Waziri wa fedha ingilia kati sakata la uboreshaji wa mashine za EFD, kamishna wa TRA ataleta balaa kubwa

Kawaida wabongo kila zoezi wanasubiri mwishoni ndio wanakurupuka wengi wanategemea watahudumiwa hio siku ya mwisho.
1.nida
2.tin verification
3.passport
Na sasa hivi zoezi hili wamesubiri mwezi umeisha ndio wanaenda na kuomba muda uongezwe.
Mimi nilipeleka mashine yangu Dec 30 wakati wengi bado wanakula sikukuu na ilikuwa upgraded siku hio hio.
 
Mtu anayelipa kodi halali 100% kwenye hii serikali ya kizuyunani hana akili.. Loopholes zipo kibao, chezeni nazo..

Mimi nacheza nazo, na nawaumiza sana tu..
 
Kuna siku nililalamika kuhusu ili jambo kuna kichaa mmoja akaona ni suala dogo. Magufuli ajaribu kuangalia sana hawa TRA hawana nia njema kbs na kama ndio anawatuma kuna jambo analitafuta. Kulikuwa na uharaka gani? EFD zina serial number zina TIN namba hili janga la BARCODE linakuja kuharibu kbs biashara za watu. TRA wajiangalie biashara haifanywi kwa sifa za kijinga unatoa mwezi mmoja ili iweje.
 
Mashine yangu ilikubali upgrade,sikununua na ilifanywa bure na supplier.
 
Unajua kwanini wameweka hio system ya barcode?
 
Unashauri zoezi lingechukua muda gani?
Swali lako lielekezwe kwa mawakala , angalau kila wakala anajua idadi ya mashine alizosambaza na bila shaka anajua kwa siku 1 angeweza kurekebisha mashine ngapi , baada ya hapo ingekuwa rahisi sana kwa TRA kujua zoezi hilo laweza kwisha kwa muda gani
 
Biashara yoyote yenye mauzo ghafi 14m na kuendelea.
hii unamaanisha Kwa mwaka mkuu sio?
mauzo ghafi Kwa ngeli ni nini?
je yakiwa chini ya 14m unataka nini mtu akinunua kitu? Au najitengezea za kwangu stationery?
 
Yes huu ujinga mawakala wanapiga watu sana

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Wacha kamba wewe, mwezi moja unatosha sana nyinyi mmezoea kazi ndogo kama hizi kufanywa kwa miezi sita. Hakuna huo mpango hivi sasa. Baada ya mwezi lazima wamalize wafanye kazi usiku na mchana.
Ndugu umewahi kufanya biashara yoyote hata ya genge lakuuza pilipili maana ulichoongea hapa inadhihirisha ni mtumwa wa ajira

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Unaongea usichokijua nadhani wee ni muajiriwa huwezi kuelewa kitu

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Ndugu nikisoma comments za huyo anaejiita natafuta naona Nchi bado ina wajinga wengi sana

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 

Mmh! Mmeshindwa kuyaongea hayo kule chamani? Mmeshindwa kujua serikali ni uwakilishi wa watu?

Huvu mnanung'unikiwa. Nyie ni wawakilishi wa nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…