Watu hawataki kutembeleana siku hizi, kila mmoja yuko bize kusaka shilingi

Watu hawataki kutembeleana siku hizi, kila mmoja yuko bize kusaka shilingi

Tatizo lilianzia kwako Mkuu, kosa lako ni hili hapa:-

Unampigia simu mtu unamuambia upo maeneo aliyopo, unaomba kuonana naye halafu unapanga kuonana naye kwake yaani unajikaribisha kwa mtu

Hata mimi ningekukataa tu Mkuu, ulitakiwa, baada tu yakumuambia upo maeneo aliyopo, ungeomba kuonana mahali mpate kuongea mambo mawili matatu.

Sasa yeye ndio angepima na kukukaribisha kwake ama kukuuliza ulipo afanye michakato muweze kuonana.

Atakuwa amekuona unataka kujua mambo/maisha yake akaona akukatae tu Mkuu, usilaumu wala, ni maisha yalivyo tu.
Kwa mzee mtu mzima si vizuri akakufuata wewe ulipo
 
Individualism ni nzuri sana katika kuleta maendeleo collectivism ya kiafrika ina upumbavu mwingi ambao ni unnecessary kama huu wa kutaka Kujuana juana.

Inshort sipendi mazoea ya hovyo hovyo na mtu katika maisha yangu binafsi regardless huyo mtu ni ndugu yangu wa damu au laaah!.
 
Binafsi nadhani ni maamuzi ya jinsi unavyotaka kuishi na cycle yako.

Tengeneza cycle ambayo mnaweza kuamua mkutane lini, wapi ili mfurahie kidogo.

Nimeijaribu hii, inatusaidia sana kwa kweli, na kuna wakati mwambie kaka/dada yako aje na familia weekend muwe pamoja. Sijui tumemuwaje hakyanani!!
Hii iko vizuri kama itatekelezwa; ingawa umbali wa kijiografia unaweza kuwa tatizo kwa baadhi ya maeneo
 
Zamani watu waliweza kutembeleana kwasababu hatukuwa na matumizi mengi yanayohitaji hela.

Hakuna umeme (baadhi ya maeneo), simu wengine walikuwa hawana, vifurushi bei rahisi, vyakula vilikuwa vingi kwasababu hakukuwa na mabadiliko ya hali ya hewa, tunatumia antena (analogia), nauli bei nafuu, upatikanaji wa kazi ni rahisi n.k.

Sasa hivi matumizi yamekuwa mengi na upatikanaji wa pesa siyo rahisi.

Matumizi ya kila siku ambayo unatakiwa utumie, Bando ya internet, king'amuzi, bando la dk na sms, umeme na maji. Vyote hivyo vinahitaji hela.

Nikutafuta shilingi muda wote
Kwa hali hiyo, kuna dalili zozote itakuja kutokea tukaishi kama zamani?
 
Individualism ni nzuri sana katika kuleta maendeleo collectivism ya kiafrika ina upumbavu mwingi ambao ni unnecessary kama huu wa kutaka Kujuana juana.

Inshort sipendi mazoea ya hovyo hovyo na mtu katika maisha yangu binafsi regardless huyo mtu ni ndugu yangu wa damu au laaah!.
Inasaidia kupunguza conflicts za kipumbavu , tabia ya unafiki na umbea wa Kitanzania ni kero sana , Individualism ndio solution ,kila mtu apambane na hali yake.
Watz sio watu wa kuintertain kabisa ,unalikaribisha jitu kwako kesho linaenda kumwaga umbea ,Majungu na chuki + unafiki tu .
 
Si hivyo tu siku hizi adui hatoki mbali.

Unamkaribisha mtu kwako kumbe kaja kuchunguza unaishi vipi akakutangaze.

Kila mtu akae kwake tutakutana kwenye matukio, harusi au misiba
Kitu kipi kilichosababisha uadui uongezeke? Je maisha ya unayoishi sasa yanakupa furaha?
 
