Watanzania wengi wakishajenga nyumba ya kuishi wanaona wamemaliza ndoto

Watanzania wengi wakishajenga nyumba ya kuishi wanaona wamemaliza ndoto

Mi niliwahi kuambiwa nisipambane kupita kiasi, maisha hayana shukrani kila siku linazuka jipya, unaweza kuchanganyikiwa, nami nikayaacha maisha kama yalivyo.

Niliambiwa utapambana sana lakini hutoenda na kitu kaburini, nikaambiwa wengi unao waona hata matajiri hufariki wakiyaacha mabilioni benki, tena mwingine alisema wapo ambao hata wakiugua wanaona shida kutumia peza zao wenyewe kujitibu wakihofia zitakwisha na wakipona wataanza upya, au kufilisika kabisa.

Niliambiwa fanya kazi tekeleza unachokihitaji, Ridhika na ulichonacho, usitafute ziada utakufa siku si zako.

Niliambiwa utajiri ni bahati, siyo kitu unaweza kukipambania, dunia hii hujaiumba wewe, walikuwepo wakafariki wakaiacha, uliikuta na utaiacha, duh.

Hapa mnaanza kunichanganya tena, kwamba tuendeleze mapambano, ya nini kama nimetosheka na sehemu nilipo?
 
Nyumba sio hitaji muhimu kwa maoni yako ww na si kwa wengine.

Hapa duniani kila mtu ana kipaumbele chake ambacho anaona ni muhimu kwake na si lazima tufanane.
Kama ww unavyo uona nyumba sio muhimu,pia na ww kuna kitu unacho kiona ni muhimu lakini mimi sioni umuhimu wake kwenye maisha yangu.

Na ndio maana kipindi ww unamshangaa mtu anaye pata pesa akaipeleka kwenye ujenzi wa nyumba itakayo dumu miaka na miaka kuna mtu akipata pesa anaenda kuzinywa pombe ambayo ndani ya dakika 10 anaenda kuzikojoa ,kuna mwingine ana zitumia kuhonga wanawake, au ana enda kuzichezea kamari zinaliwa zote.

Mkuu acha kujifariji ww kama umeshindwa kujenga ni kwasababu ya umasikini wako na si kwa sababu eti haupendi.
Yaani ww hoja yako ni sawa na kumshangaa mtu ni kwanini ananunua gari la million 70 badala ya kununua gari la milion 10 alafu na hizo tabia huwa wanazo masikini.

Umeniuliza kuwa kwani Ulaya hakuna ardhi ya kujenga?
Na ww nikuulize kwani Africa hatuna ardhi ya kujenga miundo mbinu mizuri kama iliyoko Ulaya,mbona hatujaijenga?
Au Africa hatuna ardhi ya kujenga viwanda kama vilivyoko ulaya?
Akh hapo sasa unajikanyaga umesema nyumba ni hitaji la muhimu kwa kila mtu hapo hapo umesema tusifananishe ulaya na Africa kwasabab ulaya wameendelea hawana haja ya kujenga... unajivururunganya tena 😅 unasema kutokuwa na mawazo ya kujenga ni umasikini..

Imebidi tu niattack majibu yako sababu hauijui point yako ni nini 😀
 
Shukuruni sana mmekuta wazazi wenu wamejenga, mnaishi kwenye nyumba za urithi so mnajisahau na kuja na mada za ajabu ajabu hapa eti mtu akijenga anajisahau anaona katoaboa asiee kujenga siyo sana na kununua gari show room hizo hesabu zenu za kusoma kwenye vitabu za hao motivation speaker endeleeni nazo tu na ndio maana mnazaa matoto yanakuwa mashoga kwa huu ujinga ujinga wakusiliza watu wanaoishi dunia nyingine kabisa na wewe

Hivi mnajua uhalisia wa maisha yetu watanzania au kwaku mpo mjini basi mnaona kila kitu easy tu mzee heshimu mtu anayetoka kwake watu wametoka maisha mabovu vijijini uko nyumba ya tope kaka na dada mnalala chumba kimoja choo hakuna ni kwenda vichakani tu, watu wamelelewa nyumba za kupanga kutwa wazazi kusimangwa kisa kodi, kufukuzwa nk leo hii eti kujenga nikupoteza pesa aisee acheni mawazo yakipuuzi, mtu ana mke na watoto wanne jinsia tofauti anamwambia ambeti kwenye uwekezaji asijenge hivi nchii hii nyie wageni eti

