Watatu walioteuliwa Ukuu wa Wilaya, akiwemo Japheth Maganga wadaiwa kukataa uteuzi

Watatu walioteuliwa Ukuu wa Wilaya, akiwemo Japheth Maganga wadaiwa kukataa uteuzi

MaDC wengi njaa tupu na ombaomba wa kutupwa. Wengine wanatembeza bakuli kwenye NGOs kuomba hela ya mafuta na service ya gari.

Kwa mtu mwenye steady stream(s) of income hawezi kukubali uDC tena huko nanjirinji ndanindani.

UDC sio kazi ya heshima maana unaweza kufutwa suddenly tena bila hata kuambiwa kwanini umefurushwa
 
Nadhani inabidi ujitafakari sana kukubali kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya, kwa sababu inabidi ujitoe kabisa kwenye profession yako na kujiondoa uwezo wa kufikiri ili uweze kwenda sambamba na makada wa chama. Ukijifanya intellectual utagombana nao kila siku, hasa unapokuta mtu wa darasa la saba na ndio anakupa maagizo wakati wewe una degree zako nne!

Hayo mambo ni kuwaachia watu wa aina ya kina Hapi na Muro.

Halafu Samia aache tabia ya kuteua watu kabla ya kuwauliza kwanza, ataumbuka sana. Nyerere akitaka kukuteua alikuwa anakuuliza kwanza, utaweza? Ukisema siwezi anakuacha. Ndio maana Malecela alipoulizwa ataweza kuwa PM, akasema ndio, akafanya sherehe kabla ya kutangazwa rasmi, alitemwa.
Hiyo ya Malecela yalitokea lini?
 
CHAMA CHA WAALIMU WASHINDANA NA "RUHANI" ?

15 December 2022
Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre
Dodoma, Tanzaniap

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha CCM Bara : Vurumai CWT, Mndeme awalipua " Msikubali kutumika na wenye nia mbaya "



Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha CCM Bara, Christina Mdeme amewataka walimu kutokubali mtu kuwaingilia na kuwavunjia umoja walionao. Mdeme ameyasema hayo leo Desemba 14,2022 wakati akizungumza katika mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) unaoendelea jijini Dodoma. “Mwalimu ni mzalendo namba moja, walimu tuendelee kusimamia uzalendo kwa manufaa ya Taifa, tusikubali mtu akatuchonganisha na tusikubali mtu akatuingilia na kutuondolea umoja wetu,”amesema Mdeme na kuibua shangwe kutoka kwa walimu hao
 
UDC? Hapana bhana.Atapelekwa Chaka balaa

Aisee, humu huwa tunamtania tu Pascal Mayalla kumhusisha na hizi nafasi. Msije mkachulia kuwa watu wakisema wapo serious. The guy is the living legend na heshima yake ni kubwa sana kuwa associated na kumsaidia rais katika ngazi ya such positions. Ni heri aendelee kumsaidia rais kulipa kodi kuliko kwenye nafasi hizo
Tunapomuomba Rais amfikirie Paschali katika teuzi zake hatutanii. Paschal ana sifa zote za kuwa kiongozi katika nafasi yoyote nchi hii: elimu, ujuzi, maarifa, uzoefu na udhubutu.
 
Nadhani inabidi ujitafakari sana kukubali kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya, kwa sababu inabidi ujitoe kabisa kwenye profession yako na kujiondoa uwezo wa kufikiri ili uweze kwenda sambamba na makada wa chama. Ukijifanya intellectual utagombana nao kila siku, hasa unapokuta mtu wa darasa la saba na ndio anakupa maagizo wakati wewe una degree zako nne!

Hayo mambo ni kuwaachia watu wa aina ya kina Hapi na Muro.

Halafu Samia aache tabia ya kuteua watu kabla ya kuwauliza kwanza, ataumbuka sana. Nyerere akitaka kukuteua alikuwa anakuuliza kwanza, utaweza? Ukisema siwezi anakuacha. Ndio maana Malecela alipoulizwa ataweza kuwa PM, akasema ndio, akafanya sherehe kabla ya kutangazwa rasmi, alitemwa.
Kusema kweli anayeteua Wakuu wa Wilaya wala siyo Rais bali chawa! Ndiyo maana maadili siyo kigezo tena cha uteuzi.
 
Ukuu wa wilaya hauna dili?

Je , hawataki kufanya kazi dhuluma?

---
Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japheth Maganga ambaye ameteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ameshiriki kuongoza mkutano wa viongozi wa chama hicho jijini Tanga huku akisema kwa sasa hawezi kueleza kwanini hajaripoti katika wilaya aliyopangiwa ya Kyerwa, mkoani Kagera

Vilevile, Maganga alihojiwa na Mkuu wa Upelelezi wa Polisi Mkoa wa Tanga na Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Tanga zaidi ya dakika 50 lakini si yeye wala wanausalama hao walioweka wazi sababu za mahojiano hayo.

Maganga na Rais wa CWT, Leah Ulaya waliteuliwa wiki iliyopita na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa wakuu wa wilaya lakini wakati wenzao wakiapishwa kwenye maeneo yao leo Jumatatu, Januari 30, 2023 wao wapo Tanga wakiongoza mkutano wa viongozi wakuu wa CWT.

