Watu 12 wakamatwa kwa kula hadharani mchana Zanzibar

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu kumi na mbili kwa tuhuma za kukutwa wakila mchana hadharani kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan ambao wanaifanya kuwa idadi ya watu waliokamatwa kwa tuhuma za kutenda makosa mbalimbali kufikia sitini na mbili

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini magharibi Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Abubakar Khamis Ally amesema kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikiwaonesha baadhi ya watu katika eneo la viwanja vya mnazi mmoja Zanzibar wakila hadharani wakati wa mchana wa Ramadhani, Jeshi hilo lilifanya msako na kuwakamata watu wapatao kumi na mbili wakiwa na vielelezo ambapo amesema wanaendelea na taratibu nyengine ili kuwafikisha Mahakamani.

Aidha ameyataja makosa mengine ni pamoja na unyang’anyi, Madawa ya kulevya na makosa mengine ambapo watuhumiwa wanashikiliwa na Polisi na wengine tayari wameshahukumiwa Mahakamani.

Pia soma:
 
Zanzibar being predominantly Muslim, during Ramadan, everyone is expected to adhere to the Islamic teachings of fasting from dawn to dusk, at least in public. It is not against the law to eat publicly rather considered polite.

Hiki ndicho google inasema.

Lakini sidhani kama kuna sheria ya dini inasema hivyo ni mihemko ya watu kama asemavyo member M Z A N Z I B A R I
 
Kwani zanzibar ni nchi ya kiislam? Huo ni upumbavu kulazimisha watu waamini ujinga. Mungu gani huyo anapambaniwa na watu ili aabudiwe?

Huo upumbavu usifike bara, bara watu wanakula mchana peupe tena malangoni pa misikiti, kuna migahawa kwenye fremu zao na watu wanapata chakula kama kawaida bila kubughudhiwa
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu kumi na mbili kwa tuhuma za kukutwa wakila mchana hadharani kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan...
Tangu waanze kufunga kuna la maana lipi wamefanya zaidi ya kuweka PAUSE machafu yao, baada tu ya mfungo wana press play. Wanamchezea Mungu. Mfungo focus kwao ni chakula sio mabadiliko ya kiroho, kutwa nzima kusubiri iftar na kupanga iweje. Takataka
 
Back
Top Bottom