Waziri wa Kilimo Hussein Bashe zuieni uuzwaji wa chakula nje ya nchi, mfumuko wa bei unatisha!

Waziri wa Kilimo Hussein Bashe zuieni uuzwaji wa chakula nje ya nchi, mfumuko wa bei unatisha!

Sijui kwa nini hili hawalioni hawa watu.
Nipo Kusini huku ninanunua korosho zikiwa bado maua,na hili ni kwa kila mwaka na inafanyika kwa mazao mengi tu yakiwamo ya chakula.

Bei ya kununua kilo moja ya korosho kwa sasa ni 800 ambapo unapokuja msimu wa minada hufika 2300 kwa kilo,sasa hapo nimeshamlipa mkulima tsh 800 kwa kilo kwa korosho ambazo hazijavunwa,je akivuna na bei ya kilo ikawa 2500 mtasema mkulima ananufaika na bei hiyo?

Njooni huku mashambani muone wakulima wasivyofaidika kabisa na bei kubwa ya haya mazao kwa kuwa umasikini mkubwa umewazunguka kiasi kwamba hawezi kusubiria mpaka avune na kupeleka mnadani kesho na kulipwa baada ya mwezi wakati leo hana chumvi, sukari wala mafuta ya taa na "kangomba" nipo tayari kumpa hela ya kutatua changamoto zake za leo kwa kununua "maua" ya korosho!
Kwenye mfano wako hapo hapo.
Je, kufunga mipaka kunamsaidiaje huyo mkulima ambaye tayari ameuza mahindi au korosho kwa bei ndogo (bei ya shambani) ?
 
Mkuu

Bei ya debe la mahindi huko Tabora vijijini ni 25000/= hadi sasa, watu wameshaanza kula kwa kununua unga kwa kilo sh.1700 hadi sasa na hii ni Oktoba hatujui January hali itakuwaje!

Fungeni mipaka hali sio nzuri kabisa, watu wasije kufa njaa, mfuko wa sembe ushafika sh.37000/= tena vijijini kabisa hali sio nzuri!

Naamini utasoma na hatua zitachukuliwa!
Kajilimie chakula chako jiwekee akiba siyo wanaume wenzio wakuwekee akiba
 
Sijui kwa nini hili hawalioni hawa watu.
Nipo Kusini huku ninanunua korosho zikiwa bado maua,na hili ni kwa kila mwaka na inafanyika kwa mazao mengi tu yakiwamo ya chakula.

Bei ya kununua kilo moja ya korosho kwa sasa ni 800 ambapo unapokuja msimu wa minada hufika 2300 kwa kilo,sasa hapo nimeshamlipa mkulima tsh 800 kwa kilo kwa korosho ambazo hazijavunwa,je akivuna na bei ya kilo ikawa 2500 mtasema mkulima ananufaika na bei hiyo?

Njooni huku mashambani muone wakulima wasivyofaidika kabisa na bei kubwa ya haya mazao kwa kuwa umasikini mkubwa umewazunguka kiasi kwamba hawezi kusubiria mpaka avune na kupeleka mnadani kesho na kulipwa baada ya mwezi wakati leo hana chumvi, sukari wala mafuta ya taa na "kangomba" nipo tayari kumpa hela ya kutatua changamoto zake za leo kwa kununua "maua" ya korosho!
ili mkulima afaidike, ili watu waende kulima na wawekeze kwenye kilimo inatakiwa zoezi la kuacha mipaka wazi liwe endelevu siku zote, maisha yote.
 
Kwenye mfano wako hapo hapo.
Je, kufunga mipaka kunamsaidiaje huyo mkulima ambaye tayari ameuza mahindi au korosho kwa bei ndogo (bei ya shambani) ?
Hakumsaidii yeye binafsi kama mkulima,bali kunasaidia Watanzania wote kwani bei ya mazao ya chakula haitakuwa juu kutokana na kupatikana kwa urahisi.
 
Acha wakulima nao wapate faida Mana mmewanyinya mda mrefu nyie watu wa mjini. Wakulima ndo wengi kuliko nyie watu wa mjini. Na Samia atapita kwa kishindo 2030 kura kutoka kwa Hawa wakulima. Pia ni strategy ya kuwavutia vijana wakalime siyo zamani unalima halafu hujui ukauze wapi.
Wanaopata faida sasa hivi hata siyo Wakulima bali wafanya Biashara!!!


Mkulima kashauza mazao yake kitambo sana kwa bei ya kutupwa!!!
 
