Watu 12 wakamatwa kwa kula hadharani mchana Zanzibar
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu kumi na mbili kwa tuhuma za kukutwa wakila mchana hadharani kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan ambao wanaifanya kuwa idadi ya watu waliokamatwa kwa tuhuma za kutenda makosa mbalimbali kufikia sitini na mbili

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini magharibi Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Abubakar Khamis Ally amesema kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikiwaonesha baadhi ya watu katika eneo la viwanja vya mnazi mmoja Zanzibar wakila hadharani wakati wa mchana wa Ramadhani, Jeshi hilo lilifanya msako na kuwakamata watu wapatao kumi na mbili wakiwa na vielelezo ambapo amesema wanaendelea na taratibu nyengine ili kuwafikisha Mahakamani.

Aidha ameyataja makosa mengine ni pamoja na unyang’anyi, Madawa ya kulevya na makosa mengine ambapo watuhumiwa wanashikiliwa na Polisi na wengine tayari wameshahukumiwa Mahakamani.
Zanzibar ni taifa la kijinga mno na ndiyo maana wananchi wake hawana maendeleo. Utaendekezaje tamaduni za watu wengine na kuwa zako? Serikali ya Mapinduzi ilaumiwe kwa ujinga huu.
 
Saudia pia walikuwa na Sheria kama hizi ilikuwa wanafosi hata Kuswali Polisi wanapita Mabarabarani wakati wa Sala na kukamata wale ambao hawaendi kuswali lakini wameachana na huo upuuzi.

Sasa hivi unapata Stella Artois ya bariidi hapo Jeddah na Riyadh.
Sasa hapo hoja yako ni ipi?
 
Zanzibar ni taifa la kijinga mno na ndiyo maana wananchi wake hawana maendeleo. Utaendekezaje tamaduni za watu wengine na kuwa zako? Serikali ya Mapinduzi ilaumiwe kwa ujinga huu.
Wewe wacha porojo hizo sheria zipo kabla wewe hujazaliwa sheria zipo znz wewe mtanganyika inakuuma kitu gani sii ubaki kwenu tanganyika ujinga pia ni ugonjwa wahi haraka hospitali ukatibiwe pole sana
 
acha ujinga wewe, kwani tanganyika haina waislam, iweje chakula kiliwe mchana kweupe kwenye migahawa iliyopo misikitini na walaji hawakamatwi? Zanzibar ina udini mwingi sana inapaswa kukemewa kwa hilo
Wewe tatizo lako unadhani znz ni sawa na mkoa wa Arusha au kilimanjaro znz wana serikali yao wana katiba yao wana sheria zao tii sheria bila shuruti huwezi baki kwenu tanganyika pole sana
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja linawashikilia watu kumi na mbili kwa tuhuma za kukutwa wakila mchana hadharani kipindi hiki cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan ambao wanaifanya kuwa idadi ya watu waliokamatwa kwa tuhuma za kutenda makosa mbalimbali kufikia sitini na mbili

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini magharibi Unguja Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Abubakar Khamis Ally amesema kufuatia video iliyosambaa mitandaoni ikiwaonesha baadhi ya watu katika eneo la viwanja vya mnazi mmoja Zanzibar wakila hadharani wakati wa mchana wa Ramadhani, Jeshi hilo lilifanya msako na kuwakamata watu wapatao kumi na mbili wakiwa na vielelezo ambapo amesema wanaendelea na taratibu nyengine ili kuwafikisha Mahakamani.

Aidha ameyataja makosa mengine ni pamoja na unyang’anyi, Madawa ya kulevya na makosa mengine ambapo watuhumiwa wanashikiliwa na Polisi na wengine tayari wameshahukumiwa Mahakamani.
Serikali ya Zanzibar bado imejificha. Haijasema vizuri. Polisi wamekamata watu waliokuwa wanakula mchana Zanzibar na wanasisitiza watawakamata wengine zaidi. Serikali haijaeleza kuhusu hilo.

