Wavuvi: Hii habari ya Sangara/Sato kuhifadhiwa na chloroform ni ya kweli

Wavuvi: Hii habari ya Sangara/Sato kuhifadhiwa na chloroform ni ya kweli

Akihojiwa na Sexless , mvuvi (jina kapuni) amesema "Sato na Sangara wana minofu mikubwa kutokana na maumbo yao. Mara nyingi wamekuwa wakioza wanaposafirishwa toka Mwanza mpk mikoa mingine kwa kuwagandisha na barafu".

"Lkn maji ya kuoshea maiti (chloroform) yakitumika samaki hao hufika popote bila kuharibika" aliongeza mvuvi huyo.

"Kabla ya matumizi ya chloroform Sangara/Sato walikuwa wakipata uvundo kwenye minofu na biashara yao kuwa mbaya" aliendelea kueleza mvuvi huyo wa Sangara/Sato.

Maoni yangu. Kilichofanywa na naibu waziri ni uhuni mkubwa. Anahatarisha afya za watanzania ili tu aendelee kulinda biashara ya samaki hao. Makamu wa rais ana taarifa nyingi na nyeti kuliko naibu waziri halafu kauli yake inazodolewa kizembe namna hii?

Endelea kula Sangara/Sato at your own risk.
Tusubiri timu ya wataalamu watakuja na jibu
 
Sas ikiwa wanatumia maji hayo mbona waadhirikiaji wengi wa [emoji752] Ni watu wa uko uko Kanda ya ziwa ilitegemewa kuwa bas waadhirika wengi wawe wa mikoani Sasa nitofauti embu waangalie pia migodi na mecury inayotumika

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Pia watafiti waangalie pia ni saratani gani i.e. katika sehemu gani ya mwili na kufuatilia vyanzo vya saratani katika sehemu hizo za mwili e.g. koo, njia ya hewa, tumbo, mapafu, shingo la kizazi, damu n.k. huweza kusabababishwa na vitu gani na je, visababishi hivyo vimeshamiri zaidi maeneo ya kanda ya ziwa hususan Mwanza?
 
Jaribu kusoma uongeze maarifa na sio kubwabwaja tu. Chloroform ni maji au ni dawa? Makamu wa raisi aliimaanisha maji wanayooshea maiti mortuary na yanayotumika kwa shughuli mbalimbali za imani potofu. Kama alimaanisha chloroform, hiyo inatumika miaka mingi sana ingawa si na wasafirishaji wote wa samaki, madhara yake mlaji anaweza kuyapata baada ya exposure ya muda mrefu sana (Human Carcinogenes class2). Na kama anasema ndio chanzo cha saratani kwa wakazi wa kanda ya ziwa anadanganya mchana kweupe, sisi huku tunakula kitu ya siku hiyo hiyo haijaingia hata kwenye freezer, so hiyo saratani kwa huku watafute chanzo chake kingine.
Pale VP alichemka sana kwa kuwatisha wananchi kwa kiasi kikubwa vile bila ya uchunguzi wa kutosha

NB: miaka ya karibuni hata hayo matumizi ya chloroform yamepungua sana. Miundombinu imeboreshwa, Mwanza-Dar ni ndani ya masaa 24. Pia teknolojia ya kuwasafirisha imeboreshwa sana, so wengi wao wala hawatumii chloroform tofauti na ile miaka ya 1990s na 2000s.
Kwahili naweza kukubaliana na wewe..mana saratani haiji siku hiyo hiyo..hutokea baada ya exposure ya muda mrefu.

Kwasasa hii imebaki kuwa nadharia though sio 100%.

#MaendeleoHayanaChama
 
Akihojiwa na Sexless , mvuvi (jina kapuni) amesema "Sato na Sangara wana minofu mikubwa kutokana na maumbo yao. Mara nyingi wamekuwa wakioza wanaposafirishwa toka Mwanza mpk mikoa mingine kwa kuwagandisha na barafu".