Individualism ni nzuri sana katika kuleta maendeleo collectivism ya kiafrika ina upumbavu mwingi ambao ni unnecessary kama huu wa kutaka Kujuana juana.

Inshort sipendi mazoea ya hovyo hovyo na mtu katika maisha yangu binafsi regardless huyo mtu ni ndugu yangu wa damu au laaah!.
Labda ukiwa hoi kitandani (hospitali) kwa muda wa miezi mitatu, utapenda watu wangapi waje kukujulia hali?
 
Biblia imesema nyakati za mwisho upendo wa watu utapoa na inaonekana katika hili kuna mazingira mengi yanayoweza kuchangia hali hii. Mimi niliwahi kuwa na hali fulani ya maisha ya kawaida tu ya mkate na chai nikapambana sana na ndugu na jamaa kila aliyekuja Mkoani hapa alifikia kwangu sasa baadae mambo yaka yumba kidogo nakwambia huko kijijini hakuna ambaye hakuwa na taarifa hizo mbaya zaidi hawa ambao mimi niliwapokea na kuwapa mwongozo wa maisha wakageuka kuwa mwiba kwangu tena, sasa mazingira kama haya pia yanapunguza upendo na ukaribu kama mtu huna moyo mkuu huwezi endelea vizuri na ndugu, jamaa na marafiki.
 
Kwa hali hiyo, kuna dalili zozote itakuja kutokea tukaishi kama zamani?
Haitatokea aise.
Maana hata siku za utafutaji zimeongezeka. Watu hadi siku za wikiend wanahangaika kwenye mishemishe, wengine ndiyo muda wa kwenda bar kunywa, kuangalia mpira na michepuko (usasa ni mwingi).
Unaweza kufika kwa ndugu yako, akakuambia twende huku, kumbe bar. Ukitoka hapo saa 4 usiku, unalala, kesho ndugu yako kwenye mishemishe, unabaki wewe mwenyewe.
Unaweza kujikuta hapo nyumbani kwa ndugu yako umebaki wewe tu.
Mama yupo na kibanda chake cha nyanya anarudi usiku, watoto shule, wakirudi ni misele mpk usiku, ndugu yako anarudi saa 4 usiku. Haina maana.
Kibaya zaidi pesa hakuna halafu mahitaji ni mengi
 
Biblia imesema nyakati za mwisho upendo wa watu utapoa na inaonekana katika hili kuna mazingira mengi yanayoweza kuchangia hali hii. Mimi niliwahi kuwa na hali fulani ya maisha ya kawaida tu ya mkate na chai nikapambana sana na ndugu na jamaa kila aliyekuja Mkoani hapa alifikia kwangu sasa baadae mambo yaka yumba kidogo nakwambia huko kijijini hakuna ambaye hakuwa na taarifa hizo mbaya zaidi hawa ambao mimi niliwapokea na kuwapa mwongozo wa maisha wakageuka kuwa mwiba kwangu tena, sasa mazingira kama haya pia yanapunguza upendo na ukaribu kama mtu huna moyo mkuu huwezi endelea vizuri na ndugu, jamaa na marafiki.
Ni kweli wapo wanaokatisha tamaa; swali ni kwanini wao wamebadilika na kuwa maadui?
 
Kwa mazingira hayo, wengi hatufurahii maisha kwa sababu muda mwingi tuko bize kwenye kutafuta shilingi, mwingine jumatatu mpaka jumapili muda wote ni bize; katika hali hii tukisema maisha ni utumwa tutakuwa tumekosea?​
Ndiyo ni utumwa.
Kama sehemu yenye changamoto ya usafiri kama dar (Foleni)
Mtu anaamka saa 10 usiku anawahi usafiri anafika kazini saa 2 asubuhi.
Anarudi saa 6 usiku asubuhi saa 10 tena anaamka.
Maisha kwasasa ni utumwa halafu kibaya zaidi pesa haionekani
 
Back
Top Bottom