Waziri gani alimdhulumu Rais mstaafu Mwinyi vifaa vyake vya ujenzi?

Waziri gani alimdhulumu Rais mstaafu Mwinyi vifaa vyake vya ujenzi?

Okay, aliyasema 20 years ago. With fresh memory and faculties.

Back then alisemaje, alisema aliona ni uungwana kumuachia mtu mabati na masimenti akutunzie wakati yeye mwenyewe ndio alipanga siku ya kuondoka?
Hivi akili yako ipo sawa?? Huja soma kwamba ali pata msukumumo wa kutakiwa kuondoka ili yeye aingie kwenye hiyo nyumba , Na arudi kwao ZnZ .
Na huja soma baadae muhusika alimpelekea mabati na cement alivyokuwa "white house"
 
Kwa hisani kubwa kabisa ya Jamiiforums tarehe 23 Julai 2019
: Jinsi Natepe alivyomhenyesha Rais Ali Hassan Mwinyi

Alipojiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi mwaka 83? kama sijakosea nafasi yake aliteuliwa mzee mmoja kutoka Zanzibar anaitwa mzee Abdallah Said Natepe kushika uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi.

Meja Jenerali Abdallah Said Natepe alipoingia tu ofisini alimtaka waziri aliemtangulia kutoka katika nyumba ya waziri ili yeye aweze kukaa hapo kama waziri.

Ilikuwa shida kidogo maana waziri aliyeondoka bado alikuwa anatafuta makazi lakini alitakiwa haraka kutoka na Meja Jenerali Natepe.

Ikampasa mzee Ali Hassan Mwinyi kutoka kwa haraka na siku anatoka pale nyumbani alikuwa amenunua mabati 150 na mifuko ya saruji 100 ya kwake wala sio mali ya serikali.

Mzee Abdallah Said Natepe alimkatalia kuvichukua akidai ni mali ya serekali kweli mzee Ali Hassan Mwinyi akaviacha akaondoka.

Baada ya miezi kadhaa tu mzee Ali Hassan Mwinyi akateuliwa kuwa Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar . Mzee Abdallah Natepe wakati anajifikiria jinsi ya kwenda kumpongeza na kumuomba radhi kwa aliyomfanyia kabla ya kufikiria njia mzee Ali Hassan Mwinyi akaletwa bara mwaka 1985 kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hapa sasa Mzee Meja jenerali Abdallah Natepe akajua kazi hana na atatimuliwa haraka iwezekanavyo tena na kutengwa na nyadhifa za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwakuwa kuna mabaya ya wazi na ya sirini aliyomtendea mzee Ali Hassan Mwinyi.

Mzee Mwinyi baada tu ya kuapishwa kuwa Rais wa JMT wakati anateua baraza la mawaziri akamteua tena Abdallah Said Natepe kuwa waziri pale pale mambo ya ndani.

Siku ya kumuapisha akamwambia mzee Abdallah Natepe sio kwamba nakupenda sana hapana ila napenda kazi yako unavyofanya endelea kufanya kazi.

Siku moja mzee Mwinyi yupo ikulu kapumzika akaona malori yanaingia na akaambiwa mzigo wako huu Mh. Ali Hassan Mwinyi rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania akashtuka mbona sijaagiza kitu mie??

Ndipo akaambiwa umetoka kwa Natepe, mzee Ali Hassan Mwinyi akacheka sana akawaambia wasaidizi wake shusheni mabati 150 na saruji 100 hizo ndio haki yangu zingine mrudishieni tu.

N.B
Habari za ziada kwa hisani ya intaneti

Sunday, September 26, 2010​

MUASISI WA MAPINDUZI ZANZIBAR ABDALLA SAID NATEPE AMEFARIKI DUNIA​


Mmoja wa viongozi 14 wa Mapinduzi matukufu ya Zanzibar,Meja Jenerali Abdallah Said Natepe amefariki dunia jana mchana katika hospitali yajeshi Lugalo mjini Dar es Salaam.