"Lkn maji ya kuoshea maiti (chloroform) yakitumika samaki hao hufika popote bila kuharibika" aliongeza mvuvi huyo.

"Kabla ya matumizi ya chloroform Sangara/Sato walikuwa wakipata uvundo kwenye minofu na biashara yao kuwa mbaya" aliendelea kueleza mvuvi huyo wa Sangara/Sato.

Maoni yangu. Kilichofanywa na naibu waziri ni uhuni mkubwa. Anahatarisha afya za watanzania ili tu aendelee kulinda biashara ya samaki hao. Makamu wa rais ana taarifa nyingi na nyeti kuliko naibu waziri halafu kauli yake inazodolewa kizembe namna hii?

Endelea kula Sangara/Sato at your own risk.
Na ndio maana niliweka neno hapa. Badala ya kukamata mTanzania anayetoantaarifa walitakiwa kutafuta ukweli wa hili jambo lakini waliita mtu Mchochezi huyu Waziri husika anatakiwa ajipumzishe mwenyewe Kwa manufaa ya afya za waTanzania na dunia kote wanaokula samaki Hawa.
Viongozi Hawa ndio walenwalioko bungeni na kujifanya bunge kuwa ni dhaifu. Hawatufai hawatufai.!

Serikali ije na majibu kamilifu Baada ya huyu kujiachia mwenyewe.!
 
Kwaiyo naibu waziri anampinga makamu wa rais?

Ulega anatoa wapi kiburi?
 
Chloroform or trichloromethane is an organic compound with formula CHC13 and is a common organic solvent.
Mimi ni mvuvi huku hilo suala ni geni mno na siwezi katu kuamini uzushu huu, nina jua mambo mengi kadhaa za mbinu nyingi, ila haya c kweli kabisa.
 
Hiyo dawa uliyoitaja (chloroform) haihusiani na kuhifadhi maiti
Hawa watu wanashangaza mkuu, tangu lini chloroform ikahifadhi maiti.....chloroform haiwezi kuhifadhi hata maiti ya mjusi itakuwa kuhifadhi samaki, tatizo hadi laymen wanajikuta wataalamu...​
 
Ila na sisi Watanzani tumezidi ujinga, kama hao Samaki kwa siku za nyuma wamekuwa wanafika wakiwa wameanza kuvunda kwa nini hatukuhoji kinachofanyika sasa mpaka wafike wakiwa wazima na wabaki wazima kwa muda mrefu?.
Utamuuliza nani
 
Sinunui tena milele Sato au Sangara, nitanunua wakufugwa tu, sitakaa ninunue tena Samaki wa Ziwa Victoria, mara maji ya maiti mara Mercury.. Sitanunua tena samaki wa Ziwa Victoria, nimeogopa sana, Cancer ni kifo aisee
 
Akihojiwa na Sexless , mvuvi (jina kapuni) amesema "Sato na Sangara wana minofu mikubwa kutokana na maumbo yao. Mara nyingi wamekuwa wakioza wanaposafirishwa toka Mwanza mpk mikoa mingine kwa kuwagandisha na barafu".

"Lkn maji ya kuoshea maiti (chloroform) yakitumika samaki hao hufika popote bila kuharibika" aliongeza mvuvi huyo.

"Kabla ya matumizi ya chloroform Sangara/Sato walikuwa wakipata uvundo kwenye minofu na biashara yao kuwa mbaya" aliendelea kueleza mvuvi huyo wa Sangara/Sato.

Maoni yangu. Kilichofanywa na naibu waziri ni uhuni mkubwa. Anahatarisha afya za watanzania ili tu aendelee kulinda biashara ya samaki hao. Makamu wa rais ana taarifa nyingi na nyeti kuliko naibu waziri halafu kauli yake inazodolewa kizembe namna hii?

Endelea kula Sangara/Sato at your own risk.
Yule naibu Waziri, napenda kuheshimu utu wake, lakini majibu yale aliyoyatoa ni ya upuuzi mkubwa. Rais Samia anatakiwa kumfukuza mara moja, hastahili hata kujiuzulu.

