Madam Mwajuma
JF-Expert Member
- Sep 13, 2014
- 7,071
- 6,753
We jamaa noma sana1. Unalia sababu umechapwa, utachapwa tena
2. Umechapwa hukulia utachapwa tena
3. Ukijililia tu bila kupigwa, utachapwa
4. Kusimama wakati wazee wameketi, utachapwa
5. Ukiketi wakati wazee wamesimama. utachapwa
6. Kujipitishapitisha mahali ambapo wazee wamekaa, utachapwa .
7. Kuwajibujibu watu wazima, utachapwa
8. Usipomjibu mtu mzima, utachapwa
9. Kujifanya sugu wakati wa unachapwa, utaendelea kuchapwa.
10. Ukitoka kuchapwa, ukaimba au kupiga mruzi, utachapwa tena.
11. Usiposalimia wageni, utachapwa
12. Ukila chakula cha wageni, utachapwa.
13. Kuwalilia wageni wanapo ondoka, utachapwa.
14. Ukikataa kula, utachapwa..
15. Kuchelewa kurudi nyumbani baada ya jua kutua, utachapwa
16. Kula nyumba ya jirani, utachapwa.
17. Kujitia kisirani, utachapwa.
18. Kujitia kujuwa juwa sana, utachapwa.
19. Ukipigana na mtoto mwenzio, akakupiga ukirudi nyumbani, utachapwa.
20. Ukipigana na mtoto mwenzio, ukampiga ukirudi nyumbani, utachapwa.
21. Ukiwa unakula chakula polepole, utachapwa.
22. Ukiwa unakula haraka haraka, utachapwa.
23. Ukiwa unakula sana, utachapwa.
24. Kuendelea kulala wakati wazee wamesha amka tayari, utachapwa.
25. Ukiwa unawaangalia wageni wakati wanakula, utachapwa.
26. Ukitembea na mtu mzima, ukajikwaa na ukaanguka, utachapwa.
27. Ukitembea na mtu mzima, akajikwaa ukamcheka, utachapwa.
28. Ukijamba mbele ya wakubwa, utachapwa.
29. Mtu mzima akijamba, ukamwangalia, utachapwa.
30. Ukila na wakubwa ukachukua nyama bila ya wakubwa,utachapwa
31.Ukinawa bila ya wakubwa,Utachapwa
32.Ukimaliza kula ukanyanyuka bila ya wakubwa,Utachapwa
33.Umechelewa kutoka dukani,Utachapwa
34.U..........
KAMA UMEPITIA MALEZI HAYA NA UKAKOSA HESHIMA BASI WEWE NI KONKODIII
-kijiji cha ujamaa
-wadudu wana maajabu
-Nondo mla watu
-sadiki na sikiri
1: Nani atamfunga paka kengele?
2: Sikulamba sukari
3: Mua uliozamisha meli
4: Hawafu mwenye nguvu
5: Sizitaki mbichi hizi
6: Sadiki na Chitemo
7: Juma na Uledi
8: Chopeko na mnofu
9: Kibanga ampiga mkoloni
10: Siku ya gulio Katerero
[HASHTAG]#OldSkulz[/HASHTAG]
[emoji38]....ilikuwa ni balaaa ..Ng'ombe wakizamia mashambani
Utachapwa
Usipooga utachapwa
Ukioga usitakate utachapwa
Ukiachwa nyumbani usipofagia uwanja utachapwa
Ukifagia na using'oe vijani utachapwa
Usipoandika darasani utachapwa
Ukiandika ila mwandiko mbaya utachapwa
Usipokariri tebo utachapwa
Ukikariri tebo ukasahau kidogo utachapwa
Usipolima utachapwa
Ukilima ungoe mmea utachapwa
Dah yaani umenikumbusha mbali mjinga wewe
No mkuu,inamsaidia kwa sababu usipomchapa utamwendekeza ujinga na atakudharau...coz kwa mtoto mdg nijuavyo mimi huwezi mshauri.AU UNASEMAJE WEWE,Kuchapa mtoto ni ujinga mwingine mwafrika anauendeleza.
[emoji38]..hongera nyingi zikuendee mkuuHahaha mzee wangu na mama walitulea hivyo mi na mdogo wangu yaani ukikaa vibaya unachapwa[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] Walipoacha hii kanuni kwa wadogo zetu wengine wamekuja kuwa wa ajabu sana wajeuri mno.
Sisi hadi sasa tukiambiwa kitu chaapu tunafanya na uzee wetu wale madogo watahoji hoji kama Chadema.
Pamoja mkuuu..We jamaa noma sana
Sante mkuu
[emoji38]No 14. Hiyo nilichezea hatar
[emoji38][emoji38][emoji38]Unacheza mpira au komborela mpaka giza linaingia,hamna anayekuuliza.
Ukirudi umejikausha ktk kochi unasubiri ubwabwa,huku na kibaridi kingi bimkubwa analiamsha dude.kosea useme maji ni ya baridi utalala vibaya siku hiyo,inabidi uende kinyonge kwenda kujipaka maji na kunawa miguu,ila ukitoka bafuni ukaguzi unakuhusu.
Hiki ndo kitu ambacho kitaharibu hata maadili ya baadae,Vitoto vya siku hizi kikiguswa tu kinakupeleka dawati. Tunajenga jamii gani. Ndio maana wengine wanashabikia maandamano bila kujua hata lengo la maandamano sababu hawakuchapwa.
Hii niliichezea sanaaaUsipopokea wakubwa mizigo Utachapwa tehe tehe tee
[emoji38][emoji38][emoji38]Siku hizi haki za watoto zinazingatiwa sana...
Na pia utandawazi umepelekea hayo yote kuonekana ya kawaida...
Siku hizi unakuta mtoto anajibizana na baba au mama yake kisa remote ya TV...
Cc: mahondaw