Mkuu

Bei ya debe la mahindi huko Tabora vijijini ni 25000/= hadi sasa, watu wameshaanza kula kwa kununua unga kwa kilo sh.1700 hadi sasa na hii ni Oktoba hatujui January hali itakuwaje!

Fungeni mipaka hali sio nzuri kabisa, watu wasije kufa njaa, mfuko wa sembe ushafika sh.37000/= tena vijijini kabisa hali sio nzuri!

Naamini utasoma na hatua zitachukuliwa!
mazao ni mali ya waliolima , uzuie mtu kuuza mali yake kwa sababu ya wanunuzi masikini wasio na hela wa kitanzania ! yaani uache vibopa wa nje ? bila shaka utakuwa umelogwa tu
 
Ni kweli mnanufaika kwa bei hiyo ila mngepambana muwezeshwe muuze unga badala ya mahindi yan hapo ndio mngepiga pesa kinyama tena ingewezekana hata mkiuzia hapa hapa TZ
Hayo tuachie wenyewe wakulima hatuhitaji ushauri wa mtu aliyekaa mezani baadaye utakuja na ushauri ohh uzeni ugali badala ya unga pikeni ugali muuze nje ukiwa umeshaiva tayari mtapata pesa zaidi kuliko mkiuza unga.

Tuachie wenyewe wakulima
 
Mfumuko wa bei ni dunia nzima kutokana na vita ya Ukraine. Siyo bongo peke yake.
 
Mkuu

Bei ya debe la mahindi kwenye baadhi ya vijiji nchini ni 25000/= hadi sasa, watu wameshaanza kula kwa kununua unga kwa kilo sh.1700 hadi sasa na hii ni Oktoba hatujui January hali itakuwaje!

Fungeni mipaka hali sio nzuri kabisa, watu wasije kufa njaa, mfuko wa sembe ushafika sh.37000/= tena vijijini kabisa hali sio nzuri!

Naamini utasoma na hatua zitachukuliwa!
Kifunga mipaka na kutokuuza chakula nchi jirani sio suluhisho la mfumuko wa bei za vyakula.

Unataka kuua njaa jirani zako? Wao wanapata wapi pesa za kununulia huo unga wewe ukose?

Naamini hiyo ndio bei halisi, zidisha juhudi.
 
Hakumsaidii yeye binafsi kama mkulima,bali kunasaidia Watanzania wote kwani bei ya mazao ya chakula haitakuwa juu kutokana na kupatikana kwa urahisi.
Kwahiyo kusema kwamba mipaka ifungwe kwa hoja ya kumsaidia mkulima, sio sahihi. Si ndio ?
 
Mkuu

Bei ya debe la mahindi kwenye baadhi ya vijiji nchini ni 25000/= hadi sasa, watu wameshaanza kula kwa kununua unga kwa kilo sh.1700 hadi sasa na hii ni Oktoba hatujui January hali itakuwaje!

Fungeni mipaka hali sio nzuri kabisa, watu wasije kufa njaa, mfuko wa sembe ushafika sh.37000/= tena vijijini kabisa hali sio nzuri!

Naamini utasoma na hatua zitachukuliwa!
Kwani wakulima hawana haki ya kupata faida? Kipindi cha Magufuli tulipata hasara kubwa sana kwa hiyo wacha na sisi tuinjoi. Hakuna mpaka kufungwa, Bashe shikilia hapo hapo
 
In the long run wafanyabiashara watashindana wao kwa wao kulingana na demnd hivyo Bei itarise na wakulima kunufaika. Jifunze uchumi vizuri
Msimu ujao mvua zikiwa nzuri wakulima watalima supply itakua kubwa zaid ya demands Bei itashuka, Bei inapanda sahivi kwa sababu supply ni ndogo iliyoshababishwa na mavuno hafifu kwenye msimu wa mahindi uliopita kwa hiyo demand kubwa ndo maana bei inapaa
We ndo hujui theory za uchumi zinavyofanya kazi
 
Kwani wakulima hawana haki ya kupata faida? Kipindi cha Magufuli tulipata hasara kubwa sana kwa hiyo wacha na sisi tuinjoi. Hakuna mpaka kufungwa, Bashe shikilia hapo hapo
Ni wakulima wachache sana wenye mazao wengi walishawauzia wafanyabiashara na wengine waliuza mazao yao tokea yakiwa shambani wanufaikaji wakubwa ni wafanyabiashara wa kupanda huku kwa bei
 
Back
Top Bottom