Wengi wanaotaka wake zao wasifanye kazi wana upeo mdogo wa kufikiri halafu ni wabinafsi

Wengi wanaotaka wake zao wasifanye kazi wana upeo mdogo wa kufikiri halafu ni wabinafsi

Mwanamke ni pambo hatakiwa kufanya kazi yeyote zaidi yakumburudisha mume wake.

Ukishamuoa mwanamke amebadili koo, kutoka ukoo wao kuja upande wa mume, ndio maana wengine hubadili mpaka majina ya wazazi wao.

Baada yakumuoa apaswa kufata Sheria na taratibu za upande wa mumewe, hayo yakuhudumia ndugu zake sijui wadogo zake nimambo ya ziada. Mnapooana jukumu kubwa nilakuangalia familia yenu nyinyi wawili nakujenga mpango mkakati wa watoto wenu baadae waishije. Kila mtu akianza kuhudumia nakutoa kipaumbele kwao hapatakua na familia tena.

Kila mtu ajenge kwao, Kila mtu awe anatuma hela kwao, kwenu nyie wawili mtapajenga lini?.

Mwanamke akikubali kuolewa basi ajue na atambue anaenda kufata taratibu na Sheria za mumewe kama hayupo tayari basi asikubali kuolewa.

Sisi wengine tunaamini hata kama niko wrong basi mwanamke anafaa kunisikiliza na kutii nilichokisema.

Ndio maana Koo nyingine wanaume hawali chakula sehemu Moja na wanawake jiulize Kwa nini?. Hili nikuwafunza watoto wakiume na kike Kila mtu kujua majukumu ya baba yake na mama yake niyapi , na namna mwanamke anavyopaswa kumtii na kumuandalia chakula mumewe.

Majukumu yamwanamke ndani ya nyumba yanafahamika na majukum ya mwanamme ndani ya nyumba yanafahamika, Sasa ukitaka kila upande uingilie majukumu ya nwenzake hapatotosha, ndio maana familia nyingi zinaparaganyika Kwa Kila upande kuona unaweza kuhimili kufanya majukumu ya mwenzake.

Kila mtu aishi nakufanya yale ambayo anatakiwa kufanya nakutekeleza majukumu yake.

Nakipindi unaoa au kuolewa basi mwenzi wako ajue lengo ni nini hasa, mimi nikitaka kuoa basi lengo nimke wangu aagalie watoto basi, mengi kama yakija basi niyaziada. Lakini lengo kuu lazima hata yeye alifahamu Kwa mantiki kwamba anaolewa kuja kuwa mama wa nyumbani.
Hakuna sehemu yotote kwenye biblia wala kwenye qu'ran mwanamke analisha Familia.

Matajiri woote hadi leo hakuna Mke wake anafanya biashara za Upatu.

Ni umaskini wetu tu.

Mwanamke ni Mfalme wa familia na watoto.

Waarabu na wahindi wametuzidi hapa.
 
Kwani akifanya kazi hawezi kuwa pambo au kumburudisha mumewe?

Kuna wanawake wanaofanya kazi na bado ni warembo kuliko wanaokalizwa nyumbani.
Hoja yako haina mashiko
We naona hujui hata kazi zenyewe......awe polisi kila siku lindoz akirudi kachoka balaa.

Bado unataka awe pambo? We utakuwa ni mnyanyasaji wa wanawake sio bure.
 
WENGI WANAOTAKA WAKE ZAO WASIFANYE KAZI WANAUPEO MDOGO WA KUFIKIRI ALAFU NI WABINAFSI

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Chizi sio lazima uokote Makopo, kuna Chizi Fresh ambao ndio wengi wapo kundi hili tena wengine wasomi. Alafu kuna ambao ni Chizi Maarifa hawa wengi ukiwaona kwa mbali unaweza kudhani wako timamu lakini ukiwatazama kwa ukaribu ni wendawazimu.

