Wazazi wa mtoto huyu watakesha wanabubujikwa machozi ya furaha na kumuombea maisha marefu Rais Samia

Viongozi wa nchi hii wanadhulumu Watanzania kwa ufisadi wa hali ya juu na kushindwa kutoa huduma za msingi halafu wanamega vihela kidogo kumhudumia mtu mmoja au wawili kisha wanajifanya wana utu na wanataka watu wawaabudu na kuwaimba kwamba ni watu wema kumbe kiuhalisia ni chui waliojivika ngozi ya kondoo! Watu wabaya sana.
 
Na wewe toa pesa yako usaidie hata mmoja.
 
Na wazazi wa watoto Nchi nzima waliofutiwa bima ya AFYA na Samia huyo huyo wao watakuwa wanalaani Kweli Kweli.
 
Sasa amepewa ujumbe murua kabisa na watanzania kuwa wao siyo wajinga na hawatapeliki kijinga. Kama anataka gari la kifahari na anasa aende akanunue kwa pesa zake Mwenyewe.
Una roho ya kishetani sana wewe jamaa, ila ujue hujafa hujaumbika.
 
Na wazazi wa watoto Nchi nzima waliofutiwa bima ya AFYA na Samia huyo huyo wao watakuwa wanalaani Kweli Kweli.
Nenda kakate bima kwa ajili ya familia yako na watoto wako kwa gharama nafuu kabisa iliyowekwa na serikali yetu Sikivu.
 
Bila kumsahau yule mama.

Pili Rais ametoa wito Kwa jamii kuwa na bima ya Afya vinginevyo majanga kama hayo yakiwakuta wasije laumu Rais.

View: https://www.instagram.com/p/C9kPcA-qCbS/?igsh=MWQ1OHV6c3FmeW51dA==
 
Katika vitu/mazingira ambayo kiongozi wa nchi hapaswi kufanya au anapaswa kufanya zaidi hasa akiwa kwenye ziara rasmi ni KUONESHA UPENDELEO WA WAZI!

Ingekuwa ni ishu binafsi ningepongeza. Lakini kwenye hili Rais SSH alipaswa afanye kisera zaidi!

Hapo kasaidia tu mtoto mmoja... Je wapo wangapi kama huyo mtoto?
Je, nao watoke kokote walipo waende kwenye mikutano ya SSH kusuburia?
bahati zao?
Kwani anashindwa nini kutoa maelekezo ya kisera huyo akasaidiwa na wengine kote nchini nao wakatafutwa na kusaidiwa?

Urais siyo NGO ya kufurahisha wachache!
 
Nenda kakate bima kwa ajili ya familia yako na watoto wako kwa gharama nafuu kabisa iliyowekwa na serikali yetu Sikivu.
Kabla ya Samia kuingia, watoto chini ya umri wa miaka 5, walipata bima Bure.

Samia amefuta,

Halafu wewe chawa unakuja kutapika hapa!!
 
Kabla ya Samia kuingia, watoto chini ya umri wa miaka 5, walipata bima Bure.

Samia amefuta,

Halafu wewe chawa unakuja kutapika hapa!!
Alafu anakuja kufanya showoff kwa kusaidia mtoto mmoja mwenye mahitaji maalumu wakati wapo wengi wenye mahitaji hayo hayo hawajui hatma yao!
Shame!
 
Unaelewa maana ya upendeleo? Wewe umefanya nini kuwasaidia hao unao waona huko kwako? Acheni wivu na roho mbaya.kwa hiyo ulitaka asumsaidie mtoto huyo? Vipi angekuwa mtoto wako ndio kasaidiwa? Ungekuja kuzubgumza maneno hayo uliyoyazungumza hapa?
 
Bila kumsahay yule mama.

Pili Rais ametoa wito Kwa jamii kuwa na bima ya Afya vinginevyo majanga kama hayo yakiwakuta wasije lauku Rais.
Ni kweli kabisa alipokuwa Mlowo napo amegusa hisia za watu wengi sana .kwa yule mama mwenye mtoto pamoja na yule aliyepata majereha mabaya kwa ajali. Kiufupi ni kuwa Rais Samia anaendelea kumfikia kila mwenye kuhitaji msaada
 
Unaelewa maana ya upendeleo? Wewe umefanya nini kuwasaidia hao unao waona huko kwako? Acheni wivu na roho mbaya.kwa hiyo ulitaka asumsaidie mtoto huyo? Vipi angekuwa mtoto wako ndio kasaidiwa? Ungekuja kuzubgumza maneno hayo uliyoyazungumza hapa?
Hii ni zaidi ya wivu... Ni UPENDELEO wa wazi!
Anyways, unaweza kuweka bayana vigezo vilivyotumika kumpa huyo mtoto hiyo nafasi huku wengine nchi nzima hawajui hatma yao?

Use your brain wisely if at all you have it!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…