Watu 7 mbaroni tuhuma za kumteka mwanamke Dar wakitaka kupatiwa dola milioni 3.5 kutoka familia ya mhanga

Watu 7 mbaroni tuhuma za kumteka mwanamke Dar wakitaka kupatiwa dola milioni 3.5 kutoka familia ya mhanga

Daah. Jamaa wana kesi nzito.
Armed robbery 20 years without parole.
Car jacking 15-20 years without parole.
Kidnapping I dont know how many years.
Hapo pia wataongezewa na Attempted rape
Pia wataongezewa attempted murder
Wataongezewa bodily harm.

Duh. Hapa hawachomoki hawa maharamia.
Yani. Hivi kale kakitabu ka Penal code alikatunga nani! Kana adhabu kali kali kweli.
Umesahau kosa la kupanga njama za kumteka mtu .
 
#HABARI Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam, limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa saba wanaotuhumiwa kumteka na kumtishia kwa Silaha Honey Noah (29) mkazi wa Masaki jijini Dar es salaam, ambaye walimteka akiwa ndani ya gari lake aina ya Rav 4 na kumshikilia kwa nguvu kwa kipindi cha siku nne wakidai kiasi cha Dola milioni 3.5 kwa baba yake.

Akiongea na waandishi wa habari Kamanda Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es salaam, Jumanne Muliro anasema kutokana na chunguzi za kisayansi walifanikiwa kuwakamata watuhumiwa hao ambao mmoja wapo ni raia wa Canada mwenye asili ya Kisomali.

Aidha Kamanda Murilo anasema watuhumiwa wote siku ya Leo watafikishwa Mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kujibu tuhuma zinazowakabili za kumteka, kumtishia kwa silaha, kumshikilia kwa nguvu na kudai pesa kwa nguvu.
 
Daah. Jamaa wana kesi nzito.
Armed robbery 20 years without parole.
Car jacking 15-20 years without parole.
Kidnapping I dont know how many years.
Hapo pia wataongezewa na Attempted rape
Pia wataongezewa attempted murder
Wataongezewa bodily harm.

Duh. Hapa hawachomoki hawa maharamia.
Yani. Hivi kale kakitabu ka Penal code alikatunga nani! Kana adhabu kali kali kweli.
Penal code ilikuja na meli toka Uingereza.Hapa huwa tunafanya amendments za hapa na pale kama elimu ya Kubenea
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata watuhumiwa saba kwa tuhuma za kupanga njama, kumtishia kwa silaha, na baadaye kumteka mwanamke aliyefahamika kwa jina la Hani Hussein (29) Mkazi wa Masaki, Dar es Salaam.

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashilia watuhumiwa saba kwa madai ya kupanga njama, kumtishia kwa silaha na kumteka mwanamke aaliyefahamika kwa jina la Hani Hussein (29), mkazi wa Masaki.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro leo Oktoba 30, 2023 amesema tukio la kumteka binti huyo lilitokea Oktoba 16, 2023.

“Tukio hili limetokea Oktoba 16, 2023 saa nne asubuhi wakati Hani Hussein akiwa anaendesha gari lake aina ya Toyota Rav4, ghafla akiwa eneo la Msasani Village alisimamishwa na sehemu ya kundi la watuhumiwa hao na kuingia ndani ya gari, kumtishia kwa silaha, kumteka na kuelekea maeneo ya Mbezi Beach mtaa wa ujirani ambako walimshikilia kwa nguvu kwa siku nne huku wakidai fedha kwa vitisho kwa baba wa mtekwaji kuwa asipotoa kiasi cha Dola za Marekani 3.5 milioni mtoto wake angepoteza maisha.

"Baada ya kupata taarifa ya tukio hilo, Jeshi la Polisi lilianza ufuatiliaji wa na Oktoba 19 tulifanikiwa kumuokoa na kuwakamata watekaji wote wakiwa na gari walilomteka, pamoja na silaha ilyotumika Pistol Glock 19 iliyotengenezwa Austria ikiwa na risasi 4," amesema Kamanda Muliro.

Amewataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Hassan AbusherNur (39) raia wa Canada mwenye asili ya Somalia na mkazi wa Msasani, Nathan Lungumisa (27), Fredick Chahonza (49), Assad Abdurasur (43), Fahad Mussa (32), Ilfan Saleh (41) na Nicolas Nilay (39).

Aidha ameeleza kuwa tayari upelelezi na watuhumiwa wote watafikishwa Mahakama ya Kisutu kwa hatua zaidi za kisheria.

MWANANCHI
jeshi letu limestaarabika sana. zamani walikuwa wakikamata majambazi kama hao, tunasikia tu wameshambuliwa wakijaribu kutoroka mikononi au wakati wa majibizano. of course utawala wa sheria ni muhimu kwasababu huko ndiko hata wasio na hatia walikuwa wanafutwa.
 
Back
Top Bottom