Wewe kama huna connection ya utakatishaji pesa na pesa yako ya halili acha upuuzi wa kuiga hao wanajenga ma apartment nk utakufa na pressure bure nyumba ujenge kwa milion 40 upangishe kwa laki tatu kwa mwezi hiyo milion 40 inarudi lini, mfanya biashara anayejua mzunguko wa pesa huu ujinga hafanyi

So huo upuuzi unafanya na wizi wa pesa za serikali, nk cause pesa zao wanachota tu
 
Emb ni

Emb nipe mfano wa nyumba ambayo thamani yake imepanda mfano umejenga nyumba mwaka 2000 sasahv thamani yake ni kubwa 2025 ila kiwanja cha 2000 sio sawa na cha 2025 value


A home does not generate assets since you have to pay payments, taxes and maintenance on them so therefore it is a liability.
Jiulize nyumba za Sinza zilikuwa na thamani gani mwaka 2000 na leo nyumba ile ile tena imechoka zaidi ina thamani gani?
 
Kazi ya hicho kipato Ni kwa ajili ya nini. Kukodolea macho?
Matumizi ya Pesa unayajua?
Sisemi kwamba tusijenge nyumba ni wazo zuri kujenga nyumba ila matumizi mazuri ya pesa ni yale ya kuongeza pesa. Mfano uwekezaji au kuanzisha biashara.
 
Mi niliwahi kuambiwa nisipambane kupita kiasi, maisha hayana shukrani kila siku linazuka jipya, unaweza kuchanganyikiwa, nami nikayaacha maisha kama yalivyo.

Niliambiwa utapambana sana lakini hutoenda na kitu kaburini, nikaambiwa wengi unao waona hata matajiri hufariki wakiyaacha mabilioni benki, tena mwingine alisema wapo ambao hata wakiugua wanaona shida kutumia peza zao wenyewe kujitibu wakihofia zitakwisha na wakipona wataanza upya, au kufilisika kabisa.

Niliambiwa fanya kazi tekeleza unachokihitaji, Ridhika na ulichonacho, usitafute ziada utakufa siku si zako.

Niliambiwa utajiri ni bahati, siyo kitu unaweza kukipambania, dunia hii hujaiumba wewe, walikuwepo wakafariki wakaiacha, uliikuta na utaiacha, duh.

Hapa mnaanza kunichanganya tena, kwamba tiuendeleze mapambano, ya nini kama nimetosheka na sehemu nilipo?
Yaani uko comfortable kabisa? 🙄
 
Tunapambana kutafuta hela hekeheka za kufa mtu, halafu mtu huyu akishajenga nyumba ya kuishi anaona amemaliza ndoto yake aliyokuwa anaipigania anapunguza mapambano.

Hapo yeye anatafuta hela ya kula tu basi. Niwakumbushe kujenga si maendeleo bali ni hitaji la lazima tupambane zaidi tupate maendeleo.
Ukishajenga nyumba yako wewe tafuta tu hela ya kula duniani hapa sio pakuwekeza sana
Watoto wenyewe wa kutunza mali wako wapi??
Ndio hawa hawa wanaoliwa nyuma tunawaona mitandaoni humo, mali yako watatunzaje ukijakuondoka

Afadhali Wahindi na Waarabu kidogo watoto hawana ufala wakiachiwa mali

Mtoto wa Afrika unamwachia mali anaenda kut*ombea yote tena ushukuru sana mana wanaweza kumla yeye kumbafu
 
Ukishajenga nyumba yako wewe tafuta tu hela ya kula duniani hapa sio pakuwekeza sana
Watoto wenyewe wa kutunza mali wako wapi??
Ndio hawa hawa wanaoliwa nyuma tunawaona mitandaoni humo, mali yako watatunzaje ukijakuondoka

Afadhali Wahindi na Waarabu kidogo watoto hawana ufala wakiachiwa mali

Mtoto wa Afrika unamwachia mali anaenda kut*ombea yote tena ushukuru sana mana wanaweza kumla yeye kumbafu
Inategemea umewaleaje hao watoto.
 
Rich anaweza kuwa muajiliwa imagine mtu analipwa mshahara wa millioni 10 kwa mwezi,huyo ni rich.
Utajiri haupimwi kwa mshahara wa mtu.

Utajiri unapimwa kwa kuchukua Mali za mtu kutoa Madeni.

angalia hapa👇👇

Fomula ya kuhesabu thamani halisi ya utajiri wa mtu ni:

Net Worth = Assets - Liabilities

Maana ya Vipengele

Assets (Mali)
Hizi ni vitu vyote vyenye thamani unavyomiliki.
-Mfano: nyumba, magari, ardhi, akaunti za benki, uwekezaji, biashara, mali isiyohamishika, n.k.

