Watu 'Powerful' 12 ni akina nani hadi waachiwe kuharibu Bonde la Ihefu?

Watu 'Powerful' 12 ni akina nani hadi waachiwe kuharibu Bonde la Ihefu?

Kazi nzuri sana mmefanya Balile na Mwanahalisi. Uandishi wa habari za mazingira ni moja ya kazi hatari sana. Mi nashauri kama inawezekana hilo eneo litengwe kama Ramsar site chini ya UNESCO, labda nguvu ya kulilinda itaongezeka.
Balile ni mnafiki na mpenda sifa.
 
21 November 2022
MFEREJI ULIOJENGWA UKUTA MKUBWA KUZUIA MAJI KUINGIA MTO RUAHA MKUU WAANZA KUBOMOLEWA
-



Ni utekelezaji wa maagizo 10 ya Makamu wa Rais kuhakikisha mabanio yote haramu ya maji yanabomolewa - Inakadiriwa umegharimu zaidi ya Milioni 400.

- Kazi zaidi inahitajika kufanyika kubomoa kingo nyingine Siku chache baada ya Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kuzielekeza Mamlaka zinazosimamia mto Ruaha Mkuu kuhakikisha vizuizi vyote vinaondolewa Ili kuuruhusu mto huo kutiririsha maji kama kawada.

Moja kati ya kizuizi kikuu Cha mto Ruaha kupata maji kimeanza kuondolewa Hapa ni Kata ya Imalio Usongwe katika mfereji wa nguvu kazi Mwanavala unaopeleka maji katika mashamba ya mnazi katika eneo la Warumba yanayotakiwa kuingia katika Mto Ruaha Mkuu na kuelekea hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Bwawa la Mtera, Kidatu, Bwawa la Nyerere na hatimaye Bahari ya Hindi.

Zoezi la kubomoa mabanio haya yasiyorasmi yanayotumika kuchepusha kinyume na sheria kutoka katika Mto Mfereji huu unakadiriwa kuwa umejengwa kwa zaidi ya Milion 400 miaka kadhaa nyuma.

Jitihada za kuuokoa mto Ruaha Mkuu kuufanya uwe unatiririsha maji mwaka mzima Zinaendelea na Mto Ruaha kuacha kukauka mwaka mzima INAWEZEKANA.

Ukiokoa mtiririko wa Maji mto Ruaha Mkuu maana yake umeoko na kuilinda Hifadhi ya Taifa ya Ruaha Maana yake pia umalihakikishia Taifa Upatikanaji wa umeme katika Bwawa la Mtera, Kidatu na Nyerere linaloelekea kukamilika.
Source : JAMVI online TV
 
23 November 2022

UKUTA ULIOZUIA MAJI KUELEKEA MTO RUAHA MKUU WABOMOLEWA




Utekelezaji wa agizo la serikali la kuchukua hatua shughuli za kibinaadamu katika eneo la bonde la Usangu na Ihefu wilayani Mbarali mkoani Mbeya Tanzania ili kunusuru Mto Ruaha umeanza kwa kubomoa mifereji yote iliyochepusha maji kinyume na utaratibu.
 
Nimemsikiliza ndugu yangu Balile! Kwa aliyosema ni mambo mazito yanayofanya kama Taifa tujiulize mamlaka zetu hasa za usalama wanamuogopa nani kwenye ulinzi wa rasilimali zetu?

Balile binafsi nimekupa heshima ya pekee kwa hili.
 
Ni taarifa inayoonesha kwamba hatutaendelea. Tuna kundi la watu wa hovyo, lakini wanaitwa ni powerful!
Kwa maoni yako endelea;

wanao jiita CDE, M-NEC , Chawa karibu wote wamewekeza hapo, na wakuu wa kada fulani ambao sheria inawakataza kua kwenye siasa lakini wakistaafu tu unaskia kateuliwa nafasi flani kisiasa,
 
Apewe ulinzi
Nimemsikiliza ndugu yangu Balile! Kwa aliyosema ni mambo mazito yanayofanya kama Taifa tujiulize mamlaka zetu hasa za usalama wanamuogopa nani kwenye ulinzi wa rasilimali zetu?

Balile binafsi nimekupa heshima ya pekee kwa hili.
 
Nimemsikiliza ndugu yangu Balile! Kwa aliyosema ni mambo mazito yanayofanya kama Taifa tujiulize mamlaka zetu hasa za usalama wanamuogopa nani kwenye ulinzi wa rasilimali zetu?

Balile binafsi nimekupa heshima ya pekee kwa hili.
Boss usalama wa taifa ni mbuzi mawe,badala ya kulinda taifa wanalinda viongozi,shame
 
Back
Top Bottom