Watoto wa siku hizi hawajui kabisa enzi zetu uliweza kuchapwa kwa sababu zifuatazo...

Watoto wa siku hizi hawajui kabisa enzi zetu uliweza kuchapwa kwa sababu zifuatazo...

Hahaha mzee wangu na mama walitulea hivyo mi na mdogo wangu yaani ukikaa vibaya unachapwa[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] Walipoacha hii kanuni kwa wadogo zetu wengine wamekuja kuwa wa ajabu sana wajeuri mno.
Sisi hadi sasa tukiambiwa kitu chaapu tunafanya na uzee wetu wale madogo watahoji hoji kama Chadema.
 
1. Unalia sababu umechapwa, utachapwa tena

2. Umechapwa hukulia utachapwa tena

3. Ukijililia tu bila kupigwa, utachapwa

4. Kusimama wakati wazee wameketi, utachapwa

5. Ukiketi wakati wazee wamesimama. utachapwa

6. Kujipitishapitisha mahali ambapo wazee wamekaa, utachapwa .


7. Kuwajibujibu watu wazima, utachapwa

8. Usipomjibu mtu mzima, utachapwa

9. Kujifanya sugu wakati wa unachapwa, utaendelea kuchapwa.

10. Ukitoka kuchapwa, ukaimba au kupiga mruzi, utachapwa tena.

11. Usiposalimia wageni, utachapwa

12. Ukila chakula cha wageni, utachapwa.

13. Kuwalilia wageni wanapo ondoka, utachapwa.

14. Ukikataa kula, utachapwa..

15. Kuchelewa kurudi nyumbani baada ya jua kutua, utachapwa

16. Kula nyumba ya jirani, utachapwa.

17. Kujitia kisirani, utachapwa.

18. Kujitia kujuwa juwa sana, utachapwa.

19. Ukipigana na mtoto mwenzio, akakupiga ukirudi nyumbani, utachapwa.

20. Ukipigana na mtoto mwenzio, ukampiga ukirudi nyumbani, utachapwa.

21. Ukiwa unakula chakula polepole, utachapwa.

22. Ukiwa unakula haraka haraka, utachapwa.

23. Ukiwa unakula sana, utachapwa.

24. Kuendelea kulala wakati wazee wamesha amka tayari, utachapwa.

25. Ukiwa unawaangalia wageni wakati wanakula, utachapwa.

26. Ukitembea na mtu mzima, ukajikwaa na ukaanguka, utachapwa.

27. Ukitembea na mtu mzima, akajikwaa ukamcheka, utachapwa.

28. Ukijamba mbele ya wakubwa, utachapwa.

29. Mtu mzima akijamba, ukamwangalia, utachapwa.

30. Ukila na wakubwa ukachukua nyama bila ya wakubwa,utachapwa

31.Ukinawa bila ya wakubwa,Utachapwa

32.Ukimaliza kula ukanyanyuka bila ya wakubwa,Utachapwa

33.Umechelewa kutoka dukani,Utachapwa
34.U..........

KAMA UMEPITIA MALEZI HAYA NA UKAKOSA HESHIMA BASI WEWE NI KONKODIII

-kijiji cha ujamaa
-wadudu wana maajabu
-Nondo mla watu
-sadiki na sikiri
1: Nani atamfunga paka kengele?
2: Sikulamba sukari
3: Mua uliozamisha meli
4: Hawafu mwenye nguvu
5: Sizitaki mbichi hizi
6: Sadiki na Chitemo
7: Juma na Uledi
8: Chopeko na mnofu
9: Kibanga ampiga mkoloni
10: Siku ya gulio Katerero

[HASHTAG]#OldSkulz[/HASHTAG]
We jamaa noma sana
Sante mkuu
 
Ng'ombe wakizamia mashambani
Utachapwa

Usipooga utachapwa

Ukioga usitakate utachapwa

Ukiachwa nyumbani usipofagia uwanja utachapwa

Ukifagia na using'oe vijani utachapwa

Usipoandika darasani utachapwa

Ukiandika ila mwandiko mbaya utachapwa
Usipokariri tebo utachapwa
Ukikariri tebo ukasahau kidogo utachapwa
Usipolima utachapwa
Ukilima ungoe mmea utachapwa

Dah yaani umenikumbusha mbali mjinga wewe
[emoji38]....ilikuwa ni balaaa ..
 
Kuchapa mtoto ni ujinga mwingine mwafrika anauendeleza.
No mkuu,inamsaidia kwa sababu usipomchapa utamwendekeza ujinga na atakudharau...coz kwa mtoto mdg nijuavyo mimi huwezi mshauri.AU UNASEMAJE WEWE,
 
Hahaha mzee wangu na mama walitulea hivyo mi na mdogo wangu yaani ukikaa vibaya unachapwa[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] Walipoacha hii kanuni kwa wadogo zetu wengine wamekuja kuwa wa ajabu sana wajeuri mno.
Sisi hadi sasa tukiambiwa kitu chaapu tunafanya na uzee wetu wale madogo watahoji hoji kama Chadema.
[emoji38]..hongera nyingi zikuendee mkuu
 
Ukitumwa ukamaliza nusu saa utachapwa,

Ukienda kuzurula kwa jirani utapigwa tu,

Ukipanda juu ya miti narudia kusema utapigwa tu,

Usipokunywa dawa utapigwa tu..

Ikisadikika umetukana utapigwa tu hata mtu ukihisiwa,



Etc etc
 
Unacheza mpira au komborela mpaka giza linaingia,hamna anayekuuliza.

Ukirudi umejikausha ktk kochi unasubiri ubwabwa,huku na kibaridi kingi bimkubwa analiamsha dude.kosea useme maji ni ya baridi utalala vibaya siku hiyo,inabidi uende kinyonge kwenda kujipaka maji na kunawa miguu,ila ukitoka bafuni ukaguzi unakuhusu.
 
Kuwajibujibu watu wazima, utachapwa
Usipomjibu mtu mzima, utachapwa
dah aya mambo haya umenikumbusha mbali sana, nailikua ivyo kweli nilikua nakosa amani sana kukosa haki ya kujieleza, mpaka leo katika vyote hiki naonaga nilionewa sana bora makosa mengine nichapwe tu
 
Vitoto vya siku hizi kikiguswa tu kinakupeleka dawati. Tunajenga jamii gani. Ndio maana wengine wanashabikia maandamano bila kujua hata lengo la maandamano sababu hawakuchapwa.
 
Siku hizi haki za watoto zinazingatiwa sana...

Na pia utandawazi umepelekea hayo yote kuonekana ya kawaida...

Siku hizi unakuta mtoto anajibizana na baba au mama yake kisa remote ya TV...

Cc: mahondaw
 
Unacheza mpira au komborela mpaka giza linaingia,hamna anayekuuliza.

Ukirudi umejikausha ktk kochi unasubiri ubwabwa,huku na kibaridi kingi bimkubwa analiamsha dude.kosea useme maji ni ya baridi utalala vibaya siku hiyo,inabidi uende kinyonge kwenda kujipaka maji na kunawa miguu,ila ukitoka bafuni ukaguzi unakuhusu.
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Siku hizi haki za watoto zinazingatiwa sana...

Na pia utandawazi umepelekea hayo yote kuonekana ya kawaida...

Siku hizi unakuta mtoto anajibizana na baba au mama yake kisa remote ya TV...

Cc: mahondaw
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Back
Top Bottom