Marehemu Natepe ni miongoni mwa viongozi wa mapinduzi kumbi na mbili waliofariki dunia ambao walifanikisha kufanikiwa kwa mapinduzi ya Januari 12, 1964 yaliyoindoa serikali ya kisultani visiwa vya Zanzibar,

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, kifo hicho kimetokea jana mchana kwenye hospitali hiyo kuu ya Jeshi la Wananchi.
Taarifa hiyo inamnukuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akieleza kushtushwa na kuhuzunishwa na kifo cha mwanamapinduzi huyo na kumtumia salamu za rambirambi katibu mkuu wa CCM akielezea jinsi alivyoguswa na kifo hicho cha Mzee Natepe.

“Kifo kimemchukua mwanamapinduzi, mzalendo na mwanachama wetu mwaminifu katika kipindi ambacho taifa na chama bado kinamhitaji sana. Kifo kimetunyang’anya tunu wakati huu tunaoelekea uchaguzi mkuu; ni huzuni kubwa kwetu; ni majonzi makubwa na hatuna neno kubwa linaloweza kuelezea huzuni hii,” Rais Kikwete anakaririwa kwenye taarifa hiyo.

Rais alipokea taarifa za kifo cha Mzee Natepe jana mchana akiwa Njombe mkoani Iringa ambako yuko kwa ajili ya shughuli za kampeni.

Rais Kikwete pia ametuma salaamu za rambirambi kwa familia, ndugu na jamaa wa Marehemu Natepe.

“Mzee Natepe amekuwa sehemu ya maisha yangu ya kisiasa, kijamii na amenipa malezi na maelekezo mengi nikiwa kama kijana wake na amekuwa moja ya nguzo yangu kubwa katika shughuli zangu za kisiasa na kikazi katika maeneo yote niliyotumikia nchi yangu,” alisema rais na kuelezea kwa masikitiko huzuni aliyonayo na kuwahakikishia kuwa yuko nao katika kipindi hiki kigumu.

“Tunamshukuru mwenyezi Mungu kwa kutupa nafasi ya kuishi na Mzee Natepe na kufanya naye kazi. Tunamuomba Mungu amlaze mzee wetu mahali pema peponi na kumpa pumziko la milele, amina”
Mbona kitabu kinasema Jackson Makwetta?
IMG-20210516-WA0030.jpg
 
Mzee Mwinyi alivyorudi kivingine na kuwa rais,yule waziri alitetemeka kichiz. Ajabu mzee akamteua tena kwenye baraza lake. Siku ya kuwaapisha mawaziri,akamwambia nimekuteua sijaangalia mambo yako binafsi nimeangalia utendaji wako serikalini. Baada ya siku kadhaa mbele yule waziri akamletea mzee bati roli zima. Mzee akamjibu kama umeamua kurudisha nataka mabati yangu 200 tu na si zaidi. Ikiwezekana kama yatakuwa ni yale yale nitafurahi sana. “kuna la kujifunza hapo”.
 
It is not petty. Anataka wanasiasa vijana wajifunze kujishusha na kutolipiza visasi.

Kumbuka kuwa alipokuwa rais alikuwa anamuapisha huyo huyo aliyemfanyia unyama akiwa amesimama mbele yake akiahidi utii kwa rais.

Ni lazima huyo aliyefanya ubaya alikuwa na unyonge mwingi wakati wa kiapo na wakati wa kupokea maagizo.

Wanasiasa wengi wa afrika hawana uwezo wa kujishusha, wanajawa na kile kiburi cha elimu kinachochanganyika na ushauri mbovu wa wapambe wanaoshauri ubaya ufanyike ili waendelee kuutunza ukaribu wao na bosi wa nchi.
Nimekuelewa bwashee!
 
