#COVID19 Watendaji na walimu wakuu wanavyoenda kuteseka na fedha za COVID‐19 za IMF

#COVID19 Watendaji na walimu wakuu wanavyoenda kuteseka na fedha za COVID‐19 za IMF

Tofali 500 x 1200 = 600,000, mawe lori 5 x 120,000 = 600,000, nondo 30 x 22,000 = 660,000, bati 40 x 30,000 = 1,200,000, cement 50 x 17,000 = 850,000, mchanga lori 5 x 100,000 = 500,000, misumari 20kgs x 6,000 = 120,000, fundi 1,500,000, mlango 200,000, madirisha 5 x 150,000= 750,000, maji 100,000, kokoto 300,000, vioo na ufundi 300,000, rangi na ufundi 500,000, nauli vifaa 100,000 dharura 1,000,000 jumla 9,280,00 na chenchi inabaki mkuu
We una matatizo wewe
 
Kinachowafanya wengi wasomee ualimu Wala sio hiyo passmark,mbona kuna watu kibao wana marks za kuchechemea lkn hawajawahi somea ualimu?
Wengi wanasomea ualimu kwa sababu ya umasikini na connection.Walimu wengi unaowaona laiti Kama wangekuwa na connection pia familia zao kidogo zinajiweza wasingesomea ualimu.Ukiondoa Udaktari ni kozi gani nyingine inataka marks za Juu? Vyuo vimejaaa tele ,ukikosa bongo unaenda hata nje kwa kozi uitakayo.
Umeongea ukweli mtupu...binafsi naona kozi nyingine zinahitaji alama ndogo na za kawaida tu issue ni connection, wengi walisomea ualimu ili kujikwamua ki maisha kwani ndiyo kozi pekee ilikuwa inampa ulaji wa haraka mtu yeyote tofauti na siku za hivi karibuni ambapo ajira za ualimu zimeanza kuwa adimu pia
 
Ml 20 darasa 1 mbona nyingi sana

Upumbavu mtupu na kutupotezea muda bila sababu

Milioni 20 najenga madarasa matano na hela inabaki
Aisee mara ya mwisho umejenga lini?
 
Ticha kama ticha nakuonya tena, hizi hela ni za Moto!
Ukijitoa ufahamu utamfata sabaya
 
Tofali 500 x 1200 = 600,000, mawe lori 5 x 120,000 = 600,000, nondo 30 x 22,000 = 660,000, bati 40 x 30,000 = 1,200,000, cement 50 x 17,000 = 850,000, mchanga lori 5 x 100,000 = 500,000, misumari 20kgs x 6,000 = 120,000, fundi 1,500,000, mlango 200,000, madirisha 5 x 150,000= 750,000, maji 100,000, kokoto 300,000, vioo na ufundi 300,000, rangi na ufundi 500,000, nauli vifaa 100,000 dharura 1,000,000 jumla 9,280,00 na chenchi inabaki mkuu
Darasa moja linachukua tofali 900~1000,mawe inategemeana na eneo lakini sio chini ya trip 10, nondo ni 42 maana Kuna za beam na renta, bati darasa moja ni 56,cement sio chini ya mifuko 130 kwa darasa moja, mchanga trip 8~10.
 
Tofali 500 x 1200 = 600,000, mawe lori 5 x 120,000 = 600,000, nondo 30 x 22,000 = 660,000, bati 40 x 30,000 = 1,200,000, cement 50 x 17,000 = 850,000, mchanga lori 5 x 100,000 = 500,000, misumari 20kgs x 6,000 = 120,000, fundi 1,500,000, mlango 200,000, madirisha 5 x 150,000= 750,000, maji 100,000, kokoto 300,000, vioo na ufundi 300,000, rangi na ufundi 500,000, nauli vifaa 100,000 dharura 1,000,000 jumla 9,280,00 na chenchi inabaki mkuu
Asante mkuu umemaliza
 
Tulia headmaster, mmezoea kusema choo cha shule kimejengwa kwa m20 kumbe zinajenga darasa na ofisi na makolombwezo kibao
Hujawahi hata kujenga choo wewe. Unafikiri choo Cha shule Ni tundu moja km hicho Cha kwako Cha familia.

Halafu unadhani hao wanaotoa hizo hela wanazitoa kwamba hawajui uhalisia wa kujenga darasa moja au choo Cha matundu 16 inagharimu sh ngapi kulingana na eneo husika.

Unaongea as if mwalimu mkuu ndiye anasema naomba kiasi fulani KWA ajili ya choo au darasa , km vile hamna MHANDISI WA WILAYA ambaye ndiye anatengeneza makadirio hayo.

Mnapenda sana kuleta humu jukwaani akili za vijiweni za majungu na umbea wa mtaani. Wengine hata room moja hamjawahi kujenga. Pumbavu.
 
Nawasalimu sana kwa jina la JMT yetu pendwa!