Liabilities (Madeni)
Haya ni malipo au deni unalodaiwa.
-Mfano: mikopo ya nyumba, mikopo ya gari, madeni ya benki, kadi za mkopo, n.k.

Mfano wa Hesabu

Assets:

Nyumba: 50,000,000
Gari: 10,000,000
Akiba ya Benki: 5,000,000
Jumla ya Assets = 65,000,000


Liabilities
:
Mkopo wa Nyumba: 20,000,000
Mkopo wa Gari: 5,000,000
Deni la Kadi ya Mkopo: 2,000,000
Jumla ya Liabilities = 27,000,000

Net Worth = Assets - Liabilities

Net Worth = 65,000,000 - 27,000,000
Net Worth = 38,000,000

Thamani halisi ya utajiri ni 38,000,000.

NB:
Kazi sio Asset, ndiyo maana utajiri haupimwi kwa mshahara wa mtu bali uwekezaji unaoufanya kupitia mshahara, Unaweza lipwa mshahara wa Milioni 10 kwa mwezi ila matumizi yako + madeni yakawa Milion7 huo ni umasikini sio Utajiri.
 
Wewe unaona million 10 ni nyingi lakini haufikirii mfanyakazi anavyolipwa pesa nyingi ndio na matumizi yake anavyoyaogeza kwenye hiyo million 10 anaweza kusevu million 2 tu huwezi amini million 8 ikaishia kwenye matumizi
Rich anaweza kuwa muajiliwa imagine mtu analipwa mshahara wa millioni 10 kwa mwezi,huyo ni rich.
 
Unge-tutafsiria kwa kisukuma ili tuelewe mnaongelea nini, ili kama nasi tunaweza kuchangia tumbaku zetu au mnataka ruby pekee.
Hapana, hapa tunajadili kuhusu huu utaratibu wa watoto kuweka pilau la sherehe kwenye mifuko ya shati zao, Je utachangia vipi Tanzania kubeba kombe la dunia?
 
Wewe unaona million 10 ni nyingi lakini haufikirii mfanyakazi anavyolipwa pesa nyingi ndio na matumizi yake anavyoyaogeza kwenye hiyo million 10 anaweza kusevu million 2 tu huwezi amini million 8 ikaishia kwenye matumizi
Sasa haya ni matumizi mabaya ya pesa shida watu wakipandishwa cheo au wakiongezwa mshahara wanapandisha na standard zao za kuishi.
 
Utajiri haupimwi kwa mshahara wa mtu.

Utajiri unapimwa kwa kuchukua Mali za mtu kutoa Madeni.

angalia hapa👇👇

Fomula ya kuhesabu thamani halisi ya utajiri wa mtu ni:

Net Worth = Assets - Liabilities

Maana ya Vipengele

Assets (Mali)
Hizi ni vitu vyote vyenye thamani unavyomiliki.
-Mfano: nyumba, magari, ardhi, akaunti za benki, uwekezaji, biashara, mali isiyohamishika, n.k.

Liabilities (Madeni)
Haya ni malipo au deni unalodaiwa.
-Mfano: mikopo ya nyumba, mikopo ya gari, madeni ya benki, kadi za mkopo, n.k.

Mfano wa Hesabu

Assets:

Nyumba: 50,000,000
Gari: 10,000,000
Akiba ya Benki: 5,000,000
Jumla ya Assets = 65,000,000


Liabilities
:
Mkopo wa Nyumba: 20,000,000
Mkopo wa Gari: 5,000,000
Deni la Kadi ya Mkopo: 2,000,000
Jumla ya Liabilities = 27,000,000

Net Worth = Assets - Liabilities

Net Worth = 65,000,000 - 27,000,000
Net Worth = 38,000,000

Thamani halisi ya utajiri ni 38,000,000.

NB:
Kazi sio Asset, ndiyo maana utajiri haupimwi kwa mshahara wa mtu bali uwekezaji unaoufanya kupitia mshahara, Unaweza lipwa mshahara wa Milioni 10 kwa mwezi ila matumizi yako + madeni yakawa Milion7 huo ni umasikini sio Utajiri.
Nakubaliana na wewe ila hiyo Mill.38 sio kipato chake ni networth yake. Watu wanatakiwa wafocus kuongeza vipato vyao na ikifika muda sahihi unaweza kuongeza tu networth yako.
 
Watu wanatakiwa wafocus kuongeza vipato vyao na ikifika muda sahihi unaweza kuongeza tu networth yako.
Kuongeza tu kipato bila kuongeza net worth ni sawa na kujaza maji kwenye kinu, Hivyo vitu inapaswa viende sambamba.

