Watu hawataki kutembeleana siku hizi, kila mmoja yuko bize kusaka shilingi

Watu hawataki kutembeleana siku hizi, kila mmoja yuko bize kusaka shilingi

Hiyo ipo sana watu wanakukataa. Mwanangu nilimbeba maghetoni kwa muda life likasonga akaenda mji mwengine, wakati tukiwasiliana ananiambia ukija huku we nicheki tu mwanangu we damu yangu. Mungu si Athumani nikatia timu ule mji kwa mishe zangu baada ya siku kadhaa pale one day nikamcheki tukaongea fresh tu. Ile kumjulisha tu nipo maeneo ya ule mji mwana akanikataa.
Tatizo ilikuwa ni nini, mazingira aliyopo kwa sasa sio rafiki au ulihisi kuna tatizo gani?
 
Naona alikuwa busy kweli. Next time moe.muda wa kutosha na uende wakati hana kazi.

Binafsi sijaona tatizo lolote hapo, hakuwa na nafasi hiyo siku.
Inawezekana ikawa kweli, lakini kwa nini kuwa bize mpaka siku ya ibada, nini maana ya maisha?
 
Tatizo ilikuwa ni nini, mazingira aliyopo kwa sasa sio rafiki au ulihisi kuna tatizo gani?
Muongo Muongo tu alisema yupo busy na hapo nilipokuepo na eneo alilokuwepo ni kama 200M tu. Kichwani nikajua tu huyu hataki shobo za kijinga, nikamwambia fresh nipo leo na kesho akasema atanicheki ndio ikatoka hiyo mpaka leo.
 
Ni upumbavu kutokupanga kutembeleana na kujuliana hali uso kwa macho. Mimi mpaka leo tunatembelea ndugu, rafiki na jamaa maisha na ndohaya haya.

Kuna wengine wanajifanya wako busy ila mda wa kukaa bar, kuzini na kula bata wanao sindo yaleyale sasa.
 
Back
Top Bottom