishia malalamiko ambayo nahisi ni ya wachache kwamba hawawezi kupata nakala ya katiba pendekezwa, ila wengine ni kama hatutaki tu kuifikia katiba hiyo kwa ya kimitandao.
Nawasilisha jamvini mawazo tete haya
Ndugu yangu hili jukwaa lilianza kuharibika rasmi siku kamati kuu ya ccm ilipokaa na kutoka na wazo la kuweka vijana wa kujibu hoja mitandaoni eti kurudisha haiba ya ccm. Nadhani unakumbuka Nape alitembelea vyombo vyote vya habari na kuhakikisha eti ccm inaandikwa vizuri kwani kwa mujibu wa mitazamo yao hawakuwa wanatumia media vizuri. Sio wazo baya kwani nilitarajia kama chama kikongwe kuona kinajenga hoja zenye mashiko, lakini looh!! Nilishangaa kuanza kuona zile mbinu za ulaya mashariki ya zamani za kuingilia mijadala na kuprovoke watu ili mada iharibike. Ninaweza kusema kweli wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwenye hilo, kwani hili jukwaa kwa sasa limekuwa ni kinyaa kabisa. Na usishangae wanaoleta post za kipuuzi ni viongozi wakubwa hata wa serekali kwa kujificha kwenye id fake huku wakifanya upotoshaji mkubwa kwa makusudi kabisa.
Nani mwenye hati miliki ya kutoa elimu ya katiba mpya?
Kuna watu wanataka wenyewe tu ndo wasikilizwe. Akisema mtu mwingine wanasema 'anashawishi na kuongilia mawazo binafsi ya mtu mwenye maamuzi' akisema yeye anatoa elimu.
Watanzania tumegawanyika kwa sasa tupo:
1. Ambao hatujaisoma katiba lakini kwa kuwa fulani amesema poa au sio poa basi tutapiga kura ya ndio au hapana kwa kuwa tunamuamini huyo mtu 100% na maamuzi yake kwetu ni muafaka kabisa. Sisi hata mikutano au kusoma au makelele yoyote hayatuhusu msijisumbue na sisi. Tumeshafanya au tumeshafanyiwa maamuzi.
2. Tuko na sie ambao hatujaisoma katiba tunatamani tuipate tuisome tufanye maamuzi so kama ikitokea tukaipata mapema tukaisoma tunaweza kuikubali au kuikataa. Wenye jukumu chonde chonde mtuangalie muda uanisha. Muda ukiisha kabla ya kuisoma kura itakuwa ya hapana ila wengine hatutaenda kupiga kura.
3. Tuko wale tulioisoma kidogo na kuichukia rasmi. Tumesha fanya maamuzi hatuitaki mpaka iboreshwe. Kura ya hapana. Msijichoshe kutuhubiria.
4. Tuko ambao tumeshaona tulichotaka kwenye latiba pendekezwa tayari hata kama kwingine tunahisi hakutuhusu sana. Maadamu kikio chetu kimesikilizwa tumefurahi sana. Very risky kutokuipitisha katiba hii kwani vipengele vinaweza kutolewa. Lazima tutaipigia kura ya ndio. Hamna haja kuhangaika na sisi. Hakikisheni tu hamsogezi tarehe za upigaji kura mbele.
5. Sie ambao hatujasoma tunategemea kuendelea kusikiliza majukwaani au maredioni na kwenye vyombo vingine. Maoni ya wachambuzi. Sie ni watanzania halisi tunaenda na upepo nadhani tupo wengi endeleeni kutushawishi upepo utakapoishia ndio hapo maamuzi yetu yalipo.
Kwa mtindo huu natamani ifikie wakati tusiwe tunatumia ID feki hapa JF ili hao waliopachikwa kutuharibia jukwaa letu warudi walikotoka! Hasara inayopatikana sasa inazidi ile inayoweza kupatikana kwa kutambulika.
mtu ukiishiwa hoja si afadhali uchukue jembe ukalime au ukafanye shughuli nyingine za kukusaidia katika maisha yako kuliko kuanza kutoa hoja za kuokoteza na kuzileta humu kwenye jukwaa,kama una hoja mahususi si uzitoe hapa na uache kutapata kama mfa maji.
Ukiona mtu anababaika ni dalili ya kuishiwa na hoja na piam upeo wake umefika mwisho hana hoja wala hana swala la msingi bali anatafuta mahali pa kujiegemeza.
sorry kwa kukugusa. Kumbe na wewe ni mmoja wa wale walioletwa jf kwa malengo maalum. Vumilia tu maana uko kazini, ila watch out: Never waste your life obeying some fool's orders!