Ulaya aliteuliwa kuwa DC wa Mbogwe, Mkoa wa Geita ambapo wenzake wanaapishwa leo Jumatatu na Mkuu wa Mkoa huo, Martin Shigela.

Mara baada ya kumaliza kuhojiwa na polisi kuanzia saa 4:36 hadi saa 5:24 asubuhi nje ya ukumbi wa mkutano huo unaofanyikia katika Hoteli ya Regal Naivera, Mtaa wa Bombo jijini Tanga Maganga alirejea ukumbini na baadaye kidogo alitoka nje.

Nje ya ukumbi ambapo Mwananchi Digital limeweka kambi, Magamba amesema, “kwa sasa nimeziba mdomo labda usubiri tutakapomaliza kikao ndipo nitazungumza kuhusu nafasi ya U-DC na CWT."

Wakati Maganga akisema hayo, Rais wa CWT hakutoka ndani ya ukumbi wa mkutano huo huku maofisa wa CWT wakisema hajaruhusiwa kuzungumza na vyombo vya habari.

Kitendo cha viongozi wakuu hao wa CWT kuonekana Tanga wakati wenzao wakiapishwa kimezua mjadala mitandaoni na kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa kwamba wameomba wateuliwe wengine kwenye nafasi hizo za U-DC ili kuwawezesha kuendelea na majukumu yao katika chama cha walimu.
 
Salaam Wakuu,

Japheth Maganga aliyetuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera akataa uteuzi wa Ukuu wa Wilaya alioteuliwa na Rais Samia hivi karibuni.

Japhet kasema, baada ya Kushauriana na Familia yake, alimuandikia rais Samia kumshukuru kwa kumteua pia na kumuomba atengue uteuzi wake na achaguliwe mtu Mwingine.

Wateule wengine ambao wamekataa uteuzi ni:

Leah Ulaya aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe, Mkoa wa Geita na na Dina Mathamani aliyeteuliwa kwenda Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma

Wote waliokataa Uteuzi wa Rais Samia ni Viongozi wa juu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT).

Leah Ulaya ni rais wa CWT, Dinah Mathamani ni Makamu wa Rais wa CWT huku Japheth Maganga akiwa Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT)

======

Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japheth Maganga ambaye ameteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ameshiriki kuongoza mkutano wa viongozi wa chama hicho jijini Tanga huku akisema kwa sasa hawezi kueleza kwanini hajaripoti katika wilaya aliyopangiwa ya Kyerwa, mkoani Kagera.

Vilevile, Maganga alihojiwa na Mkuu wa Upelelezi wa Polisi Mkoa wa Tanga na Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Tanga zaidi ya dakika 50 lakini si yeye wala wanausalama hao walioweka wazi sababu za mahojiano hayo.

Maganga na Rais wa CWT, Leah Ulaya waliteuliwa wiki iliyopita na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa wakuu wa wilaya lakini wakati wenzao wakiapishwa kwenye maeneo yao leo Jumatatu, Januari 30, 2023 wao wapo Tanga wakiongoza mkutano wa viongozi wakuu wa CWT.

Ulaya aliteuliwa kuwa DC wa Mbogwe, Mkoa wa Geita ambapo wenzake wanaapishwa leo Jumatatu na Mkuu wa Mkoa huo, Martin Shigela.

Mara baada ya kumaliza kuhojiwa na polisi kuanzia saa 4:36 hadi saa 5:24 asubuhi nje ya ukumbi wa mkutano huo unaofanyikia katika Hoteli ya Regal Naivera, Mtaa wa Bombo jijini Tanga Maganga alirejea ukumbini na baadaye kidogo alitoka nje.

Nje ya ukumbi ambapo Mwananchi Digital limeweka kambi, Magamba amesema, “kwa sasa nimeziba mdomo labda usubiri tutakapomaliza kikao ndipo nitazungumza kuhusu nafasi ya U-DC na CWT."

Wakati Maganga akisema hayo, Rais wa CWT hakutoka ndani ya ukumbi wa mkutano huo huku maofisa wa CWT wakisema hajaruhusiwa kuzungumza na vyombo vya habari.

Kitendo cha viongozi wakuu hao wa CWT kuonekana Tanga wakati wenzao wakiapishwa kimezua mjadala mitandaoni na kuna taarifa ambazo hazijathibitishwa kwamba wameomba wateuliwe wengine kwenye nafasi hizo za U-DC ili kuwawezesha kuendelea na majukumu yao katika chama cha walimu.

Chanzo: DC mteule ahojiwa na polisi dakika 50, Rais CWT…
Wanataka kuua chama cha waalimu.au hao jamaa ni mwiba.yaani wakireport tuu halafu wanatenguliwa.kazi inaishia hapo
 
Ndo madhala ya kuteua watu wenye ma vitengo yao tayari ya kupiga fedha (MICHANGO ya walimu nchi nzima) .
Kwani yeye ndo anafaa kuliko vijana wengine. Mtu mmoja anacover sehemu mbili as if nchi ina underpopulation ya skilled people. NDO maana watu wanataka kuchagua upinzani sio kwamba wao ni wema watatutendea mema la hasha tunataka kubadili walaji wa mali za nchi hii Kupitia KOFIA ya siasa
 
Back
Top Bottom