Watoto wa Lemutuz walikataa kumsamehe baba yao...


Baraka za Mungu hupita kwa baba kwenda kwa mtoto
Na baraka sio pesa wala Mali, baraka ni maneno

Nilisikitika sana wale watoto kumtolea baba yao yale maneno na mama yao kukaa kimya

Wazazi, hata mzazi mwenzio akiwa mbaya kiasi gani kumbuka tuu watoto kumheshimu ni amri sio ombi. Tena ni amri pekee yenye baraka ndani yake. Ukimpenda mtoto wako jitahidi aheshimu watu wote haswa wazazi

Rest well Lembebiz
 
Mitoto ikishalelewa au kuwa upande wa mama watakiwa iacha usiiweke karibu maana inakuwa na akili za kike
Na wengi mnakuwa na mawazo ya hovyo kama hayo ila inafika muda hao hao wenye akili za kike ipo siku utawahitaji tu au utawakumbuka maana ni damu yako, Sasa wengine huwatamkia kabisa watoto hayo uliyoyaandika halafu ati unawaomba msamaha, anaweza kutokea labda mmoja akusamehe lakini si wote, ushauri chungeni midomo yenu wakati mlakula starehe au mnapojifanya ati mmewasusa watoto wakikua itawagharimu tu

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Wakikuelewa nistue

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Nyie jichanganyeni tutawaacha na watoto wenu na haturudi nyuma
 
Nashangaaa mno mtu unashndwa kusamehe, mimi nasamehe hata mtu asiponiomba msamaha.
 
Watoto wanaomkataaga Baba yao huwa hawafikagi mbali. Wanakiwa na hisia sana, hawajali chochote wala kumsikiliza mtu yoyote mpaka wakutana na watoto wa mama wenzao hapo ndo hutokea mengi.
Nakuunga mkono na mguu pia, watoto kumdharau baba yao ni laana. Hata baba Mungu hatowasamehe na wao, kina Kanumba waliowaumbua baba zao mitandaoni wapo wapi!! Biblia inasema waheshimu BABA na mama yako upate miaka mingi na yenye heri duniani.
 
mkuu achana na hizi story za watu ambao hawana experience zaidi ya kuhadithiwa, hakuna mtoto mjinga hata alishwe sumu kiasi gani asijue umuhimu wako ukionesha efforts. Kuna watu tumeona hawakulelewa na baba zao ili walipowatafauta na wakaoneshwa ushirikiano hadi leo wapo peace tu, japo kuna waliotafuta na bado wakakanwa walipowapata. so, hali halisi itategemeana na wewe utataka kujenga bond gani na mtoto wako kwa sababu yeye hakuwaomba mumzae na hakuna njia yoyote utakayoweza kuhalalisha kumfanya ateseke ili wewe uishi peaceful life

unachoweza kufanya ni kujipa space kwa muda kama unaona relationship na mama mtoto ni ngumu kiasi cha kupelekana polisi, hapo chill ila kama kuna mtu wa karibu yake anaeweza kukupa info za maendeleo ya mtoto ni vyema ukawa unatumia kumjua mtoto anaendeleaje

nakumbuka tulipokuwa wadogo, kuna mother mmoja alifukuzwa na mumewe akapigwa ban kuona hadi watoto wake ila mtoto wake mmoja tulikuwa tunasoma nae kwa hiyo kila time ya mapumziko asubuhi yule mother alikuwa anafika duka flani lipo shule, kumuona mwanae na mimi nilishawahi kumuitia 3 times. Hii ndio bond na mtoto sio mpuuzi anaona, hakuna sumu itakayofanya kazi ukiwa active ila ukiamua kupotea, watoto wakahangaika huku wanakuona unakula bata na vimada instagram, hizo sumu zitafanya kazi tu
 
Ugomvi wake na yule dada wa state sijuagi chanzo ni nini maana yule dada alikuwa anamkandia sana.

RIP
Ulianza wakati Mange alipost Nyumba na Kaburi la Mama Yake Le Mutuz huko Mbeya. From there ndio wakaanza ugomvi. Mange Pia alipost Passport take ikionesha alizaliwa 1960, jamaa ndio alikasIrika Vita ikaendelea to-date.
 
Wale watoto ni matokeo ya mama kuwahusisha kwenye ugomvi na baba yao....

Wanaume tuwe makini sana na upstairs za wanawake tunaotaka wawe mama wa wenetu.

Mange anaamini ataishi milele.
 
Le Mutuz ana story nzima ya maisha yake humu JF. Sisi kama wanaume tunakubali kwamba Le mutuz ni mwanaume aliyejikwaa kwa mwanamke wa hovyo. Watoto wamekosanishwa na baba yao na mama yao. Nawaonea huruma sababu hii laana itawatafuna
Tupe link boss tuisome
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…