Watoto wa viongozi wakuu wa nchi walipwe ili kuwatia moyo

Hii nchi tunapoelekea sijui maana wanasiasa wanazidi kuleta machukizo makubwa ndani ya jamii
 

Nitukane mkuu. Nitawaomba Mods Kwa uamuzi wangu na hiyari yangu mimi mtukanwaji ambaye ndiye mlengwa na ninayetakiwa kulalamika, wasikupige Ban wala wasikupe adhabu yoyote.

Tukiachana na hasira zako, nini ambacho kimechochea hasira zako kutokana na maoni yangu?
 
Tusiishie hapo tu hata wakwe zao yaani ukioa au kuolewa kwenye familia ya kiongozi pia ulipwe, ndugu wajomba mashangazi mabinamu na wajukuu wote walipwe.

Mpaka wafanyakazi wa ndani na wafungua mageti na madereva pia walipwe na serikali tena.

Maoni yangu naomba yaheshimiwe.👆✌️
 
Machawa watalipwa na Maboss zao.
Ila sisi wananchi tumeamua kulipa watoto wa viongozi wetu.
Ninyi wenye wivu hamna nafasi. Gombeeni muwe viongozi ili nanyi tuwalipe. Kwani shida nini
Tena waambie kabisa wagombee hadi wahakikishe wanashinda. Wakishindwa wagombee tena. Nchi tamu sana hii[emoji3]
 
kuna elimu ya utani,unafiki na uzandiki ilikua inatolewa CUBA nafikiri wewe hukubatika kuchaguliwa kusomea hii kozi?
 
Watoto wa kamishna wa magereza walipwe.
Watoto wa kamishna wa zimamoto na uokoaji walipwe.
Watoto wa kamishna wa tra walipwe
Kamishna wa madawa ya kulevya
Watoto wa watumishi wote wa umma walipwe maana sisi watumishi tunafanya kazi kwa uzalendo
 
Machawa watalipwa na Maboss zao.
Ila sisi wananchi tumeamua kulipa watoto wa viongozi wetu.
Ninyi wenye wivu hamna nafasi. Gombeeni muwe viongozi ili nanyi tuwalipe. Kwani shida nini
mkuu watoto wao wanunuliwe crown au subaru forester halafu ziwe na plate number maalumu ili wasisumbuliwe barabarani
 
Reactions: EEX
Kuna hawa wanoitwa "chawa" me nadhani na wenyewe waingizwe pay rol mana na wenyewe wana sifa kama za "wake za Viongozi" au hili unalionaje ndugu mwandishi?
Jomba unataka kusemaje?. Kwamba Viongozi nchi hii ni wanaume tu?[emoji3]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…