Wapunguze bei ya kitabu.. kutoka 70,000 wauze hata 30,000 ili wanunue watu wengi au hawajui Biashara?
 
Kawaida ya watu wenye roho za kimaskini ni kudhulumu kwa kudhani ndio njia nyepesi ya kujikwamua!! Na watu wenye mioyo iliyoridhika huwa hawajali "fukara anayeogopa umaskini" anapowadhulumu bali wao humshukuru Muumba.
 
Kwa maelezo yaliyosomwa na Prof. Mkandara, ni sahihi kusema pasi na shaka wala kumvunjia heshima, kwamba Mh. Rais Mwinyi alikuwa dhaifu kuliko rais wote katika historia ya nchi yetu!
Haswaa, Kuna tofauti ya uungwana na udhaifu uliokithiri...choose uno.
 
Kwa hisani kubwa kabisa ya Jamiiforums tarehe 23 Julai 2019
: Jinsi Natepe alivyomhenyesha Rais Ali Hassan Mwinyi

Alipojiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi mwaka 83? kama sijakosea nafasi yake aliteuliwa mzee mmoja kutoka Zanzibar anaitwa mzee Abdallah Said Natepe kushika uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi.

Meja Jenerali Abdallah Said Natepe alipoingia tu ofisini alimtaka waziri aliemtangulia kutoka katika nyumba ya waziri ili yeye aweze kukaa hapo kama waziri.

Ilikuwa shida kidogo maana waziri aliyeondoka bado alikuwa anatafuta makazi lakini alitakiwa haraka kutoka na Meja Jenerali Natepe.

Ikampasa mzee Ali Hassan Mwinyi kutoka kwa haraka na siku anatoka pale nyumbani alikuwa amenunua mabati 150 na mifuko ya saruji 100 ya kwake wala sio mali ya serikali.

Mzee Abdallah Said Natepe alimkatalia kuvichukua akidai ni mali ya serekali kweli mzee Ali Hassan Mwinyi akaviacha akaondoka.

Baada ya miezi kadhaa tu mzee Ali Hassan Mwinyi akateuliwa kuwa Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar . Mzee Abdallah Natepe wakati anajifikiria jinsi ya kwenda kumpongeza na kumuomba radhi kwa aliyomfanyia kabla ya kufikiria njia mzee Ali Hassan Mwinyi akaletwa bara mwaka 1985 kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hapa sasa Mzee Meja jenerali Abdallah Natepe akajua kazi hana na atatimuliwa haraka iwezekanavyo tena na kutengwa na nyadhifa za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwakuwa kuna mabaya ya wazi na ya sirini aliyomtendea mzee Ali Hassan Mwinyi.

Mzee Mwinyi baada tu ya kuapishwa kuwa Rais wa JMT wakati anateua baraza la mawaziri akamteua tena Abdallah Said Natepe kuwa waziri pale pale mambo ya ndani.

Siku ya kumuapisha akamwambia mzee Abdallah Natepe sio kwamba nakupenda sana hapana ila napenda kazi yako unavyofanya endelea kufanya kazi.

Siku moja mzee Mwinyi yupo ikulu kapumzika akaona malori yanaingia na akaambiwa mzigo wako huu Mh. Ali Hassan Mwinyi rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania akashtuka mbona sijaagiza kitu mie??

Ndipo akaambiwa umetoka kwa Natepe, mzee Ali Hassan Mwinyi akacheka sana akawaambia wasaidizi wake shusheni mabati 150 na saruji 100 hizo ndio haki yangu zingine mrudishieni tu.

N.B
Habari za ziada kwa hisani ya intaneti

Sunday, September 26, 2010​

MUASISI WA MAPINDUZI ZANZIBAR ABDALLA SAID NATEPE AMEFARIKI DUNIA​


Mmoja wa viongozi 14 wa Mapinduzi matukufu ya Zanzibar,Meja Jenerali Abdallah Said Natepe amefariki dunia jana mchana katika hospitali yajeshi Lugalo mjini Dar es Salaam.