Kuongeza kipato ni kuongeza pesa zaidi, kama vile kupata mshahara mkubwa au kuanzisha biashara yenye faida zaidi. Kipato ni mtiririko wa pesa unayopokea mara kwa mara.

Kuongeza net worth inahusisha jinsi unavyotumia au kuwekeza pesa zako kwa busara, kupunguza madeni, na kuongeza thamani ya mali zako. Hii inaweza kufanikishwa hata bila kipato kikubwa, mradi una nidhamu ya kifedha.


Mfano:
•Unaweza kuongeza kipato lakini ukatumia yote kwenye matumizi yasiyo ya lazima, na net worth yako haiongezeki.


•Unaweza kuwa na kipato cha kawaida lakini ukatunza pesa zako vizuri, ukawekeza, au kupunguza madeni yako, hivyo net worth yako inaongezeka.
 
Sisemi kwamba tusijenge nyumba ni wazo zuri kujenga nyumba ila matumizi mazuri ya pesa ni yale ya kuongeza pesa. Mfano uwekezaji au kuanzisha biashara.
Bado uko palepale. Inaonekana kujenga Nyumba kwako Siyo issue.

Kumbuka: unaweza kujenga Nyumba ili kuongeza kipato (biashara ya Nyumba), au wewe anafikiri biashara Ni kufungua Duka la bidhaa za viwandani au mazao ya shambani pekee?

Kuna watu wamejenga apartments kwa ajili ya kuongeza kipato, watu wamejenga Nyumba ili kuzifanyia biashara.
 
Bado uko palepale. Inaonekana kujenga Nyumba kwako Siyo issue.

Kumbuka: unaweza kujenga Nyumba ili kuongeza kipato (biashara ya Nyumba), au wewe anafikiri biashara Ni kufungua Duka la bidhaa za viwandani au mazao ya shambani pekee?

Kuna watu wamejenga apartments kwa ajili ya kuongeza kipato, watu wamejenga Nyumba ili kuzifanyia biashara.
Mimi nilizungumzia nyumba ya kukaa na si ya kuzalisha pesa.
 
Shukuruni sana mmekuta wazazi wenu wamejenga, mnaishi kwenye nyumba za urithi so mnajisahau na kuja na mada za ajabu ajabu hapa eti mtu akijenga anajisahau anaona katoaboa asiee kujenga siyo sana na kununua gari show room hizo hesabu zenu za kusoma kwenye vitabu za hao motivation speaker endeleeni nazo tu na ndio maana mnazaa matoto yanakuwa mashoga kwa huu ujinga ujinga wakusiliza watu wanaoishi dunia nyingine kabisa na wewe

Hivi mnajua uhalisia wa maisha yetu watanzania au kwaku mpo mjini basi mnaona kila kitu easy tu mzee heshimu mtu anayetoka kwake watu wametoka maisha mabovu vijijini uko nyumba ya tope kaka na dada mnalala chumba kimoja choo hakuna ni kwenda vichakani tu, watu wamelelewa nyumba za kupanga kutwa wazazi kusimangwa kisa kodi, kufukuzwa nk leo hii eti kujenga nikupoteza pesa aisee acheni mawazo yakipuuzi, mtu ana mke na watoto wanne jinsia tofauti anamwambia ambeti kwenye uwekezaji asijenge hivi nchii hii nyie wageni eti

Wewe kama huna connection ya utakatishaji pesa na pesa yako ya halili acha upuuzi wa kuiga hao wanajenga ma apartment nk utakufa na pressure bure nyumba ujenge kwa milion 40 upangishe kwa laki tatu kwa mwezi hiyo milion 40 inarudi lini, mfanya biashara anayejua mzunguko wa pesa huu ujinga hafanyi

So huo upuuzi unafanya na wizi wa pesa za serikali, nk cause pesa zao wanachota tu
Kaka ushoga ni agenda yako nyingine kabisa hata haipo kwenye hii mada na hakuna atakaye kuzuia si umeamua😀..

ukienda kwenye mada hyo laki tatu unayo iona ni ndogo Ndio faida yako wewe kulingana na thamani ya nyumba yako..

Maisha ya kijijini ni tofauti na maisha ya mjini kijijini ardhi haina uthamani Sawa na ardhi ya mjini hasa miji iliyo endelea..

Na hyo kulala wanna chumba kimoja haimaanishi ukifanikiwa ndo uje ujenge nyumba uwalaze watoto wako wanne wanne kisa wewe ulihaso na ulilala na dada yako chumba kimoja badili maisha tengeneza nyumba pangisha wajukuu zako hawato lala njaa
 
Back
Top Bottom