TANZIA Waziri wa TAMISEMI Mohammedi Mchengerwa Amefiwa na Baba Yake Mzazi Akiwa Ibadani Makka Na Atazikwa hukohuko Makka

TANZIA Waziri wa TAMISEMI Mohammedi Mchengerwa Amefiwa na Baba Yake Mzazi Akiwa Ibadani Makka Na Atazikwa hukohuko Makka

Naomba unijibu haya Maswali yangu yafuatayo ukiwa kama CHAWA GEGEDU wa Familia yake na ya Mkwe wake.....

1. Nini kimesababisha hasa Kifo cha Baba yake?

2. Kabla ya Baba yake kwenda huko alikofia alipimwa Afya?

3. Kumeshindikana nini Kuurudisha Mwili Tanzania ili azikwe na imelazimika azikwe huko huko alikofia?

4. Je, katika hizi Ratiba zote tajwa hapa juu Mama Mkwe na Dogo Dullah watahudhuria?

5. Kwa mazingira yaliyoko huko Alikofia Baba yake Mzazi na Umri wake kulikuwa na Ulazima wowote Yeye kwenda?

6. Kwanini haya Maamuzi ya Baba yake kuzikwa huko huko Alikofia yamekuwa ni ya haraka sana na yanalazimishwa?

7. Je, yale Masharti ya Watu kwenda Kuhiji huko Alikofia yalifuatwa vyema na Yeye Marehemu na Mwanae Waziri?

Nasubiria majibu yako CHAWA GEGEDU wa Familia zote mbili ya Mfiwa na Mkwe na pia ukiwa kama Mwanafunzi wangu.
Akikujibu vema ni tag
 
Pole Sana Ila nasikia kwenda huko unabidi utumie HELA ambazo hazina makando kando.
Ni kweli kabisa ibada ya HIJA au umra inatakiwa ifanyike kwa kutumia mali zilizopatilana kwa njia ya halali!
Na sisi tunamhukumu mtu kutokana na yale tunayoyaona pasi na kidhaniana dhana mbaya au kupelelezana.
Mtu ambaye hujamkamata akiiba ukimuita mwizi wapata dhambi na kimpeleleza pia ili ujue kama ni mwizi pia ni dhambi!
Allaah amekataza kupelelezana na kudhaniana dhana mbaya katika Suurat Alhujuraat Aya ya 12 pale aliposema:
"{ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱجۡتَنِبُواْ كَثِيرٗا مِّنَ ٱلظَّنِّ إِنَّ بَعۡضَ ٱلظَّنِّ إِثۡمٞۖ وَلَا تَجَسَّسُواْ وَلَا يَغۡتَب بَّعۡضُكُم بَعۡضًاۚ أَيُحِبُّ أَحَدُكُمۡ أَن يَأۡكُلَ لَحۡمَ أَخِيهِ مَيۡتٗا فَكَرِهۡتُمُوهُۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ تَوَّابٞ رَّحِيمٞ }
Enyi mlio amini! Jiepusheni na dhana nyingi, kwani baadhi ya dhana ni dhambi. Wala msipelelezane, wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi. Je! Yupo katika nyinyi anaye penda kuila nyama ya nduguye aliye kufa? Mnalichukia hilo! Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kupokea toba, Mwenye kurehemu."
 
Baba yake Wazir wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mohamed Mchengerwa, Alhaj Omary Mchengerwa amefariki leo Alfajiri akiwa kwenye Ibada ya Umrah huko Makkah.

Kwa mujibu wa taarifa ya Familia ya Mchengerwa, Mzee Omary atazikwa leo huko huko Makka.

Ifuatayo ni Ratiba ya Ibada ya Visomo vitakavyoongozwa na Mufti wa Tanzania Dkt Zuberi Bin Ali wa Mbwana nyumbani kwa Waziri Mchengerwa, Masaki Dar es Salaam.

