Watoto wawili wa familia moja wapotea baada ya kuaga wanakwenda shule Julai 24, 2024

Watoto wawili wa familia moja wapotea baada ya kuaga wanakwenda shule Julai 24, 2024

Bora hata Hao ni wakubwa. Mara nyingi nimekutana na watoto wadogo kuliko Hao (wa miaka 4 na 5) wakiniomba niwavushe highway wanaenda shule peke yao. Mzazi yupo nyumbani amelala kwa Amani kabisa. Hivi si mzazi angesogea nao awavushe Ila Hali ya kupuuza had na yan litokee
Kwakweli umasikini usiwe kisingizio cha negligence ya kiasi hicho, mtoto wa miaka mi4 ni wa kumuacha akavuke barabara bila msimamizi? Hakafu likitokea la kutokea mtu analia kabisa yaan.., utadhani sio yeye aliyewaacha wajisimamie..
 
Mungu watunze hawa watoto. Tumeshindwa kuwatunza wanasakwa kama wanyama. Wanapotea kama pin. Watunze mwenyezi Mungu kama upo.
 
Hii sasa imeshakuwa zaidi ya hatari.
Nikijaribu kuwaza nje ya Box, nahisi huenda ni zaidi ya uchaguzi.
Huenda kuna kundi Fulani Lina interest na hawa watoto, linawatumia either kama nguvu kazi, au Kwa manufaa mengine.
Serikali tunaomba itilie mkazo.
 
Mbona watoto wake huyo mama kawaanzisha shule mapepo alikuwa anakimbilia nini?
Miaka 9 darasa la 5 hapo dogo anamaliza chuo akiwa mdogo hawezi kujipambania. Asipotafutiwa ajira na mjomba anakuwa mtoto wa kula andazi kwa mama huku ndani ana degree
 
Waanze na hilo daladala, waulizwe walipowashusha
Hii ni sawa. Naunga mkono hatua hii. Tena waseme walishuka na nani mahali ambapo sio shuleni?? Hapo waliposhushiwa na aliyeshuka nao pamulikwe vizuri.
Unamshushaje mtoto wa shule mahali ambapo sio shuleni?
 
Yaani shule ndio kwanza zimetoka kufunguliwa july hii ila kwa hali hii unatamani hata zifungwe tena mpaka uchaguzi uishe. Wanasiasa tunaomba watoto wetu wasome kwa amani plz,kama vipi toeni hao wa kwenu mliowazaa😡
 
Hii sasa imeshakuwa zaidi ya hatari.
Nikijaribu kuwaza nje ya Box, nahisi huenda ni zaidi ya uchaguzi.
Huenda kuna kundi Fulani Lina interest na hawa watoto, linawatumia either kama nguvu kazi, au Kwa manufaa mengine.
Serikali tunaomba itilie mkazo.
Hili linawezekana kabisa. Kuna mahali nilisoma article inasema watoto 7-14yrs. wanatekwa na huko wanakopelekwa huwekwa kama watumwa wa kingono, kutumikishwa kazi kandamizi e.g. majumbani, migodini au majumba ya starehe(Cassino) au kuuzwa kama bidhaa - kibiashara.
Mungu aturehemu na kutuepushia hii balaa. Inauma na kusikitisha sana.
 
Nilirudi nyumbani kulala na asubuhi nilikwenda tena shule kuulizia wakasema hawajawaona, ndipo nikarudi tena Polisi.
UNAPATAJE AMANI NA UTULIVU UKALALA, HUKU HUJUI WATOTO WAKO WAPI?


Hii sheria/utaratibu wa kusubiri yapite masaa 24, hatuwezi kuibadirisha hasa kipindi hiki cha wimbi la watoto kutekwa?
Hatua za mwanzo za kusmbaza picha za watoto zinge anza.
kukagua magari yote yanayotoka nje ya mji.wilaya, mkoa
 
Yaani shule ndio kwanza zimetoka kufunguliwa july hii ila kwa hali hii unatamani hata zifungwe tena mpaka uchaguzi uishe. Wanasiasa tunaomba watoto wetu wasome kwa amani plz,kama vipi toeni hao wa kwenu mliowazaa😡
Wahenga Walisemaga "Kikulacho ki nguoni mwako" Kama Usalama wa Raia wakichachamaa na kulikomalia jambo hili (wakilishikia bango)naamini watoto watapatikana. Vinginevyo washirikishwe (lakini kwa malipo)bodaboda na vijana wengine wanusaji.
 
Kwakweli umasikini usiwe kisingizio cha negligence ya kiasi hicho, mtoto wa miaka mi4 ni wa kumuacha akavuke barabara bila msimamizi? Hakafu likitokea la kutokea mtu analia kabisa yaan.., utadhani sio yeye aliyewaacha wajisimamie..
Saa ingine sjui ni Hali ya kutojalii sjui hata
 
Nilirudi nyumbani kulala na asubuhi nilikwenda tena shule kuulizia wakasema hawajawaona, ndipo nikarudi tena Polisi.
UNAPATAJE AMANI NA UTULIVU UKALALA, HUKU HUJUI WATOTO WAKO WAPI?