Marehemu Natepe ni miongoni mwa viongozi wa mapinduzi kumbi na mbili waliofariki dunia ambao walifanikisha kufanikiwa kwa mapinduzi ya Januari 12, 1964 yaliyoindoa serikali ya kisultani visiwa vya Zanzibar,

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, kifo hicho kimetokea jana mchana kwenye hospitali hiyo kuu ya Jeshi la Wananchi.
Taarifa hiyo inamnukuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akieleza kushtushwa na kuhuzunishwa na kifo cha mwanamapinduzi huyo na kumtumia salamu za rambirambi katibu mkuu wa CCM akielezea jinsi alivyoguswa na kifo hicho cha Mzee Natepe.

“Kifo kimemchukua mwanamapinduzi, mzalendo na mwanachama wetu mwaminifu katika kipindi ambacho taifa na chama bado kinamhitaji sana. Kifo kimetunyang’anya tunu wakati huu tunaoelekea uchaguzi mkuu; ni huzuni kubwa kwetu; ni majonzi makubwa na hatuna neno kubwa linaloweza kuelezea huzuni hii,” Rais Kikwete anakaririwa kwenye taarifa hiyo.

Rais alipokea taarifa za kifo cha Mzee Natepe jana mchana akiwa Njombe mkoani Iringa ambako yuko kwa ajili ya shughuli za kampeni.

Rais Kikwete pia ametuma salaamu za rambirambi kwa familia, ndugu na jamaa wa Marehemu Natepe.

“Mzee Natepe amekuwa sehemu ya maisha yangu ya kisiasa, kijamii na amenipa malezi na maelekezo mengi nikiwa kama kijana wake na amekuwa moja ya nguzo yangu kubwa katika shughuli zangu za kisiasa na kikazi katika maeneo yote niliyotumikia nchi yangu,” alisema rais na kuelezea kwa masikitiko huzuni aliyonayo na kuwahakikishia kuwa yuko nao katika kipindi hiki kigumu.

“Tunamshukuru mwenyezi Mungu kwa kutupa nafasi ya kuishi na Mzee Natepe na kufanya naye kazi. Tunamuomba Mungu amlaze mzee wetu mahali pema peponi na kumpa pumziko la milele, amina”
Kumbe alilipwa? Asa mnakunja nn?
 
jamaa nasikia kipindi akiwa waziri aliomba gari kwa mkurugenzi kwa ajili ya shughuli za harusi ya mwanae!jamaa akamtolea nje kimadharau.mungu si hadija ndala ndefu mwisho wa siku akawa prezdaa mbona mkurugenzi hakuna rangi aliacha kuona..jamaa alikuwa alikuwa ana kisasi kinoma he never let go untouched..km gabachori manjis gas alivyomwambia wakati ni wazir kwamba mimi hapana ongea na mbwa mi iko ongea na yenye mbwa!!kitu alifanywa hatakaa asahau maisha yake
 
Kwa maelezo yaliyosomwa na Prof. Mkandara, ni sahihi kusema pasi na shaka wala kumvunjia heshima, kwamba Mh. Rais Mwinyi alikuwa dhaifu kuliko rais wote katika historia ya nchi yetu!
Umekuwa mwepesi sana kutoa hukumu kwa vile labda ulikuwa hujazaliwa kipindi hicho. Mzee Mwinyi alipokea nchi hii ikiwa hoiiii bin taaban! Yaani aliachiwa fremu tu ya nchi. Hata ukitaka sabuni ya mawingu ya kufulia ilikuwa lazima upange foleni, kwa waliokuwa vijijini ile mifuko ya kitambaa (kikiitwa Marekani) iliyokuwa ikija na mchele na unga ndiyo mavazi, redio ya mkulima ndiyo ilikuwa ya maana, eti kuwa na televisheni au friji ulikuwa mlanguzi, heeeee!