Unakuta kajamaa kametoka familia Maskini, kameoa kutoka Familia Maskini. Kanafanya kazi iwe kwa kuajiriwa au kujiajiri lakini pato lake kwa mwezi hata Milioni moja halifiki.
Lakini ukikasikiliza mawazo yake kuhusu uchumi na mahusiano utabaki kuona kalivyo na upeo mdogo.

Yaani kisa umenunua mwanamke kwa bei ya jumla(kutoa mahari) labda shilingi milioni nne. Basi Mwanamke huyo ambaye sasa ataitwa mkeo unasema asifanye kazi kisa umemuoa.

Ukiulizwa kwa nini asifanye kazi? Huna hoja ya maana hata moja zaidi ya kutokujiamini, ubinafsi na ukandamizaji kama sio unyanyasaji.

Unamwambia mkeo asifanye kazi au asimiliki kipato kingi tena inafikia hatua kwa uzuzu wako unamhujumu mkeo na kumuwekea vikwazo ili asifanikiwe. Ati unaogopa atakunyanyasa ati atakuwa jeuri. Chizi weeeh!

Mkeo asifanye kazi, unapesa za kumhudumia mahitaji yake yote?
Alafu wengi wenye mtazamo kama huu unakuta Wake zao hata mafuta ya kupaka hawana, nguo wanazovaa mtumba, tena bora mtumba lakini ziwe nyingi. Lakini hata pesa ya kuwanunulia wake zao nguo walau kila mwezi nguo moja au mbili hawana. Mke kapauka, kazeeshwa. Yaani hatamaniki tena. Kila siku kumlisha mkeo Maharage kazi kujambajamba. Alafu unakuta jitu linasema linahudumia mke. Alafu halitaki mkewe afanye kazi. Ili angalau pesa ya kubadilisha chakula hapo nyumbani iwepo sio kila siku ugali na mchicha au maharage. Nyama na samaki mpaka sikukuu. Familia inapitisha Wiki hata maziwa hakuna. Alafu ulivyo chizi unaona sawa tuu. Alafu ukijaribu mtandaoni huku ooh! Mwanamke asifanye kazi utadhani umemudu mahitaji yake. Mwehu wewe!

Watoto wako ada zenyewe zinakusumbua, lishe yenyewe hawali. Utapiamlo na kifaduro kinawasumbua. Watoto mpaka imefikia hata uwezo wa kufikiri hawana Kwa sababu kila siku unawalisha chakula kingi cha wanga kama ugali, mihogo, maandazi na maujiuji ya nafaka. Ilhali kiafya watoto chini ya miaka 20 wanatakiwa kula protein nyingi kuliko kundi jingine la chakula ili miili yao ijengwe vyema. Vyakula vya protini ambavyo vinatakiwa viwe vingi katika mlo wenu hapo nyumbani ni Samaki, nyama, maharage, maziwa, mayai n.k.
Lakini kwa vile kipato chako ni duni huwezi kuhudumia hivyo. Alafu kwa vile tayari unakifaduro cha ubongo huoni kama unahitaji usaidizi na kwa ubinafsi wako unataka watoto wako nao wakose lishe kama wewe ulivyokosa. Ati mke asifanye kazi au asikusaidie majukumu. Kwa huduma gani unazotoa mwehu wewe!

Haya, mshahara wako wenyewe haukutoshi kutunza Wazazi wako.
Alafu hutaki mkeo asifanye kazi. Hivi unafikiri wazazi wake mwanamke watahudumiwa na kutunzwa na nani kama sio huyo mke wako. Mbuzi wewe.

Pesa yako hata milioni moja haifiki kwa mwezi. Unataka wadogo wa mkeo wahudumiwe na nani?
Unataka ile nyumba ya wazazi wa mkeo ifanyiwe ukarabati na nani kama sio mkeo.

Alafu haya machizi Fresh hapohapo unayasikia yakisema, usijenge Ukweni, mara Usitoe pesa Ukweni. Alafu hapohapo unayakuta yanazuia Wake zao wasifanye kazi. Hivi kama sio Ushetani na laana hizo ni kitu gani? Hivi kuna ubinafsi na ukatili wa kutisha zaidi ya huo?