Hii sheria/utaratibu wa kusubiri yapite masaa 24, hatuwezi kuibadirisha hasa kipindi hiki cha wimbi la watoto kutekwa?
Hatua za mwanzo za kusmbaza picha za watoto zinge anza.
kukagua magari yote yanayotoka nje ya mji.wilaya, mkoa
Hii Sheria /Utaratibu (wanavyodai Polisi)ni kwamba wanakupa muda kwa wewe kujiridhisha kwamba fulani amepotea. Kwa upande mwingine hili sio sawa kwani ni kama kumpa nafasi mhalifu-mtekaji azidi kusonga mbele au kuficha uovu wake.
Kuibadilisha ni jambo jepesi sana. Ni Wakubwa watamke tu.
 
Watoto wawili wa familia moja wamepotea katika mazingira ya kutatanisha mkoani Arusha, baada ya kuaga wanakwenda shule jana Julai 24, 2024, lakini hawakurudi nyumbani na mpaka leo hawajaonekana popote.

Watoto hao wanaosoma Shule ya Msingi Olosiva, wilayani Arumeru, wamedaiwa kupotea baada ya kupandishwa kwenye daladala wakielekea shuleni, lakini hawakufika shule na wala hawakurudi nyumbani.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, SACP Justine Masejo amethibitisha kupokea taarifa hiyo leo Julai 25, 2025 asubuhi na wameanza kuifanyia kazi.

“Tumepata taarifa hiyo leo asubuhi na tunaifanyia kazi, tutakapopata chochote cha kuwaeleza tutawaambia kesho,” amesema SACP Masejo.

Akisimulia tukio hilo leo Alhamisi Julai 25, 2024, mama mzazi wa watoto hao, Elizabeth Modesta (31), amewataja watoto hao kuwa ni Mordekai Maiko (7) anayesoma darasa la tatu na Masiai Maiko (9) anayesoma darasa la tano.

Amesema jana aliwaandaa kwenda shule kama kawaida na kwenda barabarani kuwapakia kwenye daladala kuelekea shuleni.

“Kawaida saa 9:30 hadi au saa 9:45 jioni wanakuwa wamefika, lakini jana hadi saa 10 walikuwa hawajafika. Niliamua kwenda shule saa 11 jioni kuulizia nikaambiwa tangu asubuhi watoto hao hawajaonekana shule. Nikachanganyikiwa na kwenda kutoa taarifa kituo cha polisi Ngaramtoni,” amesema mama wa watoto hao.

Amesema alipofika polisi walimtaka arudi nyumbani na kusubiri hadi saa 24 kama wasipoonekana ndio arudi kwa ajili ya kukata ripoti namba (RB Namba) na kuanza kutafutwa.

“Nilirudi nyumbani kulala na asubuhi nilikwenda tena shule kuulizia wakasema hawajawaona, ndipo nikarudi tena Polisi, nikapewa RB namba NGT/RB/1265/2024, wakataka picha za watoto, ili wasambaze mitandaoni na namba yangu, nikawapa, sasa nasubiri majibu,” amesema Elizabeth.

Mama huyo ametumia nafasi hiyo kuiomba Serikali na wananchi kumsaidia kuwapata watoto wake popote watakapoonekana.

“Kwa sasa napiga tu simu kwa marafiki wanisaidie kusambaza picha za wanangu, maana nimetembea kila mahala siwaoni. Naomba walimwengu wanisaidie, popote watakapowaona wanangu wanisaidie kuwapeleka polisi, maana nafsi yangu kwa sasa imeinama kwa kweli, namwomba tu Mungu wasidhurike huko walipo hadi niwapatikane,” amesema huku akilia kwa uchungu.

Mkuu wa shule ya msingi Olosiva, Mwenzine Msuya amesema tangu jana watoto hao wanajaonekana shuleni na leo wameuliza wanafunzi kwenye halaiki ya asubuhi (paredi), lakini wamesema hawajawaona.

“Hawa watoto hawana tabia ya kutofika shule kabisa na hata jana mama yao alipokuja kuuliza tukashangaa na leo asubuhi pia amekuja, hawapo. Tunaendelea kusambserikaki aza picha kwa ajili ya kutoa taarifa za kupotea kwao, yoyote atakayewaona awasiliane na mama yao au kituo chochote cha Polisi,” amesema mwalimu huyo.

Chanzo: Mwananchi
Serikali itangaze hali ya hatari na kufunga shule zote, watoto wetu hawapo salama.
 
Mungu watunze hawa watoto. Tumeshindwa kuwatunza wanasakwa kama wanyama. Wanapotea kama pin. Watunze mwenyezi Mungu kama upo.
Hii komenti yako imenifurahisha sana.

Hii komenti yako inadhihirisha kwamba,

Watu wengi mna mashaka na uwepo wa huyo Mungu mnaye aminishwa na kuhubiriwa kila siku kwamba ana upendo na ulinzi wa kutosha kwa watu.

Ilhali kiuhalisia hayupo, Ndio maana matukio kama haya hayawezi kudhibitiwa au kukomeshwa kabisa na huyo Mungu anaye aminiwa yupo mwenye ulinzi na upendo.
 
Back
Top Bottom