LEO: TAREHE 24 FEBRUARI 2025

Dua ya Kisomo itafanyika nyumbani kwa Mhe. Mohamed Mchengerwa Masaki saa 10 Alasiri

KESHO TAREHE: 25 FEBRUARI 2025

Dua ya kisomo itafanyika Jimboni Rufiji

KESHO KUTWA TAREHE: 26 FEBRUARI 2025

Dua itafanyika nyumbani kwake Marehemu Alhaj Omary Mchengerwa Yombo.
"Allahumma ighfir lahu warhamhu wa ‘afihi wa’fu ‘anhu wa akrim nuzulahu wa wassi’ madkhalahu waghsilhu bil-ma’i wath-thalji wal-barad, wa naqqihi mina adh-dhunubi wal-khataya kama yunaqqa ath-thawbu al-abyadu mina ad-danas, wa abdilhu daran khayran min darihi, wa ahlan khayran min ahlihi, wa adkhilhu al-jannata wa a’idhhu min ‘adhabil-qabri wa min ‘adhabin-nar."

Maana yake:
“Ewe Mwenyezi Mungu! Msamehe na umrehemu, mpe afya na umuachilie. Mheshimishe kwa mapokezi mema na mpatie nafasi pana. Muoshe kwa maji, theluji na barafu. Mtakase na madhambi kama vazi jeupe linavyotakaswa na uchafu. Mbadilishie nyumba bora kuliko aliyokuwa nayo, familia bora kuliko aliyokuwa nayo, na muingize Peponi. Muepushe na adhabu ya kaburi na moto wa Jahannam.”

Dua hii inafundishwa katika Hadithi ya Mtume Muhammad (SAW) na ni nzuri sana kwa kumuombea msamaha marehemu wa kiume. Inaweza kusomwa baada ya Swala ya Janaza au wakati wowote wa kumuombea marehemu.
 
Unaleta habari nusunusu huku tunakujua unaandika sana thread ndefu. Umeshindwa nini kuleta habari iliyokamilika na timilifu? Haya sasa, jibu maswali ya GENTAMYCINE
 
"Allahumma ighfir lahu warhamhu wa ‘afihi wa’fu ‘anhu wa akrim nuzulahu wa wassi’ madkhalahu waghsilhu bil-ma’i wath-thalji wal-barad, wa naqqihi mina adh-dhunubi wal-khataya kama yunaqqa ath-thawbu al-abyadu mina ad-danas, wa abdilhu daran khayran min darihi, wa ahlan khayran min ahlihi, wa adkhilhu al-jannata wa a’idhhu min ‘adhabil-qabri wa min ‘adhabin-nar."

Maana yake:
“Ewe Mwenyezi Mungu! Msamehe na umrehemu, mpe afya na umuachilie. Mheshimishe kwa mapokezi mema na mpatie nafasi pana. Muoshe kwa maji, theluji na barafu. Mtakase na madhambi kama vazi jeupe linavyotakaswa na uchafu. Mbadilishie nyumba bora kuliko aliyokuwa nayo, familia bora kuliko aliyokuwa nayo, na muingize Peponi. Muepushe na adhabu ya kaburi na moto wa Jahannam.”

Dua hii inafundishwa katika Hadithi ya Mtume Muhammad (SAW) na ni nzuri sana kwa kumuombea msamaha marehemu wa kiume. Inaweza kusomwa baada ya Swala ya Janaza au wakati wowote wa kumuombea marehemu.
Hii Dua ni Kwa wale wanaofia Makkah au marhum Wote?
 
Sina tatizo lolote. Nimeona Wote mmetupia taarifa hiyohiyo, maudhui yaleyale, muda huohuo. Inatokea sana kwa wenye multiple ID.
Ungesoma heading usingepata shida iliyokukuta

Mimi nilimnukuu Maulid Kitenge kisha mods wakaongezea nyama na kuunganisha Uzi
 
Back
Top Bottom