Wengi mnatokwa povu tu ila huu ndio ukweli wa kwanini SA imeamua kutetea haki za wapalestina kwa kufungua kesi ya mauaji ya kimbari dhidi Israel

Wengi mnatokwa povu tu ila huu ndio ukweli wa kwanini SA imeamua kutetea haki za wapalestina kwa kufungua kesi ya mauaji ya kimbari dhidi Israel

Ni aje waungwana,

Ndugu waungwana hapa jakwaani kwetu kuna vijana wengi ambao wamekuwa waki comment ujinga katika thread za watu wenye akili, na elimu kubwa kushinda wao, lengo ni kutaka waonekane kuwa na wao ni miongoni mwa wale wanaowatetea, hata kama hao wanaowatetewa hakuna anaewajua hata mmoja.

Ndugu waungwana hapa jukwaani kuna watu wanashangaza sana, kwa kukimbilia kuishambulia SA kutokana na kitendo chao cha kufungulia Israel kesi ya mauaji ya kimbari dhidi ya raia wasiokuwa na hatia, kina mama, watoto wachanga wenye umri wa chini ya miaka mitano, vilema, vizee nk.

Washambuliaji hawa wa mitandaoni haswa hapa JF ambao wengi wao wanaongozwa na kundi la wayahudi wa huko chato na nachingwea, wameshindwa kujua sababu haswa zilizopelekea nchi hiyo ya ki afrika kujiingiza katika swala hilo na ukizingatia nchi hiyo ina asilimia ndogo sana ya wavaa kobaz ambao hata hao kidogo wenyewe hawapo serikalini na wala hawana maamuzi yoyote ndani ya serikali, chama tawala wala vile vya upinzani.

Swala hili limewaunganisha wa afrika kusini wote akiwemo mwanasiasa machachari Julius Malema, tena bila kujali utofauti wa vyama vyao.

Na sababu kuu za kuichukia na kuichukulia hatua za kuishtaki kwa ukatili Inayofanya Gaza ni hizi:

1. Afrika kusini ni moja kati ya nchi ambazo zilipitia changamoto kubwa ya kutawaliwa kimabavu, kufungwa bila hatia, kuadhibiwa bila kosa, na wengine kuuwawa kwa sababu ya kudai uhuru wao, ardhi yao na haki zao. Hili walilopitia waafrika kusini ndio wanalilopitia wapalestina kwa zaidi ya miaka 70. Hivyo waafrika kusini wanajua na kufahamu machungu wanayopitia wapalestina kule kwao.

Hili swala la watu wanaojaribu kutumia nguvu kudai haki zao walizonyimwa kwa zaidi ya miaka 70 kuitwa magaidi na nchi za magharibi (Hamas) hata wao wa afrika kusini walikumbana nalo hadi kupelekea baadhi ya vijana na wanachama wa anc kukimbilia Tanzania, Zambia, Zimbabwe na kwengineko ili kukwepa mkono wa sheria wa wazungu ambao waliwaona na kuwaita wapigania uhuru na haki zao, tena katika nchi yao wenyewe kuwa ni magaidi.

2. Pili wakati wa ubaguzi wa rangi, Israel ilikuwa ni moja ya nchi ambazo zilisupport utawala wa kibaguzi wa rangi, lakini pia makaburu wengi walienda Israel kusomea mbinu za kijeshi za kuja kupambana na vijana weusi wa afrika kusini bure bila malipo yoyote kwa wayahudi.

Yaani kwa kiswahili chepesi tunaweza kusema kuwa Israel ndio ilikuwa unadhamini askari hao kwenda kujifunza ukatili katika nchi yao ili waje wauwe wenzao kwa sababu tu ya utofauti wa kirangi nk.

Unaweza ukajiuliza inakuaje nchi nyingi zifanye ukatili na Afrika kusini isiguswe wala kufuatilia ukatili huo, lakini huu wa Israel umewagusa. Na hiyo ni kwa sababu ya historia ya kile walichowanyia kupitia makaburu na kilichowatokea.

Afrika kusini ni nchi kubwa hivyo haiwezi kukurupuka tu kuanza kuichukia nchi nyingine tena ya mbali na mipaka yake bila sababu na ukizingatia nchi wanayoitetea ni ya kiarabu wakati wao sio waarabu, ni ya kiislamu wakati wao 95% sio waislamu.

Yani kwao ni bora hata baadhi ya nchi za kizungu zilionesha kuwasaidia na kuguswa na mateso waliyokuwa wanapitie enzi zile moja ya nchi hiyo ni Denmark kuliko Israel ambayo ilikuwa upande wa wazungu ili wawaangamize na kuwauwa wazawa.

Nina imani kama kungekuwa na ukaribu fulan wa kimipaka, basi wazee wa kazi wangepenyeza silaha kadhaa kwa Hamas ili kulipiza kisasi ya kile walichofanyiwa na wayahudi enzi hizo 😄😄😄

Wale wenye akili zilizojaa kichwa karibuni mjadili ki akili ili wale wasiofahamu sababu ya ufunguaji wa kesi waweze kufahamu na kujifunza. Lakini pia na wale watakaokuja kucheuwa povu lao kama mdomo wa kinda la ndege mnaruhusiwa kwa sharti la kutotukana watu hovyo.
Afrika Kusini wako sahihi kuwashitaki Israel
 
Wewe ndio mjinga,halafu hakuna mahali nilipokwambia mm n myahudi,Sasa kama hujuwi uhusiano wa Israeli na marekani endelea kusema Israel anamtegemea mmarekani,hao south Africa hawamuwezi Israeli kwa chochote kile,na hao wapalestina waendelee kuwakumbatia Hamas ili wagawane maumivu
Maumivu ni kwa watoto wachanga, wanawake na waandishi wa habari ambao wote hao hawana silaha na wala hawapambani na Israel.

Wale vijana elf 20 tu wameshindwa kupatikana, na wale mateka wameshindwa kuokolewa na jeshi zima la Israel likishirikiana na Marekani 😂😂😂

Ndiomaana nakuona haujui unachoandika. Kwanza Afrika Kusini imeshafungua kesi pindi ambapo nchi nyingine zimeshindwa kufanya hivyo (huu ni ubabe wa kwanza wa SA imeuonesha kwa Israel)

Pili imemtimua balozi wa Israel kinoma noma (hii wameionesha Israel yako dharau)

Sasa iambie Israel yako ithubutu kufanya inachoweza kufanya kwa SA kama haijapokea kipigo ambacho haikuwahi kukumbana nacho katika maisha yao. Midege na mivifaro imeshindwa kurudisha mateka waliotekwa na vijana wachache, ndo wataweza kuingia mzigoni na jeshi kubwa lenye uwezo wa hali ya juu.
 
Hilo igizo tu on a the Hague
Mivifaru, madege ya kijeshi, jeshi zima la Israel na askari wa akiba vyote kwa pamoja vimeshindwa kuwakomboa mateka walio katika mikono ya vijana wachache wanaotumia silaha duni 😂😂😂

Hii ni aibu. Ni sawa na jwtz, polisi na askar magereza washindwe kuwakomboa watu wanaoshikiliwa na panya road pale manzese. Hilo litakuwa jeshi tena au ni kikundi cha mgambo chenye silaha.
 
Myahudi wapo kila rangi wewe sema una bifu na wazungu. Wapo wayahud weusi wako wayahud waarabu wapo wayahud wa Iran nk. Kuwa na rangi sawa na mzungu haiondoi ukweli kuwa ni wayahud. Ishu ni kwamba hawa jamaa hiyo style wanayoingia nayo ndio style waliyoondolewa nayo huko miaka ya nyuma.
Kwani uyahudi ni race, dini au taifa?

Naomba unijibu kwanza alaf tuendelee.
 
Yale waliyoyafanya Hamas kuua watoto wazee na wamama 1400 na kuteka watu yalikua sahihi? SA acha waendelee na wanachokifanya kwa sababu ni haki yao lkn hakina madhara yeyote katika mipango ya Israel kujilinda
Wewe unahesabu yale yaliofanywa na Hamas 7 October, lakini hauhesabu zile operation zilizokuwa zinafanywa na jeshi la Israel kabla ya hiyo 7 October huko West Bank.

Walipokuwa wanaingia katika nyumba za wapalestina usiku kuwatoa watu na kuwapeleka kusikojulikana , kuwanyang'anya nyumba zao na kuzikabidhi kwa wayahudi, kuvamia kambi usiku na kuuwa vijana kwa kisingizio kuwa ni magaidi. Kwamba mtu akidai haki yake kwa mapambano hata ya kurusha mawe dhidi ya askari wanaotumia bunduki huyo raia lazima aitwe gaidi. Hii mbinu ilitumiwa sana na makaburu kuwaita vijana waliokuwa wanapigania haki zao kuwa ni magaidi. So hilo ni jambo linalojulikana.

Israel alipokuwa anaingia majumbani kuuwa watu wasiokuwa na hatia hovyo, alipokuwa anavamia kambini kuuwa watu hovyo, kutumia nguvu zilizopitiliza kwa kuruhusiwa kutumia bunduki dhidi ya raia wanaotumia jiwe na manati hilo lilikuwa sawa na ilitafsiriwa kuwa wanajilinda. Lakini hawa ambao wameuwawa, wamenyang'anywa nyumba zao, wamefungwa bila sababu walipoamua kusema sasa unyonge basi acha na sisi tujitutumie kufanya kile ambacho na wao kitawatia uchungu kama tunavyotiwa uchungu sisi kila siku, tayari kikaonekana kuwa ni kitu cha ajabu na kikatili huku ule ukatili uliokuwa unafanywa na Israel kabla ya hiyo 7 October ukiwa umefunikwa kupitia mgongo wa huu mpya wa Hamas.

Cha kushangaza jeshi zima lenye askari zaidi ya laki 2 na wengine wa akiba juu wameingia na midege yao, mivifaru na mimeli ya kivita kupambana na vijana wasiozidi elf 20 tena wenye silaha duni, na mpaka leo wameishia kutumia midege na mivifaru hiyo kuuwa raia tu bila kuokoa mateka wanaoshikiliwa.
 
Ndugu waungwana hapa jakwaani kwetu kuna vijana wengi ambao wamekuwa waki comment ujinga katika thread za watu wenye akili, na elimu kubwa kushinda wao,

Hizi dharau sasa🤣🤣 kama vipi ID zionyeshe detail ya kiwango cha Elimu kisha majukwaa yatengwe kwa level za elimu.m au akili.
Detail ya kiwango cha elimu inaonekana kupitia comments ya mtu.
Sidhani kuwa kuna mtu mwenye elimu anaweza kuandika ujinga, kwa sababu ujinga mara zote huandikikwa na wajinga.
 
Ndugu waungwana hapa jakwaani kwetu kuna vijana wengi ambao wamekuwa waki comment ujinga katika thread za watu wenye akili, na elimu kubwa kushinda wao,

Hizi dharau sasa🤣🤣 kama vipi ID zionyeshe detail ya kiwango cha Elimu kisha majukwaa yatengwe kwa level za elimu.m au akili.
Detail ya kiwango cha elimu inaonekana kupitia comments ya mtu.
Sidhani kuwa mtu mwenye elimu anaweza kuandika ujinga, kwa sababu ujinga mara zote huandikikwa na wajinga.
Mimi tena Mkuu?
Myahudi wa Mbagala huyo, ashavurugwa na vita alafu mateka hajawapa 😄😄
 
Kwani uyahudi ni race, dini au taifa?

Naomba unijibu kwanza alaf tuendelee.
Jews ni jamii iliyochanganyika na race zote. Dini ya yao wanaita Judaism na Taifa ni Israel. Sasa hawa Jews wapo ambao sio waisraeli kuna raia wa Morocco Yemen Iran Iraq Jordan jews na Ethiopia. Hawa walioko Israel wengi ni wale waliorud baada ya mateso huko walipokuwa hasa ulaya kwa miaka mingi ya utawanyiko wao. Japo wapo wale waliokuwepo hapo muda wote mpaka Wakat wa anguko la ottoman empire.
 
Maumivu ni kwa watoto wachanga, wanawake na waandishi wa habari ambao wote hao hawana silaha na wala hawapambani na Israel.

Wale vijana elf 20 tu wameshindwa kupatikana, na wale mateka wameshindwa kuokolewa na jeshi zima la Israel likishirikiana na Marekani 😂😂😂

Ndiomaana nakuona haujui unachoandika. Kwanza Afrika Kusini imeshafungua kesi pindi ambapo nchi nyingine zimeshindwa kufanya hivyo (huu ni ubabe wa kwanza wa SA imeuonesha kwa Israel)

Pili imemtimua balozi wa Israel kinoma noma (hii wameionesha Israel yako dharau)

Sasa iambie Israel yako ithubutu kufanya inachoweza kufanya kwa SA kama haijapokea kipigo ambacho haikuwahi kukumbana nacho katika maisha yao. Midege na mivifaro imeshindwa kurudisha mateka waliotekwa na vijana wachache, ndo wataweza kuingia mzigoni na jeshi kubwa lenye uwezo wa hali ya juu.
Wewe ndio hujuwi unachoongea,hao Hamas wanapigana kwa kujificha kwa raia, Israeli ingetaka kupiga mtu yeyote bila kuangalia raia wapalestina wangeisha,halafu hiyo SA haimuwezi Israeli kuanzia uchumi mpaka technology,hao waarabu wanaomzunguka Israeli kwa pamoja walichezea kichapo ndani ya siku sita,SA anatafuta kiki,hamuwezi Israel kwa chochote kile,na kadiri muda unavyozidi kwenda utathibitisha mwenyewe nan anaumia pakubwa kati ya hao wapalestina na Israel
 
SA ina wanasheria bora sana hiyo kesi watawakimbiza mno Israel wapo Ma Prof wawili ni wazuri sana kwa hizi kesi ngoja tusubiri muda utaongea zaidi..
 
Jews ni jamii iliyochanganyika na race zote.
Hapa nakubaliana na wewe mkuu
Dini ya yao wanaita Judaism na Taifa ni Israel.
Kwa vile Jews ni mchanganyiko wa race kutoka mataifa yote, basi ulitakiwa useme kuwa dini au imani hiyo ya Jews ilianzishwa nchini Israel na sio kwamba wote taifa ni Israel, maana hiyo ni dini kama ilivyo Ukristo na Uislam. Mfano Tanzania kuna wakristo wa dhehebu la Roma, lakini utaifa wao ni watanzania na sio waroma au waisrael ambapo inasemekana imani hiyo ya Kikristo ndipo ilipoanzia.

Vilevile hauwezi kuwapa waislam wa Tanzania au Kenya kuna utaifa wa Saudi Arabia kisa dini wanayoamini imeanzishwa nchini huko.

Hivyo unavyosema kuwa Jews au wayahudi taifa la ni Israel unakosea maana ushakiri mwenyewe kuwa kuna ambao sio waisrael, umesema kuna waithiopia, wamisri nk.
Sasa hawa Jews wapo ambao sio waisraeli kuna raia wa Morocco Yemen Iran Iraq Jordan jews na Ethiopia.
Hii ndo nimejibu hapo juu
Hawa walioko Israel wengi ni wale waliorud baada ya mateso huko walipokuwa hasa ulaya kwa miaka mingi ya utawanyiko wao.
Kwa vile umejibu vizuri swali langu kuwa wayahudi wapo wa race tofauti basi haina haja ya kubisha kuwa kina Netanyahu wanaweza kuwa wayahudi wenye asili ya kizungu. Kama wazungu haswa waingereza waliweza kwenda Marekani kusaka rasilimali za huko America kwa njia walizozijua wao, wakatawala na baadae kupigana wenyewe kwa wenyewe na kupelekea baadhi yao kuanzisha taifa la Marekani, kama wazungu waingereza waliweza kwenda kusaka rasilimali Canada, New Zealand, Australia, South Africa, Zimbabwe, Kenya, Ghana, Nigeria wakaingia katika hizo nchi kwa njia wanazozijua wao, wakatawala na wengine kubaki na kutengeneza mataifa kama New Zealand, Canada nk, je wanaweza kushindwa kuingia Israel kupitia mgongo wa wayahudi na kufanya nchi yao?

Kwa vile ni vigumu kupima DNA ni nani anaeweza kuthibitisha kuwa mtu aina ya Netanyahu ni myahudi wa asili ya Israel? Dunia ya leo haswa kwa wenzetu wazungu ambao wako tayari kufanya lolote au chochote kwa masilahi ya nchi zao usishangae kina Netanyahu wakatengenezwa toka wakiwa shuleni ili waje wajifanye wayahudi kwa malengo maalumu ya wanaomtuma.
Japo wapo wale waliokuwepo hapo muda wote mpaka Wakat wa anguko la ottoman empire.
Katika msafara wa mamba kenge nao wapo. Ukute ile mission iliyoongozwa na UK kuwarudisha waisrael nchini hapo ndio imetumiwa njia ya kupenyeza watu wao kwa sababu ya masilahi yao.
 
Wewe ndio hujuwi unachoongea,hao Hamas wanapigana kwa kujificha kwa raia, Israeli ingetaka kupiga mtu yeyote bila kuangalia raia wapalestina wangeisha,halafu hiyo SA haimuwezi Israeli kuanzia uchumi mpaka technology,hao waarabu wanaomzunguka Israeli kwa pamoja walichezea kichapo ndani ya siku sita,SA anatafuta kiki,hamuwezi Israel kwa chochote kile,na kadiri muda unavyozidi kwenda utathibitisha mwenyewe nan anaumia pakubwa kati ya hao wapalestina na Israel
Hadithi hadithi hadithi njoo utam kolea 😂😂 unajua SA inashinda nchi ngapi za Ulaya uchumi. Alafu SA ndio inategemewa rasilimali zake na Ulaya ndiomaana wazungu walikataa kuondoka.

Israel mpaka leo bado inategemea msaada wa kijeshi na fedha za kujikimu kutoka Marekani, UK na Ujerumani, wao binafsi hawana uwezo wa kujiendesha, kujilinda wala kujisimamia hili hata wewe mwenyewe rohoni kwako unalijua, sema ndo vile umeamua na wewe ujitutumue ili uonekane haushindwi.

Hayo unayosema wewe ni maelezo tu ya kusimuliwa ambayo hakuna mtu aliyashuhudia. Lakini haya yanayoendelea leo ni ya dhahiri kila mtu anaona, anasikia au kusoma kupitia simu yake. Kwa vile media na utandawazi wa mitandao haukuwepo wajinga wakawa wamejaribu kutulisha matango pori sijui operation Entebbe huko Uganda. Wajinga wengi walimezeshwa uongo ule. Sasa leo watu wanataka kuona hao makomandoo walioenda kuokoa watu Uganda wawaokoe hao ndugu zao ambao wapo hapo hapo karibu yao, lakini wapi tunakwenda mwezi wa NNE huu hakuna hata dalili ya makomandoo na jeshi lao lenye askari mpaka wa akiba, mivifaru, midege, mimeli ya kijeshi vyote vinauwa watoto wachanga tu wasiokuwa na uwezo wa kurusha hata jiwe.

Tunashukuru Mungu media na mitandao ya miaka hii imetusaidia kuuona ukweli na uongo wa makomandoo uchwara. Kusadiki kwa toma ni kujionea, sio zile porojo za kuadisiwa ambazo nyingi hazina ukweli.

Vijana elf 20 tu wanalichachafya taifa zima na vibaraka wao.
 
SA ina wanasheria bora sana hiyo kesi watawakimbiza mno Israel wapo Ma Prof wawili ni wazuri sana kwa hizi kesi ngoja tusubiri muda utaongea zaidi..
SA inajiamini katika hili, na wanajua wanachokifanya. Lazima Israel waombe poo
 
Hadithi hadithi hadithi njoo utam kolea 😂😂 unajua SA inashinda nchi ngapi za Ulaya uchumi. Alafu SA ndio inategemewa rasilimali zake na Ulaya ndiomaana wazungu walikataa kuondoka.

Israel mpaka leo bado inategemea msaada wa kijeshi na fedha za kujikimu kutoka Marekani, UK na Ujerumani, wao binafsi hawana uwezo wa kujiendesha, kujilinda wala kujisimamia hili hata wewe mwenyewe rohoni kwako unalijua, sema ndo vile umeamua na wewe ujitutumue ili uonekane haushindwi.

