Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Mbarawa azungumza kuhusu uwekezaji wa Bandari

sio usiri ni Hira, wangehusisha wanasheria wao ingesaidia, nina mashaka na ujuzi wa mwanashetia mkuu wa serikali kama kweli alihusika
Inawezekana na yeye ni mpendwa mtazamaji, mbona kwenye ufafanuzi hajaitwa kuelezea?
 
Inawezekana na yeye ni mpendwa mtazamaji, mbona kwenye ufafanuzi hajaitwa kuelezea?
Ni kuficha aibu, mana mkataba ule hautakiwi uwe hata na typing error. Kuna mmoja alitetetea hivyo ila sio kwa uzito wa mkataba huu.
 
Mpaka sasa nilichokipata ni kwamba Kujitoa kwenye mkataba ni ngumu. They are bitting about the Bush ...... Njia pekee ni ya Kutaifisha ambayo ni very costly.
 
Advocate Murshid Abdallah Mohammed wa Mvita, Kenya, Wafanyabiashara, makuli wapinga uwekezaji wa DP World nchini Kenya kwa sababu zifuatazo...
Ukiwaambia wanakimbilia kwenye manufaa tu hizo setbacks hawazisemi
 
Mpaka sasa nilichokipata ni kwamba Kujitoa kwenye mkataba ni ngumu. They are bitting about the Bush ...... Njia pekee ni ya Kutaifisha ambayo ni very costly.
Wewe umeona mbali sana. Kwenye hayo makubaliano kuna provision inayosema kwamba ukishasaini umesaini na haivunjiki na hakuna mazungumzo tena kinachofuta ni utekelezaji wa makubaliano na mikataba , walifanya hivyo UK wakafukuzwa, wakafanya hivyo Djibouti Jeshi likaingilia kati na kuwafurusha, wamejaribu Kenya wakamshiwa dude wakanyimwa mkataba ! Afadhali ya Kenya walitangaza tena, sisi tumeenda kuwaomba ndio mana wameona kondoo amekuja machinjioni Wacha tumchinje!

Uliona wapi kondoo aliyepelekwa machinjioni kuchinjwa akachomoka kirahisi! Ndio mana nguvu kubwa inatumkka kutetea faida badala ya kujibu vifungu vyenye ukakasi!

Weamua kubadilisha Sheria ili isuit matakwa ya DP world! Hatari sana mtu anakuja kwako anakulazimisha ubadili taratibu zako za kuishi ili kukidhi matakwa Yake halafu wabunge wanakenua meno tu!
 
Balile is a SELL OUT.

Amejioshesha dhahili kwenye hili kongamano ..... ameonyesha upande wake na amekuwa mpiga debe throughout kwenye hilo kongamano.
 
Reactions: Ame
Muktasari:

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof Makame Mbarawa amezitaja sababu za Serikali kuamua kuichagua Kampuni ya DP World katika kufanya shughuli za uboreshaji wa bandari hapa nchini.

Dar es Salaam; Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof Makame Mbarawa amezitaja sababu za Serikali kuamua kuichagua Kampuni ya DP World katika kufanya shughuli za uboreshaji wa bandari hapa nchini.


Akizungumza katika mkutano na Wahariri leo jijini hapa, Prof Mbarawa amesema DP World ina uwezo mkubwa katika uendeshaji wa shughuli za bandari barani Afrika, Asia, ulaya, Amerika ya Kaskazini na Kusini, na Australia.

“DP World ina uwezo na utaalamu wa kuchagiza katika mnyororo mzima wa usafirishaji kutoka maeneo ambayo bidhaa zinatoka mpaka kwa walaji wa bidhaa hizo,” amesema Prof. mbarawa.
 
Azungumzie mapungufu ya mkataba yanatatuliwaje hizo habari za ufanisi bandarini kila binadamu anazifahamu
Hotuba kama hizi ndizo zinathibitisha nia ovu ya hawa amijei.
Tuko kwenye mkataba wenyewe.
 
Ni kampuni kubwa sana hii ya DP World, ndio walioinunua P & O Nedlloyd pamoja na Maersk. Wengi wetu ni ujuaji mwingi tu ni tatizo lile lile la kukosa ufahamu wa muda husika wanaita exposure.
 
Huyu ni kanjanja hajajibu hoja za Mwabukusi, Dr. Slaa, Lisu, Dr. Nshala na wengine
Hao uliowataja wameongelea vipande vya mkataba, kwa malengo maalum ya kukupotosha wewe Retired na wasomaji wengine humu.

Hawana uwezo wa kuuongelea mkataba mzima kwa ujumla wake.
 
Kama hukusomea sheria nikupe siri.
Unaweza kufafanuliwa jambo kiufasaha lakini nje ya uhalisia wenyewe. (Out of content and context)
Uliwai kujiuliza mawakili huwa wanabishania nini mahakaman wakati sheria rejea zinakuwa zile zile!
Mfano mzuri ni huu.
Leo zimejengwa hoja nzuri kuhusu mapungufu ya bandar kwa sasa na faida za uwekezaji.
Je, hilo ndo tatizo la wanaokataa?
 
Ukiwaambia wanakimbilia kwenye manufaa tu hizo setbacks hawazisemi



Na manufaa yenyewe interms of nini Kwa mfano?

Je kiasi cha pesa kitachopatikana ni kiasi gani?

Kuanzia muda gani tangu kazi kuanza?
 
Hivi Hamza Johari ni nani katika mkataba huu? Anaupambania sana
Amesema yeye ndio alieuandaa huu mkataba na anajua tofauti ya BIT na IGA na HGA mimi najua BIT tu hizo nyingine sizijui kwa hiyo hakutufafanulia tofauti ya BIT na IGA na HGA alisema IGA na HGA ni Viena convection ya 1969 sawa lakini mikataba yote hutumia Viena convection kwa hiyo kutakuwa na confusions nyingi sana kwenye hii kitu ila time will tell
 
Hajajibu maswali ambayo mm na familia yangu pamoja na ukoo wangu tunataka kujua uyo DP - WD. Makubaliano/mkataba ni w miaka mingapi?

Yani wandishi w Habari wa Tanzania hawajui kuhoji wao ni Ndioooooooooo kama wabunge tu.
Hawakuwa waandishi walikuwa wapambe sijawahi ona mwandishi aliekwenda shule anauliza maswali namna ile??Wengine walikuwa wanauliza maswali na kujijibu wenyewe kweli Tanzania ni nchi ya miujiza
 
Kiukweli Waziri Mbarawa na timu yake wamejitahidi kujibu maswali ya wahariri na wametoa ufafanuzi mzuri.

Mimi binafsi nimefurahi kupata maelezo ya maswali mengi tuliyokuwa tunajadili hapa jamvini.

Mfano ukomo wa mkataba na namna ya kuuvunja mkataba
Kikubwa ni kwamba kumbe bado Kuna vitu vingi vinakuja kujadliwa sisi tumewahi sana kuhukumu.

Kwa maelezo ya leo naamini serikali Ina nia njema kwa nchi yetu . Tuwe na subira.
KAZI INDELEE
 
Ulipomalizia KAZI UENDELEE!
Umetia mashaka juu ya andiko lako!

Wakati mwingine unapojaribu kutoa Elimu kwa watanzania, usiweke mazingira yakufanya watu wakuhisi unaongea kwa maslahi ya CCM na Mwenyekiti wake!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…