Umewahi kuisikia 'redio kiroboto' iliyokuwa ikieleza kwa kificho jinsi nchi ilivyokuwa ikipata shida kwa kukosa mahitaji muhimu? Mbali ya kutukanwa na kushambuliwa na Nyerere na wengine hadharani Mzee Mwinyi alikuwa mvumilivu na hakuwahi kumjibu hata siku moja.

Umewahi kusikia vijana waliowahi kuteka nyara ndege ili angalau kujikwamua katika hali ngumu iliyokuwepo? Wale walikuwa desperate yaani (siyo kwamba naona ni vyema). Ilikuwa safari nje ya nchi lazima upate kibali cha Ikulu na Income tax ndiyo upatiwe tiketi.

Mzee Mwinyi hii nchi aliitoa mbali sana ambao nyinyi kwa sasa munaona ni vitu vya kawaida. Yeye kama binaadamu hakuwa mkamilifu na alifanya makosa kadhaa lakini kwa kweli aliyofanya mema ni mengi kuliko hayo mapungufu.

Lakini sisi binaadamu hatuna shukurani hata tukifanyiwa wema vipi bado baya moja litakuwa na nguvu zaidi kuliko yale mengine.
 
Na ni yeye Mwinyi ambae hakuwa muungwana.

Alitaka waziri afanyeje, amtunzie mirunda na mi kokoto yake mbele ya nyumba ya Waziri?

Au waziri asinunue vya kwake kwa sababu hakuna nafasi ya kuvitunza nyumbani kwake ?

Na kama mtu umemwona ni mdhulumati kwa nini umempa uwaziri, ili atuibie ?

Wana bahati sana wanaandika vitabu vya gibberish kama hizi huku Afrika ambako hakuna audience ya kuchambua pumba na michele wanayoisema

Nadhani ni wewe ndiyo kujafanya uchambuzi sahihi na umerukia tu.

Hebu kasome vizuri ile note ya zamani iliyoletwa na mmoja wa members humu. Ameandika kwamba alimeteua kwa vile utendaji wake wa kazi ni mzuri na ile issue ilikuwa ni personal siyo ya kiserikali.
 
Roho ya mwendazake ilijaa kutu za chuki mpk umeme wa pacemaker ukakatika.
Mtu unakuwa na roho mbaya mpaka unatia huruma .yaani wale unao waonea wanakuhurumia wewe duuu!! Hii kali.... Bongo ya ajabu sana.

Kufanya kazi vile usiku na mchana kuuumbe ilikuwa ni roho ya visasi vinamsukuma!!!

Ndo mjifunzie kwa mwenda zake ...uislamu safi sana wadumu hawa watu na ndo Dini ya kweli.
 
Miaka ile ya mwisho mwa uongozi wa Nyerere kuelekea ile ya Mwinyi hapa bongo kulikuwa na umaskini mkubwa sana. Mzee Mwinyi ikabidi akubaliane na masharti ya IMF kama yalivyoletwa.

Ni katika kipindi hicho cha miaka ya 1980 katikati ndio vijana wengi wenye uwezo na elimu waliposafiri kwenda Uingereza, Canada na Marekani. VIjana wenye elimu wakiwa ni watoto wa wazazi wenye nafasi serikalini ndio wakafanya mikakati ya kufanya mitihani ya TOEFL ili wapate nafasi za kujiunga na vyuo vikuu vya huko nje.

Hawa wanaoitwa diaspora wengi wao waliondoka nchini kipindi hicho, hali ya uchumi ilikuwa mbaya tukiwa tumetoka kupigana vita ya Kagera, na hazina ya nchi ikiwa tupu.

Hivyo Mzee Mwinyi ni shujaa mwenye kila aina ya haki ya kuenziwa. Wapo wanaojaribu kumdhihaki lakini alichokifanya kwa kutazama mazingira ya wakati ule ni chema kwa ajili ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom