Waziri Ndalichako better late than never; Mikopo ya elimu ya juu hailipiki sababu ya Value Retention fee ya 6%

Waziri Ndalichako better late than never; Mikopo ya elimu ya juu hailipiki sababu ya Value Retention fee ya 6%

Tatizo la nchi hii ni katiba mbovu alioiacha Mwalimu huku akijua ikipata kiongozi asiye na hekima yeye ndie atakuwa executive, judiciary na parliamentary. Na si hivyo tu, bsli atakuwa mungu mtu na asihojiwe na yeyote. Katiba hii inaruhusu yeye awe kila kitu. Hata wanaotakiwa kumshughulikia kiongozi anayeharibu nchi (mavipenyo) yeye ndie anawachagua na wanamuogopa. Fikiria nchi kama Marekani ingekuwa na katiba bomu kama hii, nakuhakikishia Trump angewatesa sana na asingetoka madarakani. Maskini wee, Mwalimu alifikiri wote huwa wana hekima, hakujua hata wasio na hekima (wapumbafu) huwa wana fluke na kupata vyeo vikubwa!
Na CCM ndio hawataki kubadilisha katiba
 
Haulipiki, unacholipa ni kidogo kuliko riba inayoongezeka
 
Hii ya
Madeni ya HESLB ni noma sana, plus ukosefu wa ajira na kuzuiwa kwa mafao.

Nihatari kwa Usalama wa nchi yetu. Nivema wahusika wakawajibika.

Ikitokea mtu mmoja akawaunganisha wahanga hawa nchi inaweza ingia matatani

Mh! Raisi wangu naomba uliangalie hili ili lisije chafua kazi nzuri unayofanya.
 
Mimi sijasoma LAW ila najua kuwa kabla kutunga sheria yeyote lazima uangalie impact yake mahala itakapotumika kinagaubaga. Na kama itaacha loophole yeyote basi lazima ibadilishwe ili kukidhi vigezo. Sasa walipotunga hii sheria sijui kama walifikiria kama kuna siku graduate atakosa ajira rasmi na kujiari kama bodaboda.
Hii ya
Madeni ya HESLB ni noma sana, plus ukosefu wa ajira na kuzuiwa kwa mafao.

Nihatari kwa Usalama wa nchi yetu. Nivema wahusika wakawajibika.

Ikitokea mtu mmoja akawaunganisha wahanga hawa nchi inaweza ingia matatani

Mh! Raisi wangu naomba uliangalie hili ili lisije chafua kazi nzuri unayofanya.
 
Mikopo ya elimu ya juu hailipiki na huu ndio ukweli sababu ya ujinga wa Value Retention fee ya 6%.

Mfano: Mnufaika asiye na ajira rasmi anatakiwa kulipa 100000 au 10% ya kipato anachokilipia kodi kwa mwaka. Mimi nilifungua stationery walipokuja kunikadiria kodi nilitakiwa kulipa 200,000/= kwa mwaka.

Kwahiyo 10% yangu ni 20,000/= ndio natakiwa nilipe bodi kila mwezi. Mkopo wangu ni milioni 10. Nikilipa kwa mwaka nitalipa laki 2.4. Deni litabaki milioni 9 na laki 7 na sitini elfu.

Mwaka unaofuata hili litaongezeka kwa 6% ambayo ni sawa na laki 5 na point hivyo deni langu litarudi milioni 10 laki 3. Kwa hali hii nani atajileta kwa hiari?

Bado kuna wale vijana waliosoma nje ya nchi ada zao kwa dola kisha wakija nchini mishahara laki 7, unafikiri deni watamaliza?

Peleka muswada wa mabadiliko ya sheria ya HESLB ili tuone kama kweli elimu yako ya uprofesa ni genuine.

Muda bado upo.
Wabunge wa upinzani walionya mapema bungeni. Ndugai na viherehere wa Ccm wakaoitisha kwa wingi wao. Walidhani ina wahusu Chadema na Act wazalendo. Sasa wako wenyewe wana hadaa motion wameianzisha wao.
Bado records zipo. Hata Ndugai aki rest leo, bado historia ita mhukumu.
 
Kwahiyo hili hawalioni? Hebu fikiria kijana ambae hajaajiriwa tangia 2015 retention fee yake inasoma tu na hajui ataajiriwa lini
Huyo bora asiajiriwe tu, maana deni lake now ni karibia mara 10 ya alichokopa
 
Profesa anayesikia tu tamko la mkulu kuwa lianzishwe somo la Historia ya Afrika Kusini haipiti hata saa 24 tayari ashatangaza kuanzakwa somo hilo kuanzia la kwanza mpaka kidato cha Sita tena kwa Kiswahili ili mradi mkuu afurahi yaani
 
Rudia kusoma alichoandika mkuu, pengine unaweza kuelewa na ukchangia kwa hoja nzuri na yenye mashiko.

Mleta mada hajakataa kulipa huo mkopo, anazungumzia changamoto ya retention fee na riba inayoongezeka kila mwaka kadri unavochelewa kuanza kurejesha mkopo, pamoja na ile Asilimia waliyopandisha kutoka 8% hadi 15%. Hivo vitu ni maumivu sana

Nadhani ungekuwa na mtoto anapata mateso ya huo mkopo usingeandika kwa kejeri namna hiyo.

Kuwa mstaarabu ndugu huenda wew ni mnufaika wa utawala huu kaa ukijua kuna wahitim wa vyuo vikuu wanasota kurudisha mkopo wa Bodi ya mikopo.

Kiufupi huo mkopo haulipiki, basi tu hujui adha tunayoipata.
Msamehe bure... Pengine hata haelewi alichoandika... Inawezekana hajui hata kinachoongelewa hapa... Si unaona hata mwandiko wake ulivo mbovu!!
 
Mikopo ya elimu ya juu hailipiki na huu ndio ukweli sababu ya ujinga wa Value Retention fee ya 6%.

Mfano: Mnufaika asiye na ajira rasmi anatakiwa kulipa 100000 au 10% ya kipato anachokilipia kodi kwa mwaka. Mimi nilifungua stationery walipokuja kunikadiria kodi nilitakiwa kulipa 200,000/= kwa mwaka.

Kwahiyo 10% yangu ni 20,000/= ndio natakiwa nilipe bodi kila mwezi. Mkopo wangu ni milioni 10. Nikilipa kwa mwaka nitalipa laki 2.4. Deni litabaki milioni 9 na laki 7 na sitini elfu.

Mwaka unaofuata hili litaongezeka kwa 6% ambayo ni sawa na laki 5 na point hivyo deni langu litarudi milioni 10 laki 3. Kwa hali hii nani atajileta kwa hiari?

Bado kuna wale vijana waliosoma nje ya nchi ada zao kwa dola kisha wakija nchini mishahara laki 7, unafikiri deni watamaliza?

Peleka muswada wa mabadiliko ya sheria ya HESLB ili tuone kama kweli elimu yako ya uprofesa ni genuine.

Muda bado upo.
Kuna siku kama sijakosea alisema serikali kwenye makato ya heslb ina haki ya kukata ata mpka robo tatu ya mshahara.😫😫
 
Profesa anayesikia tu tamko la mkulu kuwa lianzishwe somo la Historia ya Afrika Kusini haipiti hata saa 24 tayari ashatangaza kuanzakwa somo hilo kuanzia la kwanza mpaka kidato cha Sita tena kwa Kiswahili ili mradi mkuu afurahi yaani
Yani wanafanya kazi ya kulinda vibarua siyo masilahi ya wananchi
 
Lipa madeni ya serikali na wengine wakope ili wasome kama wewe ulivyo someshwa. Kwani kuomba mkopo ulilazimishwa? Kama ulijua huo mchanganuo, kwanini hukukataa kuchukua huo mkopo? Umeanza kuleta michanganuo ya deni na ukali wake baada ya kuhitimu shahada yako. Unafahamu kuwa wapo ambao wamesitisha masomo baada ya kukosa huo mkopoo? Dawa ya deni nikulipa.
Ajakataa kulipa tatizo lipo unalipa unategemea deni linapungua kumbe bado lipo pale pale
 
Huyo unayemuomba mwenyewe muda huu amechanganyikiwa kuandaa vitabu vya somo la historia ya Tanzania kwa ajili ya wanafunzi wa chekechea mpaka chuo kikuu!

Sijui hata kama ana muda wa kuusoma huu ushauri wako! Maana ana upigania huo Uwaziri wake kwa namna yoyote ile baada tu ya kutishiwa kutumbuliwa kwa ulegevu wake na kusuasua kuanzisha hilo somo haraka, na Mzalendo namba 1 Nchini.
Uzalendo ni kusoma historia? Yaani usome historia mpaka chuo kikuu halafu unyimwe ajira huku watoto wa vigogo wakiajiriwa kimyakimya . Ili uitwe mzalendo eti usilalamike?
 
Inashangaza sana.Halafu anaibuka mtu anasema et yeye ni mtetezi wa wanyonge!
 
Back
Top Bottom