Serikali haijaeleza mtu ambaye hajafunga Zanzibar wakati Waislam wamefunga anakuwa anavunja sheria gani za Zanzibar? Je, atafanya kosa gani ikiwa atakula mchana? Serikali imejificha, haijaeleza.

Msimamo wa serikali ya Zanzibar haujaeleza kuhusu yanayoendelea Zanzibar. Kuna watu wapo mahabusu kwa sababu wamekula mchana. Serikali inao msimamo gani kuhusu watu hao? Haijasema.

Serikali haijaeleza ni sheria gani ambazo zinawapa mamlaka polisi ya kukamata raia kwa sababh wamekula mchana Zanzibar katika nyakati za mwezi wa Ramadhan. Je, ni sheria au mihemko ya polisi?

Polisi Makao Makuu wametoa taarifa kwa umma kuhusu tukio hilo na wameunga mkono polisi wa Zanzibar kukamata watu hao wanaokula mchana bila na wao kusema wanatekeleza sheria gani?

Mwezi huu hadi leo (ndiyo itakuwa mwisho) baadhi ya madhehebu ya kikristo yalikuwa katika mwezi wa mfungo wa Kwaresma. Serikali ya Zanzibar inatakiwa kutambua haki za uwepo wa wakristo pia.

Leo ni sikukuu kubwa kwa wakristo, Pasaka wakisherekea kufufuka kwa Yesu kristo. Je, wataruhusiwa kusherekea ndani ya Zanzibar au ndiyo zitatumika sheria za Quran kuwadhibiti?

Mtawafukuza wakristo wavuke maji hadi bara wasubiri waislam wamalize mfungo? Kama watabaki, Kwaresma imekwisha, wataendelea kufunga na Ramadhan ili wasiwareke waislam waliofunga?

Tafsiri ya uvumilivu wa kidini inaweza kuwa pande zote mbili. Wanaokula mchana (hawajafunga) na wasiokula mchana (wamefunga) wote kuvumiliana kwa sababu siyo susla la kisheria kufunga.

Serikali ya Zanzibar inatakiwa kulinda haki za kila mmoja katika ardhi ya Zanzibar na kuwataka wazanzibar na polisi wao kutoingilia uhuru binafsi wa mtu mwingine kama havunji sheria za Zanzibar.

Kwa hivyo polisi wanaokamata watu wanaokula mchana na wale watu waliopiga mtu kwa visa hivyo wanatakiwa kuitwa ‘wahalifu’ na wanahatarisha umoja, amani na mshikamano Zanzibar.

Serikali ya Zanzibar inaeleza kwamba serikali inaongozwa na Katiba, na serikali inayo mamlaka ya kulinda katiba na watu wake, kwanini watu wengine wadhurike kwa sababu wanakula mchana?

Tulifikiri Zanzibar inaongozwa kwa mujibu wa sheria za dini ya kiislam. Kama sivyo, tunataka kuona watu waliokamaywa wanaachiwa mara moja na kufudiwa na wale polisi wahuni wawajibishwe na mamlaka zao.

Ni uhuni mkubwa kumkamata raia bila kumueleza kosa analotuhumiwa nalo ni kwa mujibu wa sheria gani. Kama raia hajavunja sheria ni marufuku kushikiliwa na jeshi la polisi namna yoyote vile.

Mwisho, dini ya uislam ni dini maalum sana, inafundisha upendo, uvumilivu, ustahimilivu, amani, hawa wahuni wanaoipaka matope dini hii mashuhuri huko Zanzibar kwanini wasiwajibishwe iwe fundisho?

Polisi wafundishwe legal maxim. “Everything which is not forbidden is allowed” is a constitutional principle. It is the concept that any action can be taken by an individual or a body unless there is a law against it.

Brigedia Mtikila, MMM.
 
Wewe wacha porojo hizo sheria zipo kabla wewe hujazaliwa sheria zipo znz wewe mtanganyika inakuuma kitu gani sii ubaki kwenu tanganyika ujinga pia ni ugonjwa wahi haraka hospitali ukatibiwe pole sana
Ni ujinga uliopitiliza haswa
 
Back
Top Bottom