Baada ya mheshimiwa raisi kuagiza fedha za imf kwenda kwenye elimu na kujenga madarasa ili watoto wa f1 mwakani wasipate tabu ya kusubiri, na tamisemi kazipangia bajeti na kuzigawa, kazi imeanza huku chini (wilayani). Viongozi (wakurugenzi na maafisa elimu) wakiibuka na 'majuhudi' kibao ya kutaka kufanya 'maajabu' ili wawe wa mfano. Bahati mbaya sana, 'majuhudi' yao hayo, yanaenda kuwaangukia na kuwaumiza watendaji na zaidi wakuu wa shule.

Kwa siku chache tu, kuna halmashauri fulani, kwa wakati tofauti, tayari wakuu wa shule wameambiwa (of course kuamrishwa) yafuatayo:

1. Darasa lililolengwa likamilike lakini ni lazima na kitu kingine kitokee (yaani wahakikishe wameanzisha kitu kingine pia k.v boma, ofisi, choo n.k kutoka katika fedha hizo hizo)
2. Madarasa yawekwe marumaru (tiles)
3. Bati ziwekwe za msouth
4. Madirisha ya aluminium
5. Mfumo wa umeme wote ukamilike

Barua za kuwakabidhi fedha hizo zinaandaliwa kwenda kwa wakuu hao kwa majina yao na atakayeshindwa kukamilisha majengo hayo kwa viwango tajwa kazi anayo. Ikumbukwe kuwa fedha zilizotolewa ni m.20 tu kwa chumba kimoja cha darasa. Hapo sidhani kama watendaji na wakuu hawa watakuwa na ujanja mwingine wowote zaidi ya kurudi kwa wanakijiji kuwaambia wajitolee.

AISEE! Kujitolea kipindi hiki ni vigumu kuliko maelezo, siajabu kijiji cha watu 2000 wakajitolea watu 7 tu tena kwa siku mbili tu.

Wakuu wa shule kiukweli kazi wanayo. Huku mitihani ya kitaifa, kule ujenzi uliyoongezewa maagizo. Dah!!!
Hizo kazi wafanye kwa Fosi Akaunti na fundi Maiko.
Hakuna mkandarasi atafanyakazi na wanasiasa.
 
Kwa thamani ya miloni 20 inatosha ba marupurupu wanabakiza


Kwa hiyo mh mwalimu kuwa mpole tu
KWA standard ya darasa la viwango bora Ni hela ndogo sana.

Ninaongea KWA uzoefu. Siyo maneno ya mtaani.

Mwananchi wa kawaida walio wengi wanaona darasa ni tofali zilizopangwa tu ukaweka paa na mlango wanafunzi wanaingia.
 
Darasa haliwezi kuzidi milioni 12
Duuh nikupa mkuu utajenga! Yaani unaongea kabisa ukiwa na akili zako timamu.
Uchimbe msingi, umwage jamvi na nondo zake, cement, mchanga kokoto, hela ya fundi, tofali , plasta, upauwe bati na mbao zake madirisha manne au matano. Duuuuh!

Akili za maskini hizi
 
Duuh nikupa mkuu utajenga! Yaani unaongea kabisa ukiwa na akili zako timamu.
Uchimbe msingi, umwage jamvi na nondo zake, cement, mchanga kokoto, hela ya fundi, tofali , plasta, upauwe bati na mbao zake madirisha manne au matano. Duuuuh!

Akili za maskini hizi
Anazingua huyu!
 
KWA standard ya darasa la viwango bora Ni hela ndogo sana.

Ninaongea KWA uzoefu. Siyo maneno ya mtaani.

Mwananchi wa kawaida walio wengi wanaona darasa ni tofali zilizopangwa tu ukaweka paa na mlango wanafunzi wanaingia.
Usilete maneno mengi naomba tafadhali huo mchanganuo wa gharama kwa darasa
 
Watu ni wezi saana dunia hii


Wacha niweke boq ili tuone uhalisia wa hiyo pesa.
Pia kumbuka serikal inataka madarasa mawili tu yaliyokamilika.
Kuweka ofisi +fanicha ni kujiongeza tu.
Pia tukumbuke kwamba ujenzi huu utatumia local fundi ili kubana matumizi na pia vifaa utanunua kwa mzabuni aliyepo karibu kulingana na ushindani wa bei japo pia unaweza kubana matumizi zaidi kwa kununua kwa jumla na pia kununua viwandani na pia kutumia local materials kama mawe na mchanga kama upo karibu n.kView attachment 1982268
 
Wakuu wa shule siku hizi mtamu, wanapewa posho ya madaraka nje ya mshahara.

Mkui wa shule ( primary ) = Tsh 150,000

Headmaster= Tsh 200,000.

Na watendaji wako kwenye process za kuanza kupewa posho ya Tsh 100,000 kwa mwezi nje ya mshahara.

Hivyo, utamu wa posho ni lazima uendane na majukumu.

Kijana Acha kulia lia.
Kitu usichokijua nyamaza. Pumbavuuu
 
kama ni hivyo Basi mkuu wa shule afanye haya:-
1.kila mfuko saruji utoe tofali arobaini!
2.jamvi la molam na sio kokoto na nondo!!
3.Resho(ratio) ya mchanga na saruji iwe chini!ya kujengea ndoo 35 kwa mfuko!!
4.kenchi ziwe chache halafu bati gauge 32 tena zipakwe rangi nzuri ya Bati!!!
 
Back
Top Bottom