Hayo unayosema wewe ni maelezo tu ya kusimuliwa ambayo hakuna mtu aliyashuhudia. Lakini haya yanayoendelea leo ni ya dhahiri kila mtu anaona, anasikia au kusoma kupitia simu yake. Kwa vile media na utandawazi wa mitandao haukuwepo wajinga wakawa wamejaribu kutulisha matango pori sijui operation Entebbe huko Uganda. Wajinga wengi walimezeshwa uongo ule. Sasa leo watu wanataka kuona hao makomandoo walioenda kuokoa watu Uganda wawaokoe hao ndugu zao ambao wapo hapo hapo karibu yao, lakini wapi tunakwenda mwezi wa NNE huu hakuna hata dalili ya makomandoo na jeshi lao lenye askari mpaka wa akiba, mivifaru, midege, mimeli ya kijeshi vyote vinauwa watoto wachanga tu wasiokuwa na uwezo wa kurusha hata jiwe.

Tunashukuru Mungu media na mitandao ya miaka hii imetusaidia kuuona ukweli na uongo wa makomandoo uchwara. Kusadiki kwa toma ni kujionea, sio zile porojo za kuadisiwa ambazo nyingi hazina ukweli.

Vijana elf 20 tu wanalichachafya taifa zima na vibaraka wao.
Endelea kujifariji,hivi aliyeomba vita isimamishwe kwa muda apewe msaada wa vyakula na huduma nyingine za kijamii ni nani? Ni raia wa upande upi wamekufa zaidi? Ni nani ambae amepoteza eneo lake?
 
Endelea kujifariji,hivi aliyeomba vita isimamishwe kwa muda apewe msaada wa vyakula na huduma nyingine za kijamii ni nani? Ni raia wa upande upi wamekufa zaidi? Ni nani ambae amepoteza eneo lake?
Kwahiyo wewe ubora wa vita unaupima kwa kuuwa raia. Yani wanaouwa raia wengi kwa midege, mivifaru na mimeli ndio mabingwa wako hata kama wameshindwa kuwaokoa mateka wao waliotekwa na vijana elf 20 tu 😄😄😄

Nina wasi wasi na umri wako, huenda najadiliana na mtu alieiba simu ya shemej yake au baba yake ili aje aitetee Israel.

Acha nikuache ulale kabla shemej yako hajarudi akakukuta unachezea simu yake. Siku ukikua ukinunua simu yako na kuanza kufuatilia haya mambo kwa kutulia nina imani utajifunza mengi.
 
Kwahiyo wewe ubora wa vita unaupima kwa kuuwa raia. Yani wanaouwa raia wengi kwa midege, mivifaru na mimeli ndio mabingwa wako hata kama wameshindwa kuwaokoa mateka wao waliotekwa na vijana elf 20

Kwahiyo wewe ubora wa vita unaupima kwa kuuwa raia. Yani wanaouwa raia wengi kwa midege, mivifaru na mimeli ndio mabingwa wako hata kama wameshindwa kuwaokoa mateka wao waliotekwa na vijana elf 20 tu 😄😄😄

Nina wasi wasi na umri wako, huenda najadiliana na mtu alieiba simu ya shemej yake au baba yake ili aje aitetee Israel.

Acha nikuache ulale kabla shemej yako hajarudi akakukuta unachezea simu yake. Siku ukikua ukinunua simu yako na kuanza kufuatilia haya mambo kwa kutulia nina imani utajifunza mengi.
Endelea kuwa na huo wasiwasi,unafaham maana ya vita? Unafaham kwanini Hamas wanavizia yani wanajificha kwa raia na hawawaface Idf direct? Usianze kukwepa mada mara oh sijuwi umri wako,mara unakaa kwa shemeji yako,mkuu acha ramri na tabia za kike,tubishane kwa hoja,hunifaham Wala sikufaham ila tuheshimiane
 
Endelea kuwa na huo wasiwasi,unafaham maana ya vita? Unafaham kwanini Hamas wanavizia yani wanajificha kwa raia na hawawaface Idf direct? Usianze kukwepa mada mara oh sijuwi umri wako,mara unakaa kwa shemeji yako,mkuu acha ramri na tabia za kike,tubishane kwa hoja,hunifaham Wala sikufaham ila tuheshimiane
Upuuzi mtupu.
 
Back
Top Bottom