Tuliopo Kanda ya Ziwa tunajua. Habari ya wavuvi kuvua kwa kutumia sumu na baruti, wavuvi kuhifadhi samaki kwa kutumia madawa ya kutunzia maiti, na baadhi ya wavuvi kununua barafu za kutoka kwenye majokofu ya kutunzia maiti, ni habari za kweli. Ndiyo maana, mathalani, mimi binafsi nina watu wangu ambao huwa wananiuzia samaki. Na kuna wakati narudi bila samaki, anakuambia kabisa kuwa hawa wa leo siyo wa kununua wewe. Akiniambia hivyo tu, naelewa: ama wamevuliwa kwa sumu au walivuliwa jana yake wakahifadhiwa kwa hayo madawa.

Wenye mashaka, nawahakikishia, kwa 100%, taarifa ya makamu wa Rais kuwa samaki wanahifadhiwa kwa kutumia madawa ya kutunzia maiti, ni ya kweli. Jambo ambalo hakuna uhakika, ni je, hayo madawa ndiyo yanayosababisha wagonjwa wa saratani, zaidi ya 60% watoke Kanda ya Ziwa.

WITO: KWA KUWA SERIKALI HAITAKI KUTIMIZA WAJIBU WAKE, MWANANCHI BINAFSI CHUKUA TAHADHARI KWAAJILI YA AFYA YAKO NA ZA WOTE WANAOKUHUSU.

Wala siyo samaki tu, hata kwenye nyama. Na siyo nyama na samaki tu, hata mahindi. Siku hizi kuna sumu kali kupindukia za kutoka China, zile za vidonge, ndiyo zinatumika kuhifadhia nafaka. Vidonge vile, vinarushwa ndani ya ghala, humo ndani kuwe na panya au mjusi au mdudu yeyote anakufa mara moja, anakauka kama jiwe. Siamini kama sumu zile ni salama kwa mtumiaji wa chakula.
 
Jaribu kusoma uongeze maarifa na sio kubwabwaja tu. Chloroform ni maji au ni dawa? Makamu wa raisi aliimaanisha maji wanayooshea maiti mortuary na yanayotumika kwa shughuli mbalimbali za imani potofu. Kama alimaanisha chloroform, hiyo inatumika miaka mingi sana ingawa si na wasafirishaji wote wa samaki, madhara yake mlaji anaweza kuyapata baada ya exposure ya muda mrefu sana (Human Carcinogenes class2). Na kama anasema ndio chanzo cha saratani kwa wakazi wa kanda ya ziwa anadanganya mchana kweupe, sisi huku tunakula kitu ya siku hiyo hiyo haijaingia hata kwenye freezer, so hiyo saratani kwa huku watafute chanzo chake kingine.
Pale VP alichemka sana kwa kuwatisha wananchi kwa kiasi kikubwa vile bila ya uchunguzi wa kutosha

NB: miaka ya karibuni hata hayo matumizi ya chloroform yamepungua sana. Miundombinu imeboreshwa, Mwanza-Dar ni ndani ya masaa 24. Pia teknolojia ya kuwasafirisha imeboreshwa sana, so wengi wao wala hawatumii chloroform tofauti na ile miaka ya 1990s na 2000s.
Unazungula, unajichanganya.

Umesema matumizi ya Chloroform madhara yake ni baada ya muda mrefu. Halafu unasema ilikuwa inatumika miaka ya 2000. Halafu eti kwa sababu siku hizi haitumiki, basi haiwezi kuwa sababu ya Kanda ya ziwa kuwa na cases nyingi za saratani.

Kama ilikuwa inatumika miaka 2000, na madhara yake ni baada ya muda mrefu, si ndiyo unathibitisha kuwa madhara ya matumizi ya madawa yaliyokuwa yakitumika hapo zamani, ndiyo yanaonekana sasa?
 
Nasikia hata Maharage hutiwa Paracetamol ili yaive haraka hii ndio Dar bhana 😆
 
Back
Top Bottom