Bado umfulishe na kumfanyisha makazi mengi bila kumpa lishe bora. Zaidi ya hapo umpige kisa ameona mambo sio mambo na umemgeuza msukule wake hapo.

Embu acheni Upumbavu wenu.
Ni mara elfu Mwanamke asioelewe au awe single Mother alee Watoto wake kitabutabu kuliko kuishi na mwanaume mwenye Ushetani wa namna hiyo.

Mwanaume elewa kuwa kama wewe unavyopenda na kuhitaji kuhudumia Wazazi wako ndio hivyohivyo mkeo naye anataka wazazi wake wahudumiwe.

Na ndio maana Watibeli Hawatoi Mahari kwa sababu inaharufu ya manunuzi au biashara ya binadamu kwa visingizio vya kishetani.

Hutaki mkeo afanye kazi alafu ukiombwa pesa ya kuwasomesha wadogo zake unapiga yowe na kulalamika. Wewe mwehu nini.

Na mimi nawaambia Wanawake hasa Watibeli ni lazima wafanyekazi. Kufanya kazi ni amri ya kila kiumbe ili kiwe huru na kujitegemea chenyewe. Binadamu asiyefanya kazi ni mfu.
Mtu mwenye akili na Mwanamke kamili na mke mwema hujisikia aibu na fedheha kumtegemea mumewe kwa kila kitu.

Mimi nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mdogo wangu Robert,, umeowa? Kweli,,, oa kwaza utatuletea mlejesho..
 
Mkuu mimi mke wangu nilimruhusu afanye kazi ila saa kumi na mbili jioni awe home kunipikia (maana anajua kabisa chakula cha jioni anatakiwa apike yeye na sio dada wa kazi)

Siku akaniletea pigo zake kuniambia Boss alimsubirisha

Nikamuuliza, "Huyo Boss wako anakulipa sh ngapi kwa mwezi?"
Aliponijibu nikamwambia haya kuanzia sasa hakuna kwenda kazini maana pesa ninayompa mimi kwa ajili ya kutumia kazini ni nyingi mara mbili ya mshahara wake

Yaani alipwe mshahara wa miezi miwili ndo afike pesa ninayompa kwa ajili ya matumizi yake

Sasa nikamwambia akae Nyumbani huo mshahara anaolipwa huko nitakuwa namlipa mimi
 
Hizo ni blue print za mifumo dume ambazo umeaminishwa hivyo.

mtoto wakike alikuwa apelekwi shule sababu yeye alikuwa kama mtumwa tu itafika umri atachukuliwa na mwanaume kwenda kumtumikia.

Hii ni karne ya ngapi? Unataka dunia iendelee kuwa vile vile miaka 1000 nyuma?
Wanawake wa sasa bila kuwa na mfumo dume hutoboi

Wapo wa kuishi nao hivyo unavyotaka wewe ila sio hawa wa Haki Sawa
 
Nilikuwa nao marafiki wa hivi nikaachana nao.

Tabia zao ni za hovyo.

Ukiwauliza kwanini unataka mwanamke wa hivi wanadai eti Mwanamke awasaidie majukum na bills za nyumbani.

Yule jamaa mmoja alipigwa vibuti hadi akajuta.
Yeye alikuwa analazimisha lazima apate Mwl, Secretary na hata Yeyote mwenye Degree.....sasa mademu wakawa wanamlia pesa tu kumbe wana watu wao.
Ni mtihani sana.
 
Nakipindi unaoa au kuolewa basi mwenzi wako ajue lengo ni nini hasa, mimi nikitaka kuoa basi lengo nimke wangu aagalie watoto basi, mengi kama yakija basi niyaziada. Lakini lengo kuu lazima hata yeye alifahamu Kwa mantiki kwamba anaolewa kuja kuwa mama wa nyumbani.
Sasa kwamsimamo wako huo sio vibaya. Ila elewa hakuna mwenye maagano na Muumba. Ikitokea mume akaumaliza mwendo akaacha watoto unadhani ninani ayawalea ikiwa mama hana a,b,c juu ya kujishuhulisha?
Watu wafanye kazi. Tasiige mabilionea kupumzisha wake zao nyumbani wakati maskini hata mkewe ameshindwa kumuwekea house girl
 
Mleta mada ameandika kwahasira inaonekana jambo hilo limemgusa mojakwamoja ndani mwake. Anazohoja nzuri lakini uwasilishaji wake umekosa utulivu
 
Hapa mkuu naona umetaka tu kujifurahisha na kujipa matumaini kwa uongo.
matumaini yapi mfungie mkeo aliwe kwa kuona hana kazi ya kufanya na anataka pesa... ataliwa hadi na waokota makopo....
 
Tafuta pesa, imeandikwa mwanaume atakula kwa jasho, mwanamke atazaa kwa uchungu
 
WENGI WANAOTAKA WAKE ZAO WASIFANYE KAZI WANAUPEO MDOGO WA KUFIKIRI ALAFU NI WABINAFSI

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Chizi sio lazima uokote Makopo, kuna Chizi Fresh ambao ndio wengi wapo kundi hili tena wengine wasomi. Alafu kuna ambao ni Chizi Maarifa hawa wengi ukiwaona kwa mbali unaweza kudhani wako timamu lakini ukiwatazama kwa ukaribu ni wendawazimu.

Unakuta kajamaa kametoka familia Maskini, kameoa kutoka Familia Maskini. Kanafanya kazi iwe kwa kuajiriwa au kujiajiri lakini pato lake kwa mwezi hata Milioni moja halifiki.
Lakini ukikasikiliza mawazo yake kuhusu uchumi na mahusiano utabaki kuona kalivyo na upeo mdogo.

Yaani kisa umenunua mwanamke kwa bei ya jumla(kutoa mahari) labda shilingi milioni nne. Basi Mwanamke huyo ambaye sasa ataitwa mkeo unasema asifanye kazi kisa umemuoa.

Ukiulizwa kwa nini asifanye kazi? Huna hoja ya maana hata moja zaidi ya kutokujiamini, ubinafsi na ukandamizaji kama sio unyanyasaji.

Unamwambia mkeo asifanye kazi au asimiliki kipato kingi tena inafikia hatua kwa uzuzu wako unamhujumu mkeo na kumuwekea vikwazo ili asifanikiwe. Ati unaogopa atakunyanyasa ati atakuwa jeuri. Chizi weeeh!

Mkeo asifanye kazi, unapesa za kumhudumia mahitaji yake yote?
Alafu wengi wenye mtazamo kama huu unakuta Wake zao hata mafuta ya kupaka hawana, nguo wanazovaa mtumba, tena bora mtumba lakini ziwe nyingi. Lakini hata pesa ya kuwanunulia wake zao nguo walau kila mwezi nguo moja au mbili hawana. Mke kapauka, kazeeshwa. Yaani hatamaniki tena. Kila siku kumlisha mkeo Maharage kazi kujambajamba. Alafu unakuta jitu linasema linahudumia mke. Alafu halitaki mkewe afanye kazi. Ili angalau pesa ya kubadilisha chakula hapo nyumbani iwepo sio kila siku ugali na mchicha au maharage. Nyama na samaki mpaka sikukuu. Familia inapitisha Wiki hata maziwa hakuna. Alafu ulivyo chizi unaona sawa tuu. Alafu ukijaribu mtandaoni huku ooh! Mwanamke asifanye kazi utadhani umemudu mahitaji yake. Mwehu wewe!

Watoto wako ada zenyewe zinakusumbua, lishe yenyewe hawali. Utapiamlo na kifaduro kinawasumbua. Watoto mpaka imefikia hata uwezo wa kufikiri hawana Kwa sababu kila siku unawalisha chakula kingi cha wanga kama ugali, mihogo, maandazi na maujiuji ya nafaka. Ilhali kiafya watoto chini ya miaka 20 wanatakiwa kula protein nyingi kuliko kundi jingine la chakula ili miili yao ijengwe vyema. Vyakula vya protini ambavyo vinatakiwa viwe vingi katika mlo wenu hapo nyumbani ni Samaki, nyama, maharage, maziwa, mayai n.k.
Lakini kwa vile kipato chako ni duni huwezi kuhudumia hivyo. Alafu kwa vile tayari unakifaduro cha ubongo huoni kama unahitaji usaidizi na kwa ubinafsi wako unataka watoto wako nao wakose lishe kama wewe ulivyokosa. Ati mke asifanye kazi au asikusaidie majukumu. Kwa huduma gani unazotoa mwehu wewe!

Haya, mshahara wako wenyewe haukutoshi kutunza Wazazi wako.
Alafu hutaki mkeo asifanye kazi. Hivi unafikiri wazazi wake mwanamke watahudumiwa na kutunzwa na nani kama sio huyo mke wako. Mbuzi wewe.

Pesa yako hata milioni moja haifiki kwa mwezi. Unataka wadogo wa mkeo wahudumiwe na nani?
Unataka ile nyumba ya wazazi wa mkeo ifanyiwe ukarabati na nani kama sio mkeo.

Alafu haya machizi Fresh hapohapo unayasikia yakisema, usijenge Ukweni, mara Usitoe pesa Ukweni. Alafu hapohapo unayakuta yanazuia Wake zao wasifanye kazi. Hivi kama sio Ushetani na laana hizo ni kitu gani? Hivi kuna ubinafsi na ukatili wa kutisha zaidi ya huo?

Bado umfulishe na kumfanyisha makazi mengi bila kumpa lishe bora. Zaidi ya hapo umpige kisa ameona mambo sio mambo na umemgeuza msukule wake hapo.

Embu acheni Upumbavu wenu.
Ni mara elfu Mwanamke asioelewe au awe single Mother alee Watoto wake kitabutabu kuliko kuishi na mwanaume mwenye Ushetani wa namna hiyo.

Mwanaume elewa kuwa kama wewe unavyopenda na kuhitaji kuhudumia Wazazi wako ndio hivyohivyo mkeo naye anataka wazazi wake wahudumiwe.

Na ndio maana Watibeli Hawatoi Mahari kwa sababu inaharufu ya manunuzi au biashara ya binadamu kwa visingizio vya kishetani.

Hutaki mkeo afanye kazi alafu ukiombwa pesa ya kuwasomesha wadogo zake unapiga yowe na kulalamika. Wewe mwehu nini.

Na mimi nawaambia Wanawake hasa Watibeli ni lazima wafanyekazi. Kufanya kazi ni amri ya kila kiumbe ili kiwe huru na kujitegemea chenyewe. Binadamu asiyefanya kazi ni mfu.
Mtu mwenye akili na Mwanamke kamili na mke mwema hujisikia aibu na fedheha kumtegemea mumewe kwa kila kitu.

Mimi nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mwanamke akifanya kazi pesa yake itakuwa inafanya nini ?
 
Mwanamke asaidiane na mumewe au sio ?😀

Yaani wanawake hawa wasaidiane na mume zao au wanawake wengine una wazungumzia ?😀
 
Umegenerize sana, wanawake wapo wa type nyingi ni kama kuku, wapo kuku mzinga kwajil ya pambo wapo kuku wa nyama na wapo kuku wa mayai.

Ukitaka mwanamke wa kukaa ndani wapo wengi tu kwa wadigo ukitaka mpambanaji wasio bagua kazi nenda kwa waha uko, ukitaka wenye kazi nenda migodini mara uko. Na wote unaweza kuishi nao kwa raha inategemea na wewe unataka nini. Kupanga nikuchagua hayana muongozo.
 
Back
Top Bottom